Waziri wa Elimu na TAMISEMI, ni sawa Wanafunzi Shule za Serikali kuambiwa waende na dissecting kit na vitabu vya tahasusi?

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
1. Mwanangu amechaguliwa kuendelea na masomo ya kidato cha tano na sita (F. V & VI) mwaka huu 2021 Shule ya Sekondari Nyantakara katika tahususi (Combination) ya Chemistry, Biology & Geography (CBG) iliyoko wilaya ya Biharamulo mkoa wa Kagera. Hii ni shule ya serikali ya Tanzania.

2. Licha ya orodha ya mahitaji mengi anayotakiwa aende nayo mfano; fagio wa kufagilia ndani, sabuni ya maji ya chooni, fagio wa kufagilia nje, ream ya kataratasi nk nk, lipo hili ambalo mimi limeniacha hoi hata kujiuliuza kulikoni hizi shule za serikali? Nimeambiwa nimnunulie mwanangu

[A.] Vitabu yote vya tahasusi (subject combinations) anayokwenda kusoma yaani CBG & Basic Applied Maths

[B.] Dissecting Kit ya somo la Bailojia

3. Nikajiuliza ina maana shule hii anayokwenda kusoma mwanangu haina vitabu? Imekuwaje inaanza kidato cha tano huku ikiwa haina vitabu? Kipi kilipaswa kuanza, majengo au vitabu na walimu kwanza? Hivi mzazi kama nanunua vitabu vyangu kwa ajili ya mwanangu, si bora asomee nyumbani sasa na siku ya mtihani aende kufanya tu?

4. Nimelileta humu tujadiliane ili tujue majigambo ya serikali kuwa imeboresha elimu Tanzania, yana maana gani kama hali iko hivi ktk shule zake?

4. Naambatanisha na Joining instructions ya shule kwa ajili ya ushahidi na reference zaidi kwa atakayetaka kuthibitisha maelezo yangu.

5. Honestly, baada ya kuipata hii fomu ya maelekezo, nimeanza kusaka fedha tu na kufikiri kumpeleka shule ya binafsi.
Screenshot_20210625-202109.png
Screenshot_20210625-202129.png
Screenshot_20210625-202139.png
 
We lalama hivo hivo wenzio sa hivi wamakaribia kumaliza topic zote,nikwambie tu kingine wamesahau calculator,Ile ni advanced level sio Olevel na ile ni kombi ya sayansi,sema siku hizi wamedilute sana paper zamani ulikuwa ukileta upuuzi sayansi unazungusha au unapata matokeo ya hovyo

Hata shule kongwe hazina kila kitu sembuse hizo za juzi?kingine kwa advance kombi za sayansi zina vitabu vingi mno huwezi tumia kitabu kimoja kwa maana shule inavitabu vyake lakini na wewe lazima uongeze vya kwako

Mzazi be positive hayo ni maisha ya mwanao otherwise useme hauna uwezo aende akaunge unge,au ukiona serikali wanazengua unaweza mpeleka private

Kama unaona elimu ni ghari,jaribu ujinga
 
Huenda kwa upande wako uko sawa, ila kwa upande wangu vitabu mimi nitamnunulia mtoto wangu bila hata kuuliza, utanisamehe tu kwa kweli mkuu.
Uko Sahihi Mkuu, yani Mzazi mwenye uelewa kabisa analalamika kisa ameambiwa Elimu bure Basi anadhani serikali ina uwezo wa kutoa Elimu yenye quality Kwa kutoa vitendea kazi vyote Kwa uwiano Sahihi
 
We lalama hivo hivo wenzio sa hivi wamakaribia kumaliza topic zote,nikwambie tu kingine wamesahau calculator,Ile ni advanced level sio Olevel na ile ni kombi ya sayansi,sema siku hizi wamedilute sana paper zamani ulikuwa ukileta upuuzi sayansi unazungusha au unapata matokeo ya hovyo

