Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

Zile shuhuda kwenye maombezi ya Manabii

Na ni kwanini watu wote ambao huombewa na kupona ni wale wenye magonjwa yasiyoonekana / yasiyo na ushahidi dhahiri (mfano kuumwa kichwa, tumbo, matatizo ya akili nk.)

Sijawahi kuona mtu aliekatika mguu/mkono akapelekwa kwenye maombi kuombewa na mguu ukarudi! Kama Yesu alivyorudisha sikio la yule jamaa.
Utakuwa unawapa mtihani mgumu, dizaini kama hiyo wanahitimisha kwamba hana imani...
 
Katika vitu nilivyo shindwa kuviamini ni zile shuhuda zinazo tolewa, Ukikaa ukasoma between the line zile shuhuda kama kuna za kweli basi ni moja kati ya 1000 zinazo bakia ni za ku frame ku attract watu.

Na cha kushangaza watoa Shuhuda wengi huwa ni wageni maachoni mwa waumini. Unakuta ni Sura ngeni au mpya.

Na huu Usanii anaufanya sana anaye jiita Mwaponsa yule Jamaa ni Master wa ku frame shuhuda
Nireteeni gwajima
😀😀
 
Ww huna miguu na unatamani kutembelea, ukasikia nabii flani anaweza kukusaidia, akakuombea na bado ukashindwa kutembea na kukuambia huna Imani, kweli kweli huna miguu na huna imani kweli.? Em kuwa serious mzee
Haya mambo ni magumu sana mkuu. Mimi nna ndugu yangu tangu mwaka 1995 ame paralyze miguu. Hakuna maombi ambayo hajapelekwa, mafanikio hakuna na always kisingizio kimekua "hana imani"! Hivi mtu mwenye imani anatakiwa aweje?
 
Me kuna kipindi nilienda kwa Peter Nyaga Nabii na Dr
Wakati tupo mle ndani ghafla akaja jamaa akakaa upande wetu wakati huo msaidizi wa Dr Peter Nyaga anaendelea na mahubiri ghafla yule jamaa akaanguka chini nakuanza kugalagala kisha wakampeleka mbele, hazikupita dk2 yule jamaa akazindukika na akawa yuko fresh na kuonyesha alijipangwa alivaa nguo za kawaida
Daah! Huyo nae ni msanii tu kanisani kwake ameweka mpaka fridge linasoda na maji.
Watu wanamchezea sana Mungu
 
Haya mambo ni magumu sana mkuu. Mimi nna ndugu yangu tangu mwaka 1995 ame paralyze miguu. Hakuna maombi ambayo hajapelekwa, mafanikio hakuna na always kisingizio kimekua "hana imani"! Hivi mtu mwenye imani anatakiwa aweje?
Mm hapo ndipo naposhangaa, mtu ana shida na anauona msaada lakini et anaambiwa hana imani
 
Kwa siku moja mtume na nabii mwamposa. Anaingiza Zaid ya watu elf 15 kwa siku ibada iko mbili pale ..najuulizaga hv kweli watu wote hao hawashtuki kuwa wanatapeliwa ...na kila siku watu utoa ushuhuda pale kwake ..nashindwa kuelewa na kuamini kuwa mtu huyu Kuna kitu nyum ya Kaz zake hiz za ibada mnk watu wanajah haswaa haswa .....

Huwenda. Ikawa Ni mpakwa mafuta kweli
Ni ngumu Sana kumshuhudia uongo ..
 
Wanawake wanashikiwa sana akili hadi kuvuruga mahusiano na waume zao na kuvuruga mipango ya familia, maana mwanamke akiifuma laki mbili kwenye wallet hesabu ya kwanza ni kupeleka sadaka kwa mchungaji au nabii....
Naua mtu.![emoji19]
 
Back
Top Bottom