World Bank: Tanzania kinara wa Dunia upelekaji maji vijijini, yaongeza Dola Milioni 300

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,076
49,785

View: https://twitter.com/WBTanzania/status/1724805228581781607?t=rIJGgp2j31MJan_0GHtG-w&s=19

Tanzania imetajwa kuongoza Duniani kwa upelekaji wa huduma ya maji ya bomba Duniani kupitia program ya Lipa kwa Matokeo.

Kupitia programu hiyo jumla ya miradi 1,500 imetekelezwa vijijini na inafanya kazi na kuwezesha upatikanaji wa maji kwa vijijini imefikia 78%.

Mambo kama haya yanawachukiza sana Machadema.
Kazi iendelee 👇

--
Screenshot 2023-11-15 112142.png
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika Dkt. Victoria Kwakwa ameitaja na ameipongeza Tanzania kuwa kinara namba moja na mfano katika utekelezaji wa programu ya uendelevu wa huduma ya maji na usafi wa mazingira vijijini Mashariki na Kusini mwa Afrika na Duniani kwa kutumumia utaratibu wa malipo kwa matokeo yaani Programme for Results (PforR) ambayo inatekelezwa katika Nchi zaidi ya 50 na kufadhiliwa na Benki ya Dunia ambapo Wizara ya Maji kupitia programu hii imetekeleza zaidi ya miradi ya maji 1,500 ambayo imekamilika na inatoa huduma.

Akiongea na Waziri wa Fedha Dkt Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa Maji Jumaa Aweso nchini Ethiopia, Makamu wa Rais Kwakwa amesema Tanzania ni mfano bora katika utekelezaji wa Programu ya PforR na ameiomba itoe uzoefu wa mafanikio yake kwa Nchi zaidi ya 23 kutoka kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika zinazoshiriki mkutano wa maji na usafi wa mazingira (WASH Leadership Summit).

Amesema awali Tanzania ilipata Dola za Kimarekani milioni 350 katika miaka mitano lakini ndani ya miaka mitatu ya kwanza ilikuwa imefikisha maji kwa zaidi ya Watu wapya millioni 4.7 vijijini katika mikoa 17. Kufuatia mafanikio hayo, kulingana na matokeo hayo, Benki ya Dunia imeiongezea Tanzania Dola za Marekani milioni 300 na hivyo kupanua wigo wa utekelezaji kufikia mikoa 25, kwa sasa shillingi milioni 970 zimepelekwa katika kila Halmashauri kwa ajili ya kuanza utekelezaji.

Wizara ya Maji imesema mafanikio haya yamefungua rasmi milango ya uendelevu wa programu hii ambayo inafikia ukomo Julai 2025 na kufuatia hoja ya Tanzania ya kuwa na PforR Awamu ya Pili, Benki ya Dunia imeonesha utayari wa kuwa na PforR Awamu ya Pili katika kipindi cha 2025-2030.

Millard
 
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika Dkt. Victoria Kwakwa ameitaja na ameipongeza Tanzania kuwa kinara na mfano katika utekelezaji wa programu ya uendelevu wa huduma ya maji na usafi wa mazingira vijijini Mashariki na Kusini mwa Afrika na Duniani kwa kutumumia utaratibu wa malipo kwa matokeo yaani Programme for Results (PforR) ambayo inatekelezwa katika nchi zaidi ya 50 na kufadhiliwa na Benki ya Dunia.

Akizungumza na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso, Makamu wa Rais Kwakwa amesema Tanzania ni mfano bora katika utekelezaji wa Programu ya PforR na ameiomba itoe uzoefu wa mafanikio yake kwa nchi zaidi ya 23 kutoka kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika zinazoshiriki mkutano wa maji na usafi wa mazingira (WASH Leadership Summit).

