Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano Tarehe 26 Machi 2014

Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumatano Tarehe 26 Machi 2014

Chabruma

JF-Expert Member
Joined
Sep 19, 2013
Posts
5,660
Reaction score
1,782
Wadau, ni matumaini yangu kuwa hamjambo na Mwenyezi Mungu amewaamsha mkiwa salama. Kwa wale wagonjwa tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu awajaalie wapone mapema. Kwa wale waliofikwa na mauti, tuwaombee kwa Mwenyezi Mungu ili wawe na makazi mema huko waendako.

Baada ya zoezi la kuchagua Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati za Bunge Maalum kukamilika ambapo majina yao yametangazwa jana asubuhi, kazi ya leo kwa mujibu wa ratiba iliyotangazwa juzi Jumatatu na Mwenyekiti, Sammuel Sitta ni kwamba leo asubuhi zile kanuni za 37 na 38 za Bunge Maalum ambazo ziliwekwa kiporo zitafanyiwa maamuzi. Vifungu hivi vinahusu namna ya kufanya maamuzi wakati wa vikao vya Bunge Maalum. Ni maamuzi gani yamefikiwa, sote tuwe sambamba kwenye mjadala huu.

Vilevile, ni kwamba siku ya leo, Wabunge watapata fursa ya kujadili hotuba za Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Sinde Warioba aliyoitoa Bungeni Dodoma Jumanne tarehe 18 Machi 2014 pamoja na ile ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete aliyoitoa Bungeni Dodoma Ijumaa tarehe 21 Machi 2014. Mjadala huu utategemea hali itakavyokuwa kwenye zoezi la kupitisha kanuni za 37 na 38. Kwamba, ikiwa hakutakuwa na mivutano mikubwa wakati wa kupitisha kanuni hizo, ni wazi kuwa wabunge watapata muda wa kutosha kujadili hotuba hizo. Ama ikiwa mivutano iliyozoeleka itajitokeza, ni wazi kwamba wabunge watajinyima fursa hiyo kwani muda uliotengwa wa kujadili hotuba hizo ni leo tu.

Kama kawaida, ni matumaini yangu kuwa wadau mbalimbali watashiriki kwenye mjadala huu .

Stay Connected.

------------------------------

- Mwenyekiti anasema kuwa kwa mujibu wa taarifa aliyotoa woki iliyopita, alisema kuwa kwa siku ya leo wangeweza kujadili hotuba ya JK na ya Warioba. Hata hivyo amesema kuwa hiyo ingekuwa ni sawa na kutanguliza mjadala. Pia inapingana na kanuni za bunge hilo ambazo zinasema kuwa bunge litajadili vifungu viwili vya kanuni. Kwa vile wabunge wasingeweza kuzuiliwa ya kuongea, sasa ametangaza kusitisha mjadala huo.

- Bunge limeahirishwa mpaka leo saa kumi jioni.

-------------------------------

BUNGE JIONI YA LEO


- Bunge linaendelea tena muda huu. Mwenyekiti ametoamnafasi kwa wenye miongozo. Lissu amesimama na anazungumza. Anasema kuwa kanuni zimekuwa zikivunjwa na Mwenyekiti amekuwa akiyumba sana katika kusimamia kanuni hizo

- Lissu anasema kuwa wameletewa jedwali la marekebisho ya kanuni ya bunge maalum. Kwamba marekebisho kuhusu kanuni za 14, 32,33,35,37,38,58,61(1),64(1), 85(4). Anasema kuwa mabadiliko haya yanaletwa na Katibu wa Kamati ya Uongozi. Alisema kuwa hiyo si sahihi kwa vile kanuni inaeleza bayana. Anasema kuwa kanuni hazina hata wiki tatu na bado zinaanza kuchakachuliwa. Anasema kuwa viporo vya 37 na 38 ndivyo vinavyotakiwa viwasilishwe. Alisema kuwa hayo marekebisho hayatakiwi kuwasilishwa. Pia anasema kuwa kamati ya uongozi haina mamlaka ya kuleta mabadiliko ya kanuni. Anasema kuwa hii takataka, uchafu nk hataki iingizwe kwenye bunge hili. Mwenyekiti anasema kuwa tuhuma za Tundu Lissu ni nzito na amezitoa bila yamkuwa na karatasi ya marekebisho hayo. Anasema kuwa Kamati ya Uongozi imefanya kazi ya kuandaa kazi za kila siku. Anasema kuwa kamati ya kanuni ndiyo inapaswa kuwasilisha marekebisho ya kanuni. Anasema kuwa tusubiri hicho kinachopaswa kuwasilishwa na kikionekana ndipo bunge litaamua.

