Kama Mosses Linjenje ni marehemu - ifahamike kwa wote kuwa - "Unyama huu haukubaliki."
Ndiyo hivyo tena, kwani akina Ben Saanane na wengine "unyama" ulikubalika?

Ni hivi: Panapokuwepo na kiongozi wa nchi legelege kama Tanzania, kuwa ni "Shetani", mfumo mzima wa uongozi huo unaruhusu vishetani vyote vilivyomo ndani ya nchi hiyo kujitokeza waziwazi ili kutumika katika mfumo huo wa kishetani.

Hawa waTanzania wenzetu ambao 'ushetani' wao haukuwahi kuonekana siku za nyuma wakati ambapo hatukuwa na kiongozi mkuu akiwa shetani, wakati huu walikuwa wamepata ruhusa ya kuuonyesha ushetani wao.
 
wee hushangai nchi nzima magaidi watatu tu. upelelezi woote tangu mwaka jana watatu tu tena kwa ufadhili wa laki sita.
Huoni kuwa kimantiki ni maelekezo ya mtu mkubwa? tena lengo kuu likiwa kuangamiza upinzani kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa 2019. Huu ulikuwa mpango mkakakati na hii ni aibu tupu
Kawaida wanatakiwa wawe magaidi wangapi?
 
Nimeanza kuona mbele kuna kitu kitakuja kutokea haiwezekani mpuuzi mmoja kama kingai na genge lake wajifanye wanajua ,tutanyooshana tu hata kama watakuwa wakongwe hata watoto wao watalipa maana tumeona Mahita naye amerithisha kizazi kama chake
 
Hivi hii kesi ikiisha na watuhumiwa wakaachiwa kwamba hawakuwa na kosa je hao polisi waliowatesa wanaweza kuchukuliwa hatua ?

Hapa ndo kuna changamoto, ni wazi Mbowe hana kosa ila serikali inaogopa kuumbuka hivyo wataonewa tu, ili serikali isipate fedheha, Mungu tenda miujiza haki isimame.
 
Kwa hiyo Kingayi na wenzake wamemwua komandoo Linjenje!! Huenda Linjenje alikataa kukamatwa kama kuku, wakaamua wammalize! Mungu wa rehema, tunaomba, uipokee roho ya Linjenje, apumzike kwa amani, na wauaji wake walaanike Duniani na mbinguni.

Sasa naelewa kwa nini Hamza alifikia hatua ile. Hivi hili kweli ni Jeshi la Polisi au genge la wauaji na watesaji?

Siro, pamoja na kutokuendelea kufikia ngazi ya upadre, yale mafundisho ya dini, ukiwa mseminari, hayakuweza kukusaidia angalao kuwa tu muumini wa kawaida anayejitahidi kufuata maelekezo na mafundisho ya Mungu?

Hakika hawa wanastahili kufungwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa majini.

Alaanike sana kingayi kwa mauaji anayoyafanya. Haya ni machache tuliyobahatika kuyajua, lakini huenda kuna rundo la watu aliowaua.

Tunakoelekea ata ya kina Ben saanane yatajulikana, Jeshi la polisi ni dhaifu sana,
 
Dah nimesoma hadi nakaribia kutoka machozi.
Yaani askar polisi anamtesa komandoo kwa sababu za kisiasa!!!

Ila hii mbegu aliyoipanda mwendazake isiporekebishwa kuna siku tutashuhudia mauaji kati ya hawa walinzi wetu.

Kwa mfano wajeda wakiambiana tusikubali udhaliliashaji na unyanyasaji waliofanyiwa wenzetu nyie polisi mutalala majumbani mwenu?

Kumbukeni hakuna maelewano mazuri kati yenu polisi na wanajeshi halafu mnaongeza majanga dah!

"Once a soldier is a soldier"
 
Dah nimesoma hadi nakaribia kutoka machozi.
Yaani askar polisi anamtesa komandoo kwa sababu za kisiasa!!!

Ila hii mbegu aliyoipanda mwendazake isiporekebishwa kuna siku tutashuhudia mauaji kati ya hawa walinzi wetu.

Kwa mfano wajeda wakiambiana tusikubali udhaliliashaji na unyanyasaji waliofanyiwa wenzetu nyie polisi mutalala majumbani mwenu?

Kumbukeni hakuna maelewano mazuri kati yenu polisi na wanajeshi halafu mnaongeza majanga dah!

"Once a soldier is a soldier"
What goes around comes around.Hao polisi hawawezi kufanya watachofanya hao wajeshi? Acha kuvichonganisha vyombo vyetu vya dola.
 
Wakala wa shetani!Kuna aliyeita kule CCM Kuna magroup mengi na Kuna kazi za kufanya nenda huku

Msabato uone hata aibu ulicho kiandika Kati ya Mbowe na serikali nani anatapatapa ???Aibuuu halafu unajiita mkristo tena SDA .Umeandika iliupewe 7000/- nakuomba hiyo 7000/- usije ukaileta Kanisani Jumamosi kama sadaka
Kwasababu itakuwa haramu, siyo?
 
Dah nimesoma hadi nakaribia kutoka machozi.
Yaani askar polisi anamtesa komandoo kwa sababu za kisiasa!!!

Ila hii mbegu aliyoipanda mwendazake isiporekebishwa kuna siku tutashuhudia mauaji kati ya hawa walinzi wetu.

Kwa mfano wajeda wakiambiana tusikubali udhaliliashaji na unyanyasaji waliofanyiwa wenzetu nyie polisi mutalala majumbani mwenu?

Kumbukeni hakuna maelewano mazuri kati yenu polisi na wanajeshi halafu mnaongeza majanga dah!

"Once a soldier is a soldier"
Point of correction, "once a soldier always a soldier".
 
Leo tena upande wa utetezi katika kesi ya Mbowe wanaendelea kutoa ushahidi wao katika kesi ndogo ya kesi kubwa ambapo leo tarehe 28/09/2021 Mtuhumiwa Lig'wenya anaendelea na ushahidi wake.

=======



Jaji: ameshaingia Sasa

Kesi namba 16 Inatajwa

Kesi namba 16 ya Mwaka 2021,Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire,Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe

Watuhumiwa wanapandishwa Kuzimbani

Jaji: wakili wa Serikali

Robert Kidando
Abdallah Chavula
Nasoro Katuga
Easter Martin
Tulimanywa Majigo
Jenitreza Kitali

Wakili Peter Kibatala nayeye anatambulisha Orodha yake
Gaston Garubindi
Idd Msawanga
Bonifasia Mapunda
Evaresta Kisanga
Hadija Aron
Michael Mwangasa
Dickson Matata
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Nashon Nkungu

Jaji: Wote Mpo tayari kuanza?

Pande zote Mbili wamesema wapo tayari

Jaji: niombe apande Shahidi wapili ambaye alikuwa bado ajamaliza Kutoa Ushahidi wake

Shahidi: anapanda Kizimbani

Kimyaaaaa Kidogo

Jaji:
wakili Nashon Nkungu

Nashon: ni kweli Kule Rau Madukani....

Jaji: aina hiyo ya Mswali Ndiyo inaletaga Utata

Nashoni: Ulipoluwa Madukani Ulikuwa unamuona Mshitakiwa wapili, Kweli si Kweli

Shahidi: Ni kweli
Nashon: Wakati tukio linatendeka ulikwepo.?

Shahidi: nilikwepo

Nashon: wakati tukio linatendeka Palikuwa na watu wengi wanashihudia.?

Shahidi: ndiyo palikuwa na watu wengi wanashuhudia

Nashon: Je hapa Mahakamani ulishawahibKuona Mtu yoyote aliyekuwa anashuhudia tukio

Shahidi: Hapana sijaona yoyote

Nashon: ulipokuwa Central Police Moshi, Je ulishuhudia taratibu za Kipolisi zilifanyika kama Kukuandikisha

Shahidi: Hapana Sijaiona

Nashon: Ulishawahi Kuona Detention Register Ya Mosho hapa Mahakamani.?

Shahidi: Hapana

Nashon: Kuna Shahidi alikuja anaitwa Detective Msemwa alisema aliwapokea Central Police Dar je Unamfahamu

Shahidi: Simfahamu

Nashon: Unasemaje kuhusu Maneno yake kuwa aliwapokea Central Police Dar,.Je unamfahamu.?

Shahidi: Simfahamu wala sijawahi Kufika Central Dar

Nashon: Unasemaje kuhusu Detention Register aliyokuja nayo hapa Mahakamani

Shahidi: sifahamu alitoa wapi

Nashon: Kuna sehemu yoyote katika Ile Detention Register ambayo amekuinyesha Ulisaini wakati wanakupokea

Shahidi: sikuona

Nashon: Wakati Dective Msemwa anatoa Ushahidi Anasema alikuwa na Afande Fatuma kama CRO incharge,Je ulishwa kumuina FATUMA hapa Mahakamani.?

Shahidi: Hapana

Nashon: ni Kweli Kwamba Wakati Mkiwa mnaelekea Mbweni walikwambia watakupoteza.?

Shahidi: Afande Goodluck aliniambia Tutakupoteza Kama Moses Lijenje

Jaji: alisema wakati gani

Shahidi: Wakati tunayoka Tazara kwenda Mbweni,Tukiwa kwenye Gari

Nashon: ulielewa nini Kwa Maneno tutakutupa..?

Shahidi: nilijua kuwa watanipoteza,Wataniua alafu hakuna atakaye jua nipo wapi

Nashon: nitakuwa sahihi Nikisema walikupa DEATH THREAT

Shahidi: ni sahihi kwa sababu niliona Moses tulikuwa naye Kweli Rau Madukani alafu ajulikani alipo na wala hatupo naye,nikajua wamemuua na watanifanyia kama yeye nilijisikia Vibaya

Jaji: je Wakili wa Mshitakiwa watatu Fredrick Kihwelo

Jaji: je Mawakili wa serikali Mnaona ni sawa

Fredrick Kihwelo: Sitokuwa na Swali Mheshimiwa Jaji

Jaji: je ni sahihi kwa yeye kuuliza swali kabla hatujafika kama atauliza au lah

Fredrick Kihwelo: nimeamua Kujinyima Haki Mheshimiwa

Jaj: sawa Wakili wa Mshitakiwa wa Nne

Kibatala: Kitendo cha Kugongwa gongwa na Bastola na kukwambia watakutupa,Je tishio liliongezeka Moyoni Mwako kutokana na yalivyo kuwa yameshatokea kabla..?

Shahidi: Hofu ilizidi kuwa Kubwa Kufuatia Kilichokuwa Kimeshatendeka Moshi

Kibatala: Moses Lijenje unamfahamu wakati unaambiwa hayo maneno

Shahidi: Ndiyo nilikuwa namfahamu tulikuwa naye pale Rau Madukani

Kibatala: haiba yake ni nani

Shahidi: alikuwa Mwanajeshi Wa 92 KJ lakini wakati yeye akiwa Mwanajeshi pale mimi nilikuwa bado sijaanza kazi

Kibatala Wakati kesi inaendelea hapa Uliwahi Kusikia kuwa nayeye ni Mshitakiwa.?