Awali Tanzania ilipata Dola za Kimarekani milioni 350 katika miaka mitano lakini ndani ya miaka mitatu ya kwanza ilikuwa imefikisha maji kwa zaidi ya watu wapya millioni 4.7 vijijini katika mikoa 17. Kufuatia mafanikio hayo, kulingana na matokeo hayo, Benki ya Dunia imeiongezea Tanzania Dola za Marekani milioni 300 na hivyo kupanua wigo wa utekelezaji kufikia mikoa 25. Kwa sasa shillingi milioni 970 zimepelekwa katika kila Halmashauri kwa ajili ya kuanza utekelezaji.
402110561_1017251562898295_173582582527386250_n.jpg
402085933_317764554449513_4168799882777095474_n.jpg
 
Mradi wa kwenu nyinyi wafadhili, unatupongeza sisi kwa nini kama sio kutuma ujumbe kwamba vijimaendeleo vinavyooneka Afrika ni vile vya misaada tu.

Wafadhili wanajaribu ku justify uwepo wao na mpango mzima wa utoaji misaada na utegemezi wa nchi changa, na kulinda ajira zao kwenye miradi hii. Wanataka kutubakiza kwenye issue zao hizo hizo za visima vya maji, matundu ya vyoo, vyumba vya madarasa na vizahanati vya kugawa ARV za WHO.

Tunataka kuongeza ajira, kukuza uchumi, kujenga mihimili imara, judiciary inayoweza kufunga wahalifu, accountable leaders and legislature, civil liberties, quality healthcare and education, reliable energy. Tujipime kwa hayo.

Ningekuwa Aweso ningekataa kupokea pongezi za misaada, tena mko Ethiopia mwambie aende mwenyewe TZ akawaambie. Kwa saab inadhihirisha nyimbo za kina Juma Aweso oooh Mama ametoa hapa, Mama ametoa pale, kumbe ni uongo na utapeli mtupu!
 
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika Dkt. Victoria Kwakwa ameitaja na ameipongeza Tanzania kuwa kinara na mfano katika utekelezaji wa programu ya uendelevu wa huduma ya maji na usafi wa mazingira vijijini Mashariki na Kusini mwa Afrika na Duniani kwa kutumumia utaratibu wa malipo kwa matokeo yaani Programme for Results (PforR) ambayo inatekelezwa katika nchi zaidi ya 50 na kufadhiliwa na Benki ya Dunia.

Akizungumza na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa Maji Mhe. Jumaa Aweso, Makamu wa Rais Kwakwa amesema Tanzania ni mfano bora katika utekelezaji wa Programu ya PforR na ameiomba itoe uzoefu wa mafanikio yake kwa nchi zaidi ya 23 kutoka kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika zinazoshiriki mkutano wa maji na usafi wa mazingira (WASH Leadership Summit).

Awali Tanzania ilipata Dola za Kimarekani milioni 350 katika miaka mitano lakini ndani ya miaka mitatu ya kwanza ilikuwa imefikisha maji kwa zaidi ya watu wapya millioni 4.7 vijijini katika mikoa 17. Kufuatia mafanikio hayo, kulingana na matokeo hayo, Benki ya Dunia imeiongezea Tanzania Dola za Marekani milioni 300 na hivyo kupanua wigo wa utekelezaji kufikia mikoa 25. Kwa sasa shillingi milioni 970 zimepelekwa katika kila Halmashauri kwa ajili ya kuanza utekelezaji.
 
kuna mtu mmoja amesema Tanzania imeshika nafasi ya kwanza duniani kusambaza maji vijijini. nimejiuliza sana, dunia gani huyo mtu ametembea? viongozi wetu yapaswa wawe wanachukuliwa mzobamzoba hadi ulaya, wanazungushwe weee kama mang'ombe na warudishwe hapa waendelee na kazi. unaposema Tanzania ya kwanza duniani, jua kwamba kuna nchi hapahapa duniani hawajui nini maana ya shida ya maji, mjini na vijijini. hawajawahi kuiona. vijijini kuna maji sehemu zote kwa zaidi ya miaka 50 iliyopita, na sio maji tu, bali MAJI SAFI ambayo hauhitaji kuchemsha, hata ukienda chooni kwenye bomba ni kukinga na kunywa ni safi kama hayo ya kwenye chupa tu. nchi kama za scandinavia, maeneo ya rural areas tuseme wamezidiwa na Tanzania kweli? hivi wanatuona sisi mambuzi sana kwamba tunaweza kudanganywa kirahisi namna hiyo?
 
