Mawaziri wa Elimu na TAMISEMI, Shule ya Msingi Nyerere, Moshi kuna shida kubwa. Tunaomba mtusaidie

The Supreme Conqueror

JF-Expert Member
Feb 13, 2017
323
906
Habari kaka? Sisi ni wazazi wa watoto wanaosoma shule ya msingi JK Nyerere, iliyopo Manispaa ya Moshi. Mwaka jana uongozi wa shule uliitisha kikao cha wazazi na kueleza nia ya serikali ya kuigeuza shule hiyo kuwa ya mchepuo wa kiingereza (English Medium school).

Katika kikao hicho wazazi tulihoji hatma ya watoto wetu wanaosoma hapo. Tukajibiwa hakuna athari zozote zitakazotokea kwani wanafunzi wa darasa la pili hadi la 7 wataendelea na masomo yao katika mchepuo wa Kiswahili, isipokua wale watakaodahiliwa darasa la awali na la kwanza ndio wataanza na mchepuo wa kiingereza.

Lakini jana tumepigiwa simu kwamba kila mzazi mwenye mtoto shuleni aende akajaze fomu ya kumhamisha. Tukauliza kwanini wahamishwe wakati tuliambiwa wataendelea na masomo hapohapo. Na kwanini iwe ghafla hivi? Tukajibiwa DEO amesema watoto wote waondolewe.

Tukampigia simu hakupokea. Leo tumefika shuleni tukapewa hivi vikaratasi tujaze ili kuhamisha watoto wetu. Unajaza jina la mwanafunzi, darasa alilopo na shule unayotaka ahamie. Shule nyingi ziko mbali na mtoto atalazimika kupanda gari mbili kufika. Huu usumbufu ni kwa gharama ya nani?

Sisi wazazi tunaona hatujatendewa haki. Kwanini hatukushirikishwa mapema? Kama mpango ulikua ni kuondoa wanafunzi wote si wangetuambia tangu mwaka jana ili wazazi tujipange? Wanakuja kutuambia leo, zimesalia siku mbili shule zifunguliwe, wanataka tufanyeje?

Na bahati mbaya hakuna wa kutusikiliza. Hata ofisi ya Mbunge tumeenda lakini hatujasikilizwa. Tumeomba kikao na Afisa elimu lakini amekataa na kusema maelekezo aliyotoa hayana mjadala. Kama mwanzoni aliitisha kikao na wazazi, kwanini sasa hivi anaogopa kuitisha kikao kutueleza mabadiliko yaliyojitokeza? Kuna siri gani nyuma y pazia?

Hivi mtoto wa darasa la 7 unamtoa leo kumpeleka shule nyingine ataweza fanya vyema? Kwanini hili suala wamefanya kwa mabavu? Halafu kama watadahili darasa la awali na la kwanza tu kama walivyoeleza, hayo madarasa mengine yatatumika kwa ajili ya nini? Je yatabaki wazi kwa miaka 6 ijayo? Si yatageuka magofu? Kwahiyo wameona bora yageuke magofu kuliko watoto wetu waendelee kusoma hapo?

Tunaomba utusaidie kupaza sauti.

Screenshot_20240105-051349.png
 
xxx.jpeg


Sisi ni wazazi wa watoto wanaosoma shule ya msingi Kibo ambayo kisiasa ilibadilishwa jina na kuwa JK Nyerere, iliyopo Manispaa ya Moshi njia panda ya kwenda KCMC Hospital. Mwaka jana uongozi wa shule uliitisha kikao cha wazazi na kueleza nia ya serikali ya kuigeuza shule hiyo kuwa ya mchepuo wa kiingereza (English Medium school).

Katika kikao hicho wazazi tulihoji hatma ya watoto wetu wanaosoma hapo. Tukajibiwa hakuna athari zozote zitakazotokea kwani wanafunzi wa darasa la pili hadi la 7 wataendelea na masomo yao katika mchepuo wa Kiswahili, isipokua wale watakaodahiliwa darasa la awali na la kwanza ndio wataanza na mchepuo wa kiingereza.

Lakini jana tumepigiwa simu kwamba kila mzazi mwenye mtoto shuleni aende akajaze fomu ya kumhamisha. Tukauliza kwanini wahamishwe wakati tuliambiwa wataendelea na masomo hapohapo. Na kwanini iwe ghafla hivi? Tukajibiwa DEO amesema watoto wote waondolewe.

Tukampigia simu hakupokea. Leo tumefika shuleni tukapewa hivi vikaratasi tujaze ili kuhamisha watoto wetu. Unajaza jina la mwanafunzi, darasa alilopo na shule unayotaka ahamie. Shule nyingi ziko mbali na mtoto atalazimika kupanda gari mbili kufika. Huu usumbufu ni kwa gharama ya nani?

