Whistleblower: Kashfa nzito suala la sukari, wamo vigogo wazito

Mnataka kumtoa waziri majaliwa! Was$&@ nge watu wa msoga. Tutawapata na hicho kiichwa cha nyoka wenu, tutakipata soon.
 
When it comes to sugar Saga, waagizaji wa sukari lazima wawe wakali… ninyi ndio chanzo cha kupandisha bei ya sukari…. inafika hatua sasa mnaatack each and ever1, sina shaka na uzalendo wa Majaliwa ila naliona kundi la wapigaji wakimchafua huyu baba, yaan unasoma andiko unaona chuki kabisa.. zipo hoja ambazo umezisema ambazo Rais samia kama kiongozi aliyekuwa awamu ya 5 na sasa sita lazima anazijua, kama Saga lingekuwa kama ulivyosema basi Mama asingekaa kimya, acheni kuchonganisha viongozi acheni watu wafanye kazi. Hili ni andiko trash i ever seen this weekend. Mtoa hoja inaonekana ni mnufaika mkubwa wa ulanguzi wa Bidhaa ya Sukari, Rais Samia ameshatoa muelekeo kuhusu suala la sukari acheni viongozi wafanye kazi.
Kaka binadamu kutiliwa mashaka ni jambo la kawaida. Tunaweza kushupalia KMK hahusiki kumbe yumo.
 
Yule majaliwa hafai kabisa sijui kwa Nini mama alikunaliana naye kuwa aendelee kuwa pm. Alivyonishangaza ni pale aliponiletea majina yake eti nihakikishe yanapita kipindi kile afasi za ualimu elfu 13 zimetangazwa. Mana yake anachikiongeaga Ni tofauti kabisa na anachokitenda. Yuko pale kwa ajiri ya kumuangusha mama. Mama ashtuke mapema
Duuuuh..na YAKAPITA?
 
Mwongo mkubwa wewe unayejiita whistleblower unamtuhumu hayati JPM, Kasimu Majaliwa, Jenista Mhagama nk kwamba ni wezi.........are you serious?

Wewe unafahamika vizuri wewe ni genge la majizi yanayotafuta kumpoteza njia rais ili mpate mwanya wa kutekeleza uhujumu na dhuluma zenu na wanaowafadhili wanafahamika bayana.
 
Upo vizuri sana. Fair Competition Commission (FCC) wanatakiwa kuingilia kati swala hili kwani kunaonekana kweli kuna kupanga bei ya sukari na kuhodhi soko la sukari na hii inaondoa ushindani ambao ungemfaidisha mlaji. Naomba pia uchunguze bei ya cement na namna viwanda wanavyopanga bei yake maana nazo zinafanana au kuwa na tofauti ndogo. Kwa nini hawaruhusu uingizaji wa cement kutoka nje. Wananchi tunapigwa sana kwa huu ubia wa wanasiasa na wenye viwanda hivi (vya Sukari na cement)
 
Aisee ndiyo ushahidi wako huu.??
ushahidi wa nn wee boya. Hizi dili vyombo vya usalama wanazijua vzr sana . Hapa ni Kama wameamshwa tu wafanye kazi yao. Sababu wao wanafanya usalama wa CCM.

Unataka ushahidi i humu mtandaoni
ili mjue namna ya kujipanga na uovu wenu huu.
 
Nimesoma kwa umakini mkubwa..between the line.

**Rais unaempelekea issue/kesi hii unafikiri hajui hayo yote?
Kesi ya nyani unapeleka kwa ngedere!

**Maoni yangu: tunasumbuka na hizi syndicates za CCM ambazo zinatofautiana tu kwenye maslahi,yaani ugomvi wa kimaslahi binafsi ndani ya CCM ndio unaopelekea tofauti za kifikra na hoja kinzani(Polepole&co.),Samia won't solve anything,she'll only make the matter worse by creating another deadly cartel!

**Solution: Kuondoa hali hii ya kupokezana uraji wa kifisadi na kelele za kimakundi ya kugombea uraji wa kimaslahi binafsi ni kuleta yafuatayo:

*Katiba mpya yenye mfumo mpya kabisa,eg.tume huru.

*Kuanzisha kampeni mpya yenye kuhusisha wadau wote bila kujali vyama ili kuwaondoa viongozi maslahi wote au CCM kwa ujumla,tuanze upya.