Shahidi: Hapana

Kibatala: Ulishawahi Kusikia kuwa watamleta baadae

Shahidi: Hapana

Kibatala: Pale Rau Moshi Mkiwa Pale,hawa wakati wanamkamata Adamoo ulisikia Askari yoyote anasema ana HATI YA UKAMATAJI

Shahidi: Hapana

Kibatala: Wakati unaingilia Ukamataji wa Adamoo,Uliskia Askari Polisi yoyote hasa Kingai Kuwa Tafadahali Usiingilie zoezi la Ukamataji , Kwa sababu za Kisheria.?

Shahidi: Hapana sijasikia

Kibatala: Uliwahi Kumsikia hapa Mahakamani Kingai ametoa Warrant of Arrest (Hati ya Ukamataji)

Shahidi: Hapana

Kibatala: Wakati wa Ushahidi Mahita alisema Kingai ndiyo alikuwa akiongozi wao

Shahidi: Ndiyo nilimsikia

Kibatala: Kingai tangu wanatoka Arusha walisema walikuwa wanafahamu wanaenda Kumkamata Adamoo kwa Tuhuma za Ugaidi

Shahidi: Ndiyo nilisikia hivyo

Kibatala: lakini alipokuja hapa alishawahi Kutoa Ruhusa ya Mahakama kwamba wanaenda Kumfanyia Adamoo kitu fulani.?

Shahidi: Hapana Sikusikia

Kibatala: Adamoo alitekwa au Alikamatwa

Shahidi: alitekwa

Kibatala: Kwanini ulikumbuoa mambo ya Rau Madukani Mpaka Maduka ya Mtu na Mpaka Majina ya ya Mwenye Duka

Shahidi: Mimi ndiye niliyemshauri Adamoo twende pale kwa Sababu nilikuwa na Dada yangu na pale ni sehemu ya familia

Kibatala: Umeweza Kufafanua Mpala kutuchorea picha Kwasababu ni Mambo uliyowahi kuyaishi

Wakili wa Serikali: OBJECTION Shahidi ajasema kuwa amewahi Kuishi Rau Madukani

Kibatala: sijasema ameishi Rau Madukani, Nimesema ameeleza Kwa sababu Maelezo yake ameyaishi

Jaji: wakili wa Serikali

Wakili wa Serikali: hilo neno kuyaishi Mbeleni linawezakutumika Vibaya

Jaji: Kibatala

Kibatala: Wacha nibadirishe swali kwa Sababu ya Muda

Kibatala: Wakati Kingai anasema aliwakuta Kwenye kibanda Umiza alitaja Jina.?

Shahidi: Hakutaja Jina

Kibatala: tofauti na Kingai,Wewe umetaja Mpaka Jina

Shahidi: nimetaja Mpaka Jina

Wakili Kibatala: nilisikiabkuwa wakati Unakamatwa ulitoa Vitu Vyako ukaweka Kwenye Kibaraza cha huyo Dada,Nilisikia Vizuri.?

Shahidi: upo sahihi

Kibatala: Je ungejisikia Vizuri kama yule Dada angekwepo wakati wa Ukamataji wako kwa Sababu alikwepo Dukani

Shahidi: Ndiyo ningepata Amani zaidi kama angekuwa Shaidi

Jaji: jana Ulisema Adamoo amekamatiwa wapia

Shahidi: Kati kati ya Glocery na Flemu za Madukani

Jaji: unaweza sasa Kuendelea Kumjibu wakili

Shahidi: Ndiyo ningejisikia Vizuri kama Dada yangu angekwepo

Jaji: unamaanisha Athma

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Wakati wanamshambulia Adamoo hao Askari walikuwa na Silaha

Shahidi: hawakuwa na Silaha,labda wa Nje Kwa sababu katika Ukamataji kwa ufahamu wangu kuna "Inn and Outer" labda walifunga Nje ndiyo walikuwa wamezunguka eneo lile au waliokuja baadae

Kibatala: kwanini unasema Adamoo hakuwa na Bastola wakati wa Ukamataji kwa uhakika

Shahidi: kwa sababu Adamoo nimesafiri naye,Nimelala naye Chumba Kimoja na Tukatoka kuja wote kwa Dada yangu. na Koti ndiyo alikuwa ametoka Kulinunua

Kibatala: Kwa Ufahamu wako ile Bastola imetoka kwa nani.?

Shahidi: kwa Jumanne,Ndiye aliyesema ana bastola na watu walikuwa wamejaa Sana

Kibatala: kwa Ulivyoshuhudia Ule siyo Ukamataji ni Ugomvi

Shahidi: siyo Ukamataji ni Ugomvi

Kibatala: Shahidi umesema Jumanne alimuweka Adamoo Madawa,ulijuaje kuwa yale ni Madawa

Shahidi: kwa sababuJumanne ndiye aliye tamka kama alivyo tanka anapistol ndiyo alitamka Ana madawa

Kibatala: kwanini unaamini Adamoo hakuwa na Madawa ya Kulevya

Shahidi: Mimi ndiye niliyemshauri Adamoo twende pale kwa Sababu nilikuwa na Dada yangu na pale ni sehemu ya familia

Kibatala: Umeweza Kufafanua Mpala kutuchorea picha Kwasababu ni Mambo uliyowahi kuyaishi

Wakili wa Serikali: OBJECTION Shahidi ajasema kuwa amewahi Kuishi Rau Madukani

Kibatala: sijasema ameishi Rau Madukani, Nimesema ameeleza Kwa sababu Maelezo yake ameyaishi

Jaji: wakili wa Serikali

Wakili wa Serikali: hilo neno kuyaishi Mbeleni linawezakutumika Vibaya

Jaji: Kibatala

Wacha nibadirishe swali kwa Sababu ya Muda

Kibatala: Wakati Kingai anasema aliwakuta Kwenye kibanda Umiza alitaja Jina.?

Shahidi: Hakutaja Jina

Kibatala: tofauti na Kingai,Wewe umetaja Mpaka Jina

Shahidi: nimetaja Mpaka Jina

Wakili Kibatala :nilisikiabkuwa wakati Unakamatwa ulitoa Vitu Vyako ukaweka Kwenye Kibaraza cha huyo Dada,Nilisikia Vizuri.?

Shahidi: upo sahihi

Kibatala: Je ungejisikia Vizuri kama yule Dada angekwepo wakati wa Ukamataji wako kwa Sababu alikwepo Dukani

Shahidi: Ndiyo ningepata Amani zaidi kama angekuwa Shaidi

Jaji: jana Ulisema Adamoo amekamatiwa wapia

Shahidi: Kati kati ya Glocery na Flemu za Madukani

Jaji: unaweza sasa Kuendelea Kumjibu wakili

Shahidi: Ndiyo ningejisikia Vizuri kama Dada yangu angekwepo

Jaji: unamaanisha Athma

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: Wakati wanamshambulia Adamoo hao Askari walikuwa na Silaha

Shahidi: hawakuwa na Silaha, labda wa Nje Kwa sababu katika Ukamataji kwa ufahamu wangu kuna "Inn and Outer" labda walifunga Nje ndiyo walikuwa wamezunguka eneo lile au waliokuja baadae

Kibatala: kwanini unasema Adamoo hakuwa na Bastola wakati wa Ukamataji kwa uhakika

Shahidi: kwa sababu Adamoo nimesafiri naye,Nimelala naye Chumba Kimoja na Tukatoka kuja wote kwa Dada yangu. na Koti ndiyo alikuwa ametoka Kulinunua

Kibatala: Kwa Ufahamu wako ile Bastola imetoka kwa nani.?

Shahidi: kwa Jumanne,Ndiye aliyesema ana bastola na watu walikuwa wamejaa Sana

Kibatala: kwa Ulivyoshuhudia Ule siyo Ukamataji ni Ugomvi

Shahidi: siyo Ukamataji ni Ugomvi

kibatala: Shahidi umsema Jumanne alimuweka Adamoo Madawa,ulijuaje kuwa yale ni Madawa

Shahidi: kwa sababuJumanne ndiye aliye tamka kama alivyo tanka anapistol ndiyo alitamka Anamadawa

Kibatala: kwanininunaamini Adamoo hakuwa na Madawa ya Kulevya

Shahidi: kwa sababu Adamoo nilikuwa naye kwa kila hatua na alikuwa Mgeni kule Moshi, Ndiyo maana nilimpeleka kwenda Kumtembelea Dada Yangu

Kibatala: Unasemaje Madai ya Mahita kuwa walipowakamata walianza Kuwachukua Muwatembeze Maeneo Mbali kamaViongoza Njia katika Kumtafuta Lijenje

Shahidi: Ni Uongo

Kibatala: husianisha Sasa Swala la Ugeni wa Adamoo na jambo la Mahita kwamba aliwatumia kama Viongoza Njia

Shahidi: ni Uongo kwa sababu Adamoo alikuwa Mgeni afahamu eneo Lolote

Wakili wa Serikali: OBJECTION Shahidi anaulizwa Maswali yanayompeleka Kutoa Opinioni zake, Jambo hili ni Kinyume na Sheria ya Ushahidi

Jaji: unaweza Kusoma hicho Kifungu

Wakili wa Serikali ,anasoma.................

Jaji: Kulingana na Ulichokisoma umaanisha nini kwa neno Persive

Jaji: Kibatala Kama kweli angerejea sheria angetumia Kifungu cha 62 (c) kwa Maoni yangu Shahidi anaulizwa Perception yake yeye,Very strait

Jaji: wakili wa Serikali Sisi tunaendelea Kusisitiza Hilo swali lisiruhusiwe, Kwenye Ushahidi tunaona ni Jambo ambalo si sawa

Jaji, nimewasikiliza pande zote Mbili mimi naona Kuwa Kifungu cha 62 (c) kinaruhusu Shahidi Kutoa Mtazamonwake Kuhusu Jambo analoyolea Ushahidi

kibatala: haya elezea Sasa Unahusinisha Vipi Ugenibwa Adamoo na Maelezo ya Mahita ya kuwatumia kama Viongoza njia

Shahidi: Ni Uongo Adamoo alikuwa Mageni Moshi tulifika Sikubya kwanza, Siku ya Pili,siku ya tatu tunakamatwa

Kibatala: Kingai anasema aliwachukua wadada wawili Mpaka Central Kwenda Kutoa Maelezo je ulishihudia.?

Shahidi: Sikushuhudia

Kibatala:Je Wallet yako na Simu yako Ulisikia Afande Kingai au Mahita kuwa Vifaa Hivyo viliingizwa Kwenye Register Moshi.?

Shahidi:Sikusikia

Kibatala: Mashahidi hao wawili pia walizungumzia Hati ya Uchukuaji wa Vielelezo CERTIFICATE OF SEIZURE je ulisikia

Jaji: Kiswahili Chake Kikosawa

Jaji: tafiri iwe Hati ya Kuhodhi Mali

Kibatala: Ulisikia Kuwa Pistol,Madawa ya Kulevya na Vitu vyako ulisikia kama Viliingizwa kwenye Hati ya Kuhodhi Mali

Shahidi: Sikusikia

Kibatala: Bila shaka Kile kitabu cha Komito Unacho,Je umewahi Kuona Mle Kuna Sehemu yoyote Imeandikwa kuhusu Madawa ya Kulevya

Shahidi: Hapana Hakuna na sijaona

Kibatala: Moaka Leo unatoa Ushahidi hapa Mahakamani uliwahi kusikia au Kuona Adamoo alipatatikana na Madawa ya Kulevya.?

