Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Waziri wa Kenya aidharau Tanzania

Watanzania mpotezeeni huyo juha.

Hiyo comment ya Mr. Kamau ni ya kijinga. Ni comment ya mtu ambaye hajasoma demand-and-supply. Ukweli ni kwamba bandari ya Dar hata ifanyeje haiwezi kuiua Mombasa. Na ya Mombasa haiwezi kuua ya Dar.

Kila bandari ilimradi ipo itapata wateja. Kwa kuwa kuna urahisi kwa wakenya kutumia bandari ya Mombasa kutokana na ukaribu na watanzania kutumia ya Dar kutokana na ukaribu. Wachache wanaweza kutumia bandari ya huku na kule, lakini haiwezekani mfano wakenya wote wakatumia bandari za Tanzania hata zingekuwa na ufanisi kiasi gani.

Kingine ni kwamba bandari ya Dar hivi sasa imebanwa na eneo hata uchapakazi ukiwa mzuri vipi bado kunakuwa na foleni za meli na mizigo kutokana na eneo. Ndio maana inajengwa ya Bagamoyo ambayo itaboresha mambo.
 
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.

anayo sema ni kwelin tupu.siasa za ujamaa na zidumu fikra ndio zimedidimiza nchi hii...watu hawataki facts....mara nyingi njonjo pia amekua akisema....
ingekua hii bandari imeendelezwa tangu enzi za ujamaa basi leo tungekua mbali...hivyo kwa sasa ndio kama tumeanza wakati wakenya wapo mbele....
 
Kweli kabisa ujamaa thinking ndio mawazo aliyotuwachia nyerere na ndio philosophy aliyokufa nayo. Leo hii mbongo akiona mtu kamzidi pesa basi ni fisadi, mawazo ya kijamaa hayana tofauti na ki comunist..
 
ngoja tu tudharaulike sasa, tunaelekea kukata tamaa, kila siku baba kiguu na njia kwenda kutembea angani na kubembea kwenye nchi za watu sisi huku mataifa ya nje yanatucheka na kutudharau namna hii.
 
Ukweli mtupu. Tunafanya mambo polepole ndo mana wenzetu wanatumia hii loop hole. Thanks waziri kwa kutuambia ukweli!
 
Hii yoote ni kutokAna na udhaifu wa ,rais, ccm, na

Be confident! tukufahamu wewe ni nani wa kusema rais dhaifu? tueleze umefanya nini? kukosoa ni rahisi! tueleze sifa zako na faida kwa nchi yetu! what potential do you have au kuropoka tuu?
 
From: Cartels a threat to efficiency at port, JKIA, says Kamau - News - nation.co.ke 9/7/2013


kamau.jpg
Transport and Infrastructure Cabinet Secretary Michael Kamau gestures during a meeting with the Senate Committee on Energy and Transport at the Kenyatta International Conference Centre (KICC) July 9, 2013. On the left is Infrastructure Principal Secretary John Mosonik. ANN KAMONI


Waziri wa Usafirishaji na Miundo Mbinu wa Kenya Bwana Michael Kamau, leo ametoa kauli ya dharau kwa Tanzania kwenye kikao cha Kamati ya Seneti ya Wizara hiyo ya Usafirishaji na Miundombinu. Kikao hicho kilifanyika kwenye ukumbi wa Kenyatta International Conference Center.

Wakati wa kikao hicho, pamoja na mambo mengine Bwana Kamau alisema: "iwapo watanzania wasingekuwa watu wa namna walivyo, bandari ya Mombasa ingekuwa imekufa kitambo. Kwa bahati nzuri, kwa mawazo yao ya kijamaa, hawawezi kupeleka vitu haraka"
“If the Tanzanians were not people that they are; Mombasa would have died a long time ago. Fortunately, with their Ujamaa thinking, they are not able to develop things very fast,”.

Maneno haya si maneno mazuri kutoka kwa Waziri wa nchi ambayo tunapanga kuingia nayo katika ushirikiano wa karibu katika Jumuiya ya Africa Mashariki.

Watanzania tunataka viongozi wetu wasimame imara na kuturudishia heshima mbele ya nchi za jirani na katika jumuiya ya kimataifa.

Ikumbukwe hivi karibuni tumesikia kauli za kejeli toka kwa Rais wa Rwanda, sasa hii nayo toka kwa Waziri wa Kenya na zingine zitafuata...


