Afadhari umemjibu ,nisiku 7 unaweza savaivu nasio nne nje nahapo kue namajiAlisema sello kulikuwa na bomba la Maji so alikuwa anajisevia, soma vizuri mfululizo wa kesi sio unakuja kujamba tu humu jukwaani
Ndiyo hivyo tena, kwani akina Ben Saanane na wengine "unyama" ulikubalika?Kama Mosses Linjenje ni marehemu - ifahamike kwa wote kuwa - "Unyama huu haukubaliki."
Wewe na huyo Numbisa wako, naona kama akili zenu wote zinafanana vile. Tuufunge huu mjadala tafadhali.
Kawaida wanatakiwa wawe magaidi wangapi?wee hushangai nchi nzima magaidi watatu tu. upelelezi woote tangu mwaka jana watatu tu tena kwa ufadhili wa laki sita.
Huoni kuwa kimantiki ni maelekezo ya mtu mkubwa? tena lengo kuu likiwa kuangamiza upinzani kuanzia uchaguzi wa serikali za mitaa 2019. Huu ulikuwa mpango mkakakati na hii ni aibu tupu
Hivi hii kesi ikiisha na watuhumiwa wakaachiwa kwamba hawakuwa na kosa je hao polisi waliowatesa wanaweza kuchukuliwa hatua ?
Kwa hiyo Kingayi na wenzake wamemwua komandoo Linjenje!! Huenda Linjenje alikataa kukamatwa kama kuku, wakaamua wammalize! Mungu wa rehema, tunaomba, uipokee roho ya Linjenje, apumzike kwa amani, na wauaji wake walaanike Duniani na mbinguni.
Sasa naelewa kwa nini Hamza alifikia hatua ile. Hivi hili kweli ni Jeshi la Polisi au genge la wauaji na watesaji?
Siro, pamoja na kutokuendelea kufikia ngazi ya upadre, yale mafundisho ya dini, ukiwa mseminari, hayakuweza kukusaidia angalao kuwa tu muumini wa kawaida anayejitahidi kufuata maelekezo na mafundisho ya Mungu?
Hakika hawa wanastahili kufungwa jiwe la kusagia shingoni na kutupwa majini.
Alaanike sana kingayi kwa mauaji anayoyafanya. Haya ni machache tuliyobahatika kuyajua, lakini huenda kuna rundo la watu aliowaua.
What goes around comes around.Hao polisi hawawezi kufanya watachofanya hao wajeshi? Acha kuvichonganisha vyombo vyetu vya dola.Dah nimesoma hadi nakaribia kutoka machozi.
Yaani askar polisi anamtesa komandoo kwa sababu za kisiasa!!!
Ila hii mbegu aliyoipanda mwendazake isiporekebishwa kuna siku tutashuhudia mauaji kati ya hawa walinzi wetu.
Kwa mfano wajeda wakiambiana tusikubali udhaliliashaji na unyanyasaji waliofanyiwa wenzetu nyie polisi mutalala majumbani mwenu?
Kumbukeni hakuna maelewano mazuri kati yenu polisi na wanajeshi halafu mnaongeza majanga dah!
"Once a soldier is a soldier"
Kwasababu itakuwa haramu, siyo?Wakala wa shetani!Kuna aliyeita kule CCM Kuna magroup mengi na Kuna kazi za kufanya nenda huku
Msabato uone hata aibu ulicho kiandika Kati ya Mbowe na serikali nani anatapatapa ???Aibuuu halafu unajiita mkristo tena SDA .Umeandika iliupewe 7000/- nakuomba hiyo 7000/- usije ukaileta Kanisani Jumamosi kama sadaka
Point of correction, "once a soldier always a soldier".Dah nimesoma hadi nakaribia kutoka machozi.
Yaani askar polisi anamtesa komandoo kwa sababu za kisiasa!!!
Ila hii mbegu aliyoipanda mwendazake isiporekebishwa kuna siku tutashuhudia mauaji kati ya hawa walinzi wetu.
Kwa mfano wajeda wakiambiana tusikubali udhaliliashaji na unyanyasaji waliofanyiwa wenzetu nyie polisi mutalala majumbani mwenu?
Kumbukeni hakuna maelewano mazuri kati yenu polisi na wanajeshi halafu mnaongeza majanga dah!
"Once a soldier is a soldier"
Nitafurahi sana JWTZ nao wakaanza kiteka Police... finito hii haikubalikiKama Mosses Linjenje ni marehemu - ifahamike kwa wote kuwa - "Unyama huu haukubaliki."
Hii kesi inatabirika kabisa, on face of records inaonekana mashahidi wamepikwa (coaching of witnesses) ambayo ethically haitakiwi.Leo tena upande wa utetezi katika kesi ya Mbowe wanaendelea kutoa ushahidi wao katika kesi ndogo ya kesi kubwa ambapo leo tarehe 28/09/2021 Mtuhumiwa Lig'wenya anaendelea na ushahidi wake.
=======
Jaji: ameshaingia Sasa
Kesi namba 16 Inatajwa
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021,Jamuhuri dhidi ya Halfan Bwire,Adam Hassana Kasekwa (Adamoo), Mohammed Abdalah Ling'wenya na Freeman Aikael Mbowe
Watuhumiwa wanapandishwa Kuzimbani
Jaji: wakili wa Serikali
Robert Kidando
Abdallah Chavula
Nasoro Katuga
Easter Martin
Tulimanywa Majigo
Jenitreza Kitali
Wakili Peter Kibatala nayeye anatambulisha Orodha yake
Gaston Garubindi
Idd Msawanga
Bonifasia Mapunda
Evaresta Kisanga
Hadija Aron
Michael Mwangasa
Dickson Matata
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Nashon Nkungu
Jaji: Wote Mpo tayari kuanza?
Pande zote Mbili wamesema wapo tayari
Jaji: niombe apande Shahidi wapili ambaye alikuwa bado ajamaliza Kutoa Ushahidi wake
Shahidi: anapanda Kizimbani
Kimyaaaaa Kidogo
Jaji: wakili Nashon Nkungu
Nashon: ni kweli Kule Rau Madukani....
Jaji: aina hiyo ya Mswali Ndiyo inaletaga Utata
Nashoni: Ulipoluwa Madukani Ulikuwa unamuona Mshitakiwa wapili, Kweli si Kweli
Shahidi: Ni kweli
Nashon: Wakati tukio linatendeka ulikwepo.?
Shahidi: nilikwepo
Nashon: wakati tukio linatendeka Palikuwa na watu wengi wanashihudia.?
Shahidi: ndiyo palikuwa na watu wengi wanashuhudia
Nashon: Je hapa Mahakamani ulishawahibKuona Mtu yoyote aliyekuwa anashuhudia tukio
Shahidi: Hapana sijaona yoyote
Nashon: ulipokuwa Central Police Moshi, Je ulishuhudia taratibu za Kipolisi zilifanyika kama Kukuandikisha
Shahidi: Hapana Sijaiona
Nashon: Ulishawahi Kuona Detention Register Ya Mosho hapa Mahakamani.?
Shahidi: Hapana
Nashon: Kuna Shahidi alikuja anaitwa Detective Msemwa alisema aliwapokea Central Police Dar je Unamfahamu
Shahidi: Simfahamu
Nashon: Unasemaje kuhusu Maneno yake kuwa aliwapokea Central Police Dar,.Je unamfahamu.?
Shahidi: Simfahamu wala sijawahi Kufika Central Dar
Nashon: Unasemaje kuhusu Detention Register aliyokuja nayo hapa Mahakamani
Shahidi: sifahamu alitoa wapi
Nashon: Kuna sehemu yoyote katika Ile Detention Register ambayo amekuinyesha Ulisaini wakati wanakupokea
Shahidi: sikuona
Nashon: Wakati Dective Msemwa anatoa Ushahidi Anasema alikuwa na Afande Fatuma kama CRO incharge,Je ulishwa kumuina FATUMA hapa Mahakamani.?
Shahidi: Hapana
Nashon: ni Kweli Kwamba Wakati Mkiwa mnaelekea Mbweni walikwambia watakupoteza.?
Shahidi: Afande Goodluck aliniambia Tutakupoteza Kama Moses Lijenje
Jaji: alisema wakati gani
Shahidi: Wakati tunayoka Tazara kwenda Mbweni,Tukiwa kwenye Gari
Nashon: ulielewa nini Kwa Maneno tutakutupa..?
Shahidi: nilijua kuwa watanipoteza,Wataniua alafu hakuna atakaye jua nipo wapi
Nashon: nitakuwa sahihi Nikisema walikupa DEATH THREAT
Shahidi: ni sahihi kwa sababu niliona Moses tulikuwa naye Kweli Rau Madukani alafu ajulikani alipo na wala hatupo naye,nikajua wamemuua na watanifanyia kama yeye nilijisikia Vibaya
Jaji: je Wakili wa Mshitakiwa watatu Fredrick Kihwelo
Jaji: je Mawakili wa serikali Mnaona ni sawa
Fredrick Kihwelo: Sitokuwa na Swali Mheshimiwa Jaji
Jaji: je ni sahihi kwa yeye kuuliza swali kabla hatujafika kama atauliza au lah
Fredrick Kihwelo: nimeamua Kujinyima Haki Mheshimiwa
Jaj: sawa Wakili wa Mshitakiwa wa Nne
Kibatala: Kitendo cha Kugongwa gongwa na Bastola na kukwambia watakutupa,Je tishio liliongezeka Moyoni Mwako kutokana na yalivyo kuwa yameshatokea kabla..?
Shahidi: Hofu ilizidi kuwa Kubwa Kufuatia Kilichokuwa Kimeshatendeka Moshi
Kibatala: Moses Lijenje unamfahamu wakati unaambiwa hayo maneno
Shahidi: Ndiyo nilikuwa namfahamu tulikuwa naye pale Rau Madukani
Kibatala: haiba yake ni nani
Shahidi: alikuwa Mwanajeshi Wa 92 KJ lakini wakati yeye akiwa Mwanajeshi pale mimi nilikuwa bado sijaanza kazi
Kibatala Wakati kesi inaendelea hapa Uliwahi Kusikia kuwa nayeye ni Mshitakiwa.?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Ulishawahi Kusikia kuwa watamleta baadae
Shahidi: Hapana
Kibatala: Pale Rau Moshi Mkiwa Pale,hawa wakati wanamkamata Adamoo ulisikia Askari yoyote anasema ana HATI YA UKAMATAJI
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati unaingilia Ukamataji wa Adamoo,Uliskia Askari Polisi yoyote hasa Kingai Kuwa Tafadahali Usiingilie zoezi la Ukamataji , Kwa sababu za Kisheria.?