Shahidi: Sijawa Kusikia wala Kuona

Kibatala: Uliwahi Kushuhudia Kuwa Adamoo wamemchukua Sampuli ya mwili wake kwa ajili ya Kwenda Kupima utumiaji wa Madawa ya Kulevya

Shahidi: sijawahi kuona

Kibatala: Uliwahi Kushudia Adamoo akipewa hati ya kumiliki Mali

Shahidi: sikuwahi Kushahidi

Kibatala: uliwahi Kupewa hati ya Kumiliki Mali

Shahidi: Hapana sijawahi

Kibatala: Uliwahi Kushudua Adamoo akipewa nafasi wa Kushuhudia wakatibakitoa Maelezo pale Moshi

Shahidi: Hapana sijawahi

Kibatala:Uliwahi wewe Kupewa nafasi ya Kumyita Shahidi wa Kushudia wakati Ukitoa Maelezo

Shahidi: Hapana

Kibatala: Unauhakika gani Kuwa Adamoo alifanyiwa Mateso akiwa Moshi Polisi Central Station

Shahidi: niliwahi Kumuona Adamoo akiwa anaburutwa,na Baadae wakawahi Kunipiga Kitambaa,lakini nilishawahi Kuona

Kibatala: hayo yanaweza Kuwa ni Matokeo ya Adamoo Kuteswa ,Je ulishuhudia Vipi kuwa Adamoo anateswa

Shahidi: Nilislia Kilio cha Adamoo kwa Sababu Sauti ya Adamoo naijua nilikuwa mwalimu wake katika kozi za Ukomandoo,Nilikuwa namuita Sauti ya Zege tangubakiwa Mwanafunzi wangu 92 KJ

Kibatala: kumbe wewe ni Mwalimu wa Adamoo.?

Shahidi: Ndiyo Mwalimu Mzuri sana

Kibatala: Ukiwa kama Mwalimubwa Adamoo ulishawahi Kusikia anatumia Madawa ya Kulevya

Shahidi: Hapana

Kibatala: ungesikia Adamoo anatumia Madawa Ya Kulevya wakati Mkiwa Jeshini Utaratibu unakuwaje

Shahidi: hayo ni Mambo yakushughulikiwa na Millitary Police

Kibatal:a Mwambie Mheshimiwa Jaji jambo Lingine unalothibitsha kuwa yale Mateso yalikuwa ni ya Adamoo

Shahidi: kwa sababu hata tulipokuwa Cello tuliongea akaniambia ,poa tuh ila mikazo tuh,Nikamwambia na Mimi hivyohivyo,Ila navumilia

Jaji: Unaposema Poa ila Nikazo maana yake nini.?

Shahidi: Kwamba tumeumia ila tunajitahdi Kuvumilia

Kibatala: nakutoa Moshi nataka kwenda Kwenye kusafiri nilisikia unasema wewe ulisafiri na Adamoo kwenye gari Moja

Jaji: ni kweli ulisema wewe na Adamoo mlisafiri kwa gari Moja.?

Shahidi: hapana sifahamu nilihisi tuh kwa sababu sikuona

kibatala: Sasakwa Ufahamu wako wa Kawaida Ulisafiri naye au hukusafiri naye

Shahidi: kama nilivyosema sikuona akipanda ila niliskia Nyuma Buti limefungukiwa anakapndishwa Mtu,Kwa fahamu zangu naweza Kusema tulisafiri naye

Kibatala: katika hisia za Kusafiri naye hapohapo ni kweli Kwamba Gari ilisimama.Sehemu mkala

Shahidi:Hapana ni Uongo

Kibatala: kwamba Gari mkiharibika Mkasimama na Kubadili gari nikweli Usingefahamu..?

Shahidi: Nisingefahamu Japo kuwa nilikuwa nimefungwa Kitambaa,Kakini gari ikisimama nafahamu

Kibatala: Kumbukumbu yako Wakati Shahidi anawapokea Pale Central alisema aliwapokea Kwenye gari Moja.?

Shahidi: kwa Kumbukumbu zangu alisema tulifika pamoja

Shahidi: Kwa Mkupuo mmoja

Kibatala: je kwa mkupo Mmoja au Tofauti Tofauti.?

Kwa Ufahamu wako Nani alikuwa anawapa wenzie Amri tangu huko Moshi

Shahidi: Kingai

Kibatala: Umefanya kazi Jeshini,Mwambie Mheshimiwa JajibKwenye Msafara pakiwa na Senior Officer na Junior Officer Inawezekana vipi Junior Officer Kutoa Amri.?

Kibatala: Inaezekana Vipi Shahidi watatu kwa Maneno yake kwamba alikabidhiwa Watuhumiwa na Junior Officer wakati Kingai Alikwepo

Shahidi: haiwezekani

Shahidi: Haiwezekani,Kwa sababu Kingai alitakiwa kutukabidhisha kwa sababu alikwepo

kibatala: Ulisikia akisema alipokea Chochote kile ili akiingize kama Kidhibiti kwa Kujibu wa sheria

Shahidi: Sikumsikia

Shahidi: Hapana sikusikia

Kibatala: Rudi Tazara ACP kingai alikiri Kuwa Mlienda Mbweni ila hamkwenda Tazara,Je unathibitishaje kuwa Mlienda Tazara

Shahidi: Natihibitisha kwa sababu nilimuona Alex na Chuma Chungulu ambao nilikuwa nao Jeshini,Nathibitisha kwamba Ilikuwa Tazara

Kibatala: Ulijisikiaje safaribyote Kutoka Moshi Mpaka Dar es salaam Ukiwa Umefungwa Pingu

Shahidi: Nilijisikia Vibaya

Kibatala: na Ukahisi nini

Shahidi: Mateso

kibatala: kwa Ufahamu wako Umesema ulipokuwa Tazara ulishuhudia nani alikuwa ametoka kuteswa.?

Shahidi: Denis Urio

Kibatala: Kwenye Kitabu Cha Komito ulimuona ni Shahidi wangapi wa Mashtaka

Shahidi: Shahidi wa Tatu

Kibatala: Urio aliwahi Kukutembele Gerezani ujue kuwa Yupo huru.?

Shahidi Hapana

Shahidi: Ndiyo

Kibatala: na Unamfahamu Vizuri Denis Urio

Shahidi: Ndiyo ni Mwalimu wangu kabisa wakati naingia Jeshini,na mimeishi naye achumba Kimoja Nikowa kwenye Misheni DARFUR SUDAN

kibatala: uliwahi kwenda sudani na Wapi Kwa Misheni za Kikazi

Shahidi: CONGO

kibatala: unathibitisha Vipi Kwamba Mwenzako Adamoo alikwepo Tazara

Kibatala: Nakutoa Tazara nakurudisha Mbweni,Kuna sehemu unasema Kuwa Ulimuona Kuwa Kingai alikuwa ameingia Kuna kachumba Fulani

Shahhid: Baada ya Mahabusu wenzangu Kusema Mwenzako yupo,Niliita Adamoooooo na akaitaika

Jaji: wapi

Kibatala: Mbweni

Shahidi: palikuwa na Vyumba Vitatu,Mimi niliwekwa kwanza kwenye Chumba cha Kwanza, Kingai akaingia kwenye Chumba Kinachofuata

Jaji: Subiri Kidogo

Jaji: Subiri Kidogo

Jaji :Ukamuona Kingai naingia

Shahidi: Kingai alipoingia akapitiliza Mlangowa Chumba cha Pili, Mimi nilikuwa Chumba cha kwanza Nipo na Jumanne

Kibatala: Goodluck alikuwa ameshika Kitu chochote

Shahidi: alikuwa ameshika Bastola

Kibatala: Kwa Uelewa wako Batola ilikuwa na maana gani

Shahidi: ilikuwa kunitishia na Kutaka kunifanyia Kitendo chochote,kama alivyosema Kunitupa

Nikiwa palepale nilimuona alikuwa Adamoo akitolewa katika Kile Chumba

Kibatala: alikuwa na hali gani

Shahidi: alikuwa amechoka sana na hajala

Kibatala: Ulijuaje kama hajala

Shahidi: Kama mimi sikuwa nakula nayeye pia alikuwa ajala

Kibatala: Hukula kwa siku ngapi

Shahidi: Sikuwa nimekula kwa Muda wa siku 10 Kuanzia tarehe 09 Mpaka tarehe 08 tarehe 09 Mpaka 19 Mwezi wa Nane,Chakula tulienda Kupewa Mahakamani

Kibatala: Inakuwaje Mtu akae Siku zote hizo bila Chakula

Shahidi: walikuwa wanawahudumia Mahabusu Wengine

Jaji:Mahakamani nani alikupa Chakula Mahakamani

Shahidi: Afande Goodluck alileta Ugali na Dagaa na hapo tulishakuwa wengi tayari

Kibatala: inakuwa Ngumu mimi kuamini Kuwa hukula kwa siku 10te 10

Shahidi: Ndiyo ni kweli sikula Chakula

Kibatala: Je maji

Shahidi: Chumba Changu Cha Mahabusu palikuwa na Bomba la maji ndiyo kilichonisaidia

kibatala: ukisema Chakula unamanisha nini.?

Shahidi: Chakula cha Mahabusu,kama wenzetu maana walikuwa Wanatuambia kuwa hawahusiki na sisi Chakula Chao wanawapa Mahabusu wao tuh

Kibatala: Sasa Ikawaje

Shahidi: Yule Afande sasa tuliyejenga naye Urafiki ndiyo alikuwa ananiletea Biscuit na Soda ua Maji special na Pia nilikuwa namuomba ampe Maagizo Adamoo

kibatala: Sasa tunaenda Sawa

Kibatala: Wakati wote Umefungwa Pingu ,ilikuwa Rahisi au Ugumu kiasi gani wakati wa kujisaidia

Shahidi:. .... .... ....

Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji nilikuwa nazingatia hilo

Jaji: Wakati tunasubiri Majibu ya shahidi,Nashauri tujikite sasa kwenye nini hasa Kilitokea wakati wa akumvhujua Maelezo Mashtakiwa wa Pili,

Kibatala: Wakati wote Mkiwa rumande Mwambie Mheshimiwa Jaji kuwa kama Mlishawahi Kupelekwa Hospotali

Shahidi: Hapana

Kibatala: ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji

Jaji:ninatumaini sijakuzuia

Kibatala: Hapana Mheshimiwa Jaji nimemeliza tuh

Jaji Naomba tubreak Kwa Dakika 15 Kwa Afya Zetu

Jaji anatoka Sa 4 na Dakika 54

Tumesharudi Mahakamani watu wote

Jaji ameshaingia

Kesi inatwajwa tena

Wakili wa Serikali:
Tupo tayari Kuendelea

Jaji: Utetezi Mpo tayari.?

