Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Sioni tatizo hata kidogo katika kauli hii....Huu ni ukweli usiopingika kwamba the public sector hapa nyumbani ni kama imekufa.Bandari ya Dar-es-salaam ni gateway ya almost 90% ya biashara za Tanzani na inafanya clearance ya USD $ 15 billion kila mwaka(60% ya GDP YETU)...Strategically and Geographically bandari hii ina nafasi kubwa kuliko hata ya Mombasa kwa sababu inatoa huduma kwa nchi 6 ambazo ni landlocked(Malawi,Zambia,DRC,Rwanda,Burundi,Uganda)Lakini uzembe na ufisadi unakwamisha sana mchango wa bandari hii katika pato la taifa.Juzi hapa tumepata taarifa kwamba bandari hii ndo ya mwisho Afrika kimapato.Sasa sijui tukiambiwa ukweli tunalalamika nini.Mikataba mibovu kama ya TICCS,ufisadi,uzembe,ukiritimba usioa wa lazima,wizi na udokozi ndo vinafanya kitega uchumi hiki kishindwe kabisa kuchangia vizuri ktk pato la taifa.Leo hii bunge linakaa na kupitisha sh 1,000/= ktk kila line ya simu ilhali tuna vitega uchumi vingi tu.Ukweli unauma lakini wenye busara wakiambiwa ukweli wanajipanga na kujirekebisha.Tujirekebishe!
 
mtu shamba nimejaribu sana kutafuta namna ya kukujibu bila kukukwaza! samahani mkuu ni dhahir huna exposure kabisa ww maana mwenendo wa fikra zako ndio kikwazo kikubwa sana cha maendeleo nchini kwetu!
Yani tunaepuka kusema facts kisa eti itifaki hairuhusu! Viongozi wetu ni wajinga na wazembe, na kama sisi wananchi tumeshindwa kuwa hold responsible tumshukuru Mungu kuwa labda dharau kutoka nje zitawaamsha!
Sasa ww unataka usifiwe uongo jamani wakati ukweli uko wazi eti ndio itifaki inazingatiwa. What utter nonsense!
Unafahamu cobnstructive criticism?
Mkuu, naomba nikupe context ya hili.

1. Nakubali kuwa kuna ukweli katika maneno ya Waziri huyo wa Kenya.

2. Pamoja na ukweli huo, viongozi huongozwa na mipaka yao katika kauli na kutenda. Mojawapo ni kutoa kauli tata kwa NCHI RAFIKI. Kama ni nchi adui kauli kama hizo zinatolewa sana. Inapotokea kiongozi wa nchi moja kutoa kauli tata kuhusu NCHI RAFIKI, hii huitwa kwa kiingereza DIPLOMATIC GAFFE! Au IRRESPONSIBLE STATEMENT.

3, Hii si kwa Tanzania tu ni pote duniani. Nchi rafiki zinaendesha shughuli zao katika KUHESHIMIANA.

4. Waziri huyo aliyatamka maneno hayo wapi? Katika mazingira gani? Alikuwa anaongea na Watanzania? Watanzania walikuwepo? Kwa nia gani?

5. By the way hata kwenye blogs za Kenya Waziri huyo amekosolewa kwa kutoa kauli hiyo.

6. Ukisoma katika post zangu, hata mimi siungi mkono uzembe wa serikali yetu na ninakosoa mengi tu. Na hata kuileta thread hii pia nia yangu ni kuchokoza mjadala unaotufanya tujikosoe zaidi.
 
Kwani alilolikosea ni nini? Unless u Tzanians stop your outdated ideologies and trash your outdated party CCM, you will always be a "family of complaining members"
 
Wanasiasa wetu wamezidi kuifanya kenya ndo roll model ya maendeleo kila mbunge akisimama utaskia wenzetu kenya lakin ki ukweli hawa watu wana dharau sana na wanapenda mashindano yasiyokua na tija.. Lakin pia kauli yake ina ukweli ndan yake bandar yetu inashindwa kuchangamkia opportunity kwa wachache kuendekeza ubinafsi na sio mawazo ya kiujamaa kama alivyosema. Tungekua na viongozi shupavu na wazalendo mfano wa mwalimu serikali ya kenya ingebidi iombe msamaha.
hawa jamaa huwa wanatudharau sana na kujiona wao wanajua kila kitu kumbe hamna lolote, wana majivuno yaliyopindukia na kujiona wana akili pengine kuliko mataifa mengine ndani ya EAC................weakness za baadhi ya viongozi wetu zimetufanya watanzania tunaonekana ni watu wa hovyo sana kumbe laa!!!!!!!!!
 