Sisi wazazi tunaona hatujatendewa haki. Kwanini hatukushirikishwa mapema? Kama mpango ulikua ni kuondoa wanafunzi wote si wangetuambia tangu mwaka jana ili wazazi tujipange? Wanakuja kutuambia leo, zimesalia siku mbili shule zifunguliwe, wanataka tufanyeje?

Na bahati mbaya hakuna wa kutusikiliza. Hata ofisi ya Mbunge tumeenda lakini hatujasikilizwa. Tumeomba kikao na Afisa elimu lakini amekataa na kusema maelekezo aliyotoa hayana mjadala. Kama mwanzoni aliitisha kikao na wazazi, kwanini sasa hivi anaogopa kuitisha kikao kutueleza mabadiliko yaliyojitokeza? Kuna siri gani nyuma y pazia?

Hivi mtoto wa darasa la 7 unamtoa leo kumpeleka shule nyingine ataweza fanya vyema? Kwanini hili suala wamefanya kwa mabavu? Halafu kama watadahili darasa la awali na la kwanza tu kama walivyoeleza, hayo madarasa mengine yatatumika kwa ajili ya nini? Je yatabaki wazi kwa miaka 6 ijayo? Si yatageuka magofu? Kwahiyo wameona bora yageuke magofu kuliko watoto wetu waendelee kusoma hapo? Tunaomba utusaidie kupaza sauti
 
Mmeambiwa watahamishwa kwenda shule nyingine, mnadhani shule ni kama dini au kabila kwamba huwezi kubadil, acheni mambo ya hovyo. Na masomo ni yale yale huko wanakohamia.
 
Poleni sana wazazi wa huko,mlichofanyiwa sio haki ni bora mngepewa taarifa mapema,hii januari ina mshikemshike
 
Hili suala limekaa ki mtambuka...

Hivi Kwanini basi shule zote zisibadilishwe to English medium..
Lakini kwani wanafikiri ndo ufaulu!? Hao walimu wanao!? Wamewafundisha lini? Resources wanazo, materials..!?

Hili haliko vizuri kabisa
 
Hivi shule ni mali ya nani? Kama wazazi ni sehemu ya wamiliki, walishirikishwa? Vile vikao na kamati za shule ambazo huongozwa na wazazi, mchango wake katika hili ukoje.

Kilichonisukuma kuchangia ni huu mtindo unaozidi kusambaa nchini ambapo shule kadhaa za msingi zinageuzwa kuwa za mkondo wa kiingereza.

Binafsi naona hili sio sawa. Ni Ubaguzi wa waziwazi. Inawezekana vipi watoto wa baba mmoja wakapata huduma tofauti kutoka kwa mzazi wao.

Kama tumekubaiiana lugha ya kufundishia iwe kiingereza basi na iwe hivyo kwa wanafunzi wa Olympio, JK Nyerere, Kazilamihunda na nyingine zote.

Pia,, uamuzi huu haukinzani na sera ya nchi ya elimu bure hadi kidato cha sita? Vinginevyo hiuo ada ya 700000 imewekwa kwa vigezo gani?

Na, mbona serikali imetangaza kuwa haifanyi biashara, haya mageuzi yameanza lini kwa serikali kujiingiza kufanya biashara?
 
Mmeambiwa watahamishwa kwenda shule nyingine, mnadhani shule ni kama dini au kabila kwamba huwezi kubadil, acheni mambo ya hovyo. Na masomo ni yale yale huko wanakohamia.
Kwenye mambo ya msingi ndipo akili ysko huonyesha huna akili ya kufikiri, unaropoka kama mlevi
 
Kilichonisukuma kuchangia ni huu mtindo unaozidi kusambaa nchini ambapo shule kadhaa za msingi zinageuzwa kuwa za mkondo wa kiingereza.

Binafsi naona hili sio sawa. Ni Ubaguzi wa waziwazi. Inawezekana vipi watoto wa baba mmoja wakapata huduma tofauti
Hili limenishangaza sana.
.yani ni kama serikali inasema sasa ' kila mmoja na lwake'...
 
Tanzania ni nchi pekee ambayo lugha inabadili hadhi ya shule! Kabla na baada ya uhuru kiingereza kilitumika kwenye shule zote nchini hata za vijijini, na hazikutukuzwa kwa kuitwa eti English Medium! Kiingereza ni utukufu ambao kukijua unatakiwa ulipie zaidi!

Ni ulimbukeni na ujinga nfiyo maana elimu ya Tanzania ni ya kiwango cha chini. Wakati ule kabla na baada ya uhuru ambapo wanafunzi wote walifundishwa kiingereza hatukuuona utukufu wowote kati yao zaidi ya kuweza kuwasiliana kwa lugha mbili yaani kiswahili na kiingereza.

