Zawadi ya ngono

cha kujiuliza, wote tumeng'aka sasa wanaofanya ni akina nani?
Ningependa kusikia ushahidi toka kwa victim angau mmoja

tunawahukumu bila kuwapa nafasi ya kusikia upande wao
Kongosho nafasi ya upande wa pili hatujaisikia hapa JF tu ila sio kama mitaani hawaongei.Wengine hata kufurahia wanafurahia kuweza kupata vitu kwa kutumia miili yao.
 
1. Kuna wanawake wanaojali sana miili yao kuiheshimu na wanautu, hawa wanatabia ya kuwa na misimamo na hawababaishwi na lolote mbele yao ili mradi anaujuzi na taaluma yake kichwani hawa hawadanganyiki.

2.Kuna wanawake wengine wanajiheshimu kwa kiwango cha uvuguvugu.hii inamaana kwenye tabia nzuri,kuheshimu miili yao na kuwa na msimamo wapo kiaia,na kwenye kutoiheshimu miili yao,kutokuwa na msimamo na kuwa na tabia mbaya napo wapo kiaina.hawa ni wa uvuguvugu.hawa huweza kurudi katika pointi namba moja endapo watapata ushauri mzuri na endapo wakipata ushauri wa hovyo wataangukia katika kundi namba tatu hapa chini.

3.Kuna wengine hao wanaitwa "i dont care",hawa hawana cha kupoteza,wao wana open their nanii na kutoa kuanzia atakaye mkutanisha na mabosi,bosi mwenyewe.yani wanasemaga niangushage a.k.a ma mama huruma walichopewa na mungu kumnyima mwanaume dhambi,na asipompa itapata kutu.

Kwa makundi hayo matatu hapo juu wenye kufall katika namba 1 ndo wanaunafuu wakutoa gift ,but group la 2 wanaweza change kutokana na mshauri atakaye mpata.

Wanawake mkazanie hapo kwenye namba 1.
Hapo ndipo salama yenu ilipo.

Niiiiice.
Alafu namba tatu sio kina "i don't care". . . .ni wajasirimiili. Wao mawazoni hawaoni kwanini wakose kitu wakati uwezo wa kukipata upo ndani yao.
 
EMT tuko pamoja, ila swala la kulaumu wapokeaji pekee mimi nakubaliana nalo pale inapotokea anaelazimika kutoa hiyo rushwa anapokua hajitambui kutokana na umri. Zaidi ya hapo, wanaendekeza wenyewe.Kama ambavyo mwalimu halazimiki kupokea ,ndivyo ambavyo mwanafunzi nae halazimiki kutoa .Utayari wao ndio unaopaswa kulaumiwa.

Huwa naamini kuwa kama kungekuwa hakuna wapokea rushwa, then watoa rushwa wasingekuwepo. Watampa rushwa nani? Chukulia kwa mfano, hata kama ni mtoa rushwa uliyekubuhu utampa nani rushwa Norway? Lakini kama wala rushwa wapo hasa kwenye sekta za nyeti za elimu na afya, utajikuta unatoa rushwa tuu hata kama hutaki.

Kuhusu rushwa ya ngono, unakuta, kwa mfano, mwalimu wa chuo kikuu mwneye mamlaka ya mwisho juu ya elimu yako ya chuo anakudai umpe ngono or otherwise unakwenda na maji. Ukienda kulalamika, kama Husiniyo alivyoelezea hapo juu ndio hivyo tena. Nimeshaona hata wanafuzi wa kiume wanafelishwa makusudi na walimu wanaume kwa vile tuu hawaivi au mwanafunzi alimake complain juu ya huyo mwalimu. Kwa vyoyote vile itakuwa ngumu kwa msichana kudhibitisha kuwa amedaiwa ngono na mwalimu wake. It will be difficult to prove.

Kuhusu walimu waliojiunga na ualimu ili tu wapate ajira nakubaliana na wewe kwa 105%. Nakumbuka mara ya mwisho kwenda kutembelea shule yangu ya sekondari nilikuta walimu wengi kweli vijana, baadhi nilisikia wana mahusiano na wasichana wa pale shuleni, tena tofauti tofauti. Na mmoja nilihakikisha mwenyewe, sadly alikua anatembea na binti ambae ni ndugu yangu na alikua na miaka 14 tu at the time. Pamoja na kwamba inawezekana binti alijirahisi mwenyewe ila ni dhahiri kwamba mwalimu ndie mwenye makosa zaidi maana yeye ndie aliyetakiwa kuwa mlinzi badala ya mtumiaji.Inasikitisha sana!!

