Wito kwa Waziri ya elimu, TAMISEMI na Serikali kwa ujumla

This is...

JF-Expert Member
Dec 28, 2014
4,903
4,979
Sote tunajua kwamba matokeo ya darasa la Saba mwaka 2023 yametoka.

Matokeo haya yanajumuisha ya wanafunzi waliosoma shule za serikali na wale wa sekta binafsi.

Ukiyaangalia matokeo haya utagundua kwamba shule zenye ufaulu mzuri zaidi Ni zile za binafsi ukilinganisha na zile za serikali.

Kimsingi watoto wanaosoma ktk shule za binafsi wanatoka angalao ktk zile familia za vipato vya kati na juu tofauti na hawa wa shule za serikali ambao hawana chaguo lolote zaidi ya kusoma ktk shule za serikali ambazo Zina changamoto lukuki zikiwepo uhaba wa madawati, msongamano madarasani wakati mwingine hata kufikia wanafunzi 60 ktk chumba kimoja,uhaba wa vitabu achilia mbali tatizo sugu la uhaba wa walimu hasa kwa shule za vijijini.

Katika mazingira haya ya shule za serikali kumkuta mwanafunzi ameweza kupata daraja/wastani wa alama 'A' Basi mwanafunzi huyu anahitaji pongezi na motisha chanya.Anahitaji kuangalia kwa jicho la tatu sababu Ni wachache sana.Kwa shule za serikali Ni mmoja ,wawili ,watano na pengine hamna kabisa.Ila kwa shule za binafsi kwao Ni kawaida.

USHAURI/OMBI

Serikali ihakikishe wanafunzi wote wa shule za serikali waliopata wastani wa daraja 'A' wanapewa kipaumbele kujiunga na kidato Cha kwanza ktk shule za serikali zile maalumu mfano Mzumbe,Ilboru, Tabora,Moshi,Ashira na nyinginezo.

Sioni sababu ya watoto kutoka shule binafsi za Watakatifu/Saints kupewa hizi nafasi,waendelee na utaratibu wao wa sekta binafsi sababu wanajiweza. Walishazikimbia shule za serikali tangu shule za vidudu/awali/ chekechea.

Hii ndiyo njia ya kuzisaidia familia duni kuendeleza watoto wale wenye uwezo/ vipanga wanaoachwa ktk shule za kata ambazo hazijaimarika.

Huu uwe Ni mkakati wa kuokoa hivi vipaji kutoka ktk familia maskini kule vijijini.

Kwa kufanya hivi tutaokoa watoto wote wenye vipaji kutoka ktk sekta zote binafsi na umma.Hawa binafsi wazazi wanajimudu.

NB: Unaweza kutafsiri km ubinafsi na ubaguzi lkn km tangu awali wewe km mzazi/mlezi uliona shule za umma hazimfai mwanao kwanini leo unaona kidato Cha kwanza zinamfaa? Kwanini leo unaona mzumbe Ni shule nzuri?(

Ni ukweli kwamba Hali za maisha Kuna kupanda na kushuka lkn watoto wa maskini wapewe kipaumbele kwanza. Hao wengine elimu bora wanaweza kuipata mahali popote.


Mtazamo:

1.Kila wilaya ichaguliwe shule moja ya serikali iimarishwe kwa vifaa vya kufundisha na kujifunza,mabweni na walimu wa kutosha halafu ifanywe shule ya vipaji maaalumu kimkoa na hata kikanda tuokoe vipaji.

2.Tanzania haina uhaba wa walimu bali mgawanyo mbovu/hovyo wa mgawanyo na uhamishaji wa walimu.
Unakuta shule ya mjini/manispaa Ina wanafunzi 1000 Ina walimu 30-40 lkn kule kijijini shule idadi hiyo ya wanafunzi Ina walimu 10 au 12. Na serikali iko kimya.

