Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,820
- 59,407
Baada ya majadiliano na rafiki yangu kuhusiana na rushwa (zawadi) ya ngono mashuleni, vyuoni na maofisini nimejikuta najiuliza maswali mengi ambayo ningependa tusaidiane kuyajibu kwasababu kwa namna moja ama nyingine matokeo yake yanaathiri hata mahusiano, ndoa na malezi.
Kwanza ni wazi kabisa kwamba mtu akishaanza ni ngumu kuacha kutokana na ukweli kwamba anakuwa amejipa ukilema wa aina fulani. Kwamba kama alifaulishwa sekondari kuna nafasi kubwa atahitaji kufaulishwa chuoni, na akifaulishwa chuoni kuna nafasi kubwa atahitaji kubebwa pale atakapokuwa kwenye mchakato wa kupata kazi na baadae kwenye kujiendeleza (kupandishwa cheo, kupata nafasi za masomo, kushirikishwa kwenye semina zinazolipa n.k).
Sasa, Je:-
1. Mtu anapoanza kuhonga mwili wake ili afanyiwe kazi yake (kusoma, kuwa na CV kali, good work ethics, experience n.k) kwanini anafanya hivyo? Ni kutojiamini (mwenyewe siwezi) au ni kuzungukwa na watu wasio na imani nae (wazazi, ndugu na jamaa wasioisha kumwambia hatofika popote)?
2. Je, kuna hatari gani mtu kutegemea mwili wake badala ya akili na uwezo unaohitajika kupata kazi, kufaulu n.k?
3. Mtu kama huyu akija kuwa mzazi atakuwaje? Ataweza kumfundisha mtoto wake kuwa tofauti na alivyo yeye?
4. Malezi yanachangia vipi kuwafanya ndugu zetu wawe hivyo?
Najua kwa kiasi kikubwa hata system yetu (kupeana kazi kwa kujuana bila kujali sana uwezo wa kazi) inachangia kwa kiasi kikubwa, maana isingekuwa inaruhusu ingekuwa ngumu kutoa na kupokea rushwa ya aina hii ila napenda kuangalia kile kinachowasukuma wahusika zaidi.
Kwanza ni wazi kabisa kwamba mtu akishaanza ni ngumu kuacha kutokana na ukweli kwamba anakuwa amejipa ukilema wa aina fulani. Kwamba kama alifaulishwa sekondari kuna nafasi kubwa atahitaji kufaulishwa chuoni, na akifaulishwa chuoni kuna nafasi kubwa atahitaji kubebwa pale atakapokuwa kwenye mchakato wa kupata kazi na baadae kwenye kujiendeleza (kupandishwa cheo, kupata nafasi za masomo, kushirikishwa kwenye semina zinazolipa n.k).
Sasa, Je:-
1. Mtu anapoanza kuhonga mwili wake ili afanyiwe kazi yake (kusoma, kuwa na CV kali, good work ethics, experience n.k) kwanini anafanya hivyo? Ni kutojiamini (mwenyewe siwezi) au ni kuzungukwa na watu wasio na imani nae (wazazi, ndugu na jamaa wasioisha kumwambia hatofika popote)?
2. Je, kuna hatari gani mtu kutegemea mwili wake badala ya akili na uwezo unaohitajika kupata kazi, kufaulu n.k?
3. Mtu kama huyu akija kuwa mzazi atakuwaje? Ataweza kumfundisha mtoto wake kuwa tofauti na alivyo yeye?
4. Malezi yanachangia vipi kuwafanya ndugu zetu wawe hivyo?
Najua kwa kiasi kikubwa hata system yetu (kupeana kazi kwa kujuana bila kujali sana uwezo wa kazi) inachangia kwa kiasi kikubwa, maana isingekuwa inaruhusu ingekuwa ngumu kutoa na kupokea rushwa ya aina hii ila napenda kuangalia kile kinachowasukuma wahusika zaidi.