Yako wapi makovu ya risasi miguuni mwa Lissu?

Unadhani alipelekwa dispensary yenu ya kijiji
 
Kama mtu katibiwa hadi makovu yamefutika si itakua kapona?Kama ni hivyo si arudi tu Nyumbani?au kunauwezekano makovu yakawa yamepona lkn kwa ndani basi kuna ttz?Nahoji tu.
 
Mkuu mbona hasira hivo?Hili ni jukwaa la Great thinker na sifa ya great thinker ni kuwa open minded, sasa kosa la muuliza swali ni nn?Je haruhusiwi kuhoji?Au kuna mipaka great thinker amewekewa na haruhusiwi kuvuka ktk kuhoji?

Mkuu hata mimi naamini kwamba Lissu kapigwa risasi, na kwa mujibu wa maelezo kuna risasi zilipiga mguu wa kushoto, mkononi na maeneo mengine ya mwili wake. Ila hata mimi kwa hizi picha sioni mahali penye kovu. Wangalau mpiga picha angejitahidi kupiga mguu huo wa kushoto vizuri ili kuondoa shaka shaka. Na kama ametibiwa vizuri kiwango cha kutuoonyesha makovu ni suala la kupata maelezo ya kidaktari. Hata mimi sioni haja ya kubishana iwapo tunataka kupata ukweli. Ni vyema hao wanaompiga Lissu picha wakapiga na eneo lenye makovu ili kutoa hii shaka inayojitokeza, bado hutajafikia kuzuia wenye kutaka kuhoji maana hata mimi napenda kuhoji na kupata majibu sahihi.
 
Kama mtu katibiwa hadi makovu yamefutika si itakua kapona?Kama ni hivyo si arudi tu Nyumbani?au kunauwezekano makovu yakawa yamepona lkn kwa ndani basi kuna ttz?Nahoji tu.

..mbona hamkumkagua Mzee Kikwete makovu ya upasuaji aliofanyiwa?

..hivi mnataka kubishana mpaka kama TL amepigwa risasi au la?

..kwanini msiulize Madaktari wa serekali waliomtibu Dodoma walimkuta na risasi wapi?

Cc tindo
 
Swali lataka jibu. Kovu la risasi lina mounekano kama huu.
Au huu kwa makovu ya zamani.


Ukizumu vizuri picha ya Lissu kuna kovu moja linaonekana mguu wa kulia wa Lissu. Ingawaje siwezi kusema kwa uhakika ni kovu la risasi.

Watu wanaleta uongo kuwa ooh hakupigwa mguuni, ukitibiwa vizuri kovu halionekani. Bullshit ni kuleta uchama kwenye kisa cha kutatanisha. Na ndio maana ni muhimu kwa polisi kumuona muhusika na shahidi ili kupata ufumbuzi wa kesi. Idadi ya makovu ikiwa tofauti na maelezo yaliyotolewa na watoa habari yake pia inaweza kuwa ishu na inaweza kupelekea kujua kama kuna muongo mahali fulani.
 
We umelewa? Shida yako makovu au apone?
 
Mguu unaanzia kwenye makalio, kama unabisha rudi darasani. Kwa maana hiyo sehemu zingine haziwezi kuoneshwa hadharani
 
Hakutibiwa muhimbili huyo
 
Of course nilitegemea utetezi wa yako wapi makovu.Sijaona shida ya hili swali na sioni umuhim wa ktukana.Mwenyewe sijayaona na nilitegemea maelezo ya kitaalam
Hata na wewe tumepoteza nafasi hujajibu swali
 
Umejibu swali mkuu
 
Nimeipenda hii...... "Watu wako busy wanatafuta pesa, wewe uko busy unatafuta makovu"

Period
 
Hata wanafunzi wake bwana Yesu hawakuamini hadi walipoona makovu so muacheni kijana adai makovu
 
Yako wapi makovu?Au yamefutika?Wengine ni matomaso wanataka makovu na sioni ttz wakihoji.
Matomaso waende na Nairobi au wansubiri akirudi Tz kwani kwa kawaida ya " Matomaso" hawaamini mpaka .......kama alivyokuwa Tomaso (original)
 
Mchawi sio lazima ashike tunguli,hii uliyo onyesha ni dalili ya uchawi baada ya kuona lengo lako halikutimia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…