Bongolander
JF-Expert Member
- Jul 10, 2007
- 5,067
- 2,226
Wanasiasa wetu wamezidi kuifanya kenya ndo roll model ya maendeleo kila mbunge akisimama utaskia wenzetu kenya lakin ki ukweli hawa watu wana dharau sana na wanapenda mashindano yasiyokua na tija.. Lakin pia kauli yake ina ukweli ndan yake bandar yetu inashindwa kuchangamkia opportunity kwa wachache kuendekeza ubinafsi na sio mawazo ya kiujamaa kama alivyosema. Tungekua na viongozi shupavu na wazalendo mfano wa mwalimu serikali ya kenya ingebidi iombe msamaha.
Mkuu ukianza kuangalia yanayoendelea Tanzania kwa sasa ni lazima tukubaliane na jinsi tunavyodharauliwa. Dharau tumejitafutia wenyewe, wanaposema kuwa tunaakili mgandao inatokana na tunavyofanya mambo yetu. Mfano mzuri kabisa ni bandari yetu uliyoitaja.
Kama unaweza kukumbuka huko nyuma, Nyerere akiongea watu walikuwa wanasikiliza, na watu wakitaka kufanya jambo lolote kwenye nchi zao walikuwa wanakuja Tanzania.
Leo hata vikao muhimu vya kikanda nchi yetu inawekwa pembeni, sasa East African community inaanza kuonekana kuwa ni ya Kenya, Rwanda na Uganda. na kama utakuwa umefuatulia unaweza hata kusoma hapa JF anayosema Kagame kuhusu Tanzania na rais wetu.
Kutoka nchi iliyoheshimika duniani na Afrika nzima, na kuwa nchi ambayo Kagame anayweza kumkejeli rais wake, serikali yake na hata kumtishia, siwezi kushangaa waziri wa kenya kusema anayosema.