Shahidi: Hapana sijasikia
Kibatala: Uliwahi Kumsikia hapa Mahakamani Kingai ametoa Warrant of Arrest (Hati ya Ukamataji)
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati wa Ushahidi Mahita alisema Kingai ndiyo alikuwa akiongozi wao
Shahidi: Ndiyo nilimsikia
Kibatala: Kingai tangu wanatoka Arusha walisema walikuwa wanafahamu wanaenda Kumkamata Adamoo kwa Tuhuma za Ugaidi
Shahidi: Ndiyo nilisikia hivyo
Kibatala: lakini alipokuja hapa alishawahi Kutoa Ruhusa ya Mahakama kwamba wanaenda Kumfanyia Adamoo kitu fulani.?
Shahidi: Hapana Sikusikia
Kibatala: Adamoo alitekwa au Alikamatwa
Shahidi: alitekwa
Kibatala: Kwanini ulikumbuoa mambo ya Rau Madukani Mpaka Maduka ya Mtu na Mpaka Majina ya ya Mwenye Duka
Shahidi: Mimi ndiye niliyemshauri Adamoo twende pale kwa Sababu nilikuwa na Dada yangu na pale ni sehemu ya familia
Kibatala: Umeweza Kufafanua Mpala kutuchorea picha Kwasababu ni Mambo uliyowahi kuyaishi
Wakili wa Serikali: OBJECTION Shahidi ajasema kuwa amewahi Kuishi Rau Madukani
Kibatala: sijasema ameishi Rau Madukani, Nimesema ameeleza Kwa sababu Maelezo yake ameyaishi
Jaji: wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: hilo neno kuyaishi Mbeleni linawezakutumika Vibaya
Jaji: Kibatala
Kibatala: Wacha nibadirishe swali kwa Sababu ya Muda
Kibatala: Wakati Kingai anasema aliwakuta Kwenye kibanda Umiza alitaja Jina.?
Shahidi: Hakutaja Jina
Kibatala: tofauti na Kingai,Wewe umetaja Mpaka Jina
Shahidi: nimetaja Mpaka Jina
Wakili Kibatala: nilisikiabkuwa wakati Unakamatwa ulitoa Vitu Vyako ukaweka Kwenye Kibaraza cha huyo Dada,Nilisikia Vizuri.?
Shahidi: upo sahihi
Kibatala: Je ungejisikia Vizuri kama yule Dada angekwepo wakati wa Ukamataji wako kwa Sababu alikwepo Dukani
Shahidi: Ndiyo ningepata Amani zaidi kama angekuwa Shaidi
Jaji: jana Ulisema Adamoo amekamatiwa wapia
Shahidi: Kati kati ya Glocery na Flemu za Madukani
Jaji: unaweza sasa Kuendelea Kumjibu wakili
Shahidi: Ndiyo ningejisikia Vizuri kama Dada yangu angekwepo
Jaji: unamaanisha Athma
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati wanamshambulia Adamoo hao Askari walikuwa na Silaha
Shahidi: hawakuwa na Silaha,labda wa Nje Kwa sababu katika Ukamataji kwa ufahamu wangu kuna "Inn and Outer" labda walifunga Nje ndiyo walikuwa wamezunguka eneo lile au waliokuja baadae
Kibatala: kwanini unasema Adamoo hakuwa na Bastola wakati wa Ukamataji kwa uhakika
Shahidi: kwa sababu Adamoo nimesafiri naye,Nimelala naye Chumba Kimoja na Tukatoka kuja wote kwa Dada yangu. na Koti ndiyo alikuwa ametoka Kulinunua
Kibatala: Kwa Ufahamu wako ile Bastola imetoka kwa nani.?
Shahidi: kwa Jumanne,Ndiye aliyesema ana bastola na watu walikuwa wamejaa Sana
Kibatala: kwa Ulivyoshuhudia Ule siyo Ukamataji ni Ugomvi
Shahidi: siyo Ukamataji ni Ugomvi
Kibatala: Shahidi umesema Jumanne alimuweka Adamoo Madawa,ulijuaje kuwa yale ni Madawa
Shahidi: kwa sababuJumanne ndiye aliye tamka kama alivyo tanka anapistol ndiyo alitamka Ana madawa
Kibatala: kwanini unaamini Adamoo hakuwa na Madawa ya Kulevya
Shahidi: Mimi ndiye niliyemshauri Adamoo twende pale kwa Sababu nilikuwa na Dada yangu na pale ni sehemu ya familia
Kibatala: Umeweza Kufafanua Mpala kutuchorea picha Kwasababu ni Mambo uliyowahi kuyaishi
Wakili wa Serikali: OBJECTION Shahidi ajasema kuwa amewahi Kuishi Rau Madukani
Kibatala: sijasema ameishi Rau Madukani, Nimesema ameeleza Kwa sababu Maelezo yake ameyaishi
Jaji: wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: hilo neno kuyaishi Mbeleni linawezakutumika Vibaya
Jaji: Kibatala
Wacha nibadirishe swali kwa Sababu ya Muda
Kibatala: Wakati Kingai anasema aliwakuta Kwenye kibanda Umiza alitaja Jina.?
Shahidi: Hakutaja Jina
Kibatala: tofauti na Kingai,Wewe umetaja Mpaka Jina
Shahidi: nimetaja Mpaka Jina
Wakili Kibatala :nilisikiabkuwa wakati Unakamatwa ulitoa Vitu Vyako ukaweka Kwenye Kibaraza cha huyo Dada,Nilisikia Vizuri.?
Shahidi: upo sahihi
Kibatala: Je ungejisikia Vizuri kama yule Dada angekwepo wakati wa Ukamataji wako kwa Sababu alikwepo Dukani
Shahidi: Ndiyo ningepata Amani zaidi kama angekuwa Shaidi
Jaji: jana Ulisema Adamoo amekamatiwa wapia
Shahidi: Kati kati ya Glocery na Flemu za Madukani
Jaji: unaweza sasa Kuendelea Kumjibu wakili
Shahidi: Ndiyo ningejisikia Vizuri kama Dada yangu angekwepo
Jaji: unamaanisha Athma
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati wanamshambulia Adamoo hao Askari walikuwa na Silaha
Shahidi: hawakuwa na Silaha, labda wa Nje Kwa sababu katika Ukamataji kwa ufahamu wangu kuna "Inn and Outer" labda walifunga Nje ndiyo walikuwa wamezunguka eneo lile au waliokuja baadae
Kibatala: kwanini unasema Adamoo hakuwa na Bastola wakati wa Ukamataji kwa uhakika
Shahidi: kwa sababu Adamoo nimesafiri naye,Nimelala naye Chumba Kimoja na Tukatoka kuja wote kwa Dada yangu. na Koti ndiyo alikuwa ametoka Kulinunua
Kibatala: Kwa Ufahamu wako ile Bastola imetoka kwa nani.?
Shahidi: kwa Jumanne,Ndiye aliyesema ana bastola na watu walikuwa wamejaa Sana
Kibatala: kwa Ulivyoshuhudia Ule siyo Ukamataji ni Ugomvi
Shahidi: siyo Ukamataji ni Ugomvi
kibatala: Shahidi umsema Jumanne alimuweka Adamoo Madawa,ulijuaje kuwa yale ni Madawa
Shahidi: kwa sababuJumanne ndiye aliye tamka kama alivyo tanka anapistol ndiyo alitamka Anamadawa
Kibatala: kwanininunaamini Adamoo hakuwa na Madawa ya Kulevya
Shahidi: kwa sababu Adamoo nilikuwa naye kwa kila hatua na alikuwa Mgeni kule Moshi, Ndiyo maana nilimpeleka kwenda Kumtembelea Dada Yangu
Kibatala: Unasemaje Madai ya Mahita kuwa walipowakamata walianza Kuwachukua Muwatembeze Maeneo Mbali kamaViongoza Njia katika Kumtafuta Lijenje
Shahidi: Ni Uongo
Kibatala: husianisha Sasa Swala la Ugeni wa Adamoo na jambo la Mahita kwamba aliwatumia kama Viongoza Njia
Shahidi: ni Uongo kwa sababu Adamoo alikuwa Mgeni afahamu eneo Lolote
Wakili wa Serikali: OBJECTION Shahidi anaulizwa Maswali yanayompeleka Kutoa Opinioni zake, Jambo hili ni Kinyume na Sheria ya Ushahidi
Jaji: unaweza Kusoma hicho Kifungu
Wakili wa Serikali ,anasoma.................
Jaji: Kulingana na Ulichokisoma umaanisha nini kwa neno Persive
Jaji: Kibatala Kama kweli angerejea sheria angetumia Kifungu cha 62 (c) kwa Maoni yangu Shahidi anaulizwa Perception yake yeye,Very strait
Jaji: wakili wa Serikali Sisi tunaendelea Kusisitiza Hilo swali lisiruhusiwe, Kwenye Ushahidi tunaona ni Jambo ambalo si sawa
Jaji, nimewasikiliza pande zote Mbili mimi naona Kuwa Kifungu cha 62 (c) kinaruhusu Shahidi Kutoa Mtazamonwake Kuhusu Jambo analoyolea Ushahidi
kibatala: haya elezea Sasa Unahusinisha Vipi Ugenibwa Adamoo na Maelezo ya Mahita ya kuwatumia kama Viongoza njia
Shahidi: Ni Uongo Adamoo alikuwa Mageni Moshi tulifika Sikubya kwanza, Siku ya Pili,siku ya tatu tunakamatwa
Kibatala: Kingai anasema aliwachukua wadada wawili Mpaka Central Kwenda Kutoa Maelezo je ulishihudia.?
Shahidi: Sikushuhudia
Kibatala:Je Wallet yako na Simu yako Ulisikia Afande Kingai au Mahita kuwa Vifaa Hivyo viliingizwa Kwenye Register Moshi.?
Shahidi:Sikusikia
Kibatala: Mashahidi hao wawili pia walizungumzia Hati ya Uchukuaji wa Vielelezo CERTIFICATE OF SEIZURE je ulisikia
Jaji: Kiswahili Chake Kikosawa
Jaji: tafiri iwe Hati ya Kuhodhi Mali
Kibatala: Ulisikia Kuwa Pistol,Madawa ya Kulevya na Vitu vyako ulisikia kama Viliingizwa kwenye Hati ya Kuhodhi Mali
Shahidi: Sikusikia
Kibatala: Bila shaka Kile kitabu cha Komito Unacho,Je umewahi Kuona Mle Kuna Sehemu yoyote Imeandikwa kuhusu Madawa ya Kulevya
Shahidi: Hapana Hakuna na sijaona
Kibatala: Moaka Leo unatoa Ushahidi hapa Mahakamani uliwahi kusikia au Kuona Adamoo alipatatikana na Madawa ya Kulevya.?