Hebu tusubiri wanafunzi wote wakishahamishwa kama wataletwa mashehe na manabii kuitakasa shule.
 
Tanzania ni nchi pekee ambayo lugha inabadili hadhi ya shule! Kabla na baada ya uhuru kiingereza kilitumika kwenye shule zote nchini hata za vijijini, na hazikutukuzwa kwa kuitwa eti English Medium! Kiingereza ni utukufu ambao kukijua unatakiwa ulipie zaidi! Ni ulimbukeni na ujinga nfiyo maana elimu ya Tanzania ni ya kiwango cha chini. Wakati ule kabla na baada ya uhuru ambapo wanafunzi wote walifundishwa kiingereza hatukuuona utukufu wowote kati yao zaidi ya kuweza kuwasiliana kwa lugha mbili yaani kiswahili na kiingereza.
Hebu tusubiri wanafunzi wote wakishahamishwa kama wataletwa mashehe na manabii kuitakasa shule.
Mpaka hapo, tutakapoondoa utumwa wa akili, tutaendelea kuboronga kwa kutojua tunataka nini na tunakipata vipi.

Huyu afisa elimu pengine ni msomi" lakini amekataa kufanya mazungumzo na wazazi ili kuwaelimisha sababu za maamuzi hayo. Na hao ni wengi, wako nchi nzima, wanajificha chini ya mwavuli wa taratibu za serikali na serikali imeamua!
 
Ushauri wangu ni kwa hao wazazi wanaotarajia kuwapeleka watoto wao kwenye hiyo shule inayobadili kutoka Swahili kwenda English medium.

Ni vema wajiandae kisaikolojia na wasiwe na mategemeo makubwa kwamba watoto wanasoma english medium

Mimi ni shuhuda ninayehangaika na mwanangu sasa hivi. Kwenye ripoti ana A A A lakini cha ajabu nikimpa mtihani huo huo aufanye tena hawezi na kila shule anayofanya usaili ili nimuhamishe majibu nayopewa ni kwamba nimrudishe nyuma darasa moja ili aende sawa na wenzake

Najuta kukimbilia shule hizo za serikali zinazobadilishwa kutoka Swahili kwenda English, walimu hawabadiliki kirahisi kwenda na mazingira

NB: Maoni yangu yasichukuliwe kama nadharau shule hizo au walimu wa shule hizo. Nimetoa uzoefu wangu wa huku nilipo. Huenda huku walimu hawasimamiwi vizuri na kwingine wakisimamiwa vizuri watatoa matokeo chanya
 
Ushauri wangu ni kwa hao wazazi wanaotarajia kuwapeleka watoto wao kwenye hiyo shule inayobadili kutoka Swahili kwenda English medium.

Ni vema wajiandae kisaikolojia na wasiwe na mategemeo makubwa kwamba watoto wanasoma english medium

Mimi ni shuhuda ninayehangaika na mwanangu sasa hivi. Kwenye ripoti ana A A A lakini cha ajabu nikimpa mtihani huo huo aufanye tena hawezi na kila shule anayofanya usaili ili nimuhamishe majibu nayopewa ni kwamba nimrudishe nyuma darasa moja ili aende sawa na wenzake

Najuta kukimbilia shule hizo za serikali zinazobadilishwa kutoka Swahili kwenda English, walimu hawabadiliki kirahisi kwenda na mazingira

NB: Maoni yangu yasichukuliwe kama nadharau shule hizo au walimu wa shule hizo. Nimetoa uzoefu wangu wa huku nilipo. Huenda huku walimu hawasimamiwi vizuri na kwingine wakisimamiwa vizuri watatoa matokeo chanya
Mkuu.

Pole kwa masaibu yaliyokukuta. Nchi hii hawa watu wanaojiita watoa maamuzi wanaipeleka ndiko siko.
Wanawageuza watanzania kama wakufanyia majaribio. Wiki iliyopita maafisa elimu kata na wilaya 1750 kutoka mikoa sita nchini, walikuwa Butimba kwa semina ya siku mbili juubya mtaala mpya!

Maafisa hawa walipaswa ndani ya wiki hii kuwakusanya aalimu wa maeneo yao na kuwaelekeza juu ya nini cha kwenda kufanya kuhusu mtaala mpya! Hakuna maandalizi kama inavuotokea kwa jizo English Medium, ingawa siziungi mkono
 
Hili limenishangaza sana.
.yani ni kama serikali inasema sasa ' kila mmoja na lwake'...
Elimu NI pesa.Hakuna Elimu bure.ndo muelewage.ndo maana wakwao hutawakuta huko mnakoambiwa elimu bure.akili za kuambiwa changanya na zako.mtabakia kuwa na watu wanaojua kupiga kura tu.wenzenu wanatengeneza wapigiwa kura.
 
Back
Top Bottom