Enough is enough!
Hiyo kampeni yenye kuhusisha wadau wote lazima uwakute hao wapigaji wa CCM
 
Yule majaliwa hafai kabisa sijui kwa Nini mama alikunaliana naye kuwa aendelee kuwa pm. Alivyonishangaza ni pale aliponiletea majina yake eti nihakikishe yanapita kipindi kile afasi za ualimu elfu 13 zimetangazwa. Mana yake anachikiongeaga Ni tofauti kabisa na anachokitenda. Yuko pale kwa ajiri ya kumuangusha mama. Mama ashtuke mapema
Duh mkuu kwa hyo zile ajira 13elfu wanasiasa waliwawekea mashinikozo wapite watu wao

Vp kuhusu Hawa watoto wa masikin ambao hawana wakuwashika mkono ?



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
ushahidi wa nn wee boya. Hizi dili vyombo vya usalama wanazijua vzr sana . Hapa ni Kama wameamshwa tu wafanye kazi yao. Sababu wao wanafanya usalama wa CCM.

Unataka ushahidi i humu mtandaoni
ili mjue namna ya kujipanga na uovu wenu huu.
Pole Mkuu, Mchana mwema.
 
Nimesoma kwa makini sana waraka alioandika mtu anayejiita mchambuzi kuhusu lile analodai kama ufisadi kwenye sekta ya Sukari. Katika maelezo yake, mtu huyu mbali na kuwataja viongozi wakuu wa serikali katika porojo lake hilo, hakuainisha ushahidi wowote unaoweza kuthibitisha hoja alizozitoa.

Lakini kikubwa nilichokiona hapa, mtu huyu hana uelewa hata kidogo wa sekta ya sukari nchini, historia yake, na kukua kwake mpaka kufikia hapa leo hii. Mtu yeyote makini akisoma porojo hii atagundua mara moja kuwa hii ni stori ya uongo, uzushi, na imejaa uzandiki wenye lengo la kumchonganisha Mheshimiwa Rais na watendaji wake wakuu ndani ya serikali, wananchi, na wawekezaji kwa nia ya kuua uchumi wa nchi. Lakini pia mtu huyu akijua fika anaandika habari za uongo tena kwa Mheshimiwa Rais, ameshindwa hata kutaja jina lake halisi, basi angalau angewataja waliomtuma.

Sasa hebu nianze kwa kumchambua mwandishi anayejiita mchambuzi katika hoja alizoziongelea. Hoja zake zimegusa maeneo yafuatayo; ulanguzi katika bei ya sukari, ufisadi uliopo katika bidhaa hiyo, kundi dogo la wazalishaji lisilo rasmi linalodhibiti upatikanaji wa bidhaa hiyo nchini, na utolewaji wa vibali vya sukari nchini.

Nirudi nyuma kidogo nimfahamishe mtu huyu kwa faida yake na kwa faida ya waliomtuma kwamba nchi yetu imetoka katika athari kubwa ya uhaba wa sukari kabla serikali haijaamua kubinafsisha viwanda vya sukari nchini. Ni dhahiri kwamba wazo la serikali la kubinafsisha viwanda hivyo na kuwaruhusu wawekezaji kuwekeza katika sekta hiyo ngumu nchini limeikomboa nchi yetu kutoka uzalishaji mdogo usiotosheleza mahitaji ya nchi na mpaka kufikia leo nakisi ya uzalishaji imebaki kidogo sana.

Ni miaka michache tu iliyopita, serikali ilikuwa ikitoa vibali vya kuagiza sukari kutoka nje ya nchi kwa zaidi ya tani 150,000 kila mwaka ili kufidia nakisi ya uzalishaji wa bidhaa hiyo nchini, lakini leo hii nakisi hiyo imepungua kutoka tani 150,000 mpaka tani 20,000 tu kutokana na kuongezeka kwa uzalishaji nchini. Haya ni mafanikio makubwa na ya kujivunia yanayotokana na sera na dira ya serikali katika sekta hii muhimu.

Kumthibitishia mchambuzi huyu, toka nchi yetu ilipopata uhuru, si yeye wala hao wafanyabiashara anaowasemea walithubutu kuwa na ujasiri wa kuwekeza katika sekta hiyo ngumu sana nchini. Wengi wao wanataka utajiri wa haraka haraka kujipatia vibali vya uagizaji wa sukari kutoka nje ya nchi jambo ambalo linadhoofisha uchumi wa Tanzania na kuifanya kuwa tegemezi katika bidhaa hiyo.

Mchambuzi anadai eti kuna ulanguzi katika bei ya sukari. Katika maelezo yake anadai kwamba ulanguzi huu unafanyika kwa njia mbili; ya kwanza ni kuamua ni kiasi gani sukari izalishwe lakini pili ni kupandisha bei kwa kudhibiti kiwango cha supply na demand. Ambacho hakielewi mchambuzi huyu ni kwamba uzalishaji wa sukari nchini unapangwa na kudhibitiwa na serikali ukizingatia uwezo wa viwanda vyote katika kuzalisha bidhaa hiyo ili kukidhi azma ya serikali ya nchi kujitosheleza katika uzalishaji wa bidhaa hiyo miaka michache ijayo.