Tanzania imetajwa kuongoza Duniani kwa upelekaji wa huduma ya maji ya bomba Duniani kupitia program ya Lipa kwa Matokeo.

Kupitia programu hiyo jumla ya miradi 1,500 imetekelezwa vijijini na inafanya kazi na kuwezesha upatikanaji wa maji kwa vijijini imefikia 78%.

Mambo kama haya yanawachukiza sana Machadema.
Kazi iendelee 👇

--
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika Dkt. Victoria Kwakwa ameitaja na ameipongeza Tanzania kuwa kinara namba moja na mfano katika utekelezaji wa programu ya uendelevu wa huduma ya maji na usafi wa mazingira vijijini Mashariki na Kusini mwa Afrika na Duniani kwa kutumumia utaratibu wa malipo kwa matokeo yaani Programme for Results (PforR) ambayo inatekelezwa katika Nchi zaidi ya 50 na kufadhiliwa na Benki ya Dunia ambapo Wizara ya Maji kupitia programu hii imetekeleza zaidi ya miradi ya maji 1,500 ambayo imekamilika na inatoa huduma.

Akiongea na Waziri wa Fedha Dkt Mwigulu Nchemba pamoja na Waziri wa Maji Jumaa Aweso nchini Ethiopia, Makamu wa Rais Kwakwa amesema Tanzania ni mfano bora katika utekelezaji wa Programu ya PforR na ameiomba itoe uzoefu wa mafanikio yake kwa Nchi zaidi ya 23 kutoka kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika zinazoshiriki mkutano wa maji na usafi wa mazingira (WASH Leadership Summit).

Amesema awali Tanzania ilipata Dola za Kimarekani milioni 350 katika miaka mitano lakini ndani ya miaka mitatu ya kwanza ilikuwa imefikisha maji kwa zaidi ya Watu wapya millioni 4.7 vijijini katika mikoa 17. Kufuatia mafanikio hayo, kulingana na matokeo hayo, Benki ya Dunia imeiongezea Tanzania Dola za Marekani milioni 300 na hivyo kupanua wigo wa utekelezaji kufikia mikoa 25, kwa sasa shillingi milioni 970 zimepelekwa katika kila Halmashauri kwa ajili ya kuanza utekelezaji.

Wizara ya Maji imesema mafanikio haya yamefungua rasmi milango ya uendelevu wa programu hii ambayo inafikia ukomo Julai 2025 na kufuatia hoja ya Tanzania ya kuwa na PforR Awamu ya Pili, Benki ya Dunia imeonesha utayari wa kuwa na PforR Awamu ya Pili katika kipindi cha 2025-2030.

Millard
Hongera Rais Samia Kwa utashi wako wa Kisiasa kuwatua wanawake wenzako ndoo kichwani

View: https://www.instagram.com/p/CztMm3HoSVs/?igshid=MTc4MmM1YmI2Ng==
 
Sisi maji tunayafuata Kenya hizo he'll na mabomba ya kuweka njian ilhali ndani ndani hayapo...wawwapelekee mama zao.
 
Ni mikopo,Tutalipa..Mianya mipana ya wizi,ubadhirifu,Ufisadi na matumizi mabaya ya fedha Za miradi idhibitiwe Kwa kuhusisha taasisi zenye uzalendo mkubwa Kwa nchi na Taifa
 
Back
Top Bottom