Naweza kusema hakuna pembetatu ambayo pia ni duara katika Euclidean geometry siyo?
Kwa sababu najua pembetatu si duara na duara si pembetatu na hivyo hakuwezi kuwa na pembatetu ambayo hapo hapo ni duara, siyo?
Kwa sababu pembetatu ambayo hapo hapo ni duara ni dhana yenye contradiction, siyo?
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana kufanyika wakati alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezi kufanyika naye hawezekani kuwepo kwa sababu ana contradiction hivyo hivyo kama pembetatu ambayo hapo hapo ni duara katika Euclidean geometry.
Kitu kinachojipinga chenyewe katika dhana, hakiwezi kuwapo katika uhalisia.
Pembetatu si duara na duara si pembetatu, hivyo hakuna pembetatu duara. Inajipinga katika dhana. Haip katika uhalisia.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote (proposotion p) kwenda kuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani ni kukanusha asili za muhimu kabisa zake yeye mwenyewe huyu Mungu (negation of p)
Kama vile hakuwezi kuwa na pembetatu ambayo ni duara katika Euclidean geometry, due to contradiction, ndivyo hakuwezekani kuwepo kwa Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote aliyeumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani, due to contradiction
This is clear and simple logic.