Kabisa.Kumetokea wimbi la vijana wanaojiunga katika mafunzo ya ualimu wakiwa na matokeo mabaya hususan daraja la nne na sifuri katika masomo yao ya kidato cha nne na wengi wao wakiwa na historia isiyo nzuri. Hali hii inasababisha kuwepo kwa walimu wahuni, wasio na nidhamu kwa wanafunzi na wenye uwezo duni wa kufundisha hivyo kuhatarisha mikakati ya kuinua ubora wa elimu hasa ile ya msingi. Vijana wengi ambao wanajiunga na ualimu hawana sifa ya walimu wala hawana wito ila wanaona bora tu kupata ajira. Vyeti feki ni vingi na wenye daraja la nne na sifuri pia wapo vyuoni. Walimu hao kweli tunategemea kuboresha elimu ya watoto au kuharibu sio tuu kielimu bali pia sociallly?

Kuhusu suala la ngono, uhusuano wa kimapenzi kati ya mwalimu na mwanafunzi is a total breach of professional ethics. Mwalimu hawezi kumfundisha mwanafunzi ambaye mind yake (mwanafunzi) is preoccupied with the last sexual episode with the teacher. Kuna mwalimu alikuwa anamfukuzia mwanafunzi kwa miaka mitatu imagine lakini yule mwanafunzi alipoamua kulalamika mwalimu mlalamikiwa alidai kuwa mwanafunzi ndiye aliyekuwa anamfukuzia. Zipo kesi nyingi za aina hiyo na wananfuzi wengi wanaogopa hata kulalamika kutokana na power imbalance iliyopo.

Sio mbaya kuwa mwanafunzi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwalimu provided that both parties are over the age of consent na uhusiano sio wa kirushwa rushwa. Lakini uhusiano unapokuwa ni kati ya mwalimu na mwanafunzi ambaye ni under age, then hapo kuna tatizo. Hata kama mwanafunzi ni ana age of consent, power imbalance kwenye mahusiano hata ya elimu kati ya mwalimu na mwanafunzi makes the whole idea of "consent" very absurd.
 
Hivi katika hili anayetoa rushwa ni mwanamke au mwanaume? Mara zote?

Binafsi naona suala hili kwa sehemu kubwa linachangiwa na mfumo(dume). Ni kwa kiasi gani mwili wa mwanamke unachukuliwa na wanajamii (wakiwemo wanawake wenyewe) kama bidhaa? Hili ni moja...la pili ni suala la kimaadili(rushwa) katika jamii zetu. So 'rushwa ya ngono' ni zao la matatizo haya mawili katika jamii yetu.

Kwa hiyo, pengine sio mara zote tunaweza kumlaumu mwanamke au mwanaume...hili ni zao la jamii yetu.
 
Niiiiice.
Alafu namba tatu sio kina "i don't care". . . .ni wajasirimiili. Wao mawazoni hawaoni kwanini wakose kitu wakati uwezo wa kukipata upo ndani yao.

Uwezo huo unapewa kiburi na kuwapumbaza eti b'se wana k...a.then wanaifaja kama ndo mtaji au dhamana wa kupata watakacho hata kama hawana vigezo.
 
3.Mtu kama huyu akija kuwa mzazi atakuwaje?Ataweza kumfundisha mtoto wake kuwa tofauti na alivyo yeye?
Mimi hapa nitazungumzia hili la mwisho tu. Ni kitu cha ajabu lakini ndio ukweli kuwa wazazi matata na wenye tabia mbaya ndio wanaokuwa wakali kwa kutaka watoto wao wasiwe na tabia njema.
Fikiria baba kicheche, anayehonga na kurubuni visichana vidogo, huyu huwa kama mbogo kwa wanawe. Vivyo hivyo kwa mama mwenye jicho la nje, aliyewahi kutoa zawadi ya ngono hatotaka mtoto wake aangukie alikoangukia yeye.