Hata shule kongwe hazina kila kitu sembuse hizo za juzi?kingine kwa advance kombi za sayansi zina vitabu vingi mno huwezi tumia kitabu kimoja kwa maana shule inavitabu vyake lakini na wewe lazima uongeze vya kwako

Mzazi be positive hayo ni maisha ya mwanao otherwise useme hauna uwezo aende akaunge unge,au ukiona serikali wanazengua unaweza mpeleka private

Kama unaona elimu ni ghari,jaribu ujinga
Kuna vitu ukiambiwa kununua vinaleta mantiki na vingine havileti. Tatizo la shule za Tanzania wanajaribu ku-complicate mambo bila sababu. Kwa mfano hili la shuka. Kwani ni lazima yawe na rangi moja? Vitu kama vitabu inaweza kueleweka lakini vitu kama dawa ya chooni, mafyekeo etc ni vitu vinatakiwa kutolewa na shule.
 
Hahahaha Yan mkuu wew n zwazwa kweli kweli hivo vitu lazima mwanafunz wa hayo masomo pamoja na pcb wawe navyo mm nimeona hayo masomo tena private sembuse government acha usipeleke mwanao atakuletea zero yako Saf tena umesau scientific calculator
 
A
Pole Mzazi... Advance siyo Elimu bure...
Tafuta Pesaaa..
😂😂😂😂
Aache ung'ombe huyu mang'aa.nunulia vifaa hivyo mtoto iende skuli aisee.usilinganishe shule ya kata sukamahela secondary School na Advance. Enzi zetu pale bukoba tuliambiwa twende na kiroba Cha senene na wazee hawakuwa wabishi kutupatia natukamaliza na kufaulu Safi kabisa
 
Wewe mzazi wewe😅

Kama unataka mwanao atumie vitabu vya A'level vya serikali ni sawa atavipata na vinagawiwa bure shuleni.

Ila utambue kuwa A'level vitabu vingi huwa ni vya nje mfano Physics na Chemistry ni Chand,Biology ni kitabu fulani hivi kinaitwa Biological Science, Advanced Mathematics kuna Pure 1,2 ,Tranter n.k.Hivi vitabu inabidi mzazi mwnyw ujipinde uvinunue.

Ila pia sio lazima kwenda navyo.Ila fanya hima umnunulie hata baadhi maana hiyo level ni habari nyingine💪
 
Kama hutaki muache mwanao abaki nyumbani, wazazi wegine ni tatizo kumnunulia mwanao vitabu unaona shida dah
No! No! No kauli mbiu elimu bure!!!!. Tukubaliane ni kauli ya kitapeli. Rudini kwa wazazi muwaelishe. Mzazi mshari hapa mtoto atashindwa kutimiza ndoto zake. Ndiyo maana watoto wanajiingiza kwenye Mambo ya kishetani kwa ajili ya kauli hizi.

Hujui watoto wa wenzako wanapata ushawishi wa ajabu kwa ajili hiyo. We tuliza ushetani.

Mpaka ufagio ? Kumbe safari ya utumwa bado ipo.
 
Vitabu lazima anunue hata Sisi tuliosoma zamani tulikuepo tunanunua tuu. Dissecting kit ni vizuri Kwa maana hiyo itakuepo ni Mali yake. Understanding biology, understanding chemistry
 
3. Nikajiuliza ina maana shule hii anayokwenda kusoma mwanangu haina vitabu? Imekuwaje inaanza kidato cha tano huku ikiwa haina vitabu? Kipi kilipaswa kuanza, majengo au vitabu na walimu kwanza?

Hivi mzazi kama nanunua vitabu vyangu kwa ajili ya mwanangu, si bora asomee nyumbani sasa na siku ya mtihani aende kufanya tu?

Hili wazo lako zuri pia, asomee nyumbani ataenda tu kufanya mitihani, na hao panya chura atawapasua hapo hapo nyumbani na wembe wa topaz.
 
Back
Top Bottom