3.Katika mwaka wa fedha Walimu 10 wanapangwa kazi ktk halmashauri ya Wilaya lkn ndani ya halmashauri hiyo hiyo Kuna walimu 5au 7 wanapewa uhamisho kwenda shule za manispaa au nje ya mkoa kwa mwaka huo huo .Hivyo tatizo linabaki Kama lilivyo. Mwalimu anakuja na barua ya uhamisho direct toka TAMISEMI,inabaki afisa elimu kusaini tu.Japo Sasa hivi kidogo hali hii imepungua.

4.Serikali ibadilishe mtazamo wake kwamba lazima mwalimu mkuu awe na shahada/digrii moja.Uongozi Ni talanta.Wako walimu wenye shahada za uzamili lkn hata kuongoza drasa la kwanza hawawezi.Sembuse hata zamu shuleni hawawezi.Uongozi uangalie uwezo pia.Wale wenye elimu ndogo na Wana uwezo mzuri waachwe.Waandaliwe programu za kuwaimarisha ili waweze kudeliver vitu positive ktk elimu.Tunashughudia vijana waliotoka vyuoni wakipewa Ualimu mkuu na hakuna wanachojua.Hii Ni hatari Sana.

Nb:Mimi naamini ktk kuwekeza kwanza kwa WALIMU,Mwalimu anayeliowa vizuri hata km miundo mbinu siyo rafiki lkn utaona matokeo chanya.

Serikali inakazania uwekezaji ktk vitu badala ya rasilimali watu/walimu bora wanaolipwa vizuri.NA HAPA NDIPO ILIPO SIRI YASHULE BINAFSI ZINAZOFANYA VIZURI.Wekeza kwa walimu kwanza!

Sasa serikali hailipi vizuri walimu ,haina learning facilities bora ,matokeo bora yatatokea wapi.

Huwezi kushinda mechi kwa hamasa bila uwekezaji.

Wasalaamu,mwalimu kijana niliyejistaafisha baada ya miaka 12 ya kushika chaki.

Karibu!
 
Sote tunajua kwamba matokeo ya darasa la Saba mwaka 2023 yametoka.

Matokeo haya yanajumuisha ya wanafunzi waliosoma shule za serikali na wale wa sekta binafsi.
Wengi huaema wanafunzi wakifundishwa kwenye lugha mama ya kiswahili hufauli sana kiliko wanafundishwa katika kiingereza, sasa hapa inakua je english medium zina perform kuliko kiswahili medium.
 
Walimu wa serikali wanalipwa mara mbili ya wa saint...... Serikalini hawafundishi na wanaofundishi ni kuwachekesha tu wanafunzi.

Na jf inavyoshadadia mijadala ya kuwadhalilisha walimu huku wanasiasa wakionesha dharau za hadharani...... walimu wanaendelea kukusanya mitaji na kuanzisha ujasiliamali. Nakuhakikushua kuwa ifikapo 2030 nusu ya walimu watakuwa wajasiliamali.


K
 
Walimu wa serikali wanalipwa mara mbili ya wa saint...... Serikalini hawafundishi na wanaofundishi ni kuwachekesha tu wanafunzi.

Na jf inavyoshadadia mijadala ya kuwadhalilisha walimu huku wanasiasa wakionesha dharau za hadharani...... walimu wanaendelea kukusanya mitaji na kuanzisha ujasiliamali. Nakuhakikushua kuwa ifikapo 2030 nusu ya walimu watakuwa wajasiliamali.


K
Yaani mwalimu wa St. Francis Mbeya, St Mary's Mazinde Juu, St. Dominic Savio, Marian Girls/Boys, nk walipwe nusu ya mshahara wa walimu wa serikalini!!
You are not serious at all. Inawezekana unachanganya kati ya shule za taasisi za kidini dhidi ya zile za wajasiriamali wapambanaji, wanazolipa mishahara ya laki 2-5.

