Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Mwanaukweli

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2007
Posts
4,789
Reaction score
1,732
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.
 
Wanasiasa wetu wamezidi kuifanya kenya ndo roll model ya maendeleo kila mbunge akisimama utaskia wenzetu kenya lakin ki ukweli hawa watu wana dharau sana na wanapenda mashindano yasiyokua na tija.. Lakin pia kauli yake ina ukweli ndan yake bandar yetu inashindwa kuchangamkia opportunity kwa wachache kuendekeza ubinafsi na sio mawazo ya kiujamaa kama alivyosema. Tungekua na viongozi shupavu na wazalendo mfano wa mwalimu serikali ya kenya ingebidi iombe msamaha.
 
Wanasiasa wetu wamezidi kuifanya kenya ndo roll model ya maendeleo kila mbunge akisimama utaskia wenzetu kenya lakin ki ukweli hawa watu wana dharau sana na wanapenda mashindano yasiyokua na tija.. Lakin pia kauli yake ina ukweli ndan yake bandar yetu inashindwa kuchangamkia opportunity kwa wachache kuendekeza ubinafsi na sio mawazo ya kiujamaa kama alivyosema. Tungekua na viongozi shupavu na wazalendo mfano wa mwalimu serikali ya kenya ingebidi iombe msamaha.
Ndicho hicho nachosema.

Viongozi wetu hawachangamki mpaka majirani wanatudharau.

Lakini kwa Waziri kutamka maneno hayo ni kosa la kidiplomasia. Nchi rafiki/mshirika lazima iheshimiwe katika kauli za viongozi.
 
Jamani hebu tuachane na mambo ya wakenya kwa sasa wakuu, wakitaka kusema waseme tu sisi tuangalie nini tunafanya! Kwani hamjiulizi kwanini mwanzo walikuwa hawasemi negative kuhusu Tanzania? Ni wazi kuwa speed yetu inawatisha, they are not at easy tena kuhusu TZ, wanaona kabisa with no time tutawapita mbali tu kiuchumi, lets not focus on them! Waseme tu watakacho. Kweli tuna matatizo yetu fulani fulani hasa ya kiuongozi lakini uchumi wa TZ unausogelea sana wa Kenya kwa sasa.
 
kwani ubaya uko wapi? Tatizo le2 wa tz hatupendi kuambiwa ukweli,tunapenda m2 anaye tujaza ujinga na kutupa misifa ya kijinga!Huo ni ukweli mtupu mawazo ya viongozi we2 ni mgando hivyo hadi yayeyuke ni muda mrefu.
 
kwani ubaya uko wapi? Tatizo le2 wa tz hatupendi kuambiwa ukweli,tunapenda m2 anaye tujaza ujinga na kutupa misifa ya kijinga!Huo ni ukweli mtupu mawazo ya viongozi we2 ni mgando hivyo hadi yayeyuke ni muda mrefu.
Wewe kama huoni ubaya nenda basi huko uhamie Kenya unakowaona wa maana. Tuachie Tz yetu na ujamaa wetu.
 
I liked his argument! Watanzania ujamaa umetulemaza sana tumekuwa mazezeta. Yaani pamoja na umaskini wote tulionao na kuchelewa kote huku kwa maendeleo tulikonako utakuwa mijitu inakaa hapa kuitetea na kuisimamia CCM, sasa unabaki unajiuliza hivi tuna watanzania wenye akili timamu kweli. Worse enough watu walioenda shule wamekuwa waoga, hawahoji wala hawajishughulishi na chochote chenye impact kwa taifa lao. Hii nchi ni kama ina laana hivi. Inapata viongozi wachovu, lakini wakikosolewa wakali na wapo tayari kung'oa watu meno na kucha ili waendelee kuwepo madarakani.
 
kwani ubaya uko wapi? Tatizo le2 wa tz hatupendi kuambiwa ukweli,tunapenda m2 anaye tujaza ujinga na kutupa misifa ya kijinga!Huo ni ukweli mtupu mawazo ya viongozi we2 ni mgando hivyo hadi yayeyuke ni muda mrefu.
Waziri anazuiwa na itifaki kutamka kauli tata zinazohusu nchi rafiki au nchi washirika.

