Mwakajembe kama kuna mtu anahusisha uislam na ugaidi wala sio tatizo huo utakuwa ni mtazamo wake binafi.Kwa maneno haya pindi uisilamu unapohusishwa na ugaidi huwa mnakasirika nini?
Lakini kama na ww umo ktk hao basi mm nataka kukuambia uislam sio mtu sio taasisi wala taifa UISLAM NI QURAAN.
Kama wako waislam magaidi huo ni wakwao binafsi ingawa mm sijui maana ya ugaidi mpaka umri huu nilio nao.
Na kuhusu tangazo la SMZ la kukataza kula hadhari mwezi mtukufu wa ramadhani ni tangazo la SMZ sio tangazo la waislam wa znz.
Nafikiri kama waislam wa znz wengekuwa na uwezo wa kukataza mambo yanayoenda kinyume na uislam wasinge ishia kukataza kula mchana hadharani tu mwezi wa ramadhani wangeenda mbali zaidi na wangetumia fursa hiyo kukata kila aina ya uchafu unaomghadhibisha allah muumba ardhi na mbingu na vilivyomo.
Znz kuna mambo mengi yanayo fanyika yaliyo katazwa na allah tusifanye na naamini waislam wa znz wanatamani wapate fursa na yenyewe yakatazwe lakini hawana uwezo wa kufanya hivyo.
kwahiyo ww usipate taabu na waislam wala uislam hili ni katazo la SMZ serikali halalali iliyochaguliwa na wananchi ww lia na SMZ tu sisi waislam hatuna shida na mtu yeyote anae kula mchana anae lewa anae zini huo ni uwamuzi wake mm nipo Dsm umri wangu wote na nafunga miaka yote na napisha na watu wanakula wanalewa wanatembea uchi lakini sijawahi hata kukasirika.
Kila mtu atabeba msalaba wake huu nimsemo maarufu nadhani unaujua.