Kibatala: Tupo tayari

Wakili wa Serikali: Chavula anaendelea

Jaji: Shahidi nakukumbusha Kuwa bado Upo Chini ya Kiapo

Wakili wa Serikali: Wewe ni Mohammed Abdilah Ling'wenya

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: wewe ni Komandoo

Shahidi: Ndiyo

Jaji: Umeacha Kuwa Komandoo

Mahakama Kicheko

Wakili wa Serikali: Ujeshi Ukomandoo haufutiki

Shahidi: Ndiyo ni sahihi

Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamsahrti yake.? yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya

Shahidi: Rudia swali

Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamasharti yake.? Yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya

Miiko inakufunga bado

Shahidi: Wakati nipo Kwenye Himaya ya Jeshi

Wakili wa Serikali: Kuna Miiko ya Kijeshi ya hutakiwi Kuongea

Shahidi: kama Yapi

Wakili wa Serikali: Wewe ndiyo utuambie

Shahidi: Wewe ndiyo umeyaleta Ndiyo Utuambie sasa

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo kule Jeshimi si Kuna Miiko hata Ukimatila Jeshini utakiwi kuyaeleza

Shahidi: Siyo sahihi

Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Jeshini kozi ya Komandoo ulikula Kiapo

Shahidi: Kiapo gani

Wakili wa Serikali: si Ulikula Kiapo,je nikiapo gani

Shahidi: Nitalitumiakia Jeshi Mpaka Kufa

Wakili wa Serikali: Ulikuwa unatumikia Jeshi Kwa Mambo gani

Wakili wa Serikali: Kingime lipi ulikuwa unafanya Jeshini

Shahidi: Kulinda Nchi,Kulinda ,Silaha,Vifaa na Amani ya Ndani na Nje ya Nchi

Shahidi: Force Keeping Congo

Jaji:Focrce Keeping Maana yake nini

Shahidi: tulikuwa tunaforce amani Congo

Jaji: unaw3leza Kutofautisha Peace Keeping na Peace Keeping

Shahidi: Moja Sudani Hatutakiwi Kupigana na Waasi Mpaka watuonyeshee silaha /Mtutu lakini Congo tulikuwa tunatoka tunaenda sehemu kama Tunguu kwa Maelezo kuwa yoyote tutakaye mkuta Tunapigana au Kumuua

Wakili wa Serikali: ni sahihi nikisema Kuwa yna Degree Sita za martial Arts

Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe Mwalimu gani ujui Martial Arsts,Wewe Unafundisha nini

Shahidi: Siyo sahihi

Shahidi Nafundisha kuruka na parashuti,Kupigana Juu ya Maji kwa kutumia silaha na Combats

Wakili wa Serikali kwa hiyo wewe unafahamu kupigana Karates

Shahidi nafahamu

Jaji: Naona Hamuelewani Wakili uliza kwa Yale Mambo ya kawaida hayo ni Mambo ya Kijeshi

Wakili wa Serikali: Nilifikiri ni Mwalimu atakiwa anajua Mambo yote

Wakili wa Serikali: Kipindi Cha Muda Gani ulitumia kujifunza Kupigana katares Mpaka ukaweza

Jaji: Ndiyo Mwalimubwa amambo ya Jeshi siyo Kiswahili

Shahidi: Miezi Sita ya Kozi,92K

Naomba tubreak Kwa Dakika 15 Kwa Afya Zetu

Jaji: anatoka Sa 4 na Dakika 54

Tumesharudi Mahakamani watu wote

Jaji: ameshaingi

Kesi: inatwajwa tena

Wakili wa Serikali: Tupo tayari Kuendelea

Jaji: Utetezi Mpo tayari.?

Kibatala: Tupo tayari

Wakili wa Serikali: Chavula anaendelea

Jaji: Shahidi nakukumbusha Kuwa bado Upo Chini ya Kiapo

Wakili wa Serikali: Wewe ni Mohammed Abdilah Ling'wenya

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: wewe ni Komandoo

Shahidi: Ndiyo

Jaji: Umeacha Kuwa Komandoo

Mahakama Kicheko

Wakili wa Serikali: Ujeshi Ukomandoo haufutiki

Shahidi: Ndiyo ni sahihi

Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamsahrti yake.? yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya

Shahidi: Rudia swali

Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamsahrti yake.? yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya

Miiko inakufunga bado

Shahidi: Wakati nipo Kwenye Himaya ya Jeshi

Wakili wa Serikali: Kuna Miiko ya Kijeshi ya hutakiwi Kuongea

Shahidi: kama Yapi

Wakili wa Serikali: Wewe ndiyo utuambie

Shahidi: Wewe ndiyo umeyaleta Ndiyo Utuambie sasa

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo kule Jeshimi si Kuna Miiko hata Ukimatila Jeshini utakiwi kuyaeleza

Shahidi: Siyo sahihi

Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Jeshini kozi ya Komandoo ulikula Kiapo

Shahidi: Kiapo gani

Wakili wa Serikali: si Ulikula Kiapo,je nikiapo gani

Shahidi: Nitalitumiakia Jeshi Mpaka Kufa

Wakili wa Serikali: Ulikuwa unatumikia Jeshi Kwa Mambo gani

Wakili wa Serikali: Kingime lipi ulikuwa unafanya Jeshini

Shahidi Kulinda Nchi,Kulinda ,Silaha,Vifaa na Amani ya Ndani na Nje ya Nchi

Shahidi Force Keeping Congo

Jaji: Focrce Keeping Maana yake nini

Shahidi: tulikuwa tunaforce amani Congo

Jaji: unaweleza Kutofautisha Peace Keeping na Peace Keeping

Shahidi: Moja Sudani Hatutakiwi Kupigana na Waasi Mpaka watuonyeshee silaha /Mtutu lakini Congo tulikuwa tunatoka tunaenda sehemu kama Tunguu kwa Maelezo kuwa yoyote tutakaye mkuta Tunapigana au Kumuua

Wakili wa Serikali: ni sahihi nikisema Kuwa yna Degree Sita za martial Arts

Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe Mwalimu gani ujui Martial Arsts,Wewe Unafundisha nini

Shahidi: Siyo sahihi

Shahidi: Nafundisha kuruka na parashuti,Kupigana Juu ya Maji kwa kutumia silaha na Combats

Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe unafahamu kupigana Karates

Shahidi: nafahamu

Jaji: Naona Hamuelewani Wakili uliza kwa Yale Mambo ya kawaida hayo ni Mambo ya Kijeshi

Wakili wa Serikali: Nilifikiri ni Mwalimu atakiwa anajua Mambo yote

Wakili wa Serikali: Kipindi Cha Muda Gani ulitumia kujifunza Kupigana katares Mpaka ukaweza

Jaji: Ndiyo Mwalimubwa amambo ya Jeshi siyo Kiswahili

Shahidi: Miezi Sita ya Kozi,92Kj

Wakili wa Serikali: Ulikaa Miezi sita 92KJ ukijifunza kupigana karates

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Ulifanya Phase ngapi.?

Wakili wa serikali: ni sehmu Gani Nyingine ulienda Kupata Mafunzo ya karates

Shahidi: phase Moja,Mengine niliyapatia Mahala pengine

Shahidi: nilienda Kujifunza Kick Boxing kwa Wafaransa

Wakili wa Serikali: Kwa Miezi Mingapi

Shahidi: Miezi Mitatu

Wakili wa Serikali: Kozi Nyingine ilikuwa ni nini.?

Shahidi: Kuzuia Uharamia

Shahidi: Sijui wewe

Wakili wa Serikali: Uharamia ni nini

Jaji: tudaidie kama Unaufahamu wowote kwa sababu wengine hatujui ila tumesikia sikiasikia

Shahidi: kwanza Ni Navy kwa Maana kuna kupambana Majini

Shahidi: Mapigano kwenye Majumba

Wakili wa Serikali: Kozi Nyingine

Wakili wa Serikali: Kwa Muda gani

Wakili wa Serikali: Kwa Muda gani

Shahidi: Kwa Miezi Mitatu

Wakili wa Serikali: Kwenye Majumba mnakuwa Mnampiga nani

Shahidi: Jinsi ya Kumtoa Adui Kwenye Majumba

Wakili wa Serikali: hayo Mapigano ya kwenye Majumba ,ni yepi uliyojifunza,Mieleka,ngumi...

Shahidi: Kutumia Silaha

Wakili wa Serikali: Silaha Zipi

Shahidi Kisu,SMG

Wakili wa Serikali Pamoja na Panga

Shahidi: panga sijataja

Wakili wa Serikali: Kisu ulifundishwa namna ya Kukitumia

Shahidi: kisu nilifundishwa

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo ulifundishwa kupigana kutumia Mikono

Shahidi: Mheshimiwa Jaji nimeshalijibu swali anarudia tena

Jaji: na mimi naona unarudia tena

Wakili wa Serikali: Hukufundishwa Kupambana na Maadui wako kwa Kutumia Miguu au Mikono

Shahidi: sikufundishwa

Wakili wa Serikali: Katila kozi ya wafaransa ulipata Kujifunza Kickboxing

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Kwahiyo baada ya Mafunzo hayo unauwezo wa akukabiliana na Adui Mahala Popote anapotokea,Kweli au si Kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Kwa kuchukuliwa kufanya kazi 92KJ wewe Umeaminika Sana,Kweli au Si Kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Na Nidhamu yako ni Yajuu sana Kweli ama si Kweli

Shahidi: Si kweli

Jaji: Ndiyo

Wakili wa Serikali: ili ndani ya 92KJ uoate Bahati ya Kuwa Mwalimu,ni kwamba kwenye Mafunzo uliyopita Umefanya Vizuri kwa kiwango cha Juu

Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe ni Mahiri sana

Shahidi: Kweli

Shahidi: kwa Wastani

Wakili wa Serikali: Mafunzo ulikuwa umefaulu ukaambiwa kawafundishe wenzio

Shahidi: Sikuambiwa hivyo,Jina lilitoka kwenda Starter nikatakiwa kwenda Kuwa Mkufunzi

Wakili wa Serikali: Ili uwe Mkufunzi unatakiwa uwe na Sifa gani

Shahidi: sijuibwakubwa wenyewe, lakini wanakaa kikao na inatoka ORDER kuwa Jina limetoka Kuwa Mkufunzi

Wakili wa Serikali: Umekuwa Mwalimu kwa Muda gani

Shahidi: Mwaka Mmoja

Wakili wa Serikali: bila shaka uliokuwa unawafundisha ulikuwa na maelewano mazuri na wao

Wakili wa Serikali: na Bila shaka wanafunzi wako walifaulu Vizuri

Shahidi: Kweli

Shahidi: Ndiyo walifaulu

Wakili wa Serikali: na wengibwa wanafunzi wako Mlikuwa mkielewana sana

Shahidi: Ndiyo tulikuwa tunaelewana

Wakili wa Serikali: wengi wao walikuwa na upendo na wewe

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Wale wanafunzi wako ukiachana na Adamoo Kuna waliokuja kukutembelea

Shahidi: hapa sijaona,ila walikuwa wanakuja Segerea

Wakili wa Serikali: Taja ni nani alikuwa anakuja kukutembelea

Shahidi: ni One Two One

Mallya: OBJECTION wakili anakoelekea Kutaka kutajana Majina ambayo tena ya wanajeshi,Wengine tulishaomba MAHAKAMA wale ambao Ni WANAJESHI wasitajwe Kwakuwa wapo kazini na Wengine Wapo Kwenye USHAHIDI

Wakili wa Serikali: Taja Majina yake,hapa Tupo Mahakamani lazima uwe na Nidhamu

Jaji: Kuna Mtu anataka Kurespond,

Wakili wa Serikali;: Shahidi amekuwa akitaka Wengine Kwa Majina sasa sioni tatizo kwa kutaja huyo anayemtembelea

Mallya: Kuna Taarifa tunayo tangu tuseme Kuwa Kuna Mashahidi ambao wapo Jeshini, Wapo Wanajeshi wawili wameshaitwa Kutishiwa wasije kutoa Ushahidi.