Halafu kama walimu wa serikalini hawafundishi; inakuwaje kwenye matokeo ya kidato cha sita shule hizo hizo za serikali zinafaulisha kwa 100%?
Yaani unashindwa kabisa kugundua changamoto lukuki kwenye shule za kata kote nchini?

Kuanzia mlundikano wa wanafunzi, kupeleka wanafunzi wote form one hata kama hawana uwezo, ukosefu wa mabweni, wanafunzi kusoma katika mazingira yale yale, ukosefu wa nyumba za walimu, ukosefu wa motisha kwa walimu, kufuta mtihani wa mchujo wa kidato cha pili, nk!!

Mapungufu yote haya huwezi kuyakuta kwenye shule za Saints! Halafu unategemea wanafunzi wote wafaulu kwa kiwango sawa!! Hilo halipo. Serikali inatakiwa kuacha siasa kwenye elimu. Full stop.
Na kama ingekuwa haifanyi siasa, viongozi wote wa serikali wasingewasomesha watoto wao shule za private.
 
Walimu wa serikali wanalipwa mara mbili ya wa saint...... Serikalini hawafundishi na wanaofundishi ni kuwachekesha tu wanafunzi.

Na jf inavyoshadadia mijadala ya kuwadhalilisha walimu huku wanasiasa wakionesha dharau za hadharani...... walimu wanaendelea kukusanya mitaji na kuanzisha ujasiliamali. Nakuhakikushua kuwa ifikapo 2030 nusu ya walimu watakuwa wajasiliamali.


K
Wewe umesoma shule gani mkuu?

Binafsi nimesoma shule za serikali tangu msingi hadi chuo; na walimu wangu wamekuwa msaada mkubwa sana kwangu. Wamenifunza mengi ambayo sikuyafahamu.
Sasa hao unaowasemea wasiofundisha sijui ni wa shule zipi labda??
 
Wengi huaema wanafunzi wakifundishwa kwenye lugha mama ya kiswahili hufauli sana kiliko wanafundishwa katika kiingereza, sasa hapa inakua je english medium zina perform kuliko kiswahili medium.
Mkuu, elimu bora inajumuisha :
1.Walimu Wenye Ari
2Wazazi Wenye malengo na watoto wao
3.Wanafunzi walio tayari kujifunza.

Hivi vyote unavipata kwenye sekta binafsi na unavikosa sekta ya umma.

Kiingerza Ni Kama kilivyo kisukuma,kihaya ,kichaga nk.Na bahati watoto wadogo Ni rahisi sana kushika lugha haraka hivyo kiingerza siyo tatizo ikiwani lugha yake darasani tangu darasa la awali.

Tatizo Ni mfumo wetu wa ELIMU.Miaka Saba lugha ya kufundishia Ni kiswahili ghafla miaka minne lugha ya kufundishia Ni kiingerza, mtoto anajitafuta Sana. Wanapata tabu Sana. Wote Mwalimu na mwanafunzi hawana msingi wa kiingereza.

Kumbuka: Kuna tofauti ya kiingereza km lugha na kiingerza km taaluma. Kuzungumza kiingereza hakuna uhusiano wowote na uwezo wa kiakili.Sababu naona wazazi wengi wanadhani mtoto kuongea kiingerza Basi ana uwezo kiakili au kitaaluma.

Rejea pale juu mwanzo
1.Mwalimu analipwa vizuri
2.Wazazi wanafuatilia kwa kina maendeleo ya watoto wao na kufanya yawapasayo.
3.mtoto anasoma ktk mazingira bora,chakula,nk
 
Wewe umesoma shule gani mkuu?

Binafsi nimesoma shule za serikali tangu msingi hadi chuo; na walimu wangu wamekuwa msaada mkubwa sana kwangu. Wamenifunza mengi ambayo sikuyafahamu.
Sasa hao unaowasemea wasiofundisha sijui ni wa shule zipi labda??
NENDA mijini Mfano DSM walimu hawafundishi. Nasema jawafundishi kabisa!

