Kwa nini kama ana taarifa akamatwe au ukiwa na taarifa za uhalifu mpaka ukamatwe? Kama hivyo ndivyo, nani yuko tayari kukamatwa ili atoe taarifa? Kama anaona inatakiwa angesema 'Zitto awasaidie polisi kupata taarifa kuhusu kuchoma shamba lake'.Huu ni uzandiki mbaya sana kwa mwanasiasa kumchafua kiongozi aliyetangulia mbele za haki.
Maadamu jinai haina mwisho na huyu Zitto anadai kuwa hayati Magufuli alituma watu kuchoma mali zake, nyumba iliyoko Kigoma na shamba la korosho huko mtwara.
Kama huyu Zitto sio muongo basi akamatwe na kusaidia jeshi la polisi liwakamate hao waliotumwa kuchoma mali zake. Maana hili ni kosa la jinai na adhabu yake ni kifungo cha maisha.
My take; Kufuga wanasiasa kama huyu Zitto kwenye taifa letu ni kufuga maadui wasiofaa kabisa.
Zaidi, soma: 'Mtwara: Shamba la Korosho linalodaiwa kuwa la Zitto lachomwa moto na watu wasiojulikana. Zitto alikana...
Nyumba ya Mbunge Zitto Kabwe Mkoani Kigoma yaungua moto
Nyumba ya Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe (ACT-Wazalendo) iliyopo Mwandiga, mkoani Kigoma yaungua moto. Bado chanzo hakijajulikana. Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amezungumzia tukio la kuteketea moto nyumba yake jioni ya leo na kueleza kuwa licha ya moto huo kuunguza vitu...www.jamiiforums.com