Umesema ukweli Kenya wako mbali ndomaana wanatudharau:tufa ye kazi
 
Kwa hapa sioni kosa lolote kwake. Ukweli utatuweka huru na tutauwa huru kwekli kweli.
 
Hii yoote ni kutokAna na udhaifu wa ,rais, ccm, na

Nchi ya Tanzania ina watu wengi wenye weledi na akili; lakini Kikwete ndio chanzo cha matusi yote nchi yetu inayotukanwa. Obama alipokuwa katika ziara yake hapo juzi wakenya wakatutukana kuwa wao sio OMBA OMBA!!! I am missing Chinga Ben Mkapa, with all his human failings he was a leader!!!
 
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.

There is a figment of truth in that statement; Watanzania tuko too slow; hatupendi criticism na hatuwezi self criticism; kupenda kubebwa na kulalamika kwingi sana bila vitendo; ufisadi kedekede!

Angalia madudu ambayo Dr Mwakyembe amekuwa anapambana nayo; how can we compete with Mombasa?! binafsi naichukulia kauli ya huyo waziri kama a wake up call; tubadilike; Huko nyuma Gen Kagame aliwahi kunukuliwa akisema kama angepewa bandari ya Dar, umasikini basi!
 
I liked his argument! Watanzania ujamaa umetulemaza sana tumekuwa mazezeta. Yaani pamoja na umaskini wote tulionao na kuchelewa kote huku kwa maendeleo tulikonako utakuwa mijitu inakaa hapa kuitetea na kuisimamia CCM, sasa unabaki unajiuliza hivi tuna watanzania wenye akili timamu kweli. Worse enough watu walioenda shule wamekuwa waoga, hawahoji wala hawajishughulishi na chochote chenye impact kwa taifa lao. Hii nchi ni kama ina laana hivi. Inapata viongozi wachovu, lakini wakikosolewa wakali na wapo tayari kung'oa watu meno na kucha ili waendelee kuwepo madarakani.
Ni mmoja wa wana JF ambao napenda sana michango yao,umenena mkuu ukiona mtu anaitetea sana CCM hadi mishipa ya shingo inamtoka ujue ana maslahi binafsi si bure,huwezi kuitetea maiti isizikwe unahitaji moyo wa chuma vinginevyo wenye akili zao hawatakuelewa.
 
Tulipaswa tuwe na bandari kuu zenye ufanisi si chini ya nne.
Bandari ya Dar, Mtwara, Tanga na Bagamoyo.
Lakini tupo kama konokono. tumejaa urasimu na wizi tuu katika bandari zetu.
Mizigo inacheleweshwa bila sababu.
 
huo ndo ukweli wetu, very lazy and slow na ufisadi mwingi sana.
 
Ikiwa Baba atamwambia mwanae wewe ni MJINGA SANA... basi tegemea kwamba umeshamfanya ajifikirie kuhusu ujinga wake na cha kushangaza atakuwa kama ulivyo muita. Mara nyingi sana wakati wa vikao vya Bunge kule Dodoma nimekuwa nikisikia waheshimiwa wabunge wakitoa michango yao na ili kulinganisha mambo wamekuwa wakiilinganisha Tanzania na nchi ya Kenya kama nchi ya mfano.

Please Tanzanian Officials DON'T MAKE KENYA AS YOUR ROLL MODEL COUNTRY FROM NOW ON.

