Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Ni kweli aliyosema,kama Bandari ya Tanga ingepewa kipa umbele,na kufanya kla njia za kuvutia wenye mizigo kushusha Tanga,Bandari ya Mombasa ingekufa,lakini Bandari ya Tanga kushusha mzigo,ni Tabu tupu.Watu wanatoka Tanzania nchi yenye Bandari,na kushusha mizigo yao kenya,kutokana na urasimu uliyopo.Kwa nini bandari ya Tanga haipewi uwezo na kusimamiwa,na kuweka iwe kivutio kwa meli za mizigo?Tungepata mapato mengi kupitia Bandari hii.

location ya bandari ya tanga pale haifai kwa meli kubwa kina kifupi,,ila nnavoskia ilipaswa kujengwa bandari kuelekea pangani huko ila mpango ukawekwa pangoni naskia sasa umehamishiwa bwagamoyo!
 
Lakini kawambia ukweli sema nyie hamtaki kukubali

Sasa huo mkutano ulikuwa ni wa kuwaambia Watz ukweli ama? Sasa kulala kwetu si ndio faida kwao! Sidhani kama huyo jamaa anaipenda Tz kiivo mpaka atuambie ukweli, kana kwamba anataka tuchangamke tuinuke ili tuendelee kama wao au hata kuwazidi. Halafu mwisho wa siku iweje? Hizi ni kauli za wivu hasa pale unapoona jirani yako anapiga hatua kimaendeleo. Na bandari ya bgmyo inakuja, gesi, n.k. ngoja tu wataongea mengi.
 
Wala siyo ujamaa ni ufisadi, na kama kwa mtazamo wake anatusaidia kujifahamu sioni kosa lake. wala Tanzania hatuko maskini kabisa, nasubutu kusema Kenya ni maskini zaidi kuliko sisi usiangalie GDP yao ambayo uchumi uko mikononi mwa asilimia 10% ukawasifia wakati watu wanalala ndani ya mabox Tz hiyo kitu hakuna, wala wasitutishe.
 
Hajakosea lolote. Amesema kweli tupu! Kimkakati TZ ina faida nyingi dhidi ya Kenya. Ardhi kubwa na nzuri, amani na utulivu, bandari tatu, mbuga za wanyama, madini, maliasili na idadi kubwa ya watu. Ujinga wetu, siasa za hovyo, uvivu, kupenda majungu, uongo na uongozi wa hovyo ndio sababu ya kuachwa nyuma na wakenya. Tukubali kukosolewa na tubadirike.
 
Nasisitiza siasa za hovyo ni siasa zinazowezesha mambumbumbu, wezi, mafisadi, wavivu na wajinga kuweza kuchukua nafasi za juu kabisa ktk uongozi wa taifa. Bila uongozi thabiti wenye uwezo nchi itaendelea kukosa dira na kunyonywa hovyo mpaka na wajinga.
 
Wanasiasa wetu wamezidi kuifanya kenya ndo roll model ya maendeleo kila mbunge akisimama utaskia wenzetu kenya lakin ki ukweli hawa watu wana dharau sana na wanapenda mashindano yasiyokua na tija.. Lakin pia kauli yake ina ukweli ndan yake bandar yetu inashindwa kuchangamkia opportunity kwa wachache kuendekeza ubinafsi na sio mawazo ya kiujamaa kama alivyosema. Tungekua na viongozi shupavu na wazalendo mfano wa mwalimu serikali ya kenya ingebidi iombe msamaha.

ndo aina ya serikali ya propaganda tuliyoko nayo na isiyojua kujifunza hata kwa makosa yao wenyewe
 
Jamani hebu tuachane na mambo ya wakenya kwa sasa wakuu, wakitaka kusema waseme tu sisi tuangalie nini tunafanya! Kwani hamjiulizi kwanini mwanzo walikuwa hawasemi negative kuhusu Tanzania? Ni wazi kuwa speed yetu inawatisha, they are not at easy tena kuhusu TZ, wanaona kabisa with no time tutawapita mbali tu kiuchumi, lets not focus on them! Waseme tu watakacho. Kweli tuna matatizo yetu fulani fulani hasa ya kiuongozi lakini uchumi wa TZ unausogelea sana wa Kenya kwa sasa.

Ntashukuru kupata takwimu za kiuchumi. Nijuavyo wako mbali sana kiuchumi na wako serious kuulinda uchumi wao. Niliwahi kushuhudia containers za maua zinavyoondoka Jomo Kenyatta kwenda Ulaya, Amerika kusini na kaskazini na Australia na New Zealand. Idadi ya containers kwa siku nilishangaa sana.
 
