EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,477
- 15,347
Kwa hiyo tukioana alafu uninyime nitakufanya nini? Au mimi nikikunyima utafanya nini?
Inakua haki yako kivipi? Mi naona ni zawadi ya kupeana mkiamua.
Na it is so obvious to me hata nakosa argument za kujieleza hapa... lol
Unanipa talaka. Au ukininyima mimi naweza kukupa talaka. Kama mwanamume hana uwezo au hataki kutenda tendo la ndoa kutokana na kukosa nguvu za kumwezesha kufanya hivyo au basi tuu hataki tena kufanya tendo la ndoa na wewe, then unayo haki ya kisheria kuomba talaka.
Kwa maneno mengine, sheria inatoa fursa kwa mwanamke kuwasilisha maombi ya kubatilisha ndoa husika kwa sababu tu mume wake huyo hana uwezo wa kumwingilia kwa ajili ya kutimiliza tendo la ndoa au basi tuu hataki kufanya, jambo ambalo ni haki ya msingi (sio zawadi) miongoni mwa wanandoa.
Hapa haina maana kuwa mume ameshindwa kumridhisha mkewe, bali mume ameshindwa kabisa hata kuwa na hisia za kukutana na mkewe pindi mke anapohitaji. Kwa hiyo basi, tukioana usije kuomba talaka eti kisa nimeshindwa kukufikisha huko kileleni. Hapo patachimbika. LOL.