Huyu waziri wa Kenya ameidharau nchi kwa kiasi kikubwa sana zamani tamko hilo tu lingehatarisha uhusiano wa kidiplomasia. Mfano huu ni sawa na kutwambia kwamba "Tanzania inafundishwa na mwalimu wa Kenya ambaye ni ZEZETA na bado wanafaulu mitihani, ikiwa wangefundishwa na mwalimu mwenye akili timamu wangeweza kuwa most brilliant lakini kwa bahati wanamwamini sana zezeta tuliye wapelekea"
 
Nimemsikiliza jamaa tangu anaanza mpaka alipofika kwenye kauli hiyo,hakusema kwa ubaya kama mtu alimsikilza kwa makini,ni kwamba alisema uhalisia kwamb kama watanzania tusingekuwa hivi tulivo bandari yao ya mombasa ingeshakufaa,alimaanisha kwamba element za ujamaa tulizonazo watz ndo zinaishanya bandqri ile ipo mpaka sasa kwa kuwa ujamaa unatekelezeka polepole na hauna ushindani kwa sasa.alimaanisha tu hivo hasa swala la ushindani lakini sii kwamba alisema kwa dharau inayotakiwa kujadiliwa hapa.ukwel ni kwamba tunakuwa wagumu sana katika kutekeleza mambo muhimu ama kuchangamkia fursa ambazo wenzetu hadi wanaziona na kutupiku.huu ujamaa ulishashindwa zamani hatuna budi na sisi kuuancha kabisa maaana hauna faida kwa sasa zaidi ya kutetea hasara
Ni kweli Mkuu. Kile kipindi ambacho nchini Kenya ilikuwa na ukosefu wa amani kutokana na mashambulizi Al shabaab, watalii wengi walisita kwenda huko. Hapo ndipo nchi yetu ingechukua "advantage" hiyo kuvutia watalii waje TZ, kutokana na utulivu uliyokuwepo katika nchi yetu. Lakini wapi!!!!! Sikio la kufa halisikii dawa. Hatuna wabunifu katika nchi hii kweli?
 
kwani ubaya uko wapi? Tatizo le2 wa tz hatupendi kuambiwa ukweli,tunapenda m2 anaye tujaza ujinga na kutupa misifa ya kijinga!Huo ni ukweli mtupu mawazo ya viongozi we2 ni mgando hivyo hadi yayeyuke ni muda mrefu.

Sure tusiishie kupinga bali tushughulikie changamoto zinazotukabili kwa vitendo.
 
from: cartels a threat to efficiency at port, jkia, says kamau - news - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
transport and infrastructure cabinet secretary michael kamau gestures during a meeting with the senate committee on energy and transport at the kenyatta international conference centre (kicc) july 9, 2013. On the left is infrastructure principal secretary john mosonik. Ann kamoni


waziri wa usafirishaji na miundo mbinu wa kenya bwana michael kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa tanzania kwenye kikao cha kamati ya seneti ya wizara hiyo ya usafirishaji na miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa kenyatta international conference center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine bwana kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“if the tanzanians were not people that they are; mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika jumuiya ya africa mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa rais wa rwanda, sasa hii nayo toka kwa waziri wa kenya na zingine zitafuata...


watanzania wenzangu naomba maoni yenu.

ni ukweli mchungu, tuumeze tu na tujisahihishe
 
mbona sioni kama huyo waziri kakosea! kasema ukweli ati! kama Bandari ya Dar es Salaam ingekuwa effective ni kweli bandari ya Mombasa ingekufa! Ni njia rahisi kupitia TZ kupeleka mizigo Zambia, DRC, Burundi na Rwanda kuliko kutoka Mombasa kupitia Kenya na Uganda!
 
Kwa kauli hii huyu Waziri kajitafutia matatiza, Wakenya hawatamuelewa kwa maana wanaona kama ametufumbua macho, au inawezekana hata yeye hii kauli kaitamka kwa bahati mbaya.
 
Tuache kulalamia turekebisha haya mambo nchi isonge mbele, alichosema ndio uhalisia.
 
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013



kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.

Tuwe wakweli hii siyo dharau bali ni ukweli mtupu. tukisha kubali ukweli bila kupepesa tutafute dawa. Hivyo kusema waziri huyo alitoa kauli ya dharau kuhusu tanzania tutakuwa tunamuonea.
 
Back
Top Bottom