Jamani mimi niliwahi kufanya kazi serikalini. Kule kuna watu wengi wazuri. Smart guys. Tatizo ni attitude. Wengi ni wezi, wavivu, demotivated na wanawaza ULAJI ktk kila kitu and any initiative. Tabia hii ipo katika sehemu kubwa ya watendaji wa serikali ktk ngazi zote. Hili ndio tatizo kubwa. Hakuna kazi bila wizi kule!
 
Katuambia ukweli lakini kakosea kidogo kwenye ujamaa. Moja ya tatizo kubwa la bandari ya Dar ni kuendeshwa kimagumashi kufaidisha wachache. Bandari yetu imekaa vizuri strategically kuhudumia nchi zisizo na bandari lakini kutokana na uzembe,ukiritimba, wizi na miundo mbinu hafifu hatuwezi kutoa ushindani wa kibiashara kwa bandari ya Mombasa. Uongozi mbovu kuanzia ngazi za juu serikalini hadi bandarini haujachukua hatua madhubuti kuboresha bandari ya Dar ambayo ingeweza kuchangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa. Tukiichukulia hoja ya Waziri kama changamoto tunaweza kuwa mbali.
 
Kwani alilolikosea ni nini? Unless u Tzanians stop your outdated ideologies and trash your outdated party CCM, you will always be a "family of complaining members"

I agree. Hususan hiki chama. Ni kizee na kimechoka sana. Hakiwezi kuwa na mawazo, nguvu na mkakati mpya. Hakiwezi.
 
we acha mawazo finyu jifunze kutoka kwa wenzio walikuwa mbele na siyo kuwa na mawazo kigamba hatutaendea kwa staili hiyo
Kajifunze kwanza kuandika pengine itasaidia zaidi kuliko kuwasifu watu ambao ni makapuku kama sisi/
 
Watz wanaomsapoti huyu nyang'au nashindwa kuwaelewa kabisa. Hii ni dalili sasa kua utaifa kwishney kabisa. Pengine sasa JKT irejeshwe kwa lazima na kila ajiitaye mtz aende kufunzwa upya utaifa nakulitetea taifa hili tukufu tulojaaliwa na Mola na kurithishwa na mababu zetu waliopinga kila aina ya dharau na ujivuni wa wageni na wakoloni.

Hamna nchi yeyote ilioendelea duniani ambayo wananchi wake wako indenial na kudhani nje ndio kuzuri.. huyu nyang'au anatuita sisi wajamaa wakati sote tunajua Ujamaa ulishakwisha nchini tangu enzi za Mwinyi, Nyang'au anatuita wajamaa as a figure of speech kuonesha hatuna mafikara ya kimaendeleo na watz majuha wanamshangilia. Sasa hujiulizi mbona nnchi nyingi jirani na Kenya zina bandari lakini amejilinganisha na Tz, ukwlei ni kwamba wanajua sisi ni threat kwao na ndio maana wanatutajataja kudhihiri hofu yao. Tunachotakiwa kufanya ni kusimama kama kitu kimoja kuijenga na kuipenda nchi yetu na vizazi vyetu, tukianza kupambana na kumuunga mkono mgeni hatutoeza kusimama/
 
Tusipende sana kusifiwa, sometimes ni vizuri kuambiwa ukweli japo huwa unauma,

Wakati bandari ya Tanga ipo karibu sana na Mombasa, watanzania wengi walianza kuitumia ila kutokana na ujanja ujanja na ubinafsi wakaamua kuifanya isiweze kutoa huduma ya kiwango cha juu kwa watu wa maeneo hayo. Frankly speaking watu wengine wanaoishi hata Dar huamua kupitisha mizigo yao mombasa kutokana na ubabaishaji mwingi wa mamlaka za bandari hapa tz.
 
Kasema kweli tena nampongeza maana watanzania walishalala na wakiamshwa huwa wanalalamika. Unataka wakenya watupongeze kwa lipi?
 
Watanzania mkiambiwa ukweli, mnakuwa wakali.... manataka vita, sasa hao wakenya tuwapige vita sasa.
infact jamaa kasema kweli bandari zetu mambo sio mazuri..hata Mwakyembe anakubali, ndio mana kila kukicha wanafukuzana huko.
 
watz tukae tukijua tumezungukwa na majirani"wachawi" hivyo tusimwamini jirani yoyote yule........upande wa pili hii serikali imelala sana sijui itaamka lini:Cry::Cry::Cry:
 