Shahidi: Sijawa Kusikia wala Kuona
Kibatala: Uliwahi Kushuhudia Kuwa Adamoo wamemchukua Sampuli ya mwili wake kwa ajili ya Kwenda Kupima utumiaji wa Madawa ya Kulevya
Shahidi: sijawahi kuona
Kibatala: Uliwahi Kushudia Adamoo akipewa hati ya kumiliki Mali
Shahidi: sikuwahi Kushahidi
Kibatala: uliwahi Kupewa hati ya Kumiliki Mali
Shahidi: Hapana sijawahi
Kibatala: Uliwahi Kushudua Adamoo akipewa nafasi wa Kushuhudia wakatibakitoa Maelezo pale Moshi
Shahidi: Hapana sijawahi
Kibatala:Uliwahi wewe Kupewa nafasi ya Kumyita Shahidi wa Kushudia wakati Ukitoa Maelezo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unauhakika gani Kuwa Adamoo alifanyiwa Mateso akiwa Moshi Polisi Central Station
Shahidi: niliwahi Kumuona Adamoo akiwa anaburutwa,na Baadae wakawahi Kunipiga Kitambaa,lakini nilishawahi Kuona
Kibatala: hayo yanaweza Kuwa ni Matokeo ya Adamoo Kuteswa ,Je ulishuhudia Vipi kuwa Adamoo anateswa
Shahidi: Nilislia Kilio cha Adamoo kwa Sababu Sauti ya Adamoo naijua nilikuwa mwalimu wake katika kozi za Ukomandoo,Nilikuwa namuita Sauti ya Zege tangubakiwa Mwanafunzi wangu 92 KJ
Kibatala: kumbe wewe ni Mwalimu wa Adamoo.?
Shahidi: Ndiyo Mwalimu Mzuri sana
Kibatala: Ukiwa kama Mwalimubwa Adamoo ulishawahi Kusikia anatumia Madawa ya Kulevya
Shahidi: Hapana
Kibatala: ungesikia Adamoo anatumia Madawa Ya Kulevya wakati Mkiwa Jeshini Utaratibu unakuwaje
Shahidi: hayo ni Mambo yakushughulikiwa na Millitary Police
Kibatal:a Mwambie Mheshimiwa Jaji jambo Lingine unalothibitsha kuwa yale Mateso yalikuwa ni ya Adamoo
Shahidi: kwa sababu hata tulipokuwa Cello tuliongea akaniambia ,poa tuh ila mikazo tuh,Nikamwambia na Mimi hivyohivyo,Ila navumilia
Jaji: Unaposema Poa ila Nikazo maana yake nini.?
Shahidi: Kwamba tumeumia ila tunajitahdi Kuvumilia
Kibatala: nakutoa Moshi nataka kwenda Kwenye kusafiri nilisikia unasema wewe ulisafiri na Adamoo kwenye gari Moja
Jaji: ni kweli ulisema wewe na Adamoo mlisafiri kwa gari Moja.?
Shahidi: hapana sifahamu nilihisi tuh kwa sababu sikuona
kibatala: Sasakwa Ufahamu wako wa Kawaida Ulisafiri naye au hukusafiri naye
Shahidi: kama nilivyosema sikuona akipanda ila niliskia Nyuma Buti limefungukiwa anakapndishwa Mtu,Kwa fahamu zangu naweza Kusema tulisafiri naye
Kibatala: katika hisia za Kusafiri naye hapohapo ni kweli Kwamba Gari ilisimama.Sehemu mkala
Shahidi:Hapana ni Uongo
Kibatala: kwamba Gari mkiharibika Mkasimama na Kubadili gari nikweli Usingefahamu..?
Shahidi: Nisingefahamu Japo kuwa nilikuwa nimefungwa Kitambaa,Kakini gari ikisimama nafahamu
Kibatala: Kumbukumbu yako Wakati Shahidi anawapokea Pale Central alisema aliwapokea Kwenye gari Moja.?
Shahidi: kwa Kumbukumbu zangu alisema tulifika pamoja
Shahidi: Kwa Mkupuo mmoja
Kibatala: je kwa mkupo Mmoja au Tofauti Tofauti.?
Kwa Ufahamu wako Nani alikuwa anawapa wenzie Amri tangu huko Moshi
Shahidi: Kingai
Kibatala: Umefanya kazi Jeshini,Mwambie Mheshimiwa JajibKwenye Msafara pakiwa na Senior Officer na Junior Officer Inawezekana vipi Junior Officer Kutoa Amri.?
Kibatala: Inaezekana Vipi Shahidi watatu kwa Maneno yake kwamba alikabidhiwa Watuhumiwa na Junior Officer wakati Kingai Alikwepo
Shahidi: haiwezekani
Shahidi: Haiwezekani,Kwa sababu Kingai alitakiwa kutukabidhisha kwa sababu alikwepo
kibatala: Ulisikia akisema alipokea Chochote kile ili akiingize kama Kidhibiti kwa Kujibu wa sheria
Shahidi: Sikumsikia
Shahidi: Hapana sikusikia
Kibatala: Rudi Tazara ACP kingai alikiri Kuwa Mlienda Mbweni ila hamkwenda Tazara,Je unathibitishaje kuwa Mlienda Tazara
Shahidi: Natihibitisha kwa sababu nilimuona Alex na Chuma Chungulu ambao nilikuwa nao Jeshini,Nathibitisha kwamba Ilikuwa Tazara
Kibatala: Ulijisikiaje safaribyote Kutoka Moshi Mpaka Dar es salaam Ukiwa Umefungwa Pingu
Shahidi: Nilijisikia Vibaya
Kibatala: na Ukahisi nini
Shahidi: Mateso
kibatala: kwa Ufahamu wako Umesema ulipokuwa Tazara ulishuhudia nani alikuwa ametoka kuteswa.?
Shahidi: Denis Urio
Kibatala: Kwenye Kitabu Cha Komito ulimuona ni Shahidi wangapi wa Mashtaka
Shahidi: Shahidi wa Tatu
Kibatala: Urio aliwahi Kukutembele Gerezani ujue kuwa Yupo huru.?
Shahidi Hapana
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Unamfahamu Vizuri Denis Urio
Shahidi: Ndiyo ni Mwalimu wangu kabisa wakati naingia Jeshini,na mimeishi naye achumba Kimoja Nikowa kwenye Misheni DARFUR SUDAN
kibatala: uliwahi kwenda sudani na Wapi Kwa Misheni za Kikazi
Shahidi: CONGO
kibatala: unathibitisha Vipi Kwamba Mwenzako Adamoo alikwepo Tazara
Kibatala: Nakutoa Tazara nakurudisha Mbweni,Kuna sehemu unasema Kuwa Ulimuona Kuwa Kingai alikuwa ameingia Kuna kachumba Fulani
Shahhid: Baada ya Mahabusu wenzangu Kusema Mwenzako yupo,Niliita Adamoooooo na akaitaika
Jaji: wapi
Kibatala: Mbweni
Shahidi: palikuwa na Vyumba Vitatu,Mimi niliwekwa kwanza kwenye Chumba cha Kwanza, Kingai akaingia kwenye Chumba Kinachofuata
Jaji: Subiri Kidogo
Jaji: Subiri Kidogo
Jaji :Ukamuona Kingai naingia
Shahidi: Kingai alipoingia akapitiliza Mlangowa Chumba cha Pili, Mimi nilikuwa Chumba cha kwanza Nipo na Jumanne
Kibatala: Goodluck alikuwa ameshika Kitu chochote
Shahidi: alikuwa ameshika Bastola
Kibatala: Kwa Uelewa wako Batola ilikuwa na maana gani
Shahidi: ilikuwa kunitishia na Kutaka kunifanyia Kitendo chochote,kama alivyosema Kunitupa
Nikiwa palepale nilimuona alikuwa Adamoo akitolewa katika Kile Chumba
Kibatala: alikuwa na hali gani
Shahidi: alikuwa amechoka sana na hajala
Kibatala: Ulijuaje kama hajala
Shahidi: Kama mimi sikuwa nakula nayeye pia alikuwa ajala
Kibatala: Hukula kwa siku ngapi
Shahidi: Sikuwa nimekula kwa Muda wa siku 10 Kuanzia tarehe 09 Mpaka tarehe 08 tarehe 09 Mpaka 19 Mwezi wa Nane,Chakula tulienda Kupewa Mahakamani
Kibatala: Inakuwaje Mtu akae Siku zote hizo bila Chakula
Shahidi: walikuwa wanawahudumia Mahabusu Wengine
Jaji:Mahakamani nani alikupa Chakula Mahakamani
Shahidi: Afande Goodluck alileta Ugali na Dagaa na hapo tulishakuwa wengi tayari
Kibatala: inakuwa Ngumu mimi kuamini Kuwa hukula kwa siku 10te 10
Shahidi: Ndiyo ni kweli sikula Chakula
Kibatala: Je maji
Shahidi: Chumba Changu Cha Mahabusu palikuwa na Bomba la maji ndiyo kilichonisaidia
kibatala: ukisema Chakula unamanisha nini.?
Shahidi: Chakula cha Mahabusu,kama wenzetu maana walikuwa Wanatuambia kuwa hawahusiki na sisi Chakula Chao wanawapa Mahabusu wao tuh
Kibatala: Sasa Ikawaje
Shahidi: Yule Afande sasa tuliyejenga naye Urafiki ndiyo alikuwa ananiletea Biscuit na Soda ua Maji special na Pia nilikuwa namuomba ampe Maagizo Adamoo
kibatala: Sasa tunaenda Sawa
Kibatala: Wakati wote Umefungwa Pingu ,ilikuwa Rahisi au Ugumu kiasi gani wakati wa kujisaidia
Shahidi:. .... .... ....
Kibatala: Asante Mheshimiwa Jaji nilikuwa nazingatia hilo
Jaji: Wakati tunasubiri Majibu ya shahidi,Nashauri tujikite sasa kwenye nini hasa Kilitokea wakati wa akumvhujua Maelezo Mashtakiwa wa Pili,
Kibatala: Wakati wote Mkiwa rumande Mwambie Mheshimiwa Jaji kuwa kama Mlishawahi Kupelekwa Hospotali
Shahidi: Hapana
Kibatala: ni hayo tuh Mheshimiwa Jaji
Jaji:ninatumaini sijakuzuia
Kibatala: Hapana Mheshimiwa Jaji nimemeliza tuh
Jaji Naomba tubreak Kwa Dakika 15 Kwa Afya Zetu
Jaji anatoka Sa 4 na Dakika 54
Tumesharudi Mahakamani watu wote
Jaji ameshaingia
Kesi inatwajwa tena
Wakili wa Serikali: Tupo tayari Kuendelea
Jaji: Utetezi Mpo tayari.?
