Toa ushahidi kama katika dini kuna utumwa.
Akili yako unavyoipeleka ndivyo utakavyoona.Mfano mwepesi,ukiona pombe ndio inayokutatulia matatizo,utakunywa sana,kumbe ndio wajiongezea matatizo.
Wewe usiyeamini uwepo wa Mungu,akili yako umeepeleka upande wa kufikiria dini ni utumwa,wakati hakuna utumwa ndani ya dini,ila walio nje ya dini ni dhana potofu iliyojengeka ndani ya akili zao.Ni sawa na mtu anayepita kwenyw jangwa au barabara ya lami wakati wa jua kali,akiona mbele yake mang'azing'azi,akifikiria kuna maji mbele yake.Akifika ile sehemu yenye mang'azimang'azi,hakuti maji,anayaona mbele yake tena.