Fundi Mchundo
Platinum Member
- Nov 9, 2007
- 12,803
- 11,257
Fundi Mchundo,
..huyo Mandela alikuwa wapi siku zote anakuja kusema leo? alikuwa wapi wakati wa-Congo milioni 3 wanakufa? ni hilo disco analopigiwa huko London ndiyo limemfanya aseme?
..nimeuliza kule inakuwaje Mugabe ambaye aliweza kuendesha uchumi ukakua hata kwa double digits leo hii agueze nchi kuwa mufilisi?
..pia inakuwaje nchi ambayo inakabiliwa na janga la njaa ikawekewa vikwazo na vyombo vya fedha, na zaidi ikalazimishwa kulipa madeni yake on time?
..kuna ripoti zinazomnukuu Mtanzania Peter Ngumbula, aliyekuwa head wa African desk IMF, akilalamika kwamba Zimbabwe imenyimwa fedha za budjet support kwasababu za kisiasa.
..sikumsikia Mandela, Askofu Desmond Tutu, Askofu Sentamu,...wakilaani ukatili huo wa vyombo vya fedha vya kimataifa. ndiyo maana wengine tunaona hawa wamekuwa kama vibaraka.
..kwa yeyote yule ambaye amejisumbua kufuatilia historia ya Zimbabwe, lazima ataelekeza lawama kwa wote[Mugabe,Tsivangarai,Tony Blair,ZANU,MDC,Labor Party] wanaohusika na mgogoro huu kwa kutufikisha hapa tulipofika.
..ni uhuni kwa chama cha Upinzani kupiga kampeni kwa wafadhili ili serikali iliyoko madarakani ikatiwe misaada, kwa nia ya kuifanya ichukiwe na wapiga kura, ili kukiwezesha chama cha upinzani kuingia madarakani. hicho ndicho walichofanya MDC for more than 10 yrs.
..NAOMBA NIMALIZE KWA KUSEMA KWAMBA HALI YA KISIASA IMECHAFUKA MNO ZIMBABWE KWA SASA HIVI. ZANU NA MDC WANAHUSIKA MOJA KWA MOJA KWA SIASA CHAFU ZA KUWAGAWA WANANCHI.
..KWA MAONI YANGU NI BORA JESHI LITWAE MADARAKA ZIMBABWE. SHUGHULI ZA SIASA ZISIMAMISHWE, NA BADALA YAKE SERIKALI YA MPITO IJIELEKEZE KTK KUTATUA MATATIZO YA KIUCHUMI YA ZIMBABWE.
Mandela alikuwa wapi wakati wa Sierra Leone wanauawa? Mandela alikuwa wapi wakati wa Ivory Coast wanachinjana, Mandela alikuwa wapi wakati waSomali wanachinjana, Mandela alikuwa wapi wakati wa Liberia wananyongana? Mandela ni retired president. Kuna watu wameuliza kwa nini hakutolea tamko South Afrika? Madiba anachelea sana kum'criticise' rais wake na tamko lolote kutoka nyumbani kwake itaonekana hivyo. Tofauti na Tutu. Tutu anajisemea bila kujali yuko wapi. Yeye atasema tu linalomuuma. Hawa wawili hata wangenyambaza, hauwezi kuwaita vibaraka. Kama alivyosema Madiba kwenye hilo Disco, mzigo ni mzito kwa mtu mwenye umri wa miaka 90!
Ameiba. Amewanyang'anya waliokuwa wanachangia uchumi na kuwapa mashoga zake ambao hawana nia yeyote na maendeleo ya nchi yao. Wezi wenzake. Hata sisi mara baada ya uhuru uchumi wetu ulikuwa unakuwa sana. Mpaka tulipoamua kushikawenyewe utamu. Bila maandalizi. Uka nosedive. Lakini pengine yote haya kwako ni simulizi tu. Kuwa si ajabu kiongozi kuharibu uchumi wa nchi yake katika muda mfupi kwa maamuzi na matendo mabovu.
Vikwazo ambavyo mnang'ang'ania kutumia kama kisingizio ni kwake yeye binafsi na viongozi 140 wa serikali yake. Baada ya uchaguzi huu haramu ndiyo Marekani inafikiria kufanya vikwazo hivyo vijumuishe familia za wahusika.Hakuna trade embargo dhidi ya Zimbabwe iliyowekwa na serikali yeyote. Kama una ushahidi to the contrary, uweke humu badala ya kutumia talking points za Mugabe. Hii ni www kwa hiyo haitakuwa vigumu kupata tamko la kiongozi yeyote wa nchi za magharibi akitamka kuwekewa vikwazo vya uchumi Zimbabwe.
Hata ungekuwa wewe ungetoa hela kusupport nchi yenye inflation rate iliyo katika maelfu? Nchi ambayo badala ya kunua chakula kwa watu wake inakimbilia silaha? Nchi ambayo ime'unilaterally seize assets za raia zake na za mashirika ya kigeni? IMF misaada yake inatanguliwa na conditions. Moja ya conditions ni ku'control inflation. Nyingine ni structural adjustments. Huyo mtanzania amesema kuwa Zimbabwe ilikubali hizi conditions na muhimu zaidi, je, walishaanza kuzitimiza? Ukumbuke si lazima kukubali hizi conditions. Malaysia walikataa, wakanyimwa msaada, na bado wanapeta. Unasahau kuwa Mwalimu alitamka yeye hawezi kuzitimiza na ni moja ya sababu zilizomfanya amwachie Mwinyi? Kama ni kweli huyo bwana katamka hayo, ni yeye anayeingiza siasa. Sitoshangaa maana pengine anajipalilia kuukwaa ugavana siku za mbeleni.
Ukatili upi wa vyombo vya fedha? Mbona hata sisi tulinyimwa mpaka tulipokubaliana na masharti yao? Ulitaka Madiba, Tutu na Sentamu waseme nini? Kuwa wapeni tu kama tulivyozoea kulazimisha financial institutions zetu kutoa mikopo hata pale ambapo dhahiri wanaona kuna matatizo.
Mwenye responsibility kubwa ni yule anayetawala nchi husika. Hauwezi kusema Morgan na Mugabe wote culpability yao ni sawa.
Aha! Na si uhuni kuwafanyia wananchi wako yale anayoyafanya mugabe. Au MDC wangeomba silaha ili waingie mwituni kama walivyofanya wengi katika bara ndiyo ungewaona si wahuni? MDC mpaka leo wanadai kuwa mataifa ya nje yauwekee presha utawala wa Zimbabwe. Presha si lazima iwe sanctions.
Na bila aibu, unahitimisha kwa kupendekeza jeshi ndiyo lipewe mamlaka Zimbabwe? jeshi hilo hilo lililotangaza toka awali kuwa haliko tayari kumpigia saluti kiongozi mwingine yeyote asiye Mugabe! jeshi hilo hilo linalotumika kikamilifu katika uhalifu unaofanyika Zimbabwe? Hawa waliozawadiwa mashamba ndiyo leo unataka watatue matatizo ya uchumi Zimbabwe. Are you for real?
Amandla......