Kibatala: Tupo tayari
Wakili wa Serikali: Chavula anaendelea
Jaji: Shahidi nakukumbusha Kuwa bado Upo Chini ya Kiapo
Wakili wa Serikali: Wewe ni Mohammed Abdilah Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: wewe ni Komandoo
Shahidi: Ndiyo
Jaji: Umeacha Kuwa Komandoo
Mahakama Kicheko
Wakili wa Serikali: Ujeshi Ukomandoo haufutiki
Shahidi: Ndiyo ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamsahrti yake.? yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya
Shahidi: Rudia swali
Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamasharti yake.? Yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya
Miiko inakufunga bado
Shahidi: Wakati nipo Kwenye Himaya ya Jeshi
Wakili wa Serikali: Kuna Miiko ya Kijeshi ya hutakiwi Kuongea
Shahidi: kama Yapi
Wakili wa Serikali: Wewe ndiyo utuambie
Shahidi: Wewe ndiyo umeyaleta Ndiyo Utuambie sasa
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo kule Jeshimi si Kuna Miiko hata Ukimatila Jeshini utakiwi kuyaeleza
Shahidi: Siyo sahihi
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Jeshini kozi ya Komandoo ulikula Kiapo
Shahidi: Kiapo gani
Wakili wa Serikali: si Ulikula Kiapo,je nikiapo gani
Shahidi: Nitalitumiakia Jeshi Mpaka Kufa
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unatumikia Jeshi Kwa Mambo gani
Wakili wa Serikali: Kingime lipi ulikuwa unafanya Jeshini
Shahidi: Kulinda Nchi,Kulinda ,Silaha,Vifaa na Amani ya Ndani na Nje ya Nchi
Shahidi: Force Keeping Congo
Jaji:Focrce Keeping Maana yake nini
Shahidi: tulikuwa tunaforce amani Congo
Jaji: unaw3leza Kutofautisha Peace Keeping na Peace Keeping
Shahidi: Moja Sudani Hatutakiwi Kupigana na Waasi Mpaka watuonyeshee silaha /Mtutu lakini Congo tulikuwa tunatoka tunaenda sehemu kama Tunguu kwa Maelezo kuwa yoyote tutakaye mkuta Tunapigana au Kumuua
Wakili wa Serikali: ni sahihi nikisema Kuwa yna Degree Sita za martial Arts
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe Mwalimu gani ujui Martial Arsts,Wewe Unafundisha nini
Shahidi: Siyo sahihi
Shahidi Nafundisha kuruka na parashuti,Kupigana Juu ya Maji kwa kutumia silaha na Combats
Wakili wa Serikali kwa hiyo wewe unafahamu kupigana Karates
Shahidi nafahamu
Jaji: Naona Hamuelewani Wakili uliza kwa Yale Mambo ya kawaida hayo ni Mambo ya Kijeshi
Wakili wa Serikali: Nilifikiri ni Mwalimu atakiwa anajua Mambo yote
Wakili wa Serikali: Kipindi Cha Muda Gani ulitumia kujifunza Kupigana katares Mpaka ukaweza
Jaji: Ndiyo Mwalimubwa amambo ya Jeshi siyo Kiswahili
Shahidi: Miezi Sita ya Kozi,92K
Naomba tubreak Kwa Dakika 15 Kwa Afya Zetu
Jaji: anatoka Sa 4 na Dakika 54
Tumesharudi Mahakamani watu wote
Jaji: ameshaingi
Kesi: inatwajwa tena
Wakili wa Serikali: Tupo tayari Kuendelea
Jaji: Utetezi Mpo tayari.?
Kibatala: Tupo tayari
Wakili wa Serikali: Chavula anaendelea
Jaji: Shahidi nakukumbusha Kuwa bado Upo Chini ya Kiapo
Wakili wa Serikali: Wewe ni Mohammed Abdilah Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: wewe ni Komandoo
Shahidi: Ndiyo
Jaji: Umeacha Kuwa Komandoo
Mahakama Kicheko
Wakili wa Serikali: Ujeshi Ukomandoo haufutiki
Shahidi: Ndiyo ni sahihi
Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamsahrti yake.? yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya
Shahidi: Rudia swali
Wakili wa Serikali: Ukomandoo na Uanajeshi si unamsahrti yake.? yapi ya Kufanya na yapi siyo ya Kufanya
Miiko inakufunga bado
Shahidi: Wakati nipo Kwenye Himaya ya Jeshi
Wakili wa Serikali: Kuna Miiko ya Kijeshi ya hutakiwi Kuongea
Shahidi: kama Yapi
Wakili wa Serikali: Wewe ndiyo utuambie
Shahidi: Wewe ndiyo umeyaleta Ndiyo Utuambie sasa
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo kule Jeshimi si Kuna Miiko hata Ukimatila Jeshini utakiwi kuyaeleza
Shahidi: Siyo sahihi
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Jeshini kozi ya Komandoo ulikula Kiapo
Shahidi: Kiapo gani
Wakili wa Serikali: si Ulikula Kiapo,je nikiapo gani
Shahidi: Nitalitumiakia Jeshi Mpaka Kufa
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unatumikia Jeshi Kwa Mambo gani
Wakili wa Serikali: Kingime lipi ulikuwa unafanya Jeshini
Shahidi Kulinda Nchi,Kulinda ,Silaha,Vifaa na Amani ya Ndani na Nje ya Nchi
Shahidi Force Keeping Congo
Jaji: Focrce Keeping Maana yake nini
Shahidi: tulikuwa tunaforce amani Congo
Jaji: unaweleza Kutofautisha Peace Keeping na Peace Keeping
Shahidi: Moja Sudani Hatutakiwi Kupigana na Waasi Mpaka watuonyeshee silaha /Mtutu lakini Congo tulikuwa tunatoka tunaenda sehemu kama Tunguu kwa Maelezo kuwa yoyote tutakaye mkuta Tunapigana au Kumuua
Wakili wa Serikali: ni sahihi nikisema Kuwa yna Degree Sita za martial Arts
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe Mwalimu gani ujui Martial Arsts,Wewe Unafundisha nini
Shahidi: Siyo sahihi
Shahidi: Nafundisha kuruka na parashuti,Kupigana Juu ya Maji kwa kutumia silaha na Combats
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe unafahamu kupigana Karates
Shahidi: nafahamu
Jaji: Naona Hamuelewani Wakili uliza kwa Yale Mambo ya kawaida hayo ni Mambo ya Kijeshi
Wakili wa Serikali: Nilifikiri ni Mwalimu atakiwa anajua Mambo yote
Wakili wa Serikali: Kipindi Cha Muda Gani ulitumia kujifunza Kupigana katares Mpaka ukaweza
Jaji: Ndiyo Mwalimubwa amambo ya Jeshi siyo Kiswahili
Shahidi: Miezi Sita ya Kozi,92Kj
Wakili wa Serikali: Ulikaa Miezi sita 92KJ ukijifunza kupigana karates
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulifanya Phase ngapi.?
Wakili wa serikali: ni sehmu Gani Nyingine ulienda Kupata Mafunzo ya karates
Shahidi: phase Moja,Mengine niliyapatia Mahala pengine
Shahidi: nilienda Kujifunza Kick Boxing kwa Wafaransa
Wakili wa Serikali: Kwa Miezi Mingapi
Shahidi: Miezi Mitatu
Wakili wa Serikali: Kozi Nyingine ilikuwa ni nini.?
Shahidi: Kuzuia Uharamia
Shahidi: Sijui wewe
Wakili wa Serikali: Uharamia ni nini
Jaji: tudaidie kama Unaufahamu wowote kwa sababu wengine hatujui ila tumesikia sikiasikia
Shahidi: kwanza Ni Navy kwa Maana kuna kupambana Majini
Shahidi: Mapigano kwenye Majumba
Wakili wa Serikali: Kozi Nyingine
Wakili wa Serikali: Kwa Muda gani
Wakili wa Serikali: Kwa Muda gani
Shahidi: Kwa Miezi Mitatu
Wakili wa Serikali: Kwenye Majumba mnakuwa Mnampiga nani
Shahidi: Jinsi ya Kumtoa Adui Kwenye Majumba
Wakili wa Serikali: hayo Mapigano ya kwenye Majumba ,ni yepi uliyojifunza,Mieleka,ngumi...
Shahidi: Kutumia Silaha
Wakili wa Serikali: Silaha Zipi
Shahidi Kisu,SMG
Wakili wa Serikali Pamoja na Panga
Shahidi: panga sijataja
Wakili wa Serikali: Kisu ulifundishwa namna ya Kukitumia
Shahidi: kisu nilifundishwa
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo ulifundishwa kupigana kutumia Mikono
Shahidi: Mheshimiwa Jaji nimeshalijibu swali anarudia tena
Jaji: na mimi naona unarudia tena
Wakili wa Serikali: Hukufundishwa Kupambana na Maadui wako kwa Kutumia Miguu au Mikono
Shahidi: sikufundishwa
Wakili wa Serikali: Katila kozi ya wafaransa ulipata Kujifunza Kickboxing
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kwahiyo baada ya Mafunzo hayo unauwezo wa akukabiliana na Adui Mahala Popote anapotokea,Kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Kwa kuchukuliwa kufanya kazi 92KJ wewe Umeaminika Sana,Kweli au Si Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Na Nidhamu yako ni Yajuu sana Kweli ama si Kweli
Shahidi: Si kweli
Jaji: Ndiyo
Wakili wa Serikali: ili ndani ya 92KJ uoate Bahati ya Kuwa Mwalimu,ni kwamba kwenye Mafunzo uliyopita Umefanya Vizuri kwa kiwango cha Juu
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe ni Mahiri sana
Shahidi: Kweli
Shahidi: kwa Wastani
Wakili wa Serikali: Mafunzo ulikuwa umefaulu ukaambiwa kawafundishe wenzio
Shahidi: Sikuambiwa hivyo,Jina lilitoka kwenda Starter nikatakiwa kwenda Kuwa Mkufunzi
Wakili wa Serikali: Ili uwe Mkufunzi unatakiwa uwe na Sifa gani
Shahidi: sijuibwakubwa wenyewe, lakini wanakaa kikao na inatoka ORDER kuwa Jina limetoka Kuwa Mkufunzi
Wakili wa Serikali: Umekuwa Mwalimu kwa Muda gani
Shahidi: Mwaka Mmoja
Wakili wa Serikali: bila shaka uliokuwa unawafundisha ulikuwa na maelewano mazuri na wao
Wakili wa Serikali: na Bila shaka wanafunzi wako walifaulu Vizuri
Shahidi: Kweli
Shahidi: Ndiyo walifaulu
Wakili wa Serikali: na wengibwa wanafunzi wako Mlikuwa mkielewana sana
Shahidi: Ndiyo tulikuwa tunaelewana
Wakili wa Serikali: wengi wao walikuwa na upendo na wewe
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Wale wanafunzi wako ukiachana na Adamoo Kuna waliokuja kukutembelea
Shahidi: hapa sijaona,ila walikuwa wanakuja Segerea
Wakili wa Serikali: Taja ni nani alikuwa anakuja kukutembelea
Shahidi: ni One Two One
Mallya: OBJECTION wakili anakoelekea Kutaka kutajana Majina ambayo tena ya wanajeshi,Wengine tulishaomba MAHAKAMA wale ambao Ni WANAJESHI wasitajwe Kwakuwa wapo kazini na Wengine Wapo Kwenye USHAHIDI
Wakili wa Serikali: Taja Majina yake,hapa Tupo Mahakamani lazima uwe na Nidhamu
Jaji: Kuna Mtu anataka Kurespond,
Wakili wa Serikali;: Shahidi amekuwa akitaka Wengine Kwa Majina sasa sioni tatizo kwa kutaja huyo anayemtembelea
Mallya: Kuna Taarifa tunayo tangu tuseme Kuwa Kuna Mashahidi ambao wapo Jeshini, Wapo Wanajeshi wawili wameshaitwa Kutishiwa wasije kutoa Ushahidi.
