Tetramelyz
JF-Expert Member
- Apr 25, 2014
- 4,372
- 12,479
Efeso 6:10-18 SUV
[10] Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. [11] Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. [12] Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. [13] Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. [14] Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, [15] na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani; [16] zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. [17] Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; [18] kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
[10] Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. [11] Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. [12] Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. [13] Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. [14] Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani, [15] na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani; [16] zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu. [17] Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; [18] kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;