Jaji: Je Mallya unafikiri hao wakitaka Kujua wanafunzi wa Ling'wenya waliomtembelea Magereza watashindwa.?

Mallya: watashindwa,

Jaji: kwanini

Mallya: kwa sababu wanatumia Codes

Wakili wa Serikali: Naomba Nishauriane na wenzangu

Jaji: Ikibidi nihairishe kidogo mjipange

Wakili wa Serikali: Tuendelee Mheshimiwa hilo swali naliacha

Jaji: kabla Ujaliacha tuambie kwanza ,Kuna Umuhimu wa hayo Majina

Wakili wa Serikali: Hapana Mheshimiwa

Wakili wa Serikali: Ile Kombania uliyokuwa unamfundisha Adamoo ilikuwa na Kombania ngapi

Shahidi: Sisi hatuna Kombania tunaita Squad room

Wakili wa Serikali: Kwa ile ya Adamoo ilikuwa na Watu wangapi

Shahidi: na watu 60

Wakili wa Serikali: Siyo wanajeshi wote wanaoingia 92KJ kweli si kweli

Shahidi: Nyoosha swali Vizuri

Wakili wa Serikali: Ili Mtu aingie 92 KJ unatakiwa Uwe na Sifa Maalum

Shahidi: Sielewi

Wakili wa Serikali: Sisi tulikuwa Makutopora wakakata Bogi la 92

Wakili wa Serikali Boginla Makutopora lishakatwa kuna Lipi linafanyika

Shahidi: Wanapimwa Afya

Wakili wa Serikali: kwa hiyo wanaoingia 92KJ Sifa Kuu Afya iwe Nzuri

Shahidi Ndiyo

Wakili wa Serikali: Baada ya Kufuzu Afya, kozi inaanza

Shahidi: inategemea

Wakili wa Serikali: We Umepiga Kipindi gani

Shahidi: Mwaka Mmoja na miezi nane

Wakili wa Serikali: kozi ilikuwa Ngumu sana au Nyepesi Kwako

Shahidi: Mheshimiwa Jaji siwezi Kusema Ngumu au Nyepesi kwa sababu Leo Mkipewa Ugumu kwenye Intro kesho mnapewa Mepesi kwenye Leki

Shahidi: Ndiyo

Wakili: ili uwe Mwalimu kwenye hiyo Kozi unatakiwa Uwe,Mkweli,Mtiifu,Mwenye nidhamu ya haki ya Juu

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo sifa hizo zote unazo

Shahidi: siwezibKujua waliokaa wakanichagua

Wakili wa Serikali Kwa hiyi Kuna uwezekano Mtu akafuzu akawa hana hizo sifa

Shahidi: Imawezekana

Wakili wa Serikali: na wewe unawezekana ukawa huna hizo sifa

Shahidi: inawezekana

Wakili wa Serikali: Jeshini Kuna Mahabusu.?

Shahidi: Ipo

Wakili wa Serikali: Ile Mahabusu ya Kijeshi inasimamiwa na Nani.?

Shahidi: Military Police

Wakili wa Serikali: sahihi kwamba wanaofanya Makosa na kuwekwa Mahabusu ya ya Kijeshi wanaweza Kuwekwa kwa muda wa siku 2 au Wiki 2

Shahidi: Unawekwa

Wakili wa Serikali: Uwezi Kushtuka na siyo Ajabu ukiona Mtu kakaa Mahabusu Wiki Mbili,Kule Jeshini

Wakili wa Serikali: Uwezi Kushtuka na siyo Ajabu ukiona Mtu kakaa Mahabusu Wiki Mbili,Kule Jeshini

Shahidi: Unawekwa

Wakili wa Serikali: Vipi kuhusu chakula Ukiwa Mahabusu ya Jeshi

Shahidi: Unakula Resheni yako mara tatu kwa siku

Wakili wa Serikali: Chakula Kinatoka wapi

Shahidi: Chakula cha Serikali ni Cha Jeshi

Wakili wa Serikali: Na wanaoleta Chakula ni MP tuh

Shahidi: kwa kwetu KJ 92 Unachukuliwa na Kupelekwa Mess ukimaliza Kula unarudishwa Mahabusu

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Utakubakiana na Mimi wanaowaletea Chakula ni wale Ma Mp wanaohusika na Mahabusu tuh

Wakili wa Serikali: Kwa Nidhamu ya Kwenye Majeshi wale wanaotunza wanajeshi Kuoe Mahabusu,hawana Nidhamu ya Kusema wale wanaletewa Chakula Nje ya wao wanaotunza Mahabusu

Shahidi: Si kweli

Mimi kwa 92 KJ hatupo chini ya Ulinzi kwamba Utatorika kazini,Unachukuliwa Mahabusu wanakupeleka Mess ukimaliza Kula Unarudi Mahabusu

Wakili wa Serikali: kwa hiyo haiwezekani kupewa chakula Kutoka Nje

Wakili wa Serikali: Chakula cha Nje ya Jeshi

Jaji: Shahidi kashaeleza utaratibu wa wa Chakula,unazungumzia Chakula cha Kutoka wapi

Shahidi: si elewi

Wakili wa Serikali: nitakuwa sahihi nikisema Komandoo Mmoja anaweza kupambana Askari wasio wanajeshi 50
wasiokuwa Makomandoo zaidi ya 50

Shahidi: Si kweli

Wakili wa serikali: komandoo anaweza Kukabiliana na Askari wangapi

Shahidi: Inategemea, Ukomandoo siyo Kupigana tuh,Wapo askari wanaweza Kupigana kuliko Mimi Komandoo, na Pia Ukomandoo wa kupigana na watu 50 Labda ukomandoo RAMBO siyo kawaida

Shahidi: ukomandoo ni Ujuzi tuh labda wa Kupigana, Silaha na Kutumia Vifaa vya Kivita

Wakili wa Serikali Sasa jana Ulieleza Jana Ukiwa Nje uliona Adamoo akiwa nje alikuwa anaongea na Simu

Wakili wa Serikali: kweli ama si Kweli

Shahidi: Sikumbuki

Jaji: alisema alisikia Sauti ikiitokea kwenye Corridor Akizungumza na simu

Wakili wa Serikali: ni sahihi Jana Ulisema Adamoo akizungumza na simu kwenye Uchochoro

Wakili wa serikali: Ulisema Jana Uliposikia kelele Kwenye uchochoro Ukamkuta Adamoo ameshanyanyuliwa

Shahidi: Si kweli

Mallya: OBJECTION Wakili anajaribu kumlisha maneno shahidi kuwa alikimbilia uchochoroni

Jaji: Nililwenda kule Ammbako sauti ilikuwa inatokea

Wakili wa Serikali: ni sahihi kuwa ulimkuta Kuwa ameshanyanyuliwa Juu juu

Shahidi: Nilikuwa Ndani ya Duka nikakuta wameshamsogeza karibu na Nilipokuwa

Wakili wa Serikali: Ulimkuta Adamoo amenyanyuliwa Jujuu,Kweli si kweli

Shahidi: ni kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: ulikuta anavutwa akitolewa Uchochorono kweli au si kweli

Wakili wa Serikali: Jana ukisema Ukamkuta wanamnyanyua na Leo unasema kuwa ulimkuta anavutwa

Jaji: anafikiri Shahidi alisema Jana na Leo Asubuhi siyo wakati wewe unamuhoji

Wakili wa Serikali: Mahakama Imerekodi Leo Asubuhi Kuwa Adamoo alikuwa anavutwa

Shahidi: Kweli

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: na Hiko kitendo ulikiona Kwa macho,Kweli au si kweli

Wakili wa Serikali: Wakati gani Upo sahihi Jana au Leo Asubuhi

Shahidi: Yani...........

Shahidi: Nilichosema Leo ni sahihi

Wakili wa Serikali: Chagua Moja tuh Yapi sahihi

Wakili wa Serikali: Jana Wakati unahojiwa uliona kwamba wale waliomzunguka Walikuwa wanatoa Pistol kwenye maungo ya a
Adamoo

Shahidi: kweli

Wakili wa Serikali: kwa hiyo uliona wakati wanachomoa pistol wakisema anapistol anapistol

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: na wakati wa Madawa pia uliona wanatoa Madawa wakisema anamadawa anamadawa

wakili wa Serikali: Sasa tusaidie hapa Adamoo wakati nahojiwa alisema wewe Ulishihudia wakimuwekea Madawa na Pistol

Shahidi: Kweli

Shahidi: Sikumbuki

Shahidi: Sikumbuki kwamba Adamoo alinilenga Kuwa Mimi kuwa Nimeona wakimuwekea Madawa na Pistol

Jaji: Sasa jibu kuwa Adamoo alisema au hakusema

Shahidi: Sikusikia akisema hivyo, kauli yangu ilikuwa "natoa Vitu vyangu Msije kuniweka Pistol na Madawa akama Mlivyomuwelea Mwenzangu"

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Kama.Kuna Mtu akisema Umeona atakuwa Muongo

Shahidi: akisema kwa Kauli inayosema Kweli ni Muongo

Wakili wa Serikali: Kuna Mtu anaitwa Msemwa shahidi wa tatu ulimuona

Shahidi: Ndiyo nilimuona

Wakili wa Serikali: Ulieleea Ushahidi wake

Shahidi: Kwa Uelewa Wangu nilielewa

Wakili wa Serikali Wakati Msemwana anatoa Ushahidi alisema aafande Kiingai alileta watuhumiwa Wawili waliloletwa na Afande Kingai,Ni kweli au si kweli

Shahidi: Ni kweli alisema

Alisema Saa 12 Kasoro

Wakili wa Serikali: kweli Saa 12 Kasorobo

Wakili wa Serikali: Ulisikia akisema Mohammed Abdilah Ling'wenya

Shahidi: Ndiyo nilisikia

Wakili wa Serikali: Ulijua anayesemwa ni Wewe.?