Jaji: Je Mallya unafikiri hao wakitaka Kujua wanafunzi wa Ling'wenya waliomtembelea Magereza watashindwa.?
Mallya: watashindwa,
Jaji: kwanini
Mallya: kwa sababu wanatumia Codes
Wakili wa Serikali: Naomba Nishauriane na wenzangu
Jaji: Ikibidi nihairishe kidogo mjipange
Wakili wa Serikali: Tuendelee Mheshimiwa hilo swali naliacha
Jaji: kabla Ujaliacha tuambie kwanza ,Kuna Umuhimu wa hayo Majina
Wakili wa Serikali: Hapana Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Ile Kombania uliyokuwa unamfundisha Adamoo ilikuwa na Kombania ngapi
Shahidi: Sisi hatuna Kombania tunaita Squad room
Wakili wa Serikali: Kwa ile ya Adamoo ilikuwa na Watu wangapi
Shahidi: na watu 60
Wakili wa Serikali: Siyo wanajeshi wote wanaoingia 92KJ kweli si kweli
Shahidi: Nyoosha swali Vizuri
Wakili wa Serikali: Ili Mtu aingie 92 KJ unatakiwa Uwe na Sifa Maalum
Shahidi: Sielewi
Wakili wa Serikali: Sisi tulikuwa Makutopora wakakata Bogi la 92
Wakili wa Serikali Boginla Makutopora lishakatwa kuna Lipi linafanyika
Shahidi: Wanapimwa Afya
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wanaoingia 92KJ Sifa Kuu Afya iwe Nzuri
Shahidi Ndiyo
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufuzu Afya, kozi inaanza
Shahidi: inategemea
Wakili wa Serikali: We Umepiga Kipindi gani
Shahidi: Mwaka Mmoja na miezi nane
Wakili wa Serikali: kozi ilikuwa Ngumu sana au Nyepesi Kwako
Shahidi: Mheshimiwa Jaji siwezi Kusema Ngumu au Nyepesi kwa sababu Leo Mkipewa Ugumu kwenye Intro kesho mnapewa Mepesi kwenye Leki
Shahidi: Ndiyo
Wakili: ili uwe Mwalimu kwenye hiyo Kozi unatakiwa Uwe,Mkweli,Mtiifu,Mwenye nidhamu ya haki ya Juu
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo sifa hizo zote unazo
Shahidi: siwezibKujua waliokaa wakanichagua
Wakili wa Serikali Kwa hiyi Kuna uwezekano Mtu akafuzu akawa hana hizo sifa
Shahidi: Imawezekana
Wakili wa Serikali: na wewe unawezekana ukawa huna hizo sifa
Shahidi: inawezekana
Wakili wa Serikali: Jeshini Kuna Mahabusu.?
Shahidi: Ipo
Wakili wa Serikali: Ile Mahabusu ya Kijeshi inasimamiwa na Nani.?
Shahidi: Military Police
Wakili wa Serikali: sahihi kwamba wanaofanya Makosa na kuwekwa Mahabusu ya ya Kijeshi wanaweza Kuwekwa kwa muda wa siku 2 au Wiki 2
Shahidi: Unawekwa
Wakili wa Serikali: Uwezi Kushtuka na siyo Ajabu ukiona Mtu kakaa Mahabusu Wiki Mbili,Kule Jeshini
Wakili wa Serikali: Uwezi Kushtuka na siyo Ajabu ukiona Mtu kakaa Mahabusu Wiki Mbili,Kule Jeshini
Shahidi: Unawekwa
Wakili wa Serikali: Vipi kuhusu chakula Ukiwa Mahabusu ya Jeshi
Shahidi: Unakula Resheni yako mara tatu kwa siku
Wakili wa Serikali: Chakula Kinatoka wapi
Shahidi: Chakula cha Serikali ni Cha Jeshi
Wakili wa Serikali: Na wanaoleta Chakula ni MP tuh
Shahidi: kwa kwetu KJ 92 Unachukuliwa na Kupelekwa Mess ukimaliza Kula unarudishwa Mahabusu
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Utakubakiana na Mimi wanaowaletea Chakula ni wale Ma Mp wanaohusika na Mahabusu tuh
Wakili wa Serikali: Kwa Nidhamu ya Kwenye Majeshi wale wanaotunza wanajeshi Kuoe Mahabusu,hawana Nidhamu ya Kusema wale wanaletewa Chakula Nje ya wao wanaotunza Mahabusu
Shahidi: Si kweli
Mimi kwa 92 KJ hatupo chini ya Ulinzi kwamba Utatorika kazini,Unachukuliwa Mahabusu wanakupeleka Mess ukimaliza Kula Unarudi Mahabusu
Wakili wa Serikali: kwa hiyo haiwezekani kupewa chakula Kutoka Nje
Wakili wa Serikali: Chakula cha Nje ya Jeshi
Jaji: Shahidi kashaeleza utaratibu wa wa Chakula,unazungumzia Chakula cha Kutoka wapi
Shahidi: si elewi
Wakili wa Serikali: nitakuwa sahihi nikisema Komandoo Mmoja anaweza kupambana Askari wasio wanajeshi 50
wasiokuwa Makomandoo zaidi ya 50
Shahidi: Si kweli
Wakili wa serikali: komandoo anaweza Kukabiliana na Askari wangapi
Shahidi: Inategemea, Ukomandoo siyo Kupigana tuh,Wapo askari wanaweza Kupigana kuliko Mimi Komandoo, na Pia Ukomandoo wa kupigana na watu 50 Labda ukomandoo RAMBO siyo kawaida
Shahidi: ukomandoo ni Ujuzi tuh labda wa Kupigana, Silaha na Kutumia Vifaa vya Kivita
Wakili wa Serikali Sasa jana Ulieleza Jana Ukiwa Nje uliona Adamoo akiwa nje alikuwa anaongea na Simu
Wakili wa Serikali: kweli ama si Kweli
Shahidi: Sikumbuki
Jaji: alisema alisikia Sauti ikiitokea kwenye Corridor Akizungumza na simu
Wakili wa Serikali: ni sahihi Jana Ulisema Adamoo akizungumza na simu kwenye Uchochoro
Wakili wa serikali: Ulisema Jana Uliposikia kelele Kwenye uchochoro Ukamkuta Adamoo ameshanyanyuliwa
Shahidi: Si kweli
Mallya: OBJECTION Wakili anajaribu kumlisha maneno shahidi kuwa alikimbilia uchochoroni
Jaji: Nililwenda kule Ammbako sauti ilikuwa inatokea
Wakili wa Serikali: ni sahihi kuwa ulimkuta Kuwa ameshanyanyuliwa Juu juu
Shahidi: Nilikuwa Ndani ya Duka nikakuta wameshamsogeza karibu na Nilipokuwa
Wakili wa Serikali: Ulimkuta Adamoo amenyanyuliwa Jujuu,Kweli si kweli
Shahidi: ni kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: ulikuta anavutwa akitolewa Uchochorono kweli au si kweli
Wakili wa Serikali: Jana ukisema Ukamkuta wanamnyanyua na Leo unasema kuwa ulimkuta anavutwa
Jaji: anafikiri Shahidi alisema Jana na Leo Asubuhi siyo wakati wewe unamuhoji
Wakili wa Serikali: Mahakama Imerekodi Leo Asubuhi Kuwa Adamoo alikuwa anavutwa
Shahidi: Kweli
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: na Hiko kitendo ulikiona Kwa macho,Kweli au si kweli
Wakili wa Serikali: Wakati gani Upo sahihi Jana au Leo Asubuhi
Shahidi: Yani...........
Shahidi: Nilichosema Leo ni sahihi
Wakili wa Serikali: Chagua Moja tuh Yapi sahihi
Wakili wa Serikali: Jana Wakati unahojiwa uliona kwamba wale waliomzunguka Walikuwa wanatoa Pistol kwenye maungo ya a
Adamoo
Shahidi: kweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo uliona wakati wanachomoa pistol wakisema anapistol anapistol
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: na wakati wa Madawa pia uliona wanatoa Madawa wakisema anamadawa anamadawa
wakili wa Serikali: Sasa tusaidie hapa Adamoo wakati nahojiwa alisema wewe Ulishihudia wakimuwekea Madawa na Pistol
Shahidi: Kweli
Shahidi: Sikumbuki
Shahidi: Sikumbuki kwamba Adamoo alinilenga Kuwa Mimi kuwa Nimeona wakimuwekea Madawa na Pistol
Jaji: Sasa jibu kuwa Adamoo alisema au hakusema
Shahidi: Sikusikia akisema hivyo, kauli yangu ilikuwa "natoa Vitu vyangu Msije kuniweka Pistol na Madawa akama Mlivyomuwelea Mwenzangu"
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Kama.Kuna Mtu akisema Umeona atakuwa Muongo
Shahidi: akisema kwa Kauli inayosema Kweli ni Muongo
Wakili wa Serikali: Kuna Mtu anaitwa Msemwa shahidi wa tatu ulimuona
Shahidi: Ndiyo nilimuona
Wakili wa Serikali: Ulieleea Ushahidi wake
Shahidi: Kwa Uelewa Wangu nilielewa
Wakili wa Serikali Wakati Msemwana anatoa Ushahidi alisema aafande Kiingai alileta watuhumiwa Wawili waliloletwa na Afande Kingai,Ni kweli au si kweli
Shahidi: Ni kweli alisema
Alisema Saa 12 Kasoro
Wakili wa Serikali: kweli Saa 12 Kasorobo
Wakili wa Serikali: Ulisikia akisema Mohammed Abdilah Ling'wenya
Shahidi: Ndiyo nilisikia
Wakili wa Serikali: Ulijua anayesemwa ni Wewe.?