Watanzania wenzangu naomba maoni yenu.
Ni kweli aliyosema,kama Bandari ya Tanga ingepewa kipa umbele,na kufanya kla njia za kuvutia wenye mizigo kushusha Tanga,Bandari ya Mombasa ingekufa,lakini Bandari ya Tanga kushusha mzigo,ni Tabu tupu.Watu wanatoka Tanzania nchi yenye Bandari,na kushusha mizigo yao kenya,kutokana na urasimu uliyopo.Kwa nini bandari ya Tanga haipewi uwezo na kusimamiwa,na kuweka iwe kivutio kwa meli za mizigo?Tungepata mapato mengi kupitia Bandari hii.
 
Watanzania mpotezeeni huyo juha.

Hiyo comment ya Mr. Kamau ni ya kijinga. Ni comment ya mtu ambaye hajasoma demand-and-supply. Ukweli ni kwamba bandari ya Dar hata ifanyeje haiwezi kuiua Mombasa. Na ya Mombasa haiwezi kuua ya Dar.

Kila bandari ilimradi ipo itapata wateja. Kwa kuwa kuna urahisi kwa wakenya kutumia bandari ya Mombasa kutokana na ukaribu na watanzania kutumia ya Dar kutokana na ukaribu. Wachache wanaweza kutumia bandari ya huku na kule, lakini haiwezekani mfano wakenya wote wakatumia bandari za Tanzania hata zingekuwa na ufanisi kiasi gani.

Kingine ni kwamba bandari ya Dar hivi sasa imebanwa na eneo hata uchapakazi ukiwa mzuri vipi bado kunakuwa na foleni za meli na mizigo kutokana na eneo. Ndio maana inajengwa ya Bagamoyo ambayo itaboresha mambo.
Kwa nini Bandari ya Tanga isifufuliwe?Hata ya Bagamoyo,ikijengwa,si rahisi watu wa maeneo ya kaskazini kutumia ya bagamoyo, kwa sababu bandari ya Mombasa ni karibu zaidi kwa maeneo ya Kaskazini, kama wafanyabiashara wa Tanga,moshi,Arusha,Manyara,wangetumia Bandari ya Tanga,kwa kuweka kivutio. Ukisikiya Tanga ni ya Pili kwa mapato,ni kutokana na mizigo inayoteremshwa Bandari ya Mombasa na kupita mpaka wa Tanga wa Hororo,je ni mapato mangapi ya malipo ya bandarini,na ya kuhifadhi mizigo,na matumizi kadhaa wanaotumia watoaji mizigo Bandari ya Mombasa,tunayokosa.Bali na Ajira kwa vijana wa Ki Tanzania,wangepata kama Bandari Ya Tanga,ingefanyakazi kwa ufanisi.Mizigo mingi ya Tanzania,inashushwa Mombasa,mizigo ya Dar,Tanga,Arusha,Moshi nk.
 
Nashangaa sana watanzania wenzangu wanavyoponda ujamaa hivi tatizo ni ujamaa au ni ujinga,ufisadi na uvivu wetu? Hivi sisi ni wajamaa kuliko Wachina? Mbona wao bandari zao zina ufanisi? Tatizo ni kubwa zaidi ya ujamaa ndugu zangu
 