Shahidi: Ni kweli nilijua

Wakili wa Serikali: lakini Hukusema kwamba wewe Msemwa Muongo sikuwahi Kuwa chini yako

Shahidi: Sikuwahi Kuwa Ukiwa kizimbani unaruhusiwa Kuongea

Mahakama Kichekooooooo

Shahidi: Ndiyo kabla Msemwa ajatoa Ushahidi

Wakili wa Serikali: Uliongea n wakili wako Kwamba Ulifikishwa Tazara na Siyo Central

Wakili wa Serikali: lakoni Wakili wako hakusema Kuwa Msemwa ni Muongo

Shahidi: Alisema,kwa Maelezo kwamba Nilitoka Moshi nikafikishwa Tazara ilikuwa anafikisha Ujumbe sijawahi Kuwa Central

Jaji Tupishe Hadhana*

Mahakama Kimyaaaaaaaaaa

Jaji: tunaweza Kuendelea

Wakili wa Serikali Umeelza Kwamba Habari ya Msemwa kuwa anaongea Uongo ni leo Ndiyo umesema Mahakamani Kwa kurudia Swali

Shahidi Si kweli Jambo hilo lilikuwa limeshatajwa, uongo huo umejulikana leo alisema hata Adamoo

Wakili wa Serikali: kwa hiyo siyo wewe au Adamoo wakati Msemwa anatoa Ushahidi wake Kuwa Wewe ni Uongo

Shahidi: sasa wewe unamwakilishi wako na Mwakilishi wako hazungumzi hukuona haja kwamba kumwambia Wakili kuwa Huyo anaongea Uongo

Shahidi: alisema Adamoo kabla yangu kuwa hatukuwahi Kufikishwa Central

Wakati ule Msemwa anaongea Uongo dhidi yako wewe,na wewe Unaona ni Uongo na Hukuona Sababu ya kumweleza kuwa Huyu anadanganya

Wakili wa Serikali hebu tuambie sasa ni sahihi kwamba ,Pale Rau wakati Mwenzio anavutwa ,wewe Ulitoa Vitu vyako ukaweka Kwenye kibaraza cha Duka

Shahidi: kwenye nini

Shahidi: Kibaraza Cha Duka

Wakili wa Serikali: Upo ushahidi ulioletwa Mahakamani Kuwa wewe ulipofika Pale hapa Mahakamani kwamba Msije kunifanyia Kama Mlivyomuwekea Vitu chini

kimya Kidogo

Shahidi: Lile Tukio lilivyofanyika nikasema Msije kunisingizia Kama Adamoo,na mimi natoa Vitu vyangu,nikaviweka pale Chini Kibarazani

Jaji: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ,wale watu waliowakamata pale Rau Madukani kuna Mahala popote uliwahi Kukutana nao

Shahidi: sikuwahi Kukutana nao Wala nilikuwa siwajui

Wakili wa Serikali: Kama ulikuwa uwajui hukuwahi Kuhitilafiana nao hao watu

Shahidi: Kweli Kabisa

Wakili wa Serikali: hukuwa unafahamu kuwa wale ni Polisi

Shahid:i si kweli, Nilijua ni Polisi Ndiyo maana Niliwaambia Kuwa Msimpige Adamoo

Wakili wa Serikali: Ulipowaambia tuondoke wakaondoka

Shahidi: walikusanya Vitu na kusubiri Amri ya Mkubwa wao,Siyo kwa kauli yangi ndiyo waondoke

Wakili wa Serikali: kwa hiyo Adamoo hakupigwa

Shahidi: Unanirudisha Nyuma,Nilishasema nilipotoka nilikuta wanapiga Adamoo na Kumburuza

Wakili wa Serikali: baada ya Pale Mlienda Kituoni Polisi

Shahidi ndiyo tulienda Moja Kwa moja Polisi

Wakili wa Serikali kitendo cha kujua hawa ni Askari Polisi ilikuwa ni Ukamataji au siyo Ukamataji

Shahidi: Siyo Ukamataji

Shahidi: ndiyo ni Mateso

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Kitendo kile siyo Ukamataji ni Mateso

Wakili wa Serikali: Kitendo cha kuwapeleka Kituo cha polisi mlikuwa mmekamatwa

Shahidi: Ndiyo

Jaji: Shahidi Mwanzo Umesema hukukamatwa

Shahidi: ni sahihi Mheshimiwa Jaji kwamba Wakili wangu nilimjibu Mwanzonkuwa Tulitekwa na Baaadae hapa nimejibu hatujakamatwa ananiuliza Jambo lingine

Jaji: sawa tuendeleee

Wakili wa Serikali: Umesema Adamoo kuwa alivaaje

Wakili wa Serikali: Kwani hayo Mavazi hawezi Kuvaa Mtu Mwingine

Shahidi: Raba Nyeupe,Suruali Nyesui,Shati la Mikono mirefu la Maua maua

Shahidi: anaweza

Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji naomba Maji, Maji yameisha hapa Kizimbani

Jaji: kweli Umenikumbusha Leo, Apewe Maji ,ila kazi Ngumu ya kujibu Maswali tangu Asubuhi

Wakili wa Serikal: Nilikuwa nasema Kuwa Yale mavazi si anaweza Kuvaa Mtu yoyote

Jaji: Ling'wenya ungependa tupumzike

Shahidi: ndiyo Mheshimiwa Jaji

Jaji: nahairisha Mpaka Saa 8 na Dakika 10

Jaji: ameingia

watuhumiwa wanapanda Kizimbani

Kesi Namba 16 ya 2021 inatajwa

Mafaili yanapandishwa kwa Jaji


Jaji: nnatunaini Pande zote zipo tayari kwa ajili ya kuendelea

Mashitaka Tupo tayari

Utetezi Tupo tayari

JAJI: Shahidi aliishia Kwa Upande wa Mavazi aliyokuwa amevaa Adamoo ambapo ni Raba Nyeupe,Suruali ya Jeansi na Shati la Mauamaua

Jaji: Shahidi nakukumbusha upo chini ya kiapo

Wakili wa Serikali: Mavazi aliyokuwa amevaa ulisema yanaweza Kuvaliwa na Mtu yoyote

Jaji: Wakili wa Serikali Chavula Karibu tuendelee

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Adamoo ni Mtu wako ,rafiki yako

Shahidi: Kweli ni Mtu wa karibu

wakili wa Serikali Mmekuwa na Adamoo nyakati za raha na tabu,kweli au si kweli

Shahidi: ni Kweli

Wakili wa Serikali: sasa tuambie Kabla ya tarehe 05 Mwezi wa 07 2020 haukuwahi Kupata Msukusuko ukiwa na Adamoo

Shahidi: sikuwahi Kupata Msukosuko nikiwa na Adamoo

Wakili wa Serikali: Mazingira yaliyokufanya Umpachike Adamoo wakati wa Mafunzo ,Mkiwa mnaimba

Kweli au Si kweli

Shahidi ni Kweli

Wakili wa Serikali: Unaweza Kuileza Mahakama Adamoo akiwa anaimba sauti yake ikoje

Shahidi: Siyo nyororo wala siyo Nzito sana

Shahidi: naweza Kuimba
Shahidi: anaimba Kwa Mfanano wa Sauti ya Adamoo "Tembea tembea Kidogo dogo,Melengelenge si Ugonjwa"

Mahakama Kichekoooooooo

Jaji: naona unatukumbusha 92KJ

Wakili wa Serikali: Kwahiyo hiyi Adamoo hata akiwa Kwenye giza ,Wewe Umuini utatambua huyu ni Adamoo si Mtu Mwingine

Shahidi: namtambua,Nishaieleza Mahakama

Wakili wa Serikali: Ni sahihi vile ambavyo umeimbia Mahakama ndivyo ambavyo Adamoo anaimbaga

Shahidi: Sahihi

Wakili wa Serikali: Kwahiyo Mtu anaweza Kuiga Sauti ya Adamoo

Shahidi: Ndiyo akiwa ameishi naye kama nilivyoishi naye mimi anaweza

Wakili wa Serikali Kwahiyo Sauti ya Mtu inaweza Kuigwa

Shahidi: Ndiyo Sauti ya Mtu inawezekana Kuigwa

Wakili wa Serikali: Umeeleza Mahakama Ulisikia Adamoo analiaje vileeeeee

Wakili wa Serikali:ukajua Kuwa hiyo ni ya Adamoo

Shahidi: Eeehiiiiiiii,Eeehiiiiiiiii

Wakili wa Serikali: Hukuieleza Mahakama kwamba Kabla ya Tarehe 05 niliwahi Kumsikia Adamoo akilia

Shahidi: Mahakama ipi,Miye nimeeeleza Kuwa Nilimsikia Adamoo akilia

Wakili wa Serikali: nazungumza kabla ya Shauri hili Mahakamani, uliwahi Kuieleza Mahakama kuwa Kabla ya tarehe 05 uliwahi Kumsikia Adamoo akilia

Shahidi: Sikueleza

Wakili wa Serikali Kwakuwa umeieleza Mahakama kama hukuiambia Kwamba Adamoo hukuwahi Kumsikia Adamoo akilia na Kwamba Kuna Uwezekanao Mtu aliiga Sauti ya Mtu,Utakubaliana na Mimi Kuwa Ile sauti ya Mtu aliyekuwa analia kuona nani alikuwa analia

Shahidi: Ndiyo sikuona Kwa Macho

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: Ulieleza Mahakama Mtu aliyepitishwa Mbele yako aliliwa akiinamishwa

Wakili wa Serikali: na wewe hukuileza Mahakama yule Mtu hukumtambua kwa Sura

Shahidi: Kweli

Wakili wa Serikali: anawafuata wenzie Kushauriana

Shahidi: nilimuita

Wakili wa Serikali: Yule Mtu ulisema Mahabusu Mwenzio pale Moshi,ulihisi ni Adamoo ulimwambiaje

Wakili wa Serikali ukamwambiaje

Shahidi: niliamuita Jina Lake Adamoo, akasema naam Bro Mikazo ila hali Mbaya,nikamjibu na mimi ni hivyo hivyo ila najitahidi

Wakili wa serikali: alikwambia Nimekazwa ila hali ni Mbaya

Jaji: wakili umesikia Vizuri kweli hebu rudia

Wakili wa Serikali: Nimekazwa

Jaji: wakili wa Serikali Mwingine,Katuga umesikiaje .?

Shahidi: Mikazo

Wakili wa Serikali: Katuga umesikiaje

Jaji: Wakili wa Serikali Chavula Umesikia .?

