Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Zanzibar: Watakaokula mchana hadharani Ramadhani kukiona

Status
Not open for further replies.
Znz ikifika kipindi cha ramadhani, ukienda dukani kununua vyakula vya fast food hawakuuziiw(mfano soda, mikate, maji)...
Na hata ukishikwa na kiu, ukasema uende kuomba maji kwenye nyumba hawakupi.
Inshort wanabana mianya yote ya watu kula mchana, unakuta vyakula vinauzwa hotels za kitalii tu,
Na hata kama ni mkristo, wakikuona unakula njiani wanaweza kukufanyia vurugu,
Kwani kufunga hya tunalazimishana??, hawa jamaa VP???
 
Jamani walichokataza ni kula hadharani ,lakini ukiwa ndani ni ruksa,pale Maisara ukumbi wa CCM na ukumbi wa Magereza na hata hotel kubwa bado hutoa huduma za vyakula na hii sio kitu kipya kwa Zanzibar kipo tokea enzi za Karume tena siku hizi ni nafuu zaidi kuliko miaka ya nyuma,tutake au tusitake Zanzibar ni kama nchi ya Kiislamu ,90.9% ni waisalamu.
Kwani mkuu serikali ina dini?? Au toka lini serikali inadhibiti mambo ya dini??? Nchi zetu ni huru hizi haya mambo toka lini kulazimishana?? Kila mtu awe na uhuru wake maana hii ni ibada na kila mtu ataulizwa siku ya kiama hivyo tusiingilie uhuru wa dini za wengine
 
Wengi wape kwani kufunga ni compulsory kiasi serikali iweke mkazo?? Je toka serikali ina dini au zanzibar sio Tanzania tena maana katiba inasema serikali haina dini ila wananchi wake ndio wana dini..... toka lini ssa serikali idhibiti dini za watu!!
Hata bungeni mjadala huu ulikuwa mgumu sana na kwa hakika haukupatiwa majibu mpaka leo tunatumia dhana tu ili hili jambo lipite, lakini kama unafahamu nature ya Zanzibar ilivyo bado wengi wape itaendelea tu mkuu! Huwa sifahamu viongozi wa serikali wanapata wapi nguvu kutangaza hali hii!
 
Sasa kama kila dini kuheshimu dini nyingine, kwanini waislamu nao wasile kama wakristo ili kuheshimu ukristo, mbona wao wanakula hadharani wakati ya kwaresma? Huyu kiongozi atakua na vyeti feki.
Hao wakristo wenyewe hawaeleweki ndo kwanza wangonga kweupeee
 
Zanzibar iko miaka nenda rudi.Hukatazwi kula kama ni mkristu Bali tunaambiwa usile hadharani.

Kwanza wanaweka onyo kwenye kila ofisi za serikali,public areas.Jamani hiyo IPO Zanzibar, tena ukishuka na ndege au boti hujavaa kitambaa wana kuomba ujifunge kitambaa kichwani.

Ninachokiona ni mila tu wala siyo issue ya udini nakumbuka waislamu ni 95%
Ni kweli unayosema..Mimi nimewahi kuishi Zanzibar..huu ni utaratibu walio jiwekea kila Ramadhan..Tatizo liko hapa..Wana Focus kwa wasiyofunga badala ya wanaofunga..
 
Watu wangu wanapotea kwa kukosa maarifa. Wakristo Wa tz ni walalamishi mno, watu Wa fitna na figisufigusu isipokua wale waliosoma dini na wakailewa hua wanachambua mambo kwa angle nzuri ambayo inawapa muono chanya Wa upande Wa waislamu, kama utachukulia jambo lolote linalofanywa kwa manufaa ya waislamu ni udini hilo ni tatizo lako. Zanzibar asilimia 90 - 98 ni waislamu...na mwezi Wa Ramadhani hua asilimia kubwa wanafunga. Na waislamu wapo wengi tu wasiofunga ama kisheria au kwa kutofuata kikamilifu imani yao. Wasiofunga kisheria ni wajawazito, wanaonyonyesha, waliokatika siku zao, wasafiri, wazee, wagonjwa, na wasio waislamu. Ni kundi kubwa tu LA watu ambao wanayoruksa ya kutofunga mchana Wa mwezi Wa Ramadhani....licha ya wao kuwa na ruksa ya kutofunga au kupuuza wito wa Allah Wa kufunga mwezi huo ni karaha kwa wengine yeye kutoka nje na kula HADHARANI, sio ndani kama mnavyopotosha na wala sio marufuku kula kama mnavyopotisha ili mpato mlango Wa kuwasema vibaya waislamu....laa hasha imekatazwa kutoka nje na sahani yako ya wali kuku, embe lako umelitia pilipili, chipsi kuku zako au hivi na hivi vyote hivyo kaa navyo ndani kula kwa raha zako uwe muislamu au mkristo lakini si HADHARANI na kuwatia tashwish wengine. Uislamu ulikuwepo kitambo zanzibar na hayo si mapya, wakristo waelewa na wanaheshimu sana mfungo huo na tunajumuika nao kweny uji na futari zetu. Tusipende kujenga chuki pasina ulazima Wa kufanya hivyo.
 
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) imetoa onyo kwa wananchi watakaokula hadharani katika kipindi cha mchana wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Hayo yalisemwa na Naibu Waziri wa Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma, Khamis Juma Maalim wakati akijibu swali la mwakilishi wa jimbo la Paje, Jaku Hashim Ayoub aliyetaka kujua serikali inatoa tahadhari gani kwa watu watakaobainika kula mchana wakati wa Mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Alisema utamaduni wa wananchi wa Zanzibar ni kuheshimu kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa makundi yote ikiwemo wa dini tofauti. Alifahamisha kwamba utamaduni huo upo hata kabla ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964 wa dini tofauti kuheshimu dini za watu wengine.

