Suala la mgogoro wa Kikati kuhusu kupitisha Bajeti litakuwa baya zaidi endapo tu Katiba inayopendekezwa itapitishwa katika kura ya maoni.Katiba Inayopendekezwa iliyoandikwa na Chenge,Ibara ya 132(6),Rais anapewa madaraka ya kulivunja Bunge kama bajeti au muswada hautapitishwa na Bunge.Dawa ya tatizo hili ilipatikana kupitia Tume ya Warioba Ibara ya 122(6) lakini Sita na washirika wake akina Chenge wameliondoa pendekezo hilo.Mgogoro huu wa Kikatiba ni mwanzo tu,tutaona mengi zaidi.....Kama Bunge lingekuwa na meno mikataba mibovu ingeletwa mezani kujadiliwa na waliotenda uharamia huo wangewajibika haraka kisheria.Kwa nini kila wakati awe Chenge tu?Kuna nini hapo?