Wakili wa Serikali: Chavula Nimekazwaza

Mahakama Kichekoooooo

Jaji: Nakwambia Mimi Mara ya Mwisho Mikazo,Ukiendelea tena Nitakutafsiri tofatuti

Jaji: Endelea

Wakili wa Serikali: Chavula Mikazo Mheshimiwa Jaji nilisikia Vibaya

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo hakuk and ambia Kuwa amepigwa tofauti na Maneno hayo

Shahidi: kweli hakutamka Kwamba amepigwa

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo wewe ukatafsiri kwa Ufahamu wako kwamba Mikazo ni Kupigwa

Shahidi: Sahihi Ndiyo tulivyomaanisha

Wakili wa Serikali: Ni sahihi kwamba Rau Madukani Mlikuwa Na Moses Lijenje

Shahidi: Si kweli

Wakili wa Serikali: Mlikaa naye Moshi na Moses Lijenje Mara ngapi

Shahidi: Tulikuwa naye mara Moja wakati tunaongoa na Mheshimiwa Mbowe kuhusu swala la Kazi

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa nani

Shahidi: Mheshimiwa Mbowe

Wakili wa Serikali: mliongea naye wapi

Shahidi: sifahamu Maeneo ya Hotel gani

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Siyo Aishi Hotel aliyosema Adamoo

Shahidi: sifahamu kwa sababu hatukuingia Uoande wa Hotelini

Shahidi: ni Maeneo yaleyale ya Aishi lakini siyo Hotelini

Wakili wa Serikali: lakini Maeneo ya Aishi Hotel

Wakili wa Serikali: Wakati Mnakamtwa Rau Mlikuwa na Moses Lijenje

Shahidi: tulikuwa naye Rau,

Wakili wa Serikali: Wakati Mnakamtwa Mlikuwa wapi

Shahidi: yeye alikuwa eneo ya Glocery wakati purukushani inatokea

Wakili wa Serikali: Atakuwa alikimbia au alijificha

Shahidi: Mimi sifahamu hayo

Wakili wa Serikali: Ndiyo Mimi nakwambia Sasa alilimbia kwa mujibu wa kingai

Mallya: OBJECTION Wakili anaweka Opinion zake

Jaji: na Mimi nimeona hilo,nilishakataza hayo Maneno yenu siyo lazima kuweka mimi naandika Maelezo ya Shahidi tuh

Wakili wa Serikali: wakati Kingai anatoa Ushahidi wake kuwa Moses Lijenje alikimbia akaelekea Arusha kwa Dada yake

je Ulimsikia

Shahidi: Nilimsikia Kingai akisema hivyo

Wakili wa Serikali: Maelezo ya Kingai yanatofautiana na wewe Kwamba Mlipofikishwa Polisi Central Moshi hamkutoka kabisa

Shahidi: Kweli hatukotoka kabisa

Wakili wa Serikali: Kwamba tulipotoka Rau Madukani kwamba tulifikishwa Moshi Polisi Central Yanaletwa Leo akiwa Kingai hayupo Mahakamani

Shahidi: Kweli sijamuona Kingai Hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali: Kama Umeyasema yeye akiwa hayupo Mahakamani,hana Ufahamu ya Unayoyasema kwa Sababu yeye hayupo Mahakamani

Shahidi: Ni kweli hafahamu

Wakili wa Serikali: nitakuwa Sahih,Ngoja niondoe
ikatatokea Leo wewe Watu wanazungumza wanasema Mohammed Muongo

Jaji: naona watu wanatoka toka inapoteza Utulivu wangu,na Mimi sitaki Kuzuia Watu kuingia Mahakamani,Si tumetoka Break sasa hivi tuh Naomba Mjitahidi,ingawa sisiemi watu wakibanwa wasitoke wajikojoleee

Jaji Tuendelee

Wakili wa Serikali: Kuanzia Jana Ulipoanza Kutoa Ushahidi wako Mpaka Sasa Hakuna mahala popote Kuanzia Tarehe 05 na Kabla ya siku Ile Kuwa Uliwahi Kumkagua kwemye maungo yake

Shahidi: Sikumkagua,nimkagie kama nani na sina tabia hiyo

Wakili wa Serikali: sema Kweli au si Kweli

Jaji: nafikiri ameshajibu

Shahidi: Ni sahihi Mheshimiwa Jaji

Wakili wa Serikali: Wakatibwa Maelezo yake Adamoo hakusema Moshi hakuwa kufika na Ile ndiyo Mara yake ya Kwanza

Shahidi: Kweli hakusema hivyo

Shahidi: Ni kweli nimesema

Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe ndiyo unayesema Adamoo Mji wa Moshi ni Mgeni,Kweli au Si kweli

Wakili wa Serikali: Tuambie sasa Wewe Dar es salaam ni Mwenyeji.?

Wakili wa Serikali: Tuambie sasa Wewe Dar es salaam ni Mwenyeji.?

Shahidi: siyo Mwenyeji sana

Wakili wa Serikali: Dar es salaam Unafahamu sehemu gani,

Shahidi: Napafahamu Kimara King'ong'o,

Wakili wa Serikali: Sehemu gani Nyingine

Shahidi: Kimara Matosa

Wakili wa Serikali: unapafahamu Posta..?

Shahidi: Napafahamu Posta Nilisha wahi Kufika Kanisa la Joseph

Wakili wa Serikali: Pale Ndiyo Posta

Jaji: sasa Niandike Nini

Wakili wa Serikali: Unapafahamu Posta

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Unapajua Station..?

Shahidi: nimewahi Kufika Zamani

wakili wa Serikali: Kwa hiyo Unapajua au Upajui

Mallya: OBJECTION ameshajibu Swali

Jaji: Bado hajajibu swali

Shahidi: sipafahamu kwa Sasa

Wakili wa Serikali: Vipi KuhusuTazara ..?

Wakili wa Serikali: Vipi Kuhusu Buguruni

Shahidi: Sipafahamu

Shahidi: Sipafahamu

Wakili wa Serikali: kwa hiyo ulifanya Kuambiwa Kuwa hapa ni Tazara

Shahidi: kweli

Wakili wa Serikali: kwa hiyo Ukiacha kuambiwa kwa akili yako uwezi Kujua ulikuwa Tazara

Shahidi: kwa akilinyangu nilioata Kuambiwa pale ni Tazara

Wakili wa Serikali: kwa hiyo Ujawahi Kufika Tazara kabla

Wakili wa Serikali: kwa hiyo Ujawahi Kufika Tazara kabla

Shahidi: Sijawahi Kufika Kituo cha Polisi Moshi zaidi ya kutolewa Moshi na Kuletwa Pale Tazara Kituo cha Polisi

Wakili wa Serikali: Kama Nimekusikia Katika Safari yenu Kutoka Moshi Kuja Dar es salaam, Mle ndani Ukiacha Askari polisi waliokuwa wanapiga Story zao,Hukusikia akitukingine Chochote

Shahidi: Kwanza siku safiri Tarehe 05 ni Tarehe 06

Wakili wa Serikali: Samahani nilikuwa namaanisha Tarehe 06 Ulikuwa unawasikia Askari Polisi wanapiga Story Zao

Shahidi: ni kweli nilikuwa nasikia wanaongea Maongezi yao

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Ilikuwa ni Safari ya Utulivu hapakuwa na Purukushani

Shahidi: Nimezungumza jana Purukushani zilikwepo, Kwa Sababu nilikuwa nikitaka Kuinua kichwa wananikandamiza Chini

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo ukiondoa jambo hilo hapakuwa na Purukushani Nyingine

Shahidi: Kwa binafsi yangu hapakuwa Na Lingime

Wakili wa Serikali: Ukiacha watu uliokaa nao palikuwa na watu wengine Kwenye lile gari

Shahidi: Siwezi Kujua,nilikuwa nimepigwa Kitambaa

Wakili wa Serikali: Relax nataka Ujibu Upate haki yako,Mimi sikutegi

Shahidi: Ndiyo Maana na Mimi nakwambia Ukweli

Wakili wa Serikali: kwa hiyo Palikuwa na watu wengime kwemye gari

Shahidi: Siwezi kuwatambua nilikuwa Nimepigwa Kitambaa ila nilikuwa na sikia Sauti Mbele au Nyuma ya Gari

Wakili wa Serikali: Hebu tuambie Kama ni Kweli,Ulipokuwa Mbweni Ukatolewa Ukawekwa Chumbani ukawa umewekwa na Askari gani

Shahidi: Nimeeleza Mahakama nilikaa chumba Cha kwanza Ukiingia tuh

Wakili wa Serikali: Palepale Kwenye Chumba Ulichoingia tuh

Shahidi: Nilikuwa na Jumanne na Mlangoni alikwepo Goodluck

Wakili wa Serikali: Unawza Kutuambia Vile Vyumba vikoje

Vinatizamana au Vinaongozana

Shahidi: Milango ilikuwa tofauti

Jaji: chukulia Hiki ndiyo Chumba je ulipokuwa umekaa pale Mbweni Pakoje

Shahidi: afafanua Ramani ya Vyumba Mbweni

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Wakina Kingai lazima wapite kwenye Mlango wako wewe uliopo ili waingie,ni sahihi Hiko chumba Kimetenganishwa na Ukuta

Jaji: sasa Wakili unaeeza Kuendelea Kuanzia hapo kwenye ufafanuzi ,tumeshaelewa

Shahidi: Ni kweli

Wakili wa Serikali: Licha yakuwa Chumba Chako wewe na Alipokuwa Kingai Kimetenganishwa na Ukuta ila bado uliweza Kuwaona Wakiwa Chimba Cha Pili

Shahidi: Ndiyo

Jaji: kwahiyo palikuwa na Milango Miwili

Shahidi: Ndiyo na Mlango ulikuwa wazi tuh na haujafungwa

Jaji: naona Sasa waru wanasinzia,Kama watu wanajiskia Kujinyoosha Viungo namruhusu kusimama aende Maramoja Nje isije onekana nimezuia,Kama hakuna Tuendelee

Wakili wa Serikali: Mwenzako anasema alichukuliwa na kina Goodluck akapelekwa Kwenye Chumba alichokuwa Kingai wakakaa Kwenye Meza na Goodluck akiwa Amesimama Mlangoni,Je kati ya haya Mawili lipi ni la Ukweli

Shahidi: Nilisema Wakati anapelekwa Adamu Kule sikujua anapelekwa na nani na wakati gani

Wakili wa Serikali: Kama Limeletwa Mahakamani na hili unalozungumza lipinlenye Ukweli kati ya haya Mawili

Shahidi: najua ninalolisema

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Unasema ulimuona Kingai Wakati anaingia na Adamoo analosema Mbona Kinakinzana

Shahidi: Sikwepo mimi

Wakili wa Serikali: Kati yako wewe na Afamoo nani alitangulia Kuingia Kwenye Kile Chumba

Shahidi: Nilisema hapa Sijajua Adamoo aliingia Saa ngapi

Wakili wa Serikali: Wewe na Jumanne mlikuwa namfanya nini Mlendani

Shahidi: alikuwa ananiuliza Maswali

Wakili wa Serikali: Wakati anakuuliza Maswali Jumanne akili yako ulielekeza Kwa Jumanne na Kwamba Majibu yake uyatoe au usiyatoe

Shahidi: Ni kweli

Wakili wa Serikali: Wakati wa Kutolewa Adamoo Ulikuwa unaendelea na Zoezi la Kuulizwa Maswali na Jumanne

Shahidi: Ni kweli nilikuwa naulizwa

Wakili wa Serikali: Wakati unaulizwa Warrant of Arrest sijui na Warrant hayo Maswali unayakumbuka

Hakuna Ushahidi wowote unaohusiana na Arrest Warrant kuletwa haoa Mahakamani

Shahidi: ni kweli niliulizwa

Shahidi: Ndiyo nilijibu hivyo

wakili wa Serikali: Na wewe Ukajibu kuwa hujakiona wakati unakamatwa

Wakili wa Serikali: Unajua kuhusu Warrant Arrest

Shahidi: nikibali pale unapokuja Kunikamata Kama Polisi Kunionyesha Kibali ambacho kinakuruhusu Kunikamata

Shahidi: nikibali pale unapokuja Kunikamata Kama Polisi Kunionyesha Kibali ambacho kinakuruhusu Kunikamata

Wakili wa Serikali umejuaje kama Mru akikamatwa anatakiwa akuonyeshe Arrest Warrant

Wakili wa Serikali: Je unawezekana kwa Polisi Mtaani Ananiona namchoma Mtu kisu atatakiwa awe na Arrest Warrant.?