Liko wazi na hakuna anaejali!
 
Kilichoniuma kiukweli hapa home Kuna madogo tofauti tofauti nimecheki tokeo lao mmoja TU ndo anawastani wa C wengine Chali D na nikiangalia uwezo wa familia zao Awana hata uwezo wa kuwapeleka hata hizi private uchwara mnazoita za wajasi na Mali na vitoto vya kike vidogo kabisa yaani ata kuosha vyomba sizani kama vinajua nimesikitishwa Sana yaani ningekua na mamlaka mie nafikiri kuanzia mwaka huu wanafunzi wote wangepata fursa ya kuenda shule za upili wakaendelee kukua huko ningezoa wote bila kujali wastani kapataje maana katoto ka miaka 12 na 13 unakaachaje mtaani SI utapata laana ya kumnyima elimu na ndio tunatengeneza makahaba na vibaka wa kesho
 
Una akili za kimasikini na roho mbaya sana! Eti maendelee na utaratibu wao wa kusoma Shule za private!

Hivyo hata wakitaka kwenda vyuo waende private na wakitaka ajira waajiriwe private?

Mbwaa wewe?
 
Sote tunajua kwamba matokeo ya darasa la Saba mwaka 2023 yametoka.

Matokeo haya yanajumuisha ya wanafunzi waliosoma shule za serikali na wale wa sekta binafsi.

Ukiyaangalia matokeo haya utagundua kwamba shule zenye ufaulu mzuri zaidi Ni zile za binafsi ukilinganisha na zile za serikali.

Kimsingi watoto wanaosoma ktk shule za binafsi wanatoka angalao ktk zile familia za vipato vya kati na juu tofauti na hawa wa shule za serikali ambao hawana chaguo lolote zaidi ya kusoma ktk shule za serikali ambazo Zina changamoto lukuki zikiwepo uhaba wa madawati, msongamano madarasani wakati mwingine hata kufikia wanafunzi 60 ktk chumba kimoja,uhaba wa vitabu achilia mbali tatizo sugu la uhaba wa walimu hasa kwa shule za vijijini.

Katika mazingira haya ya shule za serikali kumkuta mwanafunzi ameweza kupata daraja/wastani wa alama 'A' Basi mwanafunzi huyu anahitaji pongezi na motisha chanya.Anahitaji kuangalia kwa jicho la tatu sababu Ni wachache sana.Kwa shule za serikali Ni mmoja ,wawili ,watano na pengine hamna kabisa.Ila kwa shule za binafsi kwao Ni kawaida.

USHAURI/OMBI

Serikali ihakikishe wanafunzi wote wa shule za serikali waliopata wastani wa daraja 'A' wanapewa kipaumbele kujiunga na kidato Cha kwanza ktk shule za serikali zile maalumu mfano Mzumbe,Ilboru, Tabora,Moshi,Ashira na nyinginezo.

Sioni sababu ya watoto kutoka shule binafsi za Watakatifu/Saints kupewa hizi nafasi,waendelee na utaratibu wao wa sekta binafsi sababu wanajiweza. Walishazikimbia shule za serikali tangu shule za vidudu/awali/ chekechea.

Hii ndiyo njia ya kuzisaidia familia duni kuendeleza watoto wale wenye uwezo/ vipanga wanaoachwa ktk shule za kata ambazo hazijaimarika.

Huu uwe Ni mkakati wa kuokoa hivi vipaji kutoka ktk familia maskini kule vijijini.

Kwa kufanya hivi tutaokoa watoto wote wenye vipaji kutoka ktk sekta zote binafsi na umma.Hawa binafsi wazazi wanajimudu.

