Waziri Mkuu Pinda asitisha utekelezaji wa agizo la Magufuli la Bomoa bomoa

Namwonea huruma mhe. Pombe magufuli kwa kupigwa stop hadharani tena mbele ya wapiga kura wake ya kubomoa majengo yaliyo ndani ya hifadhi ya barabara. Sijui kama hakuwa anatambua tofauti ya Ben na Jakaya. Kama hakutambua hilo basi nampa pole tena sana.
 
Na ccm hawanahabari....watu wengi watamhurumia hadi wamfanye mtu maarufu ... kinyume na ccm wanvyolenga!!

Pole Magufuli...Kupambana na Mafisadi inahitaji roho kubwa ...hakuna kukuta tamaa MKUU!
 
Huyu Magufuli ni mkurupukaji tu,huwezi kumfananisha na Sitta hata kidogo! Angesimama kuwapinga mafisadi basi,kama na yeye yupo safi!!

Ameshaitia hasara serikali mara nyingi tuu...msijifanye mmesahau aliyowai kuboronga! Aliwai kubomoabomoa kama hivi serikali ikalipa mabillion kwa waliovunjiwa! Wale samaki tuliwahifazi kwa mamilioni mangapi, mmesahau jamani?

Hoja hapa ni utaratibu alioutumia PM kumdhalilisha waziri wake. Lakini mmnaonaje huyu Pombe angeambiwa akakanushe kauli yake mwenyewe! Angekubali? Kwa wale wanaomjua alivo mbishi, angeenda na kusema ' ..eti kuna wale wananituma nibatilishe hatua yangu hii ya kubomoa nyumba zilizo barabarani, haiwezekani; nipo radhi nijiuzulu lakini sio hili... Ajiuzulu sasa
 
Yaani nilivyosikia hii nikakata tamaa!


Waziri hawezi kumkosea heshima waziri mwenzake kwa kisingizio cha uwaziri mkuu. hii ni dharau na udhalilishaji.

Yaani kwa mujibu wa Pinda, Pombe amekurupuka tu. Hafuati taratibu za cabinet.

shame on you Pinda. ndo maana unalialia hovyo kwenye majukwaa.
 
tafadhali wakuu leteni habari kamili ,nasi tuhabarike na kuchangia japodogo neno
 
Bt Magufuri was right, tatizo wanaleta siasa ktk utendaji, sasa hzo tren za mwendokasi zitapitia wap?!
 
am real sorry for mr. Pombe he is a sheep in Den's lion guess what he will be humilated
 
Huyu Waziri wetu mkuu anataka sana aonekane muungwana sana. Sawa, lakini alishindwa kumwita faragha mhe. Magufuli na kumweleza hayo maoni yake? Ni ukosefu wa hekima ya kiuongozi. Huku ni kujipendekeza!!
 
Yaani CCM hawajui kuwa aliebaki na anayeiweka CCM hai ni Dk.Magufuli?? Nawaonea huruma sana sana, najua ni kwa sababu kesho kutwa wana uchaguzi...
 
Pinda yupo sahihi kabisa nyinyi mnaropoka bila kujua lolote hamna sheria anayolinda magufuri wala siyo kazi yake kulinda sheria za nchni na pia hajui cha kufanya ndio maana anatafuta sifa za kisiasa kwa kuonea wananchni wanyonge, mbona hawajabomoa Rose garden, kama kashindwa hiyo wizara hajitoe aondoke hata leo, hiyo wizara inatumika vibaya kisiasa na wazembe wachache wasiyo jua la kufanya, nani kasema kujenga barabara ni kubomoa nyumba za Raia?; Barabara ipo kwa ajili ya kutumikia Raia mipango yote ya barabara inapaswa kuheshimu matakwa ya wananchni siyo mtu mmoja ambaye anatafuta cheap popularity eti ya kugombe urais.

Muelewe kuwa Dar es Salaam ni Jiji inapaswa kuwa na mipango endelevu ya kupunguza umaskini siyo kuongeza umaskini kama anavyofanya Magufuri. Suala la Barabara za Mijini hao jamaa wa Wizara ya Miundombinu na TANROADS inaonekana hawaliwezi na hawalijui kabisa. Humu JF kuna Ma-engineer wao lakini ukiangalia maneno yao unajua kabisa kuwa hawajui jinsi ya kupata majibu ya matatizo waliyonayo wananchni, wao wanajua ni kubomoa tu ndio walisomea basi.

Au watwambie kama wamemshauri Waziri majibu stahili lakini ni king'ang'anizi, tujue! approach wanayotumia siyo sahihi hata kidogo.
 

Hatutapiga hatua yoyote ya maendeleo ya ujenzi wa miundo mbinu kama tutaendelea kubembelezana unavyotaka. Tumekua wa hovyo mno. Tunavunja sheria na taratibu,alafu tunajitetea ujinga. Wengi wa hao unaosema wanaonewa ni ama waliingizwa chaka na wamiliki wa maeneo hayo ambayo tayari walikwisha fidiwa ama walijenga kibabe wakijua watapata utetezi wa wanasiasa aina ya Pinda siku nyumba zao zikitaka kubomolewa.
 

Tatizo la kwanza ni kwamba mfumo mzima wa utendaji katika serikali ni mbovu. sasa lazima tuanzie mahali fulani kurekebisha hilo. miradi mbalimbali ya usafiri kama ule wa mabasi yaendayo kasi, inategemea kuwepo na nafasi ya kujenga barabara. ilikuwa ni juu ya serikali kuhakikisha kwamba maeneo hayo hayajengwi. kosa ndio liko hapo.

lakini lingeweza kurekebishwa bila kumuadhiri Magufuli kiasi hicho. unajua hii ilikusudiwa kuwa ngumi ya kumuumiza magufuli as much as possible. lugha aliyotumia Pinda, mahali alipochagua kutoa tamko hilo, yote ni designed to exact maximum pain and punishment to Magufuli
 
Tumesikia katika vyombo vya habari kuwa Pinda kamsimamishama Magufuli asiendelee na zoezi la kubomoa nyumba zilizojengwa pembeni mwa barabara kinyume cha sheria au kupisha upanuzi wa barabara kwa ajili ya kupunguza msongamano.
Hivi hii ni sawa?
 
we hujui kua hii ni serikali ya machizi, kila mtu anataka umaarufu kupitia mgongo wa mwenzio
 

Kauli za kisiasa tu hizo za Pinda, hakuna mtu asiyejua kuwa sera za ndani za CCM ni kutokuwajali wananchi bali kujijali wenyewe na familia zao.

Hayo yanathibitishwa na wanayoyatenda huku yakipingana na wanayoyasema. Wanayoyatenda ambayo yanapingana na kauli za kwamba wanawapenda wananchi ni wizi wa mali na fedha za umma kama EPA, KAGODA, MEREMETA pamoja na mikataba mibovu inayofanywa kwa makusudi ili waweze kufaidika wao na washirika wao.

The good news ni kuwa watanzania wameanza kuwaelewa wezi hao na kwa hiyo hatuangalii wanasema nini bali wanafanya nini which is completely the opposite ways.
 
kasema Magufuli alipewa kazi ya kuondoa rushwa kwa wakandarasi, ina maana ameajiriwa kama wakala wa PCCB, au bado ni waziri anaetekeleza majukumu yote ya wizara?

Jamani mbona hawa CCM hawabebeki?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…