Ndicho kinachonishangaza. Serikali inayoendeshwa kwa umakini na ustaarabu, haiwezi kuwa na statements za viongozi wake waandamizi kama mawaziri zinazokinzana. Nionavyo mimi nadhani Pinda ilikuwa vizuri na hekima kumwita Mhe. Magufuli na kujadiliana nae kuhusu zoezi hilo la bomoabomoa. Baada ya majadiliano, kama ingeonekana ni muhimu zoezi lisitishwe basi amri ya kusitisha angeitoa Mhe. Magufuli mwenyewe na siyo Pinda. Njia hiyo isingejenga taswira mbaya mbele ya wananchi na kwa Magufuli mwenyewe.
Ni kweli mkuu kwa jina jingine serikali kama hizi tunaziita serikali za bora liende, HAIWEZEKANI WAZIRI MKUU ATOE TAMKO LA WIZARA YA MAGUFURI utazani magufuri hayupo na wasaidizi wake. kwa maneno mengine tunasema SERIKALI IMESHINDWA KZI wawaachie watu wengine waendeshe nchi kwani lazima wao tu?"