Tatizo ni kuwa hatuishi katika kisiwa kisicho watu zaidi ya sisi, kwa hivyo matendo yote tunayoyafanya hutuandama sisi na vizazi vyetu maisha yetu yote; iwe ama kwa wale uliowatendea kutaka kulipiza kisasi au kwa Mungu kukurejeshea kibao kwa uliyowatendea wenzako.
 
Baada ya majadiliano na rafiki yangu kuhusiana na rushwa (zawadi) ya ngono mashuleni, vyuoni na maofisini nimejikuta najiuliza maswali mengi ambayo ningependa tusaidiane kuyajibu kwasababu kwa namna moja ama nyingine matokeo yake yanaathiri hata mahusiano, ndoa na malezi.

Kwanza ni wazi kabisa kwamba mtu akishaanza ni ngumu kuacha kutokana na ukweli kwamba anakua amejipa ulema wa aina fulani.Kwamba kama alifaulishwa sekondari kuna nafasi kubwa atahitaji kufaulishwa chuoni, na akifaulishwa chuoni kuna nafasi kubwa atahitaji kubebwa pale atakapokua kwenye mchakato wa kupata kazi na baadae kwenye kujiendeleza (kupandishwa cheo, kupata nafasi za masomo, kushirikishwa kwenye semina zinazolipa n.k).

Sasa je. . .
1. Mtu anapoanza kuhonga mwili wake ili afanyiwe kazi yake (kusoma, kuwa na CV kali, good work ethics, experience n.k) kwanini anafanya hivyo?Ni kutojiamini (mwenyewe siwezi) au ni kuzungukwa na watu wasio na imani nae (wazazi, ndugu na jamaa wasioisha kumwambia hatofika popote)???
2.Je kuna hatari gani mtu kutegemea mwili wake badala ya akili na uwezo unaohitajika kupata kazi,kufaulu n.k?
3.Mtu kama huyu akija kuwa mzazi atakuwaje?Ataweza kumfundisha mtoto wake kuwa tofauti na alivyo yeye?
4.Malezi yanachangia vipi kuwafanya ndugu zetu wawe hivyo?

Najua kwa kiasi kikubwa hata system yetu (kupeana kazi kwa kujuana bila kujali sana uwezo wa kazi ) inachangia kwa kiasi kikubwa, maana isingekua inaruhusu ingekua ngumu kutoa na kupokea rushwa ya aina hii ila napenda kuangalia kile kinachowasukuma wahusika zaidi.

LIZZY,
HONGERA KWA MADA NZURI SANA, KWANI HILI NI TATIZO KUBWA SANA KTK JAMII YETU. MIMI KITU NILICHOGUNDUA NI KWAMBA PAMOJA NA KWAMBA KUNA WANAUME WENYE TABIA CHAFU LKN KUNA WAKINA DADA AMBAO WAKIWA MASHULENI/VYUONI BADALA YA KUTUMIA MUDA WAO KUSOMA SERIOUSLY ILI WAWEZE KUFANIKIWA LKN WAO WANAKUWA NA STAREHE NYINGI SANA NA MWISHO WAKE WANASHINDWA KUFANIKIWA KTK UPANDE WA CAREER ZAO. NA INAPOFIKIA ANAKARIBIA MITIHANI NDIYO ANAKUMBUKA VINGI AMBAVYO HAKUVIFANYA NA HIVYO WAO WENYEWE WKT MWINGINE KUANDAA MAZINGIRA YA KUTOA NGONO ILI WAFANIKIWE. EBU CHUKULIA, MWANAFUNZI ANAKUPIGIA SIMU NA KUKUULIZA KAMA UPO OFISINI ANA SHIDA NAWE (MWALIMU), NDIPO ANAKUJA OFISINI HUKU AMEVAA KIMTEGO NA HUKU ANAHITAJI FAVOR. NA CHA AJABU, BINTI ANAFIKIA HATUA YA KUKUAMBIA YAANI MIMI NIKO TAYARI KWA LOLOTE ILI UNISAIDIE TU. WKT MWINGINE, HUYO MWL NAYE UZALENDO UNAMSHINDA. NA KUMBUKA KWAMBA - WENGI WA MABINTI WANAOPENDA STAREHE NI WAREMBO, NA HIVYO WAMEFIKIA HATUA YA KUFANYA MIILI YAO KAMA MITAJI YA KUFANIKIWA.