Sijui kama mtu huyu anatambua takwimu za uzalishaji nchini. Kwa sababu, Ikiwa viwanda vimeongeza uzalishaji mpaka kufikia nakisi ya tani 20,000 tu kwa mwaka kutoka tani 150,000, huyu mtu anapata wapi ujasiri wa kusema kwamba viwanda vinaamua kuzalisha sukari kidogo kwa lengo la kupandisha bei? Mantiki ya hoja yake hii iko wapi? Kwa kumsaidia mchambuzi huyu, aende Bodi ya Sukari ili apewe takwimu za ongezeko la uzalishaji sukari kila mwaka kwa kila kiwanda. Kwa mujibu wa takwimu hizo, uzalishaji unaongezeka kwa kasi kila mwaka. Kwa hiyo hoja kwamba wazalishaji wa sukari wanapanga kiwango cha uzalishaji wa sukari kwa lengo la kupandisha bei ni uzushi na uongo uliopitiliza mipaka.

Wakati tukisherehekea miaka 60 ya uhuru wa nchi yetu bado Tanzania ina viwanda vinne tu vya sukari vinavyozalisha bidhaa hiyo nchini. Hii ni ishara tosha kwamba eneo hili ni gumu kuwekeza na inahitaji ujasiri na uzalendo wa kutosha kujitoa mhanga katika sekta hii. Vinginevyo kama huko kungekuwa na faida hiyo anayoisema mtu huyu , tayari tungekuwa na wawekezaji lukuki kwenye kilimo na viwanda hivi. Ila kama ni kuagiza tu kutoka nje ya nchi, basi kila mtu anaweza kufanya hivyo japo madhara yake ni makubwa katika kudhoofisha uchumi wa nchi yetu na hilo ndio lengo la mtu huyu na wale waliomtuma.

Sukari ni bidhaa inayotokana na mfumo wa uzalishaji kiwandani. Duniani kote, malighafi (production inputs) za uzalishaji sukari zinafahamika. Hivyo basi Bei ya sukari inatokana na gharama za uzalishaji na sio vinginevyo. Ni mwaka huu huu tumeshuhudia bei ya mafuta ya dizeli ikipanda kutoka shilingi 1,650/= kwa lita mpaka shilingi 2,450/=. Hili ni ongezeko la zaidi ya asilmia 48%. Bei ya pembejeo zote za kilimo, kuanzia mbolea, madawa ya kuua wadudu n.k, zimepanda kwa zaidi ya 100%. Hapo sijazungumzia upatikanaji wa umeme na bei yake.

Mtu huyu anathibisha uelewa wake mdogo katika sekta hii pale anapowaita wazalishaji wa sukari kama kundi dogo lisilo rasmi. Cha kwanza ni muhimu aelewe kwamba waliojiotoa mhanga kuingia katika sekta hii ni wachache mno japo na yeye kama kweli ana uchungu na uzalendo wa nchi hii, ajiunge kwa kufungua kiwanda na kulima miwa ili kuzalisha sukari lakini sio kupiga porojo mitandaoni. Lakini pili, wazalishaji wana umoja wao rasmi na uliosajiliwa kisheria na serikali unaojulikana kama (Tanzania Sugar Producers Association – TSPA) na una viongozi wake rasmi kwa utaratibu waliojiwekea.

Turudi kidogo kwenya uongo wa mtu huyu kuhusu vibali vya kuingiza sukari nchini. Ikumbukwe kuwa hapo awali zoezi za uingizwaji sukari ya nakisi lilikuwa mikononi mwa wafanyabiashara. Lakini kwa kukosa uaminifu walianza kuleta sukari nchini kiholela zaidi ya kiwango kilichohitajika kwa wakati huo, kitu ambacho kilikuwa ni hatari kwa ustawi wa viwanda vya ndani. Pili, waliingiza sukari ya viwandani kwa ajili ya matumizi ya binadamu, kitu ambacho ni hatari kwa afya za wananchi. Hivyo serikali iliamua kulikabidhi jukumu hili kwa wazalishaji wa ndani ikiwa na malengo makuu yafuatayo; kwanza ni ukweli kwamba wamiliki wa viwanda, wamefaya uwekezaji mkubwa katika viwanda hivyo, kwa hiyo haitakuwa rahisi wao kujihujumu wenyewe lakini pia watapata fursa ya kuongeza uzalishaji ili kuziba pengo hilo. Pili ni ukweli kwamba kwa kuzingatia maslahi ya wafanyabishara kujitajirisha haraka haraka, ilikuwa ni muhimu kwa serikali kudhibiti uingizaji wa sukari yenye madhara kwa binaadamu. Tatu, ni kutoa fursa ya viwanda hivi kukua ili kukuza uchumi wa ndani, kuongeza ajira ambapo mpaka sasa hivi sekta ya sukari imeajiri moja kwa moja zaidi ya watu laki moja, lakini pia kutimiza lengo la serikali kutaka Tanzania ijitosheleze katika uzalishaji wa sukari ifikapo mwaka 2025.