Shahidi: Ni kweli nilijua
Wakili wa Serikali: lakini Hukusema kwamba wewe Msemwa Muongo sikuwahi Kuwa chini yako
Shahidi: Sikuwahi Kuwa Ukiwa kizimbani unaruhusiwa Kuongea
Mahakama Kichekooooooo
Shahidi: Ndiyo kabla Msemwa ajatoa Ushahidi
Wakili wa Serikali: Uliongea n wakili wako Kwamba Ulifikishwa Tazara na Siyo Central
Wakili wa Serikali: lakoni Wakili wako hakusema Kuwa Msemwa ni Muongo
Shahidi: Alisema,kwa Maelezo kwamba Nilitoka Moshi nikafikishwa Tazara ilikuwa anafikisha Ujumbe sijawahi Kuwa Central
Jaji Tupishe Hadhana*
Mahakama Kimyaaaaaaaaaa
Jaji: tunaweza Kuendelea
Wakili wa Serikali Umeelza Kwamba Habari ya Msemwa kuwa anaongea Uongo ni leo Ndiyo umesema Mahakamani Kwa kurudia Swali
Shahidi Si kweli Jambo hilo lilikuwa limeshatajwa, uongo huo umejulikana leo alisema hata Adamoo
Wakili wa Serikali: kwa hiyo siyo wewe au Adamoo wakati Msemwa anatoa Ushahidi wake Kuwa Wewe ni Uongo
Shahidi: sasa wewe unamwakilishi wako na Mwakilishi wako hazungumzi hukuona haja kwamba kumwambia Wakili kuwa Huyo anaongea Uongo
Shahidi: alisema Adamoo kabla yangu kuwa hatukuwahi Kufikishwa Central
Wakati ule Msemwa anaongea Uongo dhidi yako wewe,na wewe Unaona ni Uongo na Hukuona Sababu ya kumweleza kuwa Huyu anadanganya
Wakili wa Serikali hebu tuambie sasa ni sahihi kwamba ,Pale Rau wakati Mwenzio anavutwa ,wewe Ulitoa Vitu vyako ukaweka Kwenye kibaraza cha Duka
Shahidi: kwenye nini
Shahidi: Kibaraza Cha Duka
Wakili wa Serikali: Upo ushahidi ulioletwa Mahakamani Kuwa wewe ulipofika Pale hapa Mahakamani kwamba Msije kunifanyia Kama Mlivyomuwekea Vitu chini
kimya Kidogo
Shahidi: Lile Tukio lilivyofanyika nikasema Msije kunisingizia Kama Adamoo,na mimi natoa Vitu vyangu,nikaviweka pale Chini Kibarazani
Jaji: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Iambie Mahakama ,wale watu waliowakamata pale Rau Madukani kuna Mahala popote uliwahi Kukutana nao
Shahidi: sikuwahi Kukutana nao Wala nilikuwa siwajui
Wakili wa Serikali: Kama ulikuwa uwajui hukuwahi Kuhitilafiana nao hao watu
Shahidi: Kweli Kabisa
Wakili wa Serikali: hukuwa unafahamu kuwa wale ni Polisi
Shahid:i si kweli, Nilijua ni Polisi Ndiyo maana Niliwaambia Kuwa Msimpige Adamoo
Wakili wa Serikali: Ulipowaambia tuondoke wakaondoka
Shahidi: walikusanya Vitu na kusubiri Amri ya Mkubwa wao,Siyo kwa kauli yangi ndiyo waondoke
Wakili wa Serikali: kwa hiyo Adamoo hakupigwa
Shahidi: Unanirudisha Nyuma,Nilishasema nilipotoka nilikuta wanapiga Adamoo na Kumburuza
Wakili wa Serikali: baada ya Pale Mlienda Kituoni Polisi
Shahidi ndiyo tulienda Moja Kwa moja Polisi
Wakili wa Serikali kitendo cha kujua hawa ni Askari Polisi ilikuwa ni Ukamataji au siyo Ukamataji
Shahidi: Siyo Ukamataji
Shahidi: ndiyo ni Mateso
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Kitendo kile siyo Ukamataji ni Mateso
Wakili wa Serikali: Kitendo cha kuwapeleka Kituo cha polisi mlikuwa mmekamatwa
Shahidi: Ndiyo
Jaji: Shahidi Mwanzo Umesema hukukamatwa
Shahidi: ni sahihi Mheshimiwa Jaji kwamba Wakili wangu nilimjibu Mwanzonkuwa Tulitekwa na Baaadae hapa nimejibu hatujakamatwa ananiuliza Jambo lingine
Jaji: sawa tuendeleee
Wakili wa Serikali: Umesema Adamoo kuwa alivaaje
Wakili wa Serikali: Kwani hayo Mavazi hawezi Kuvaa Mtu Mwingine
Shahidi: Raba Nyeupe,Suruali Nyesui,Shati la Mikono mirefu la Maua maua
Shahidi: anaweza
Shahidi: Samahani Mheshimiwa Jaji naomba Maji, Maji yameisha hapa Kizimbani
Jaji: kweli Umenikumbusha Leo, Apewe Maji ,ila kazi Ngumu ya kujibu Maswali tangu Asubuhi
Wakili wa Serikal: Nilikuwa nasema Kuwa Yale mavazi si anaweza Kuvaa Mtu yoyote
Jaji: Ling'wenya ungependa tupumzike
Shahidi: ndiyo Mheshimiwa Jaji
Jaji: nahairisha Mpaka Saa 8 na Dakika 10
Jaji: ameingia
watuhumiwa wanapanda Kizimbani
Kesi Namba 16 ya 2021 inatajwa
Mafaili yanapandishwa kwa Jaji
Jaji: nnatunaini Pande zote zipo tayari kwa ajili ya kuendelea
Mashitaka Tupo tayari
Utetezi Tupo tayari
JAJI: Shahidi aliishia Kwa Upande wa Mavazi aliyokuwa amevaa Adamoo ambapo ni Raba Nyeupe,Suruali ya Jeansi na Shati la Mauamaua
Jaji: Shahidi nakukumbusha upo chini ya kiapo
Wakili wa Serikali: Mavazi aliyokuwa amevaa ulisema yanaweza Kuvaliwa na Mtu yoyote
Jaji: Wakili wa Serikali Chavula Karibu tuendelee
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Adamoo ni Mtu wako ,rafiki yako
Shahidi: Kweli ni Mtu wa karibu
wakili wa Serikali Mmekuwa na Adamoo nyakati za raha na tabu,kweli au si kweli
Shahidi: ni Kweli
Wakili wa Serikali: sasa tuambie Kabla ya tarehe 05 Mwezi wa 07 2020 haukuwahi Kupata Msukusuko ukiwa na Adamoo
Shahidi: sikuwahi Kupata Msukosuko nikiwa na Adamoo
Wakili wa Serikali: Mazingira yaliyokufanya Umpachike Adamoo wakati wa Mafunzo ,Mkiwa mnaimba
Kweli au Si kweli
Shahidi ni Kweli
Wakili wa Serikali: Unaweza Kuileza Mahakama Adamoo akiwa anaimba sauti yake ikoje
Shahidi: Siyo nyororo wala siyo Nzito sana
Shahidi: naweza Kuimba
Shahidi: anaimba Kwa Mfanano wa Sauti ya Adamoo "Tembea tembea Kidogo dogo,Melengelenge si Ugonjwa"
Mahakama Kichekoooooooo
Jaji: naona unatukumbusha 92KJ
Wakili wa Serikali: Kwahiyo hiyi Adamoo hata akiwa Kwenye giza ,Wewe Umuini utatambua huyu ni Adamoo si Mtu Mwingine
Shahidi: namtambua,Nishaieleza Mahakama
Wakili wa Serikali: Ni sahihi vile ambavyo umeimbia Mahakama ndivyo ambavyo Adamoo anaimbaga
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Kwahiyo Mtu anaweza Kuiga Sauti ya Adamoo
Shahidi: Ndiyo akiwa ameishi naye kama nilivyoishi naye mimi anaweza
Wakili wa Serikali Kwahiyo Sauti ya Mtu inaweza Kuigwa
Shahidi: Ndiyo Sauti ya Mtu inawezekana Kuigwa
Wakili wa Serikali: Umeeleza Mahakama Ulisikia Adamoo analiaje vileeeeee
Wakili wa Serikali:ukajua Kuwa hiyo ni ya Adamoo
Shahidi: Eeehiiiiiiii,Eeehiiiiiiiii
Wakili wa Serikali: Hukuieleza Mahakama kwamba Kabla ya Tarehe 05 niliwahi Kumsikia Adamoo akilia
Shahidi: Mahakama ipi,Miye nimeeeleza Kuwa Nilimsikia Adamoo akilia
Wakili wa Serikali: nazungumza kabla ya Shauri hili Mahakamani, uliwahi Kuieleza Mahakama kuwa Kabla ya tarehe 05 uliwahi Kumsikia Adamoo akilia
Shahidi: Sikueleza
Wakili wa Serikali Kwakuwa umeieleza Mahakama kama hukuiambia Kwamba Adamoo hukuwahi Kumsikia Adamoo akilia na Kwamba Kuna Uwezekanao Mtu aliiga Sauti ya Mtu,Utakubaliana na Mimi Kuwa Ile sauti ya Mtu aliyekuwa analia kuona nani alikuwa analia
Shahidi: Ndiyo sikuona Kwa Macho
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: Ulieleza Mahakama Mtu aliyepitishwa Mbele yako aliliwa akiinamishwa
Wakili wa Serikali: na wewe hukuileza Mahakama yule Mtu hukumtambua kwa Sura
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: anawafuata wenzie Kushauriana
Shahidi: nilimuita
Wakili wa Serikali: Yule Mtu ulisema Mahabusu Mwenzio pale Moshi,ulihisi ni Adamoo ulimwambiaje
Wakili wa Serikali ukamwambiaje
Shahidi: niliamuita Jina Lake Adamoo, akasema naam Bro Mikazo ila hali Mbaya,nikamjibu na mimi ni hivyo hivyo ila najitahidi
Wakili wa serikali: alikwambia Nimekazwa ila hali ni Mbaya
Jaji: wakili umesikia Vizuri kweli hebu rudia
Wakili wa Serikali: Nimekazwa
Jaji: wakili wa Serikali Mwingine,Katuga umesikiaje .?
Shahidi: Mikazo
Wakili wa Serikali: Katuga umesikiaje
Jaji: Wakili wa Serikali Chavula Umesikia .?