Lizzy, hali ni mbaya sana hata Ma-ofisini, hasa kwa masekretari ambao wengi wao wana kipato kidogo. Na hata kwenye hizi semina watu wanafanya sana ngono. Kwa kweli ni hali ya hatari sana.

Mimi naamini kwamba tatizo kuu ni Kutojiamini na Tamaa za baadhi ya madada zetu.
 
@ EMT. . .
Katika system iliyoonyooka hata mwenye mamlaka anaetaka kutumia mamlaka yake vibaya hawezi kufanikiwa kwasababu anajua fika kwa kufanya hivyo anaweza akaishia kupoteza hayo mamlaka yake kabisa. Hivyo siwezi hata kuimagine professor akiomba ngono au mwanafunzi akijitolea Norway.Kwasababu mmoja anajua haki yake na mwingine anajua mipaka yake.
Tofauti na sisi ambao kila mtu anajitengenezea sheria zake binafsi.
Kuhusu kutokuaminika, come on now.Kwenye dunia hii ya teknolojia hata nikitaka tu kuhakikisha kwamba kijana wa jirani alinitongoza naweza, sembuse ushahidi wa kwamba mkuu wa shule/kazi anataka tubadilishane favours?Labda kama mtu hajaamua tu ila sio kwamba haiwezekani.

@SMU. . . Hata wanaume nao wanatumika.Sema nadhani imezoeleka kwa wanawake zaidi.

@MAMMAMIA hivi ni rahisi kweli kumwambia mtu mwingine asiibe na kumaanisha wakati wewe mwenyewe umetoka kuiba muda sio mrefu?Ni ngumu kufundisha na kukazania maadili ambayo wewe mwenyewe huna.
 
LIZZY,
HONGERA KWA MADA NZURI SANA, KWANI HILI NI TATIZO KUBWA SANA KTK JAMII YETU. MIMI KITU NILICHOGUNDUA NI KWAMBA PAMOJA NA KWAMBA KUNA WANAUME WENYE TABIA CHAFU LKN KUNA WAKINA DADA AMBAO WAKIWA MASHULENI/VYUONI BADALA YA KUTUMIA MUDA WAO KUSOMA SERIOUSLY ILI WAWEZE KUFANIKIWA LKN WAO WANAKUWA NA STAREHE NYINGI SANA NA MWISHO WAKE WANASHINDWA KUFANIKIWA KTK UPANDE WA CAREER ZAO. NA INAPOFIKIA ANAKARIBIA MITIHANI NDIYO ANAKUMBUKA VINGI AMBAVYO HAKUVIFANYA NA HIVYO WAO WENYEWE WKT MWINGINE KUANDAA MAZINGIRA YA KUTOA NGONO ILI WAFANIKIWE. EBU CHUKULIA, MWANAFUNZI ANAKUPIGIA SIMU NA KUKUULIZA KAMA UPO OFISINI ANA SHIDA NAWE (MWALIMU), NDIPO ANAKUJA OFISINI HUKU AMEVAA KIMTEGO NA HUKU ANAHITAJI FAVOR. NA CHA AJABU, BINTI ANAFIKIA HATUA YA KUKUAMBIA YAANI MIMI NIKO TAYARI KWA LOLOTE ILI UNISAIDIE TU. WKT MWINGINE, HUYO MWL NAYE UZALENDO UNAMSHINDA. NA KUMBUKA KWAMBA - WENGI WA MABINTI WANAOPENDA STAREHE NI WAREMBO, NA HIVYO WAMEFIKIA HATUA YA KUFANYA MIILI YAO KAMA MITAJI YA KUFANIKIWA.

Lizzy, hali ni mbaya sana hata Ma-ofisini, hasa kwa masekretari ambao wengi wao wana kipato kidogo. Na hata kwenye hizi semina watu wanafanya sana ngono. Kwa kweli ni hali ya hatari sana.

Mimi naamini kwamba tatizo kuu ni Kutojiamini na Tamaa za baadhi ya madada zetu.

Hahahaha. . . Inabidi kuwe na uniform ili waalimu wasiwekwe mitegoni!!

Ila tuwe wakweli, unadhani huyo mwalimu asipokua tayari kupokea hiyo rushwa itakuaje?Maboss nao wangekua hawapokei ingekuaje? Wadada wanaotegemea miili yao kuwapeleka sehemu wangekosa wanachotaka hivyo kuwafanya waanze
kujituma.