Hivi kati ya ukweli na uongo nini kinauma? Hapa naona wengine hawataki tuambiwe ukweli sisi bado sana, kila kitu sababu haya yote sio ya serikeli pekee hata sisi raia. Naomba tusifanye makosa kupanga viongozi maana tatzo ndo linaanza hapa. Ebu ona mafisadi, serikali yenyew haina huruma na wananchi wake siku hizi hata simukadi tutalipia kodi wale. Watunishe matumbo yao na watoto wao..! Jamani kupanga ni kuchagua. Tuitoe ccm tuweke 'm4c' nao wakishindwa tuwape wengine. Naamini kuna chama kitafanya vzur tu. Sasa hvi kila wizara madudu dah.. Elimu matatzo. Kilimo ndo usiseme, utalii ndio mamaa tumeisha, michezo makocha wanakuja timu mwisho chamanzi,. Na hzo zingne ndo madudu tuu.! Kama serikali ikiwa inabaki hii., watu watapoteza matumain ya kuishi...! Huyo wazir anajarbu kutuonesha kuwa tunamakosa ktk uongozi na utendaji. Hv cheki bandari hii ya dsm wakenya wanaiogopa, sasa ukiwekwa mfumo mzuri italeta faida na ile ya mtwara, na tanga zote zkiboreshwa na kuweka miundombinu bora tutainua kipato., lakn hawaoni wanataka bandari ya bagamoyo tu., pale ndo nyumbani kwetu sote sio? Walipwe fidia za nyumba za kisasa wote kupsha bandari hii inaumaa., tuamke jamani
 
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.
Sioni ubaya wa maneno hayo. Kwani mlitegemea kiukweli kabisa wakenya wangependelea tz iwapiku? Ukweli ni kwamba, kama nchi, kenya kama zilivyo nchi zingine majirani, ni adui/mpinzani wa tz, na kamwe hawawezi furahia kusoma namba za nyuma za tz! Kenya ingependelea kubaki keleleni mwa EAC kiuchumi milele!
Hayo yaliyosemwa tuyapokee kama changamoto tukijua kuwa tunapaswa kuchangamka na tuache ubinafsi unaoididimiza nchi yetu.

sio swala la viongozi pekee yao bali ni la kila mtz, kwani viongozi wanatoka miongoni mwetu. Hebu jichukulie ww mwenyewe jichunguze unachangiaje ktk hali tuliyonayo nchini! Unafika ofisini kwa muda? unatimiza wajibu wako kikamilifu? Hebu fikiria usumbufu usio wa lazima uliopo bandarini kwetu. Fikiria hao watoa huduma ambao kimsingi wamesaini mikataba ya ajira na wanajua majukumu yao kabisa...lakini unakuta anapotezea muda na hela watu wengi sana. Huyo akipandishwa cheo anaendeleza mchezo huo huo...badala ya kupeleka mambo haraka haraka ktk kufanya maboresho ya bandari, fungu linakuwa 'diverged' sehemu kusiko, badala yake miundombinu inazidi kuchoka, na huduma zinazidi kudolola! Watu kama hawa wanao acha majukumu yao na kuweka 'bureaucracy' ndio wanaotutukanisha na kutudharaulisha! Hao wanaoiba vipuri na bidhaa bandarini, wanaochelewesha miundombinu isiboreshwe kwa wakati ndio wanaoinufaisha bandari ya mombasa, na kama hasira wao ndio wakuelekezewa. Na ukishawanyooshea kidole kimoja, vingine vinakusuta ww mwenyewe ktk sehemu yako ya kazi. Jawabu ni kutanguliza utaifa kabla ya ubinafsi wetu.
Ni muda muafaka kwetu kupokea chanamoto kama hizi na kuzifanyia kazi badala ya kuleta utetezi usio na tija. Heshima gani inayodaiwa kupotezwa kwenye ukweli? Hapo ni sawa na kukata kuwa uko uchi wakati kiukweli hujavaa nguo! Kama hatutaki kuyasikia maneno kama haya, solution ni moja tu...tutimize wajibu wetu kwa kuweka tz mbele na ubinafsi nyuma.
Haijarishi kenya ipo mbele au nyuma yetu, kama tukihakikisha utaifa kwanza, na kuhakikisha tunatimiza wajibu wetu...tutaboresha maisha ya wananchi watz...na kwa mapenzi ya Mungu...kenya haitaweza hata kuyaona mavumbi yetu kwani tutawaacha mbali na kuwa meza moja na nchi kama china....inawezekana!
Kila mtz mahali alipo ajihoji mwenyewe badala ya kupiga kelele kwa viongozi, tukitimiza wajibu hata huyo anaejiita ni kiongozi mbona hawezi kufanya ujinga!?
Ujamaa hauna tatizo hapa, mbona kuna nchi nyingi tu zimefanikiwa na ujamaa wao!? Tatizo ni sisi wenyewe kutotimiza wajibu...tena kwa kuwa hatupendi kuambiwa maneno tusiyotaka kuyasikia...mie naomba wazidi tu kuyasema ili tupate hasira ya kuweka utaifa kwanza! tz ni kama 'sleeping giant' ktk EAC! I would like it to be unleashed!
Hata adui yako ukimsikiliza kwa makini unaweza pata vitu vya kukusaidia!
 
Back
Top Bottom