Wakili wa Serikali: Chavula Nimekazwaza
Mahakama Kichekoooooo
Jaji: Nakwambia Mimi Mara ya Mwisho Mikazo,Ukiendelea tena Nitakutafsiri tofatuti
Jaji: Endelea
Wakili wa Serikali: Chavula Mikazo Mheshimiwa Jaji nilisikia Vibaya
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo hakuk and ambia Kuwa amepigwa tofauti na Maneno hayo
Shahidi: kweli hakutamka Kwamba amepigwa
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo wewe ukatafsiri kwa Ufahamu wako kwamba Mikazo ni Kupigwa
Shahidi: Sahihi Ndiyo tulivyomaanisha
Wakili wa Serikali: Ni sahihi kwamba Rau Madukani Mlikuwa Na Moses Lijenje
Shahidi: Si kweli
Wakili wa Serikali: Mlikaa naye Moshi na Moses Lijenje Mara ngapi
Shahidi: Tulikuwa naye mara Moja wakati tunaongoa na Mheshimiwa Mbowe kuhusu swala la Kazi
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa nani
Shahidi: Mheshimiwa Mbowe
Wakili wa Serikali: mliongea naye wapi
Shahidi: sifahamu Maeneo ya Hotel gani
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Siyo Aishi Hotel aliyosema Adamoo
Shahidi: sifahamu kwa sababu hatukuingia Uoande wa Hotelini
Shahidi: ni Maeneo yaleyale ya Aishi lakini siyo Hotelini
Wakili wa Serikali: lakini Maeneo ya Aishi Hotel
Wakili wa Serikali: Wakati Mnakamtwa Rau Mlikuwa na Moses Lijenje
Shahidi: tulikuwa naye Rau,
Wakili wa Serikali: Wakati Mnakamtwa Mlikuwa wapi
Shahidi: yeye alikuwa eneo ya Glocery wakati purukushani inatokea
Wakili wa Serikali: Atakuwa alikimbia au alijificha
Shahidi: Mimi sifahamu hayo
Wakili wa Serikali: Ndiyo Mimi nakwambia Sasa alilimbia kwa mujibu wa kingai
Mallya: OBJECTION Wakili anaweka Opinion zake
Jaji: na Mimi nimeona hilo,nilishakataza hayo Maneno yenu siyo lazima kuweka mimi naandika Maelezo ya Shahidi tuh
Wakili wa Serikali: wakati Kingai anatoa Ushahidi wake kuwa Moses Lijenje alikimbia akaelekea Arusha kwa Dada yake
je Ulimsikia
Shahidi: Nilimsikia Kingai akisema hivyo
Wakili wa Serikali: Maelezo ya Kingai yanatofautiana na wewe Kwamba Mlipofikishwa Polisi Central Moshi hamkutoka kabisa
Shahidi: Kweli hatukotoka kabisa
Wakili wa Serikali: Kwamba tulipotoka Rau Madukani kwamba tulifikishwa Moshi Polisi Central Yanaletwa Leo akiwa Kingai hayupo Mahakamani
Shahidi: Kweli sijamuona Kingai Hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali: Kama Umeyasema yeye akiwa hayupo Mahakamani,hana Ufahamu ya Unayoyasema kwa Sababu yeye hayupo Mahakamani
Shahidi: Ni kweli hafahamu
Wakili wa Serikali: nitakuwa Sahih,Ngoja niondoe
ikatatokea Leo wewe Watu wanazungumza wanasema Mohammed Muongo
Jaji: naona watu wanatoka toka inapoteza Utulivu wangu,na Mimi sitaki Kuzuia Watu kuingia Mahakamani,Si tumetoka Break sasa hivi tuh Naomba Mjitahidi,ingawa sisiemi watu wakibanwa wasitoke wajikojoleee
Jaji Tuendelee
Wakili wa Serikali: Kuanzia Jana Ulipoanza Kutoa Ushahidi wako Mpaka Sasa Hakuna mahala popote Kuanzia Tarehe 05 na Kabla ya siku Ile Kuwa Uliwahi Kumkagua kwemye maungo yake
Shahidi: Sikumkagua,nimkagie kama nani na sina tabia hiyo
Wakili wa Serikali: sema Kweli au si Kweli
Jaji: nafikiri ameshajibu
Shahidi: Ni sahihi Mheshimiwa Jaji
Wakili wa Serikali: Wakatibwa Maelezo yake Adamoo hakusema Moshi hakuwa kufika na Ile ndiyo Mara yake ya Kwanza
Shahidi: Kweli hakusema hivyo
Shahidi: Ni kweli nimesema
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wewe ndiyo unayesema Adamoo Mji wa Moshi ni Mgeni,Kweli au Si kweli
Wakili wa Serikali: Tuambie sasa Wewe Dar es salaam ni Mwenyeji.?
Wakili wa Serikali: Tuambie sasa Wewe Dar es salaam ni Mwenyeji.?
Shahidi: siyo Mwenyeji sana
Wakili wa Serikali: Dar es salaam Unafahamu sehemu gani,
Shahidi: Napafahamu Kimara King'ong'o,
Wakili wa Serikali: Sehemu gani Nyingine
Shahidi: Kimara Matosa
Wakili wa Serikali: unapafahamu Posta..?
Shahidi: Napafahamu Posta Nilisha wahi Kufika Kanisa la Joseph
Wakili wa Serikali: Pale Ndiyo Posta
Jaji: sasa Niandike Nini
Wakili wa Serikali: Unapafahamu Posta
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Unapajua Station..?
Shahidi: nimewahi Kufika Zamani
wakili wa Serikali: Kwa hiyo Unapajua au Upajui
Mallya: OBJECTION ameshajibu Swali
Jaji: Bado hajajibu swali
Shahidi: sipafahamu kwa Sasa
Wakili wa Serikali: Vipi KuhusuTazara ..?
Wakili wa Serikali: Vipi Kuhusu Buguruni
Shahidi: Sipafahamu
Shahidi: Sipafahamu
Wakili wa Serikali: kwa hiyo ulifanya Kuambiwa Kuwa hapa ni Tazara
Shahidi: kweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo Ukiacha kuambiwa kwa akili yako uwezi Kujua ulikuwa Tazara
Shahidi: kwa akilinyangu nilioata Kuambiwa pale ni Tazara
Wakili wa Serikali: kwa hiyo Ujawahi Kufika Tazara kabla
Wakili wa Serikali: kwa hiyo Ujawahi Kufika Tazara kabla
Shahidi: Sijawahi Kufika Kituo cha Polisi Moshi zaidi ya kutolewa Moshi na Kuletwa Pale Tazara Kituo cha Polisi
Wakili wa Serikali: Kama Nimekusikia Katika Safari yenu Kutoka Moshi Kuja Dar es salaam, Mle ndani Ukiacha Askari polisi waliokuwa wanapiga Story zao,Hukusikia akitukingine Chochote
Shahidi: Kwanza siku safiri Tarehe 05 ni Tarehe 06
Wakili wa Serikali: Samahani nilikuwa namaanisha Tarehe 06 Ulikuwa unawasikia Askari Polisi wanapiga Story Zao
Shahidi: ni kweli nilikuwa nasikia wanaongea Maongezi yao
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Ilikuwa ni Safari ya Utulivu hapakuwa na Purukushani
Shahidi: Nimezungumza jana Purukushani zilikwepo, Kwa Sababu nilikuwa nikitaka Kuinua kichwa wananikandamiza Chini
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo ukiondoa jambo hilo hapakuwa na Purukushani Nyingine
Shahidi: Kwa binafsi yangu hapakuwa Na Lingime
Wakili wa Serikali: Ukiacha watu uliokaa nao palikuwa na watu wengine Kwenye lile gari
Shahidi: Siwezi Kujua,nilikuwa nimepigwa Kitambaa
Wakili wa Serikali: Relax nataka Ujibu Upate haki yako,Mimi sikutegi
Shahidi: Ndiyo Maana na Mimi nakwambia Ukweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo Palikuwa na watu wengime kwemye gari
Shahidi: Siwezi kuwatambua nilikuwa Nimepigwa Kitambaa ila nilikuwa na sikia Sauti Mbele au Nyuma ya Gari
Wakili wa Serikali: Hebu tuambie Kama ni Kweli,Ulipokuwa Mbweni Ukatolewa Ukawekwa Chumbani ukawa umewekwa na Askari gani
Shahidi: Nimeeleza Mahakama nilikaa chumba Cha kwanza Ukiingia tuh
Wakili wa Serikali: Palepale Kwenye Chumba Ulichoingia tuh
Shahidi: Nilikuwa na Jumanne na Mlangoni alikwepo Goodluck
Wakili wa Serikali: Unawza Kutuambia Vile Vyumba vikoje
Vinatizamana au Vinaongozana
Shahidi: Milango ilikuwa tofauti
Jaji: chukulia Hiki ndiyo Chumba je ulipokuwa umekaa pale Mbweni Pakoje
Shahidi: afafanua Ramani ya Vyumba Mbweni
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Wakina Kingai lazima wapite kwenye Mlango wako wewe uliopo ili waingie,ni sahihi Hiko chumba Kimetenganishwa na Ukuta
Jaji: sasa Wakili unaeeza Kuendelea Kuanzia hapo kwenye ufafanuzi ,tumeshaelewa
Shahidi: Ni kweli
Wakili wa Serikali: Licha yakuwa Chumba Chako wewe na Alipokuwa Kingai Kimetenganishwa na Ukuta ila bado uliweza Kuwaona Wakiwa Chimba Cha Pili
Shahidi: Ndiyo
Jaji: kwahiyo palikuwa na Milango Miwili
Shahidi: Ndiyo na Mlango ulikuwa wazi tuh na haujafungwa
Jaji: naona Sasa waru wanasinzia,Kama watu wanajiskia Kujinyoosha Viungo namruhusu kusimama aende Maramoja Nje isije onekana nimezuia,Kama hakuna Tuendelee
Wakili wa Serikali: Mwenzako anasema alichukuliwa na kina Goodluck akapelekwa Kwenye Chumba alichokuwa Kingai wakakaa Kwenye Meza na Goodluck akiwa Amesimama Mlangoni,Je kati ya haya Mawili lipi ni la Ukweli
Shahidi: Nilisema Wakati anapelekwa Adamu Kule sikujua anapelekwa na nani na wakati gani
Wakili wa Serikali: Kama Limeletwa Mahakamani na hili unalozungumza lipinlenye Ukweli kati ya haya Mawili
Shahidi: najua ninalolisema
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Unasema ulimuona Kingai Wakati anaingia na Adamoo analosema Mbona Kinakinzana
Shahidi: Sikwepo mimi
Wakili wa Serikali: Kati yako wewe na Afamoo nani alitangulia Kuingia Kwenye Kile Chumba
Shahidi: Nilisema hapa Sijajua Adamoo aliingia Saa ngapi
Wakili wa Serikali: Wewe na Jumanne mlikuwa namfanya nini Mlendani
Shahidi: alikuwa ananiuliza Maswali
Wakili wa Serikali: Wakati anakuuliza Maswali Jumanne akili yako ulielekeza Kwa Jumanne na Kwamba Majibu yake uyatoe au usiyatoe
Shahidi: Ni kweli
Wakili wa Serikali: Wakati wa Kutolewa Adamoo Ulikuwa unaendelea na Zoezi la Kuulizwa Maswali na Jumanne
Shahidi: Ni kweli nilikuwa naulizwa
Wakili wa Serikali: Wakati unaulizwa Warrant of Arrest sijui na Warrant hayo Maswali unayakumbuka
Hakuna Ushahidi wowote unaohusiana na Arrest Warrant kuletwa haoa Mahakamani
Shahidi: ni kweli niliulizwa
Shahidi: Ndiyo nilijibu hivyo
wakili wa Serikali: Na wewe Ukajibu kuwa hujakiona wakati unakamatwa
Wakili wa Serikali: Unajua kuhusu Warrant Arrest
Shahidi: nikibali pale unapokuja Kunikamata Kama Polisi Kunionyesha Kibali ambacho kinakuruhusu Kunikamata
Shahidi: nikibali pale unapokuja Kunikamata Kama Polisi Kunionyesha Kibali ambacho kinakuruhusu Kunikamata
Wakili wa Serikali umejuaje kama Mru akikamatwa anatakiwa akuonyeshe Arrest Warrant
Wakili wa Serikali: Je unawezekana kwa Polisi Mtaani Ananiona namchoma Mtu kisu atatakiwa awe na Arrest Warrant.?