Alisema kazi ya kutoa elimu kuhusu ujio wa mwezi mtukufu wa Ramadhani imeanza kutolewa na Ofisi ya mufti ambayo ndiyo yenye jukumu la kushughulikia masuala ya mambo ya dini ya Kiislamu.

Alisema kazi kama hiyo imeanza kutolewa na maimamu wakuu wa misikiti mbalimbali Unguja na Pemba ikiwemo katika sala za Ijumaa ambazo hukusanya idadi kubwa ya Waislamu kwa wakati mmoja.

Alikiri kuwepo vijana wengi wanaoacha kufunga katika kipindi cha mwezi mtukufu wa Ramadhani na kula hovyo pamoja na kuvuta sigara. Maalim alisema zipo taarifa kwamba hoteli nyingi hufanya kazi wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambapo wateja wake wakubwa ni vijana wa Kiislamu. Waislamu nchini wanatazamiwa kuanza mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani wiki ijayo ambapo ibada ya funga ni moja ya nguzo tano za dini ya Kiislamu


Chanzo: Habari Leo
=====================================
Nataka kujua kipindi kwa kwaresma mbona hawakutoa tamko hili.

Kwaio wakristo wawe wanajificha wakati wa chakula cha mchana.

Hapana naona kuna harufu ya udini kuanza Zanzibar.
Matendo ya kidini yanatakiwa yawe ya hiari ukiona sirikali inaingilia kulazimisha watu kutii mambo ya kiimani jua kuna tatizo, itakuwa serikali ina atatizo au dini INA mapungufu
 
Dini ikianza kutumia nguvu ili ifuatwe inakua sio dini tena.
Je watu huwa wanakula hadharani kama sehemu ya maisha yao ya kila siku?
Dini isiharibu maisha ya kawaida ya kila siku ya watu hata wstu wa dini yako huruhusiwi kuwalazimisha sembuse watu wa dini zingine.
Ukiona jambo linasemwa ni utamaduni halafu watu hawaujui na hawaridhiki huo si utamaduni ni sheria.
Sizipendi dini zikishaanza mambo kama haya mambo ya kijinga jinga basi yanaanza kuleta hata watu wasio na dini wadharau hizo dini
 
  • Pohamba usijitoe ufahamu, Ramadhan na mambo yake huo ni utamaduni wa Wazanzibari Waislamu
  • Wazanzibari Wakristo nao wanautamaduni wao ambao umefungamana na ukristo
  • Isitoshe mbona wao Wazanzibari Wakristo hawalazimishi Waislamu wafuate ya kwao?

Kwanini tunakataza Watu kufirana wakati Nchi yetu haina dini na Upagani wa Nchi yetu haukatazi Watu kufirana na wakifanya hivyo wenyewe Hakuna athari kwa asiefanya?

Numekueleza kwa Mifano ili uelewe, Mavazi Mafupi (Mini skirts) kwny Ofisi za Serikali kwanini inakatazwa wakati ni Uhuru wa Mtu binafsi?

Umewahi kujiuliza kwanini huku Tanzania Bara tuna mapumziko ya sikukuu za Kiislam na Kikristo pekee kwanini huwa hatusherehekei Sikukuu za wengine Kama sikukuu za Kitaifa mfano Wahindu, Wabudha, Singasinga kwani Hawa hawapo?


Kajifunze maana ya neno utamaduni Wewe unachanganya Kati ya utamaduni na Uhuru!
 
Matendo ya kidini yanatakiwa yawe ya hiari ukiona sirikali inaingilia kulazimisha watu kutii mambo ya kiimani jua kuna tatizo, itakuwa serikali ina atatizo au dini INA mapungufu
Nani kakuambia matendo ya dini ni hiari? Hata Katiba ya wanadamu tu si hiari

Hapa sheria, taratibu zake full stop, kama hutaki kaishi ulimwengu wa shetani.
 
Kwani waislamu wote mnafunga mwezi wa Ramadhani?
Yaaap.madhehebu yooooote.duniani.inafahamika labda uwe na dharura.sasa zanzibar wanashindwa kukataza kula hadharani kwenye kwaresma.kwa sababu si madhehebu yote ya wakristo wanaofunga.watawatesa madhehebu mengine.
 
Matendo ya kidini yanatakiwa yawe ya hiari ukiona sirikali inaingilia kulazimisha watu kutii mambo ya kiimani jua kuna tatizo, itakuwa serikali ina atatizo au dini INA mapungufu
Hivi hamjui kama Zanzibar wana katiba yao? Hhamjui kila nchi na utamaduni wao.....haya india India ukila ng'ombe hadharani utauwawa.
Kama hamtaki hameni
 
Znz ikifika kipindi cha ramadhani, ukienda dukani kununua vyakula vya fast food hawakuuziiw(mfano soda, mikate, maji)...
Na hata ukishikwa na kiu, ukasema uende kuomba maji kwenye nyumba hawakupi.
Inshort wanabana mianya yote ya watu kula mchana, unakuta vyakula vinauzwa hotels za kitalii tu,
Na hata kama ni mkristo, wakikuona unakula njiani wanaweza kukufanyia vurugu,
Kwani ukila chakula chako ndani nani atakusumbua
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom