Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,749
- 218,338
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba; Mwamba wa Siasa za Tanzania, ambaye anatajwa kuushikilia Mustakabhali wa Tanzania kwenye kiganja cha mkono wake wa kushoto, Freeman Mbowe, amehudhuria mkutano wa Faragha wa Wakuu wa Vyama vya Siasa unaofanyika Nchini Zanzibar.
Taarifa zinaonyesha kwamba lengo la Kikao hicho cha Siri ni kujadili sheria zitakazosimamia vyama vya siasa kuelekea uchaguzi wa 2024/2025.
Cha kushangaza ni kwamba Vyombo vyote vya Habari vya Kimataifa vinamtaja Mbowe pekee huku viongozi wengine waliohudhuriwa wakiachwa.
Usiondoke JF, kwa vile Nzi wangu ndani ya kikao hicho yuko tayari kuvujisha yatakayojili.