NB: Unaweza kutafsiri km ubinafsi na ubaguzi lkn km tangu awali wewe km mzazi/mlezi uliona shule za umma hazimfai mwanao kwanini leo unaona kidato Cha kwanza zinamfaa? Kwanini leo unaona mzumbe Ni shule nzuri?(

Ni ukweli kwamba Hali za maisha Kuna kupanda na kushuka lkn watoto wa maskini wapewe kipaumbele kwanza. Hao wengine elimu bora wanaweza kuipata mahali popote.


Mtazamo:

1.Kila wilaya ichaguliwe shule moja ya serikali iimarishwe kwa vifaa vya kufundisha na kujifunza,mabweni na walimu wa kutosha halafu ifanywe shule ya vipaji maaalumu kimkoa na hata kikanda tuokoe vipaji.

2.Tanzania haina uhaba wa walimu bali mgawanyo mbovu/hovyo wa mgawanyo na uhamishaji wa walimu.
Unakuta shule ya mjini/manispaa Ina wanafunzi 1000 Ina walimu 30-40 lkn kule kijijini shule idadi hiyo ya wanafunzi Ina walimu 10 au 12. Na serikali iko kimya.

3.Katika mwaka wa fedha Walimu 10 wanapangwa kazi ktk halmashauri ya Wilaya lkn ndani ya halmashauri hiyo hiyo Kuna walimu 5au 7 wanapewa uhamisho kwenda shule za manispaa au nje ya mkoa kwa mwaka huo huo .Hivyo tatizo linabaki Kama lilivyo. Mwalimu anakuja na barua ya uhamisho direct toka TAMISEMI,inabaki afisa elimu kusaini tu.Japo Sasa hivi kidogo hali hii imepungua.

4.Serikali ibadilishe mtazamo wake kwamba lazima mwalimu mkuu awe na shahada/digrii moja.Uongozi Ni talanta.Wako walimu wenye shahada za uzamili lkn hata kuongoza drasa la kwanza hawawezi.Sembuse hata zamu shuleni hawawezi.Uongozi uangalie uwezo pia.Wale wenye elimu ndogo na Wana uwezo mzuri waachwe.Waandaliwe programu za kuwaimarisha ili waweze kudeliver vitu positive ktk elimu.Tunashughudia vijana waliotoka vyuoni wakipewa Ualimu mkuu na hakuna wanachojua.Hii Ni hatari Sana.

Nb:Mimi naamini ktk kuwekeza kwanza kwa WALIMU,Mwalimu anayeliowa vizuri hata km miundo mbinu siyo rafiki lkn utaona matokeo chanya.

Serikali inakazania uwekezaji ktk vitu badala ya rasilimali watu/walimu bora wanaolipwa vizuri.NA HAPA NDIPO ILIPO SIRI YASHULE BINAFSI ZINAZOFANYA VIZURI.Wekeza kwa walimu kwanza!

Sasa serikali hailipi vizuri walimu ,haina learning facilities bora ,matokeo bora yatatokea wapi.

Huwezi kushinda mechi kwa hamasa bila uwekezaji.

Wasalaamu,mwalimu kijana niliyejistaafisha baada ya miaka 12 ya kushika chaki.

Karibu!
Sifa kubwa ya masikini yeyote ni chuki
 
Una akili za kimasikini na roho mbaya sana! Eti maendelee na utaratibu wao wa kusoma Shule za private!

Hivyo hata wakitaka kwenda vyuo waende private na wakitaka ajira waajiriwe private?

Mbwaa wewe?
Sifa ya masikini ni chuki
 
Mkuu ushauri wako ni mbovu, mi nadhani ungeshauri sheria zetu ziwabane viongozi wote wa umma wapeleke watoto wao kwenye hizi shule za umma, uone ndani ya mwaka mmoja mazingira yatabadilika haraka. Kusema eti watoto wanaosoma shule binafsi wasipewe vipaumbele huo ni ushamba, inawezekana mtoto anatoka familia masikini kapata mfadhili au mzazi wake alimpeleka baadae akapata matatizo ama kufariki n.k.
 
Back
Top Bottom