Shahidi: kwa Uelewa Wangu
Shahidi Siyo Polisi tuh ,Hata Mimi au Mtu yoyote anaweza Kukuzuia na Kukukamata
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Siyo Mazingira yote Mtu anatakiwa akamatwe na Polisi kwa Arrest Warrant
Shahidi: Siyo Mazingira yote
Wakili Wa Serikali Chavula: Mheshimiwa Jaji naomba Niishie hapa nimuachie Mwenzangu
Wakili wa Serikali: Katuga Ling'wenya Ni kweli Adamoo ni Mtu wako wa Karibu
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: nikisikia umesema Umetoka naye Chalinze
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: ktk Ushahidi wako Umesema alikuwa na Tsh ngapi Mfukoni
Shahidi: hapana nilizungumzia Pesa zangi Mimi Mfukoni
Wakili wa Serikali: Ulipata Kufahamu alikuwa na Tsh ngapi Mfukoni
Shahidi: hapana sifahamu
Shahidi: Wakati huo nilikuwa nimeshaacha Kazi,Mambo ya kambini Jeshini siwezi Kuyafahamu tena Mbali kisaaaa
Wakili wa Serikali: Je unafahamu Adamoo alipata Battle Confusion
Wakili wa Serikali: Kwa Uelewa wako Battle Confusion ni Utovu wa Nidhamu Jeshini
Shahidi: Siyo Utovu wa Nidhamu
Wakili wa Serikali: umewahi kumuuliza nibsababu ipi iliyopelekea Kufukuzwa Kazini
Shahidi: Battle Confusion
Jaji:Ukissema Battle Confuse unamaanisha...
Shahidi: Battle Confusion
Wakili wa Serikali: Unakubaliana na Mimi uliachishwa kazi
Shahidi: Ndiyo niliachishwa kazi
Wakili wa Serikali: Sasa elezea Mafunzo yakobya Kijeshi pamoja na yale yaliyoongezeka Pale ya Ukomandoo,Unaweza Kuyatumia Uraiani
Shahidi: Ndiyo nayatumia,Kama Kuwa na Nidhamu,Kufanya Mazoezi
Wakili wa Serikali: Unaweza Kuyatumia Mazoezi yako Vinginevyo
Shahidi: Siwezi
Wakili wa Serikali: Hilo katazo unalipata wapi
Shahidi: Siwezi
Wakili wa Serikali: Hilo katazo unalipata wapi
Shahidi: ni ya Kibinadamu kuwa Utakiwi Kufanya Vitu Viovu Popote pale
Wakili wa Serikali: Katazo hilo lipo Jeshini.?
Shahidi: Ndiyo Jeshini Utakiwi Kufanya Maovu
Wakili wa Serikali:Uliulizwa Kuhusiana na Detention Register Na kwamba Ujawahi Kusaini kwenye hiyo Detention Register, ni kweli ulijibu hivyo.?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: ulifahamu lini kwamba Ulitakiwa kusaini Katika Detention Register Mtuhumiwa unapokamatwa unapotakiwa Kuingizwa Mahabusu
Shahidi: Kwa Ufahamu wangu Popote kwenye Ofisi unapoingia na Kutoka unatakiwa kusaini unapotoka ,Nalitambua Kifikra na Ufahamu
Shahidi: si Lile Book unalolikuta amapokezi,Alillileta Mahakamani
Wakili wa Serikali hicho Kitabu Unakifahamu
Wakili wa Serikali: Kuna sehemu pale umeona Unatakiwa Kusaini
Shahidi: Sikuliona Mimi
Wakili wa Serikali: Kule Ulipopita ukiwa na Jumanne ukaja ukajua Kuwa Adamoo yupo ,akina Umbali gani
Shahidi: Nimeeleza Sana Mahakama Kwamba Ukiingia Mlango Mkubwa Unaanza Kuniona Mimi
Jaji: unaweza Kukadiria ni Umbali gani Kutoka Ulipokaa Mpaka kwenye hicho Chumba
Wakili wa Serikali: Utakubaliana na Mimi kuwa Kilichokuwa Mle ndani Ujui
Shahidi: Mheshimiwa Jai ni hatua Nne au Tano
Shahidi: nimeeleza Mahakama kilichojiri kwa Adamoo na Kingai Mle ndani siwezi Kujua
Wakili wa Serikali: Katika Ushahidi wako ktk Tukio la Kukamatwa pale Rau Madukani,Hakuna sehemu Yoyote Uliyosema Kwamba Askari wlikuuliza kama Unamfahamu Adamoo
Shahidi: Kwa Kumbukumbu zangu nilisema waliponishika Mkono wakaniuliza Kuwa Unamfahamu huyu
Wakili wa Serikali: Jana wakati Mallya anakuongoza alikuuliza Swali na Swali Lilikuwa Kuwa Kama Uliona Bastola au Madawa ya Kulevya ,Mpaka Adamoo akakuoa Ishara ulipata tatizo gani Kujibu
Wakili wa Serikali: Mapaka Mnenda Moshi Masharti ya kazi mlikuwa bado hamjapewa.?
Shahidi: Sikuona hiyo Ishara,Labda Ungenishtua
Shahidi: tulikuwa bado hatujapewa
Hadhana inaliaaaaaaaaa,Wote Kimyaaaaaaaaa*
Jaji: tunaweza Kuendelea
Jaji: tuliishia Kama Masharti ya kazi walisha yapata
Wakili wa Serikali: Sasa kwa Sababu mlikuwa hamjapewa Masharti ya kazi ya VIP PROTECTION Ni Makubaliano gani mliyokuwa mmepewa Mpaka mnakuwa Moshi
Wakili wa Serikali: ujasema ni Tsh ngapi na Kwa nini,Si Ndiyo
Shahidi: tulikuwa tunajadiliana bado Kuhusu Malipo
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji nihayo tuh
Jaji: nilipanga Tukomee Saa 10,Nitamuuliza Mallya kama zitatosha au tuhairishe akajiandae kwa Muda zaidi
Mallya: Mheshimiwa Jaji nitabakiza Tatu
Mallya: Shahidi Umeulizwa Kwamba Kingai kuna Maswali hakuulizwa
Jaji: Mallya
Wakili wa Serikali: OBJECTION Sioni Kama Swali lipo sawa
Mallya: Kwa Sababu ya Muda nitarudia Swali
Mallya: Umeanza Kutoa Ushahidi jana,Na Mpaka Leo Umejitokeza mambo Mawili Kuwa Ulitekwa na Ukakamatwa sasa isaidie Mahakama ichukue Jambo gani
Shahidi: Nilitekwa
Mallya: Uliulizwa Kuhusu Corridor,Path au Uchochoro Uliokwepo kwenye eneo lile,Hili Jambo lilitokeaje kwenye eneo lile
Shahidi: Kwa Uelewa Wangi Uchochoro ni Mwembamba lakini pale kwenye Corridor Nilipomaanisha ni Palubwa sana siyo padogo,Huku Maduka Huku Baa
Shahidi: Kwa Uelewa wangu ni Kitu Kimoja
Jaji: nimeona Swala hili Kila Mtu anatumia Bar au Glocery kwa Nchi yetu ni Sehemu Moja.?
Mahakama Kicheko
Mallya: Mheshimiwa Jaji Sina Swali Zaidi
Jamaa Kabakaisha Dakika Mbili
JAJI: nashukuru
Jaji: Nashukuru Shahidi Umemeliza
Jaji: wakili Mallya
Shahidi: Asante sana Mheshimiwa Jaji
Mallya: Tunaye shahidi Mwingine,Naomba Kesho tuendele na Ushahidi wake
Jaji: wakili wa Serikali
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi na Jambo hilo
Jaji: anandika Kidogo
Mahakama Kimyaaaaaaa
Kwa sababu ya Muda naihairisha Shauri mpaka kesho saa Kesho Saa Kamili Asubuhi tutakapoendelea Kumsikiliza Shahidi Kwenye Utetezi wa shauri Dogo
Jaji: Kwa Mara Nyingime nawashukuru wote kwa Kuendelea Kuwa watulivu
Jaji: ananyanyuka Polisi anapiga Kelele HIGH CORT
This post has been staredHii kesi inatabirika kabisa, on face of records inaonekana mashahidi wamepikwa (coaching of witnesses) ambayo ethically haitakiwi.
Pili, kwenye kesi za jinai inatakiwa mlakamikaji athibitishe shtaka lake bila kuacha shaka yoyote (beyond reasonable doubts) lakini hadi sasa hivi matokeo 3-0 huku Mawakili wa Utetezi wakiongoza kwa goli 3 dhidi ya Mawakili wa Serikali. Kuthibitisha bila kuacha shaka si jambo dogo, vijana wa DPP wanaacha mashaka sana, na ikumbukwe this is grave offence (yaani Ugaidi).
Nashauri Jamhuri wasajili "Nolle" yaani kutotaka kuendelea na kesi au Jaji ajiongeze baada ya kuwasiliana na vijana wa DPP kwamba akishafunga ushahidi wa Jamhuri aseme washtakiwa hawana kesi ya kujibu (yaani no premafacie case has been established).
Otherwise, vijana wa DPP watazidi kujidhalilisha na kuidhalilisha ofisi ya mashtaka nchini na taaluma nzima ya Sheria.
Kama sikosei ni Jaji Siyani ambaye ni Jaji incharge wa kanda ya Dodoma anayeongoza kesi hii, na kwa ninavyomjua alivyotulia na anavyojua kujiratibu, wakina Mbowe wataachiwa huru, ni swala la muda tu.
Amicus Curiae.
Hapa hachonganishwi mtu lakini kuna shida kati ya hivi vyombo vyetu vya ulinzi.What goes around comes around.Hao polisi hawawezi kufanya watachofanya hao wajeshi? Acha kuvichonganisha vyombo vyetu vya dola.