Ahhh na hizo semina zinakamatisha wengi, ka extra cash kanafanya watu wajitoe bila kufikiria mara mbili.Umasikini nao unachangia kwakweli. . . . .
 
hawa tanesco nao
nimeandika wee wamekata umeme na hii sipiyu ya kichina nimepoteza vyote

dah, ngoja nianze tena

bado lawama nyingi nazielekeza kwa wanamme hasa katika sekta ya elimu ambapo wanawatumia watoto wa watu kama starehe zao.

lakini bado naamini malezi ya nyumbani yanachangia sana kumjenga binti kujitambua hata kama itamgharimu kiasi gani bado atauheshimu mwili wake . Mifano michache niliyoiona

o-level
mwalimu anatembea na wasichana afua anawapa mitihani hasa chemistry na physics
anahamia binti (G) ana kama miaka 15, lakini very bright.
Mwl anamsumbua for 14 months lakini binti anachomoa sababu alikuwa anaamini uwezo wake
mwl anahamishwa

chuo
mtihani wa mwisho wa mwaka
mwl anamfuata binti kidawa katikati ya mtihani na kuanza mtongoza
kidawa anagundua jina lake lina X kati ya watahiniwa wote
baada ya mtihani, kidawa anamfuata mzee wa heshima kama mzazi kuja kuongea na mwl
mwl anaona aibu na kuziua
anamwachia kidawa, maana alikuwa na kawaida ya kugawa sap

mabinti wawili wanaanza kazi
p anaajiriwa kufanya accounts receivables
q anaajiriwa kufanya accounts payables
accounts payables nafasi inafutwa
lakini p anaonekana mlokole sana
q anaonekana free spirit so anaweza kuliwa at any time
p anaundiwa zengwe na kuondolewa na accounts receivables anapewa q
 
@ EMT. . .

Kuhusu kutokuaminika, come on now.Kwenye dunia hii ya teknolojia hata nikitaka tu kuhakikisha kwamba kijana wa jirani alinitongoza naweza, sembuse ushahidi wa kwamba mkuu wa shule/kazi anataka tubadilishane favours?Labda kama mtu hajaamua tu ila sio kwamba haiwezekani.

Lizzy inategemea dunia ya teknolojia unayoizungumzia ni ipi. Kwenye shule zetu za msingi hata zile za sekondari kuna teknologia gani? Kama inakuwa ngumu ku-prove kuwa mwanamke amekuwa raped, unafikiri itakuwa rahisi ku-prove kuwa ametongozwa? Pia kumbuka hapa tuongelea wasichana wadogo kama wa primary na sekondari ambao hawana hata ujuzi wa kukusanya ushahidi.

Mimi nafikiri suala hapa wala sio teknologia. Imbalance relationship iliyoko kati ya mwalimu na mwanafunzi ndio inayommweka mwanafunzi katika mazingira magumu ya ku-prove. Kutongozwa na kijana wa jirani ni tofauti na kutongozwa na mwalimu wako. Kwa huyo kijana wa jirani ni rahisi kuamua lakini kwa mwalimu wako inaweza kuwa ngumu kwa wengine as it could go either way.
 
Lizzy inategemea dunia ya teknolojia unayoizungumzia ni ipi. Kwenye shule zetu za msingi hata zile za sekondari kuna teknologia gani? Kama inakuwa ngumu ku-prove kuwa mwanamke amekuwa raped, unafikiri itakuwa rahisi ku-prove kuwa ametongozwa? Pia kumbuka hapa tuongelea wasichana wadogo kama wa primary na sekondari ambao hawana hata ujuzi wa kukusanya ushahidi.

Mimi nafikiri suala hapa wala sio teknologia. Imbalance relationship iliyoko kati ya mwalimu na mwanafunzi ndio inayommweka mwanafunzi katika mazingira magumu ya ku-prove. Kutongozwa na kijana wa jirani ni tofauti na kutongozwa na mwalimu wako. Kwa huyo kijana wa jirani ni rahisi kuamua lakini kwa mwalimu wako inaweza kuwa ngumu kwa wengine as it could go either way.
EMT mbona ni rahisi hata kupata rafiki wa kuunga mkono hoja.Sema tatizo kubwa zaidi ni kutokua na uwajibishwaji. . . unaweza hata ukawa na ushahidi wa video nao ukayeyushwa tu.
 
mmezungumza mengi lakini kuna vitu viwili hatujataja

1.tamaduni za kiafrika..
fikiria mahari kwa mfano ni nini????
kwa nini waafrika mwanamke anatazamwa kama kifaa cha kununuliwa na kutumika?????
je tamaduni hizo hazichangii 'mawazo' ya 'kupata mwili wa mwanamke' kwa mbinu na hila kuwa ni jambo la kijanja na la maana???


