Swali langu kwa Mh. Juma Duni ni hili.. Hiyo serikali imeundwa na watu wa vyama gani? Je, kuna mjumbe hata mmoja kutoka chama kingine chochote kilichosajiriwa Zanzibar aloshirikishwa kuunda umoja huo? maana wagombea wote wa vyama hivi walikuwa WAZANZIBAR wakiwakilisha wanachi wao kupitia vyama vyote iwe Chadema, AFP, APPT Maendeleo, Chausta, Demokrasia Makini, DP, NCCR Mageuzi, Jahazi Asilia, NLD, NRA, SAU, TADEA,TLP, UPD,UMD, na UPDP.Watanzania wanapaswa kufahamu kwamba kilichopo pale Zanzibar ni Serikali ya umoja wa kitaifa si vyama vya umoja wa kitaifa.
Kati ya vyama vyote 18 vilivyosajili Zanzibar na wagombea wake wakiwa Wazanzibar ni vyama viwili tu CCM na CUF waliounda UMOJA wa serikali hiyo..Je, hivi kweli huu ni UMOJA wa Wazanzibar au umoja wa vyama hivi viwili kuunda serikali ya mseto!. wakati mwingine tuwe wakweli maana sidhani kama Raila au Kibaki wa Kenya wanaweza kupinga umoja wa serikali yao kuwa umetokana na vyama vyao..