Mimi nitakuwa mtu wa mwisho kumwelewa huyu rais kwa sababu zifuatazo.
1.analalamikia idadi ya watu waliotoa maoni kuwa ni ndogo wakati tume aliunda yeye na muda na bajeti katoa yeye.
kwa hapa maswali ni haya.
.Kwa nini hakutoa mwaka mzima kama wa tume ya jaji kisanga?
.Kwa nini hakuongeza bajeti ili ikibido hata chopa zitumike?
.Yeye alichaguliwa na watanzania mil ngapi kati ya watu mil45?
2.Analalamikia mfumo wa serikali tatu na si mbili maswali hapa ni haya.
.Sio yeye alitoa hadidu za rejea?
.Kama ni yeye kwa nini yote aliyotunga juzi hakutunga wakati huo na kuyafanya hadidu za rejea?
.Kama serikali tatu ni mbaya kama alivyotuambia na kwa jinsi zanzibar ilivyovunja katiba ya jamhuri haoni ni wakati sasa wa kuwa na serikali moja?
.Je haoni kama aliyokuwa akitoa juzi ni maoni yake ambapo atakuwa amevunja sheria kwa kutoa maoni wakati kisheria muda ulishaisha?
3.Kwa mujibu wa sheria walizojiwekea jaji warioba alitakiwa kuwakilisha rasimu ya pili mbele ya bunge la katiba lakini kwa kupindisha sheria aliwakilisha rasimu mbele ya semina ya wajumbe ambao wangekuja kuwa wabunge wa bunge maalu la katiba,maswali hapa ni haya.
.Mh rais haoni kavunja sheria kwa kutoa maoni na msimamo badala ya kutimiza matakwa ya sheria yaliyomtaka kulizindua bunge>
.Rais haoni kuwa spika kakiuka sheria kwa warioba kuwakilisha rasimu kwa kitu ambacho shria yenyewe haikitambui?
.Nikienda mahakamani na kumshitaki kwa ukiukwaji mkubwa wa sheria uliofanywa na yeye atatumia hela za uma kulipa gharama za kesi au atatumia mshahara wake?
.Kwa nini hakuyatoa hayo maoni anayoona kwa busara zake ni mazuri katika tume ya warioba/au ni ushauri aliokuja kuupata mbele?
.Kwa ukiukwaji huu mkubwa wa shria uliofanya na rais ambaye tulitegemea kuwa ni mfano katika kusimamia sheria haoni ametufundisha sisi wa chini kuvunja sheria?
Mwisho namalizia kwa kumwambia atake serikali 1,2,3,4,5,6,7,8,9 ahakikishe TANGANYIKA inakuwepo.