Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano Tarehe 26 Machi 2014

Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano Tarehe 26 Machi 2014

mpaka sasa naendelea kutafkari kwa nini Tundu lisu au Pro. Safari hawakugombea na wamemwacha huyu mnafiki. Kinachoendelea sasa hakitaki hata division 5 kujua kuwa bunge malum la katiba linaongozwa na ikulu.
hii nchi inaelekea kubaya.
ni vizuri Tundu lisu na Safari hawakugombea ili bunge lipate watu wa kupunguza kasi ya magamba
 
CCM wameanza mbinu chafu zitakazopelekea kuvurugika kwa mchakato wa katiba mpya.
 
Mzee Sitta asipokuwa makini atapoteza heshima yote aliyojijengea kwenye bunge la 9 na kufikia kukubaliwa na wengi nikiwemo kuwa anafaa sasa kuwa Rais,wiki moja hii ya Uenyekiti wake imenifanha nijifikirie upya kama huyu ndiye kweli Sitta niliyemdhania.Ana nafasi bado ya kurudi kwenye line otherwise ni heri asingechukua huu Uenyekiti kwani ni wazi sasa anajifutia yale ambayo yangebaki kuwa historia yake ya kutukuka.
 
kwa taarifa nilizo nazo ni kuwa kikao cha leo jioni kitakua ni moto wa kuotea mbali,ni kuhusu mwenyekiti kutengua kanuni walizotunga wajumbe wa bunge hili maalum.
 
Suluhisho ni wajumbe wasio wa CCM- wajumbe wenye nia kweli ya Katiba ya wananchi ni kususia bunge na kurudi nyumbani.

Weeeeee, waache 300,000/= per day? Nafikiri umesahau kuwa "mali ya mjinga huliwa na mwerevu". Viongozi wetu wamepoteza uzalendo na wananchi tumebaki kama kondoo wasio na mchungaji machungani!
 
Ndugu yangu mbona unauliza kama vile hujui!Haya unayoyaona yalipangwa.Kwa hali ilivyo hata angegombea Prof Safari au mpinzani yeyote asingepata kwa kuwa tayari CCM ni wengi na uteuzi wa wajumbe 201 wa rais umeendelea kuwaongeza. CCM haikuwahi kuwa na dhamira na jambo hili kwa hiyo litavurugwa kwa jinsi wanavyoweza.Hujafuatilia yaliyotokea kwenye kuchagua viongozi wa kamati 12?Fungukeni macho kwa kuwa kile wananchi mlichopendekeza kitatupwa kapuni na CCM walete kile wanachotaka cha kuwahakikishia umilele wa dola yao wanaozungumzia kila wakati.
Ccm sio wengi Bungeni tu. NI wengi nchini pia. 75% au zaidi ya wananchi NI ccm au wapenzi wa ccm.
 
Mzee Sitta asipokuwa makini atapoteza heshima yote aliyojijengea kwenye bunge la 9 na kufikia kukubaliwa na wengi nikiwemo kuwa anafaa sasa kuwa Rais,wiki moja hii ya Uenyekiti wake imenifanha nijifikirie upya kama huyu ndiye kweli Sitta niliyemdhania.Ana nafasi bado ya kurudi kwenye line otherwise ni heri asingechukua huu Uenyekiti kwani ni wazi sasa anajifutia yale ambayo yangebaki kuwa historia yake ya kutukuka.

apoteze Mara ngapi? Sasa hv Sitta ana stress nyingi kwa ajili ya mambo yanahoendelea Urambo Pia ujio Wa Wilaya lpya ya Kaliua.
Awapo hapo bungeni walio kinyume na chama chake au matakwa yake anaona Kama vile wametumwa na watu Wa Kaliua au Kapuya.
 