- Abubakar Hamisi Bakar anasema kuwa utaratibu wa kubadilisha kanuni upo kwenye kanuni ya 87. Anasema kuwa mtu anayetaka kurekebisha kanuni afuate taratibu. Anasema kuwa chochote kitakachofanyika kinyume cha sheria hakitakubalika

- Jaji Werema amesimama na kusema. Jambo analoliona ni kwamba, wabunge wanawahisha hoja. Kwamba kanuni ya 87 inasomeka hivi;

  1. Bunge maalum linaweza kuzifanyia mabadiliko au marekebisho kanuni hizi kwa azimio litakalowasilishwa kwenye bunge maalum na mwenyekiti wa kamati ya kanuni na hadhi za bunge. Hii ni kanuninya 87 (1). Anasema kuwa mchakato uliofanyika wa kupitisha kanuni haizuii kufanyia marekebisho
  2. kanuni ya 87 (2) ndiyo inayosema kuwa mjumbe yeyote anaweza kuwasilisha marekebisho ya katiba kama Tundu Lissu anavyosema. Hivyo Lissu amechanganya


- Ismail Jusa naye amesimama kumuunga mkono Tundu Lissu

- Mwenyekiti ameagiza Kamati ya Kanuni kushughulikia jambo hilo na walifanyie kazi baada ya kikao cha leo. Amesema kuwa kamati hiyo itawasilisha kesho saa 10 jioni. Kwa hali hiyo, bunge linaahirishwa mpaka kesho saa 10 jioni. Sasa mwenyekiti anasoma dua ya kuliahirisha bunge.


Ahsanteni kwa kuwa pamoja nasi. Tukutane kesho saa kumi jioni
 
Asante sana mkuu Chabruma, shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu kwa yote aliyojalia.

Nitakuwepo na nitafuatilia kwa ukaribu updates zitakazowekwa hapa nami nitachangia kwa pale nitakapoweza.

Kwa niaba ya wote watakaoshiriki, nasema karibuni sana.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, hiyo ni tafsiri yako. Ila hiyo Avatar kama unaiangalia vizuri ni moja ya majengo ambayo yamekuwa kivutio kwa watalii wengi katika moja ya nchi za ulaya
OK umetetea vizuri, lakini mmmmm! Wazungu wanafurahia sana kuonyesha utupu kwa sababu ati ni moja ya burudani kwao na ni kichocheo kwa watu wao kuunganika kwa jinsia zao tofauti. Ukienda Scandinavia nchi yoyote, hata matangazo ya kibiashara wanayahusisha sana na utupu wa kiume au kike na tendo la viungo hivyo kwani vijana wengi ndo wanataka, tena matangazo hayo zaidi ya kuhamasisha biashara yanawafanya watu wacheke kuongeza uhai na pia yanawahamasisha kuzaliana, kwani wanawake zao ni wagumu kukubali kuzaa ati wanazeeka haraka. Ndo maana kila mwanamke akizaa ni kama kitegauchumi, anaongezewa misaada kwa ajili ya mkila mtoto, mfano matumizi ya winter, matumizi ya summer, nk. Nikupe mfano: mtu wakati wa winter anataka kukojoa, mikono haiwezi kufungua zipu ingawa ametoa gloves za mkononi za winter, jamaa anahangaika sana akikata kiuno kulazimisha zipu ifunguke..... zipu inafunguka na halafu mtangazaji anasema ..."NOKIA, CONNECTING PEOPLE!" Ndo wazungu hao mkuu, wana akili nyingi na huwafungi kwa tangazo lao lenye hisia mbili tofauti.
 
Asante sana mkuu Chabruma, shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu kwa yote aliyojalia.

Nitakuwepo na nitafuatilia kwa ukaribu updates zitakazowekwa hapa nami nitachangia kwa pale nitakapoweza.

Kwa niaba ya wote watakaoshiriki, nasema karibuni sana.

asante mkuu Kamanda Skype.bunge litaanza sa ngapi
 
Last edited by a moderator:
Mbona tulisoma hapa jf jana ya kuwa Bunge Maalum la katiba limefungwa rasmi na IKULU ya Kikwete, leo tunaona linaendelea. Mambo haya ni vipi au ile taarifa ilikuwa JOKES.
 
"Leo mambo ni magumu sana kwa sababu kuna baadhi ya mambo hatutakubaliana", amesema Mtikila nje ya ukumbi akihojiwa na Joyce Mwakalinga.
 
Mwenyekiti ameingia ila kulikuwa na hitilafu ya vipaza sauti. Mwenyekiti anasoma dua sasa
 
Bunge limeanza na Sitta anasoma kitabu cha dua ya kuliombea bunge sasa
 
"Leo mambo ni magumu sana kwa sababu kuna baadhi ya mambo hatutakubaliana", amesema Mtikila nje ya ukumbi akihojiwa na Joyce Mwakalinga.
Hakika mkuu. Ndo maana wengine wanasema leo bunge litawaka moto
 
Sasa ni kiapo cha wajumbe kinaendelea, nadhani kuna baadhi ya wajumbe walikua hawajaapishwa.
 
Kiapo kwa wajumbe. Kiapo kinaendelea. Bado kuna hitilafu ya kipaza sauti wadau. Hii mara ya pili inatokea kwa siku ya leo
 
Kwa ufupi ni kwamba, baada ya wajumbe kuapishwa, kikao cha bunge kitaendelea kama kawaida.
 
Sasa ni kiapo cha wajumbe kinaendelea, nadhani kuna baadhi ya wajumbe walikua hawajaapishwa.
Hakika mkuu. Huyu Devota wakati wenzake wanaapa alikuwa kwao Songea ambako alienda kutokana na kufiwa na baba yake mzazi
 
Suluhisho ni wajumbe wasio wa CCM- wajumbe wenye nia kweli ya Katiba ya wananchi ni kususia bunge na kurudi nyumbani.
 
Back
Top Bottom