2.ni utamaduni wa 'kurushana roho' wa wanawake hasa kitanzania.....
mtu atatembea na boss wake ili tu wenzie 'awarushe roho' wanawake wenzie ofisini hata kama
hakuna malipo ya kupandishwa cheo au nini.....
 
@ EMT. . .
@MAMMAMIA hivi ni rahisi kweli kumwambia mtu mwingine asiibe na kumaanisha wakati wewe mwenyewe umetoka kuiba muda sio mrefu?Ni ngumu kufundisha na kukazania maadili ambayo wewe mwenyewe huna.

Si rahisi hata kidogo Lizy, kwani hata unapojaribu kumkataza mwengine asifanye ulicho/unachofanya wewe nafsi inakusuta, wachilia mbali jamii ambayo imekuwa ikiona matendo yako. Mara nyengine hata huyo unayemkataza anaweza kukuambia, "you're none to teach me ethics"!
 
EMT mbona ni rahisi hata kupata rafiki wa kuunga mkono hoja.Sema tatizo kubwa zaidi ni kutokua na uwajibishwaji. . . unaweza hata ukawa na ushahidi wa video nao ukayeyushwa tu.

Wabongo tunavyoogopa kuwa mashahidi. Na huyo mtuhumiwa nae si ni rahisi kupata marafiki wa kuunga mkono utetezi wake? In fact hapo ndipo tatizo lipo. Walimu wenzake wata-side na mwalimu mwenzao.
 
mmezungumza mengi lakini kuna vitu viwili hatujataja

1.tamaduni za kiafrika..
fikiria mahari kwa mfano ni nini????
kwa nini waafrika mwanamke anatazamwa kama kifaa cha kununuliwa na kutumika?????
je tamaduni hizo hazichangii 'mawazo' ya 'kupata mwili wa mwanamke' kwa mbinu na hila kuwa ni jambo la kijanja na la maana???


2.ni utamaduni wa 'kurushana roho' wa wanawake hasa kitanzania.....
mtu atatembea na boss wake ili tu wenzie 'awarushe roho' wanawake wenzie ofisini hata kama
hakuna malipo ya kupandishwa cheo au nini.....
Boss hii ya pili wengine huwa wanatamba kabisa kuwa amepata kazi baada ya kutembea na fulani na wao wanaona fahari kabisa kuwatambia wanawake wenzao..
 
mmezungumza mengi lakini kuna vitu viwili hatujataja

1.tamaduni za kiafrika..
fikiria mahari kwa mfano ni nini???
kwa nini waafrika mwanamke anatazamwa kama kifaa cha kununuliwa na kutumika?????
je tamaduni hizo hazichangii 'mawazo' ya 'kupata mwili wa mwanamke' kwa mbinu na hila kuwa ni jambo la kijanja na la maana???


2.ni utamaduni wa 'kurushana roho' wa wanawake hasa kitanzania.....
mtu atatembea na boss wake ili tu wenzie 'awarushe roho' wanawake wenzie ofisini hata kama
hakuna malipo ya kupandishwa cheo au nini.....

1.Kwahiyo kwasababu tu tunajua kwamba wanaume wapo tayari kununua ngono wote tuanze kujiuza?Nauliza hivyo kwasababu haitofautiani na kutumia kigezo cha mahari kuhalalisha biashara ya ngono sehemu za kazi a.k.a KUTUMIKA kwa malengo.Alafu mahari sio kumnunua mwanamke, hiyo ni tafsiri iliyopotoka. Mahari ni kama zawadi, thamani ya mwanadamu ni zaidi ya ng'ombe kadhaa.

2.Huo ni ulimbukeni, ila hauwezi anza kabla ya kuwajua hao anaotaka kuwarusha roho.Kurushana roho kunaanza baada ya kufahamiana na kupeana sababu za kurusha roho.
 
Back
Top Bottom