Kumbuka Kenya tuko nao katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Jumuiya ipo katika kuendelea kuongeza ushirikiano kufikia muunganiko wa sarafu. Kauli kama hizi zinajenga kutoaminiana katika nchi na zinarudisha nyuma ushirikiano huo.
 
kwani ubaya uko wapi? Tatizo le2 wa tz hatupendi kuambiwa ukweli,tunapenda m2 anaye tujaza ujinga na kutupa misifa ya kijinga!Huo ni ukweli mtupu mawazo ya viongozi we2 ni mgando hivyo hadi yayeyuke ni muda mrefu.

Nimemsikiliza jamaa tangu anaanza mpaka alipofika kwenye kauli hiyo,hakusema kwa ubaya kama mtu alimsikilza kwa makini,ni kwamba alisema uhalisia kwamb kama watanzania tusingekuwa hivi tulivo bandari yao ya mombasa ingeshakufaa,alimaanisha kwamba element za ujamaa tulizonazo watz ndo zinaishanya bandqri ile ipo mpaka sasa kwa kuwa ujamaa unatekelezeka polepole na hauna ushindani kwa sasa.alimaanisha tu hivo hasa swala la ushindani lakini sii kwamba alisema kwa dharau inayotakiwa kujadiliwa hapa.ukwel ni kwamba tunakuwa wagumu sana katika kutekeleza mambo muhimu ama kuchangamkia fursa ambazo wenzetu hadi wanaziona na kutupiku.huu ujamaa ulishashindwa zamani hatuna budi na sisi kuuancha kabisa maaana hauna faida kwa sasa zaidi ya kutetea hasara
 
HAKUNA KEJELI, AMESEMA UKWELI

UNGEONA JAMA WA BANDARINI WANAVYOFANYA KAZI, UNGEDHANI NI VIBOKO NA VIFARU WAMETEULIWA KUMUVUZISHA MAKONTENA TETU PALE

tuko very slow
 
ukweli unauma.i duly support the statement made by a kenyan minister.ujamaa kwa namna flani umetulemaza sana.
 
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
"If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,".

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.

heshima hairudi kwa maneno.......
 
Hii yoote ni kutokAna na udhaifu wa ,rais, ccm, na
 
Ukweli huwa unauma daima!kama viongozi wetu wameamua kufukuzana na wamachinga na waandamanaji mitaani huku wakiwaacha wawekezaji wa kigeni wakiendelea kujichotea rasilimali zetu kwa raha zao tena kwa misamaha ya kodi lukuki,huku wakiyapa visogo mambo ya maendeleo leo hii reli ya kati imekufa mizigo toka bandari ya dsm kwenda nchi jirani kama DRC,BURUNDI,RWANDA hakuna tena!kwa hiyo Taifa linapoteza mapato/fedha za kigeni hivi hivi.unategemea wakenya wasitoe kauli za kejeli!?viongozi wetu wapo bize kufungua kesi mahakamani kupinga ushindi wa chaguzi mbalimbali za mwaka 2010. Siasa inatumiwa vibaya inawagawa wa tz na kuleta chuki baina ya tabaka tawala v/s watawaliwa.!
 
Hivi...ni nini role ya waziri wa mambo ya nje, waziri wa ushirikiano wa afrika mashariki, na wabunge wa afrika mashariki katika hizi choko choko na dhiaka ambazo viongozi mbali mbali wa Kenya, Uganda na Rwanda wanazitupa kwetu!?
 
Amezungumza ukweli mtupu kasoro yake amechanganya itikadi ya nchi yetu na uwajibikaji kwani ni vitu mbalimbali
 
Without circulating arround the core meaning the man intended to publicize that"Tanzanian way of thinking and doing things was of benefit to the one who knows"...ni kama aina fulani ya kejeli ila yenye ukweli ndanimwe,leo pamoja na ujamaa kufa bado athari zake zipo,ukitaka kuamini fuatilia chain za ufisadi nchini utacheka yaani ni full ujamaa.
 
I liked his argument! Watanzania ujamaa umetulemaza sana tumekuwa mazezeta. Yaani pamoja na umaskini wote tulionao na kuchelewa kote huku kwa maendeleo tulikonako utakuwa mijitu inakaa hapa kuitetea na kuisimamia CCM, sasa unabaki unajiuliza hivi tuna watanzania wenye akili timamu kweli. Worse enough watu walioenda shule wamekuwa waoga, hawahoji wala hawajishughulishi na chochote chenye impact kwa taifa lao. Hii nchi ni kama ina laana hivi. Inapata viongozi wachovu, lakini wakikosolewa wakali na wapo tayari kung'oa watu meno na kucha ili waendelee kuwepo madarakani.
Sasa hapo ujamaa umetulemaza kivipi?
 
Back
Top Bottom