Shahidi: kwa Uelewa Wangu

Shahidi Siyo Polisi tuh ,Hata Mimi au Mtu yoyote anaweza Kukuzuia na Kukukamata

Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Siyo Mazingira yote Mtu anatakiwa akamatwe na Polisi kwa Arrest Warrant

Shahidi: Siyo Mazingira yote

Wakili Wa Serikali Chavula: Mheshimiwa Jaji naomba Niishie hapa nimuachie Mwenzangu

Wakili wa Serikali: Katuga Ling'wenya Ni kweli Adamoo ni Mtu wako wa Karibu

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: nikisikia umesema Umetoka naye Chalinze

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: ktk Ushahidi wako Umesema alikuwa na Tsh ngapi Mfukoni

Shahidi: hapana nilizungumzia Pesa zangi Mimi Mfukoni

Wakili wa Serikali: Ulipata Kufahamu alikuwa na Tsh ngapi Mfukoni

Shahidi: hapana sifahamu

Shahidi: Wakati huo nilikuwa nimeshaacha Kazi,Mambo ya kambini Jeshini siwezi Kuyafahamu tena Mbali kisaaaa

Wakili wa Serikali: Je unafahamu Adamoo alipata Battle Confusion

Wakili wa Serikali: Kwa Uelewa wako Battle Confusion ni Utovu wa Nidhamu Jeshini

Shahidi: Siyo Utovu wa Nidhamu

Wakili wa Serikali: umewahi kumuuliza nibsababu ipi iliyopelekea Kufukuzwa Kazini

Shahidi: Battle Confusion

Jaji:Ukissema Battle Confuse unamaanisha...

Shahidi: Battle Confusion

Wakili wa Serikali: Unakubaliana na Mimi uliachishwa kazi

Shahidi: Ndiyo niliachishwa kazi

Wakili wa Serikali: Sasa elezea Mafunzo yakobya Kijeshi pamoja na yale yaliyoongezeka Pale ya Ukomandoo,Unaweza Kuyatumia Uraiani

Shahidi: Ndiyo nayatumia,Kama Kuwa na Nidhamu,Kufanya Mazoezi

Wakili wa Serikali: Unaweza Kuyatumia Mazoezi yako Vinginevyo

Shahidi: Siwezi

Wakili wa Serikali: Hilo katazo unalipata wapi

Shahidi: Siwezi

Wakili wa Serikali: Hilo katazo unalipata wapi

Shahidi: ni ya Kibinadamu kuwa Utakiwi Kufanya Vitu Viovu Popote pale

Wakili wa Serikali: Katazo hilo lipo Jeshini.?

Shahidi: Ndiyo Jeshini Utakiwi Kufanya Maovu

Wakili wa Serikali:Uliulizwa Kuhusiana na Detention Register Na kwamba Ujawahi Kusaini kwenye hiyo Detention Register, ni kweli ulijibu hivyo.?

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: ulifahamu lini kwamba Ulitakiwa kusaini Katika Detention Register Mtuhumiwa unapokamatwa unapotakiwa Kuingizwa Mahabusu

Shahidi: Kwa Ufahamu wangu Popote kwenye Ofisi unapoingia na Kutoka unatakiwa kusaini unapotoka ,Nalitambua Kifikra na Ufahamu

Shahidi: si Lile Book unalolikuta amapokezi,Alillileta Mahakamani

Wakili wa Serikali hicho Kitabu Unakifahamu

Wakili wa Serikali: Kuna sehemu pale umeona Unatakiwa Kusaini

Shahidi: Sikuliona Mimi

Wakili wa Serikali: Kule Ulipopita ukiwa na Jumanne ukaja ukajua Kuwa Adamoo yupo ,akina Umbali gani

Shahidi: Nimeeleza Sana Mahakama Kwamba Ukiingia Mlango Mkubwa Unaanza Kuniona Mimi

Jaji: unaweza Kukadiria ni Umbali gani Kutoka Ulipokaa Mpaka kwenye hicho Chumba

Wakili wa Serikali: Utakubaliana na Mimi kuwa Kilichokuwa Mle ndani Ujui

Shahidi: Mheshimiwa Jai ni hatua Nne au Tano

Shahidi: nimeeleza Mahakama kilichojiri kwa Adamoo na Kingai Mle ndani siwezi Kujua

Wakili wa Serikali: Katika Ushahidi wako ktk Tukio la Kukamatwa pale Rau Madukani,Hakuna sehemu Yoyote Uliyosema Kwamba Askari wlikuuliza kama Unamfahamu Adamoo

Shahidi: Kwa Kumbukumbu zangu nilisema waliponishika Mkono wakaniuliza Kuwa Unamfahamu huyu

Wakili wa Serikali: Jana wakati Mallya anakuongoza alikuuliza Swali na Swali Lilikuwa Kuwa Kama Uliona Bastola au Madawa ya Kulevya ,Mpaka Adamoo akakuoa Ishara ulipata tatizo gani Kujibu

Wakili wa Serikali: Mapaka Mnenda Moshi Masharti ya kazi mlikuwa bado hamjapewa.?

Shahidi: Sikuona hiyo Ishara,Labda Ungenishtua

Shahidi: tulikuwa bado hatujapewa

Hadhana inaliaaaaaaaaa,Wote Kimyaaaaaaaaa*

Jaji:
tunaweza Kuendelea

Jaji: tuliishia Kama Masharti ya kazi walisha yapata

Wakili wa Serikali: Sasa kwa Sababu mlikuwa hamjapewa Masharti ya kazi ya VIP PROTECTION Ni Makubaliano gani mliyokuwa mmepewa Mpaka mnakuwa Moshi

Wakili wa Serikali: ujasema ni Tsh ngapi na Kwa nini,Si Ndiyo

Shahidi: tulikuwa tunajadiliana bado Kuhusu Malipo

Shahidi: Ndiyo

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji nihayo tuh

Jaji: nilipanga Tukomee Saa 10,Nitamuuliza Mallya kama zitatosha au tuhairishe akajiandae kwa Muda zaidi

Mallya: Mheshimiwa Jaji nitabakiza Tatu

Mallya: Shahidi Umeulizwa Kwamba Kingai kuna Maswali hakuulizwa

Jaji: Mallya

Wakili wa Serikali: OBJECTION Sioni Kama Swali lipo sawa

Mallya: Kwa Sababu ya Muda nitarudia Swali

Mallya: Umeanza Kutoa Ushahidi jana,Na Mpaka Leo Umejitokeza mambo Mawili Kuwa Ulitekwa na Ukakamatwa sasa isaidie Mahakama ichukue Jambo gani

Shahidi: Nilitekwa

Mallya: Uliulizwa Kuhusu Corridor,Path au Uchochoro Uliokwepo kwenye eneo lile,Hili Jambo lilitokeaje kwenye eneo lile

Shahidi: Kwa Uelewa Wangi Uchochoro ni Mwembamba lakini pale kwenye Corridor Nilipomaanisha ni Palubwa sana siyo padogo,Huku Maduka Huku Baa

Shahidi: Kwa Uelewa wangu ni Kitu Kimoja

Jaji: nimeona Swala hili Kila Mtu anatumia Bar au Glocery kwa Nchi yetu ni Sehemu Moja.?

Mahakama Kicheko

Mallya: Mheshimiwa Jaji Sina Swali Zaidi



Jamaa Kabakaisha Dakika Mbili

JAJI: nashukuru

Jaji: Nashukuru Shahidi Umemeliza

Jaji: wakili Mallya

Shahidi: Asante sana Mheshimiwa Jaji

Mallya: Tunaye shahidi Mwingine,Naomba Kesho tuendele na Ushahidi wake

Jaji: wakili wa Serikali

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi na Jambo hilo

Jaji: anandika Kidogo

Mahakama Kimyaaaaaaa

Kwa sababu ya Muda naihairisha Shauri mpaka kesho saa Kesho Saa Kamili Asubuhi tutakapoendelea Kumsikiliza Shahidi Kwenye Utetezi wa shauri Dogo

Jaji: Kwa Mara Nyingime nawashukuru wote kwa Kuendelea Kuwa watulivu

Jaji: ananyanyuka Polisi anapiga Kelele HIGH CORT
Hii kesi inatabirika kabisa, on face of records inaonekana mashahidi wamepikwa (coaching of witnesses) ambayo ethically haitakiwi.

Pili, kwenye kesi za jinai inatakiwa mlakamikaji athibitishe shtaka lake bila kuacha shaka yoyote (beyond reasonable doubts) lakini hadi sasa hivi matokeo 3-0 huku Mawakili wa Utetezi wakiongoza kwa goli 3 dhidi ya Mawakili wa Serikali. Kuthibitisha bila kuacha shaka si jambo dogo, vijana wa DPP wanaacha mashaka sana, na ikumbukwe this is grave offence (yaani Ugaidi).

Nashauri Jamhuri wasajili "Nolle" yaani kutotaka kuendelea na kesi au Jaji ajiongeze baada ya kuwasiliana na vijana wa DPP kwamba akishafunga ushahidi wa Jamhuri aseme washtakiwa hawana kesi ya kujibu (yaani no premafacie case has been established).

Otherwise, vijana wa DPP watazidi kujidhalilisha na kuidhalilisha ofisi ya mashtaka nchini na taaluma nzima ya Sheria.

Kama sikosei ni Jaji Siyani ambaye ni Jaji incharge wa kanda ya Dodoma anayeongoza kesi hii, na kwa ninavyomjua alivyotulia na anavyojua kujiratibu, wakina Mbowe wataachiwa huru, ni swala la muda tu.

Amicus Curiae.
 
Hii kesi inatabirika kabisa, on face of records inaonekana mashahidi wamepikwa (coaching of witnesses) ambayo ethically haitakiwi.

Pili, kwenye kesi za jinai inatakiwa mlakamikaji athibitishe shtaka lake bila kuacha shaka yoyote (beyond reasonable doubts) lakini hadi sasa hivi matokeo 3-0 huku Mawakili wa Utetezi wakiongoza kwa goli 3 dhidi ya Mawakili wa Serikali. Kuthibitisha bila kuacha shaka si jambo dogo, vijana wa DPP wanaacha mashaka sana, na ikumbukwe this is grave offence (yaani Ugaidi).

Nashauri Jamhuri wasajili "Nolle" yaani kutotaka kuendelea na kesi au Jaji ajiongeze baada ya kuwasiliana na vijana wa DPP kwamba akishafunga ushahidi wa Jamhuri aseme washtakiwa hawana kesi ya kujibu (yaani no premafacie case has been established).

Otherwise, vijana wa DPP watazidi kujidhalilisha na kuidhalilisha ofisi ya mashtaka nchini na taaluma nzima ya Sheria.

Kama sikosei ni Jaji Siyani ambaye ni Jaji incharge wa kanda ya Dodoma anayeongoza kesi hii, na kwa ninavyomjua alivyotulia na anavyojua kujiratibu, wakina Mbowe wataachiwa huru, ni swala la muda tu.

Amicus Curiae.
This post has been stared
 
What goes around comes around.Hao polisi hawawezi kufanya watachofanya hao wajeshi? Acha kuvichonganisha vyombo vyetu vya dola.
Hapa hachonganishwi mtu lakini kuna shida kati ya hivi vyombo vyetu vya ulinzi.

Halafu kwa nn mateso kiasi hicho wakati mahakama ilikuwa haijawatia hatiani.Au hawa polisi wako juu ya sheria😣
 
Back
Top Bottom