Nichukue fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua mchango wa wawekezaji katika kuifanya Tanzania ipige hatua kubwa za maendeleo ya kiuchumi na kutengeneza ajira za kutosha. Katika kipindi chake kifupi cha uongozi, Mheshimiwa Rais, ameonesha dira kwa kuhamasisha na kusimamia uwekezaji nchini. Tunapaswa kumpongeza sana na kumuunga mkono katika dhamira yake hii kubwa kwa maendeleo ya nchi yetu.

Lakini nitoe angalizo; watu wa aina ya huyu mchambuzi wanaotumiwa vibaya na watu wachache kwa maslahi binafsi, wasivumiliwe hata kidogo wala kuachwa kuendelea kuivuruga nchi yetu kwa kuandika maneno ya uchochezi na uongo wenye lengo la kupotosha na kuvuruga misingi endelevu ya uchumi wetu. Aina ya vitendo kama hivi vinaweza kukatisha tamaa wawekezaji wa ndani na nje.

Kwa kumalizia, naishauri serikali kuwa makini na watu wa aina hii ambao wana nia mbaya ya kumchonganisha Mpendwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan na viongozi wakuu wa serikali kwa kuzungumza maneno ya uongo na uchonganishi lakini pia kumchonganisha Mheshimiwa Rais na wawekezaji kwa maslahi yake binafsi. Viongozi wa serikali yetu waachwe wafanye kazi zao za maendeleo ya nchi kwa maslahi mapana ya taifa letu.

Mungu ibariki Afrika. Mungu ibariki Tanzania.
 
Kwanza naomba niseme wazi kuwa story hii yenye kichwa cha habari ufisadi kwenye sukari imetungwa na mtu ambae hana uelewa kabisa wa sector ya sukari ,hii story ni ya uongo,uzushi na imejaa uzandiki wenye lengo la kuchonganisha serikali,wananchi na wawekezaji kwa nia ya kuua uchumi wa nchi.

Ieleweke kuwa sector ya sukari imeajiri zaidi ya watanzania laki moja kwa ujumla wake je hao wanaopiga porojo mitandaoni wameajiri watu wangapi? Ikumbukwe kuwa Wazalishaji wa ndani walipewaa dhamana ya kuagiza sukari baada ya wafanya bishara kushindwa kuwa waaminifu wakawa wanaleta sukari nyingi kiholela na sukari ya viwanda yenye madhara kwa afya ya binadamu.

Kubwa zaidi ieleweke kuwa kabla ya wazalishaji wa ndani kuanza kuagiza sukari wakati wa nakisi ya sukari ilikuwa inaagizwa tani 150,000 kila mwaka bila kushuka kwa miaka yote, lkn baada ya wazalishaji kupewa dhamana hii ya kuagiza sukari wakati wa nakisi ya sukari, kiasi cha kuingiza sukari nchini kimeshuka kila mwaka kutoka hizo tani 150,000 mpk mwaka huu tani 30,000 pekee ndani ya miaka mitano tu, na wazalishaji wanafanya kazi usiku na mchana ili kutimiza adma ya serikali kwa upanuzi wa viwanda na mashamba unaopelekea hilo ongezeko la uzalishaji kila mwaka na muda si mrefu nchi itajitosheleza kwa sukari ya ndani.

Kuendelea kuhamasisha uagizwaji wa sukari toka nje ni kuuwa uchumi wetu wa ndani na kujenga uchumi na ajira kwa mataifa ya nje, kwa taarifa

Uwekezaji ktk kilimo cha sukari kunahitaji mitaji mikubwa na Tija yake ni ya muda mrefu sana sasa huyu mpiga porojo anapata wapi ujasiri wa kutunga story siyo na chembe ya uzalendo kwa taifa lake.

Ifike mahala tuwe serious na kuheshimu watu wanaojitoa mhanga kufanya kazi usiku na mchana kuinua uchumi wa nchi na kutowavumilia hata kdg watu wanaotumiwa kutunga story mitandaoni kwa maslahi ya watu binafsi.

Kama kuna mtu ana uchungu na uchumi wa nchi hii basi aanzishe kiwanda cha sukari kuwaunga mkono wazalishaji wa ndani sio kutetea maslahi ya wafanyabiashara wa mataifa ya nje.
 
Back
Top Bottom