Sioni tatizo hata kidogo katika kauli hii....Huu ni ukweli usiopingika kwamba the public sector hapa nyumbani ni kama imekufa.Bandari ya Dar-es-salaam ni gateway ya almost 90% ya biashara za Tanzani na inafanya clearance ya USD $ 15 billion kila mwaka(60% ya GDP YETU)...Strategically and Geographically bandari hii ina nafasi kubwa kuliko hata ya Mombasa kwa sababu inatoa huduma kwa nchi 6 ambazo ni landlocked(Malawi,Zambia,DRC,Rwanda,Burundi,Uganda)Lakini uzembe na ufisadi unakwamisha sana mchango wa bandari hii katika pato la taifa.Juzi hapa tumepata taarifa kwamba bandari hii ndo ya mwisho Afrika kimapato.Sasa sijui tukiambiwa ukweli tunalalamika nini.Mikataba mibovu kama ya TICCS,ufisadi,uzembe,ukiritimba usioa wa lazima,wizi na udokozi ndo vinafanya kitega uchumi hiki kishindwe kabisa kuchangia vizuri ktk pato la taifa.Leo hii bunge linakaa na kupitisha sh 1,000/= ktk kila line ya simu ilhali tuna vitega uchumi vingi tu.Ukweli unauma lakini wenye busara wakiambiwa ukweli wanajipanga na kujirekebisha.Tujirekebishe!
Wafanyabiashara wa maeneo ya Kaskazini,ndio wanaotumia sana Bandari ya Mombasa,mikoa Ya Tanga,Arusha,Moshi,Manyara,nk.na ni mikoa yenye Biashara sana.Kwa nini isiboreshwe Bandari ya Tanga,na kuwekwa vivutio?Hawa wa mikoa hii wanashusha Mizigo Mombasa kwa sababu ya ukaribu,ukilinganisha na Dar,na pia vivutio,na kutokuwa nq urasimu,katika Bandari ya Mombasa.Tungeimarisha Bandari ya Tanga,hawa wangetumia Bandari hii,na hata Hao wakenya wangeitumia,Ni aibu Tanzania kuwa na Bandari,lakini wa Tanzania wanashusha mizigo Kenya.
 
Wanasiasa wetu wamezidi kuifanya kenya ndo roll model ya maendeleo kila mbunge akisimama utaskia wenzetu kenya lakin ki ukweli hawa watu wana dharau sana na wanapenda mashindano yasiyokua na tija.. Lakin pia kauli yake ina ukweli ndan yake bandar yetu inashindwa kuchangamkia opportunity kwa wachache kuendekeza ubinafsi na sio mawazo ya kiujamaa kama alivyosema. Tungekua na viongozi shupavu na wazalendo mfano wa mwalimu serikali ya kenya ingebidi iombe msamaha.
SIYO AMEIDHARAU BALI KAIAMBIA UKWELI. Kenya hivi sasa usafiri wao wa treni wa mijini nairobi upo wa kisasa kabisaa. ukiingia ndani ya hiyo treni utadhania upo ndani ya ndege. sasa wewe ona usafiri wako wa treni za mjini Dar. Mabehewa yana kutu na ni mwaka 1947!

Bandari ya mombasa haina msongamano na watanzania wengi huona heri waitumie bandari ya mombasa kuleta mizigo yao toka ulaya na marekani kuliko Dar Es Salaam. Kenya walikuwa na bodi ya mikopo kusoma vyuo vikuu tangia 1967 wewe umeweka bodi ya mikopo ya kusoma vyo vikuu mwaka 2005,. Hospitali yao ya mombasa ina vifaa vya kisasa na mamailion ya watanzania wapatao ajari ya kuvunjika miguu hukimbilia mombasa badala ya muhimbili kuponya kukatwa miguu.

wanafunzi wengi wa kitanzania husoma sekondari Kenya lakini hamna mkenya ajae hapa kusoma elimu ya secondari.

wewe una vyuo vya propaganda vinne( Hombolo, handeni, CCM kivukoni na yale pale yaliofanywa majengo ya uku,mbi wa mikutano chimwaga). Nitajie ni nchi gani ya hapa africa imeingia gharama za kipumbavu kujenga na kutumia pesa za umma kuendesha mavyuo ya propaganda?

Kenya shirika lao la ndege linazunguka duniani kote, wewe shirika lako la ndege ni ubungo posta tuu.

kwa hayo niliyokutajia, kwa nini usidharaulike kuwa hujui kujenga maendeleo ya watu bali ni fundi kuimalisha chama tuu?
 
sisi ni maskini lakini ujamaa huu ndio uliotuletea udugu tulionao mpaka tunalala raha msitarehe, kama huna amani hata utajiri ni bure, waarabu ni matajiri duniani lakini angalia wanavyouana, waache weweseke hao wakenya. kwao ardhi ni mali ya mtu na aradhi yote ya kenya inamilikiwa na watu wachache huku kwetu naweza nakajenga au kulima sehemu yoyote hapa nchini. tunataka nini zaidi ya haya? wasubiri miaka 5ijayo watatusilkia kwenye bomba.
 
SIYO AMEIDHARAU BALI KAIAMBIA UKWELI. Kenya hivi sasa usafiri wao wa treni wa mijini nairobi upo wa kisasa kabisaa. ukiingia ndani ya hiyo treni utadhania upo ndani ya ndege. sasa wewe ona usafiri wako wa treni za mjini Dar. Mabehewa yana kutu na ni mwaka 1947!