Watu wametumia muda , ghalama na nguvu katika kutengeneza hizo kanuni.
Sitta anataka kuzotengua kwsabau rahisi kabisa za kimaslahi.
 
bunge limeshakuwa mali ya ccm kama viongozi wote kwenye kamati ni ccm unategemea nn hapo cha muhimu ni kuacha ccm watengeneza katiba yao kiccm
 
apoteze Mara ngapi? Sasa hv Sitta ana stress nyingi kwa ajili ya mambo yanahoendelea Urambo Pia ujio Wa Wilaya lpya ya Kaliua.
Awapo hapo bungeni walio kinyume na chama chake au matakwa yake anaona Kama vile wametumwa na watu Wa Kaliua au Kapuya.
Masikini, kuna watu wanazeeka vibaya sana.
 
Utakuwa unaumwa sana sana.

Huo ndio ukweli na wewe sishangai ukiukwepa kwa hoja za mtaani.eti naumwa!usitafute nafasi za huruma Bungeni.Wananchi hawana imani na nyie.toshekeni na kura za kiharakati. 75% ya wananchi ni ccm na wapenzi wa ccm. Bunge lionyeshe sura hii ya taifa
 
Mimi nitakuwa mtu wa mwisho kumwelewa huyu rais kwa sababu zifuatazo.

1.analalamikia idadi ya watu waliotoa maoni kuwa ni ndogo wakati tume aliunda yeye na muda na bajeti katoa yeye.
kwa hapa maswali ni haya.

.Kwa nini hakutoa mwaka mzima kama wa tume ya jaji kisanga?
.Kwa nini hakuongeza bajeti ili ikibido hata chopa zitumike?
.Yeye alichaguliwa na watanzania mil ngapi kati ya watu mil45?

2.Analalamikia mfumo wa serikali tatu na si mbili maswali hapa ni haya.
.Sio yeye alitoa hadidu za rejea?
.Kama ni yeye kwa nini yote aliyotunga juzi hakutunga wakati huo na kuyafanya hadidu za rejea?
.Kama serikali tatu ni mbaya kama alivyotuambia na kwa jinsi zanzibar ilivyovunja katiba ya jamhuri haoni ni wakati sasa wa kuwa na serikali moja?
.Je haoni kama aliyokuwa akitoa juzi ni maoni yake ambapo atakuwa amevunja sheria kwa kutoa maoni wakati kisheria muda ulishaisha?

3.Kwa mujibu wa sheria walizojiwekea jaji warioba alitakiwa kuwakilisha rasimu ya pili mbele ya bunge la katiba lakini kwa kupindisha sheria aliwakilisha rasimu mbele ya semina ya wajumbe ambao wangekuja kuwa wabunge wa bunge maalu la katiba,maswali hapa ni haya.
.Mh rais haoni kavunja sheria kwa kutoa maoni na msimamo badala ya kutimiza matakwa ya sheria yaliyomtaka kulizindua bunge>
.Rais haoni kuwa spika kakiuka sheria kwa warioba kuwakilisha rasimu kwa kitu ambacho shria yenyewe haikitambui?
.Nikienda mahakamani na kumshitaki kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria uliofanywa na yeye atatumia hela za uma kulipa gharama za kesi au atatumia mshahara wake?
.Kwa nini hakuyatoa hayo maoni anayoona kwa busara zake ni mazuri katika tume ya warioba/au ni ushauri aliokuja kuupata mbele?
.Kwa ukiukwaji huu mkubwa wa shria uliofanya na rais ambaye tulitegemea kuwa ni mfano katika kusimamia sheria haoni ametufundisha sisi wa chini kuvunja sheria?

Mwisho namalizia kwa kumwambia atake serikali 1,2,3,4,5,6,7,8,9 ahakikishe TANGANYIKA inakuwepo.
 
mie nimeshalichoka hata kabla halijaanza maana kwanza linaahirishwa kila saa na pis limekaa kama kikao cha ccm , sitta ameshaliharibu na kwa mtu mwenye akili zake sijui anafanya nini pale NATAMANI LIVUNJIKE maana tayar ccm wameshamaliza
 
Back
Top Bottom