Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Unajua maana ya whistleblower au umekuja JF 2017..?
Wewe unashindwa hata kuelewa kilichoandikwa hapo, utajuaje maana ya 'whisleblower', kunizidi mimi?
Wewe unadhani 'blower' ana'blower' tu bila lengo?

Pia nikufahamishe tu kuwa nilikuwepo hapa JF kabla hujaota meno.
 
Hakuna cha whistleblower wala nini. Mama ana akili yake Naye ni mtanzania anaelewa kila kitu mwacheni afanye kazi.

Hawa watu wanaojifanyaga whistleblower huwa ni watu hatari sana Na wakuogopa. Wakuwaga ni watu walioshindwa interests zao hivyo ili wafanikiwe wanatangaza ubaya wa kutunga ili competitors wao wakwame.
 
Sijawahi wala sitakaa nimfikirie Majaliwa kama mtu mwema kwa hili Taifa na watu wake. Mungu anisamehe ila namuona Majaliwa kama mtu mwenye roho mbaya, mnafiki, mzandiki na mwenye tamaa. Hajawahi kuwa mkweli kwa Taifa. Hata sasa namuona ndie masta mind wa anguko la Mama. Ana jionyesha kwake kama mtu mwema lakini hafai. Muda utaongea. Nani alijua yeye na Jenister ndio wako nyuma ya sakata la sukari? Bado ikija ya mafuta ya kula na mafuta ya gari utamkuta Majaliwa.
Tulimpigia Mama kelele aanze na safu yake akaona watu wana mfundisha kazi. Akabeba uchafu wa mwenda kuzimu. Sasa wazimu una mkuta. Amebaki kusema hato kubali wakati amesha kubali. Hata madudu yaliyopo bandarini ukifuatilia mkono wa Majaliwa upo. Makesi ya hovyo mahakamani Majaliwa yupo.. Say all evils lazima yupo..
Hakuna msafi nchi hii aisee,hata PM?
 
Bila shaka ulikua mmoja wao ila kuna sehem hamkwenda sawa! Inaweza ikawa ni moja kati ya chanzo cha habari Mama hapaswi kupuuzia! Lakin kuna kauongo nadhan pia
 
Mbona nchi imeguka nchi ya kuchafuana hivi.siamini kuwa uliyoyandika ni kweli.
Sababu ya kutokuuamini ni hii

Umewataja team MAGUFULI tu ..na na cha kushangaza vifo vya badhi ya hao uliyowataja vina maswali mengi hasiyokuwa na majibu

Basi iundwe tume huru kuchunguza kashfa hii.kama ni uongo napendekeza ufungwe jela miaka 99
 
When it comes to sugar Saga, waagizaji wa sukari lazima wawe wakali… ninyi ndio chanzo cha kupandisha bei ya sukari…. inafika hatua sasa mnaatack each and ever1, sina shaka na uzalendo wa Majaliwa ila naliona kundi la wapigaji wakimchafua huyu baba, yaan unasoma andiko unaona chuki kabisa..

zipo hoja ambazo umezisema ambazo Rais samia kama kiongozi aliyekuwa awamu ya 5 na sasa sita lazima anazijua, kama Saga lingekuwa kama ulivyosema basi Mama asingekaa kimya, acheni kuchonganisha viongozi acheni watu wafanye kazi.

Hili ni andiko trash i ever seen this weekend. Mtoa hoja inaonekana ni mnufaika mkubwa wa ulanguzi wa Bidhaa ya Sukari, Rais Samia ameshatoa muelekeo kuhusu suala la sukari acheni viongozi wafanye kazi.
 
Waliopo kwenye hiyo chain wanatamani uzi ufutike. Mods mkifuta uzi tunaupandisha.

Katiba Mpya ni muhimu sana. Ili tusonge inabidi kunyonga watu.
Ukiona Mods hawajafuta uzi kama huu, basi ujue na wao teyari wana taarifa fulani au wanajua kinachoendelea.
 
Acheni watu wafanye kazi, huyu mbaba wa watu mnamuandama sana, hebu njoo na facts na sio issue za kufikirika, creating fake analytical data and facts, hizo taarifa unazoweka unasahau Rais Samia alikuwa Makamu wa Rais awamu ya 5 na walifanya kazi na Majaliwa, Matycoon wa Sukari mmeanza kazi
 
Huyu jamaa ni moja ya wahuni. Kaandika majungu. Yaani ungejua tangu mwanzo wa mradi na serikali ilivyokuwa makini kuhakikisha haiibiwi.
Kilaza kinataka kipate Airtime kupitia mgongo wa mtu. Mwandiko wako tu unaonesha jinsi ulivyo-mtupu
 
Nanukuu: "Hao mabwana wakamuhakikishia Magufuli kupata chake, naye akaingia tamaa"😁😁😁

Alieandika hii barua ni punguani kwa sababu hadi yeye ambae ni kapuku anapata taarifa hizi maana yake ni kwamba Rais wa nchi ambae ana intelijensia ya hali ya juu tayari ana taarifa hizi.

Rais anayajua yote haya ila anakula kimya kwa manufaa yake.Either na yeye anapata chake cha juu au anakaa kimya kulinda urais wake ambao hauna kibali cha wananchi.

Mwandika barua ungekuwa na akili badala ya kumwandikia Rais barua hii ulipaswa utuandikie sisi wananchi hii barua ambao ndiyo wenye nchi kisha utushauri kuwa tuiondoe CCM madarakani kwa nguvu kwa kuwa CCM ni mafisadi.Ungefanya haya ungekuwa na akili.
Mtazamo wangu ni huu: Mama anayajua yote haya ila hataki kuonekana anahusika. Hivyo, kinachofanyika ni kuzuga tu kuwa na yeye taarifa hizi ndio anazipata sasa kupitia hii barua.

Halafu ukiona Mods wameacha uzi wenye tuhuma nzito kama hizi, we ujue kuna kinachoendelea kwani siamini kama wako tayari kuona Melo anasumbuliwa na hata Melo mwenyewe sio rahisi kuruhusu uzi wenye tuhuma nzito kama huu ubaki bila mwenyeww kujiridhisha au kuwa na uhakika hatosumbuliwa.

Tukumbuke mada zingine huwa zinafutwa haraka sana tena zenye tuhuma ambazo sio nzito kama hizi zinazohusu viongozi wa serikali akiwemo na Waziri Mkuu.
 
Hili ni jambo zito linapaswa kushughulikiwa yaani Kassim anavyoongea kule kwenye kiwanda cha sukari kumbe ukweli anaujua.
Nachukia miye
 
Hii ni nzito. Jumlisha kuwa mashamba pale mbigiri walichukua wazito halafu wamekodisha wakulima ambao ni wananchi wa kawaida.
Yaani ni uchafu juu ya uchafu

Sent from my SM-G955U using JamiiForums mobile app
Sehemu kubwa ya wilaya za Morogoro ikiwemo Mvomero na Kilosa mashamba makubwa yanamilikiwa na viongozi wakubwa wa serikali ambao walijimikisha wakati wa awamu ya tatu ya serikali
 
Back
Top Bottom