Bandari ya mombasa haina msongamano na watanzania wengi huona heri waitumie bandari ya mombasa kuleta mizigo yao toka ulaya na marekani kuliko Dar Es Salaam. Kenya walikuwa na bodi ya mikopo kusoma vyuo vikuu tangia 1967 wewe umeweka bodi ya mikopo ya kusoma vyo vikuu mwaka 2005,. Hospitali yao ya mombasa ina vifaa vya kisasa na mamailion ya watanzania wapatao ajari ya kuvunjika miguu hukimbilia mombasa badala ya muhimbili kuponya kukatwa miguu.

wanafunzi wengi wa kitanzania husoma sekondari Kenya lakini hamna mkenya ajae hapa kusoma elimu ya secondari.

wewe una vyuo vya propaganda vinne( Hombolo, handeni, CCM kivukoni na yale pale yaliofanywa majengo ya uku,mbi wa mikutano chimwaga). Nitajie ni nchi gani ya hapa africa imeingia gharama za kipumbavu kujenga na kutumia pesa za umma kuendesha mavyuo ya propaganda?

Kenya shirika lao la ndege linazunguka duniani kote, wewe shirika lako la ndege ni ubungo posta tuu.

kwa hayo niliyokutajia, kwa nini usidharaulike kuwa hujui kujenga maendeleo ya watu bali ni fundi kuimalisha chama tuu?

Ni kweli sisi ni maskini na ni swala la kuchelewa tu, kenye walianza kutumia rasilimali zao tangu enzi za uhuru sisi tuliziacha kwanza sasa ndiyo tunaanza kuzitumia tatizo tunazitumiaje? kwa bahati mbaya zimeangukia kwenye mikono ya wachache. Kumbuka kenya wakoloni waliwekeza sana huko kwa kujenga viwanda nk. hivyo walianza kuwa na direct contact na ulaya na us nakupata exposure zaidi yetu, Tanzania kimkakati wa ukoloni ilikuwa imeandaliwa kuwa sehemu ya kutafutia mali ghafi tu kisha kusafirishwa kenya ndiyo maana mindombinu ya reli anazunguka Tz then kenya. kenya hawana ardhi nzuri kwa kilimo na hawana rasilimali nyingi km TZ ndiyo maana wakoloni waliamua kufanya eneo la uzalishaji mali. ili mkoloni apate wafanayakazi wenye uwezo kundesha viwanda (skilled labour) aliwapa elimu bora kuliko sisi TZ kwaani watz tuliandaliwa kufanya kazi ngumu mashamabani na wachache sana kupata elimu ya ukalani. Hivyo hatuna haja ya kujilaumu sana muda bado tunao.

Katika swala la elimu nafikiri wakati wa Mwl Nyerere watz walisoma kuanzia msingi mpaka chuo bure, hakuna aliyefaulu masomo ya juu akakosa kusoma, sasa ulitaka hiyo bodi ya mikopo ya nini wakati watu walisoma bure bila gharama? secondari hata nauli ya likizo walipewa warrant ya kusafiria, bado walipewa mikate ya kula na walimu wakuwasindikiza. Tuache kulaamu kila kitu muda ndiyo huu tunamshukuru waziri wa kenya kutufumbua macho. kama uchumi wa kenya unakua kwa vyanzo vya bandari tu na viwanda wasubiri wawekezaji wanakuja baada ya kupata umeme wa uhakika, kumbuka tz kuna cheap labour kuliko Kenya, US amejenga viwanda vya magari na computer THAILAND-FORD NA CHINA-COMPUTER na IT equipments.
 
Naunga mkono hoja ya waziri Kamau...haya sasa hii ni changamoto yapaswa tuifanyie kazi kwa kuanzia ni mimi na wewe!
 
Naunga mkono hoja ya waziri Kamau...haya sasa hii ni changamoto yapaswa tuifanyie kazi kwa kuanzia ni mimi na wewe!..tena hapo uyo waziri aliogopa tu kusema "KWA UBOYA WAO"
 
Kwani alichokisema ni uongo? Hivi ni lini Watanzania tutajifunza kuukubali ukweli hata kama ni mchungu?
 
Back
Top Bottom