Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

"Yesu akamwambia, Wewe, kwa kuwa umeniona, umesadiki; wa heri wale wasioona, wakasadiki."
Yohana 20:29.

Ndio hapo sasa tunarudi kwenye uhalisia wa swala zima la imani. Mimi nafikiri kuna tatizo kubwa sana kwenye uumbaji, au la basi kuna tatizo kwenye maandiko!

Haiingii akilini kwamba eti Malaika walioumbwa na Mungu, wakaishi nae mbinguni, eti wanaweza kufika mahali wakamgeuka na kuanza kupigana nae vita!!! Ina maana malaika wenyewe hawakua wanamuamini Mungu, walikua wanamuona anazingua maana otherwise kwanini waingie msituni kama kila kitu kilikua poa?

Adam na Hawa, wameongea na Mungu ana kwa ana kama mimi na wewe tunavyoongea hapa, wanapiga stori, wanacheka fresh, ila mwisho nao wakaona huyu anazingua wakamgeuka!!

Akina Musa, mfalme Daudi, Sulemani nk mpaka hao wa agano jipya kina Petro, Yuda, Tomaso na wengine wengi hatukutegemea kabisa wawe na chembe ya mashaka kwani wao waliona "first hand" kila kitu Mungu alichofanya!

Sasa kama hao walishindwa kuwa na imani, hivi sisi huku madongokuinama tunawezaje kujidai kua na imani?? Hiyo imani tunaitolea wapi kwa mfano? Huku wengi tunazuga tuu hamna cha imani wala nini.
 
Na mtapigwa sana nasema mtapigwa tuu. ##Wanawake##
 
We hupendi vizuri mkuu? Au unaishi kwenye nyumba ya makuti na taa za vibatari?!
Napenda mkuu. Ndio maana wanatumia hiyo weakness kuwapuna wafuasi mkuu. We uuziwe maji buku,mafuta buku, chumvi sijui buku. Mtu ananunua vyote hivyo let's say jumla Tshs.3,000/=, imagine wamehudhuria waumini buku tatu tu na wote wakanunua zaga, inaleta 9M hapo hujaongelea sadaka zaidi ya tano. Sijui shukrani, malimbuko, kukombolewa etc.
 
Unajua kuna uwongo mwingi sana kwenye haya masuala ya kiimani nowdays. Watu wanacheza na psychology yako, wakijua unataka pesa/utajiri na kuponywa certain disease. Kuna mwengine naskia Yuko pale maeneo ya lufungila anaitwa nabii Mussa. Huyo mafuta yake ya upako yanauzwa Tshs. 15,000/= . Siwezi kuwasemea vibaya watumishi wa bwana Ila kiukweli akili yako changanya na za kuambiwa. Siku hizi watu hatupendi injili ya kuhusu ufalme wa Mungu tunataka kupokea miujiza ya vitu vizuri vizuri tu.
Huyo jamaa ndio balaa kuna mtu alikuja kuombewa kwake mwanae kapotea baada ya siku kadhaa akapatikana huko Kariakoo
Ila hawa jamaa kama pesa wanawarubuni sana watu
 
Kuna mdogo wangu wa kike yeye na mme wake huwaambii kitu kuhusu prophet Bushiru yule mzambia sijui. Akanipelekaga hadi kanisani kwao makongo juu Linaitwa Enlightened Christian Gathering (ECG). Nikakuta asilimia kubwa watoto wa chuo na watu wanaoonekana maisha Bora, nikaona udwanzi sikwenda Tena. Sasa bwana Bushiru akaja kupata msala Sauzi nikamwambia dogo unaona sasa huyo mchungaji wenu, still dogo bado anaamini eti Ni shetani tu anataka kumchafua nabii wao. SMH
 
Kuna mama mmoja ni mstaafu wa jeshila wananchi, alipopokea mafao yake chap kwa ukali akammegea mtumishi wake milioni 25 za shukran kmmmk.
Hapo utakuta mama aliaminishwa kwamba maombi ya mchungaji ndio yamepelekea yeye kupata mafao 😂😂😂
 
Huyo jamaa ndio balaa kuna mtu alikuja kuombewa kwake mwanae kapotea baada ya siku kadhaa akapatikana huko Kariakoo
Ila hawa jamaa kama pesa wanawarubuni sana watu
Mtoto akipotea unaenda polisi kuomba msaada wa kumtafuta.
 
Back
Top Bottom