Waziri Mkuu Kassim Majaliwa: UKIMWI bado upo, ninawaomba suala hili lipewe kipaumbele wakati wa mahubiri.

Nyafwili

JF-Expert Member
Nov 27, 2023
2,773
6,885
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa dini kuwaangalia zaidi vijana, akilitaja kama kundi ambalo liko hatarini zaidi kupata maambukizi ya virusi vya UKIMWI, huku akiwataka kuimarisha huduma za unasihi na malezi yenye mlengo wa kustahimili mabadiliko yanayotokana na utandawazi.

Waziri Majaliwa emetoa wito huo leo Disemba 02, 2023 wakati akizungumza na washiriki pamoja na wadau mbalimbali kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam, mara baada ya kushiriki matembezi hayo kwa km. 5, ambayo yameratibiwa na Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT).

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo pia kuwaomba viongozi wa dini wawaeleze waumini wao kwamba licha ya mafanikio ambayo Serikali imeyapata kwenye mapambano dhidi ya VVU, wanapaswa watambue kuwa UKIMWI bado upo.

“UKIMWI bado upo, ninawaomba suala hili lipewe kipaumbele wakati wa mahubiri, hotuba na mihadhara. Endeleeni kuwakumbusha waumini kuhusu umuhimu wa kubadili tabia hususan zile zinazochangia maambukizi.” - Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
download (2).jpeg
 
Zamani ukimwi ulikuwa ni kitisho kikuu na watu wanakufa katika hali ya kutisha. Ukihubiriwa acha uasherati utakufa kwa ukimwi unaacha kweli, siku hizi ukiingiza ukimwi kwenye mahubiri utaonekana wa ajabu kwa sababu humo ndani ya ibada wapo ambao tayari wana maambukizi na kuhubiri ukimwi ni kuwanyanyampaa watajisikia vibaya
 
Zamani ukimwi ulikuwa ni kitisho kikuu na watu wanakufa katika hali ya kutisha. Ukihubiriwa acha uasherati utakufa kwa ukimwi unaacha kweli, siku hizi ukiingiza ukimwi kwenye mahubiri utaonekana wa ajabu kwa sababu humo ndani ya ibada wapo ambao tayari wana maambukizi na kuhubiri ukimwi ni kuwanyanyampaa watajisikia vibaya
Yeah ni kweli kabisa,, jambo fulani likiwa linazungumzwa alafu unakua miongoni mwao, lazima nafsi iiumie.
 
Zamani ukimwi ulikuwa ni kitisho kikuu na watu wanakufa katika hali ya kutisha. Ukihubiriwa acha uasherati utakufa kwa ukimwi unaacha kweli, siku hizi ukiingiza ukimwi kwenye mahubiri utaonekana wa ajabu kwa sababu humo ndani ya ibada wapo ambao tayari wana maambukizi na kuhubiri ukimwi ni kuwanyanyampaa watajisikia vibaya
zamani elimu unayoisema iliwezekana kwa sababu maambukizi yalikuwa chini.

saivi idadi imeongezeka sana. mm huwa nazani hata izi idadi wanazotangaza ni za kisiasa tu wasije kuleta taharuki. watu hawapendi tena kusikia habari izi, maana inajulikana ukishapata hakuna unachoweza kubadili. unaweza kuona hata spidi ya konokono ya huu uzi ilivyo. jamii haitaki kusikia habari izi, watu wamehamia MMU na kwenye siasa uko!

Kwa ujumla mazingira ya kutoa elimu hii yamebadilika sana. hata huyo mchungaji wa kuhubiri habari izi asipokuwa makini kwenye mahubiri yake anaweza kujikuta amebaki yeye na mkewe mama mchungaji tu.
 
zamani elimu unayoisema iliwezekana kwa sababu maambukizi yalikuwa chini.

saivi idadi imeongezeka sana. mm huwa nazani hata izi idadi wanazotangaza ni za kisiasa tu wasije kuleta taharuki. watu hawapendi tena kusikia habari izi, maana inajulikana ukishapata hakuna unachoweza kubadili. unaweza kuona hata spidi ya konokono ya huu uzi ilivyo. jamii haitaki kusikia habari izi, watu wamehamia MMU na kwenye siasa uko!

Kwa ujumla mazingira ya kutoa elimu hii yamebadilika sana. hata huyo mchungaji wa kuhubiri habari izi asipokuwa makini kwenye mahubiri yake anaweza kujikuta amebaki yeye na mkewe mama mchungaji tu.

Ukisiliza wizara ya afya inavyo jinadi, wao wanasema kufikia mpaka mwaka 2030, ukimwi utakua umeisha, hizi ni siasa au imekaaje maana kila nikifiria naona UKIMWI ndo unakuja high speed sana.
 
Ukisiliza wizara ya afya inavyo jinadi, wao wanasema kufikia mpaka mwaka 2030, ukimwi utakua umeisha, hizi ni siasa au imekaaje maana kila nikifiria naona UKIMWI ndo unakuja high speed sana.
Hapo hawajamaanisha hakutakuwa na maambukizi ya virus bali wanamaanisha kufikia hiyo 2030 hakutakuwa na hali ya watu kuishiwa kinga mwilini (Ukimwi) kwa sababu ukinywa dawa unakuwa fresh tu huwezi kufikia hali ya kupungukiwa kinga.
 
Hapo hawajamaanisha hakutakuwa na maambukizi ya virus bali wanamaanisha kufikia hiyo 2030 hakutakuwa na hali ya watu kuishiwa kinga mwilini (Ukimwi) kwa sababu ukinywa dawa unakuwa fresh tu huwezi kufikia hali ya kupungukiwa kinga.
Hapo nimekupata mkuu, Tuzidi kumuomba mungu huu gonjwa siyo kabisa, kuna case fulani nilipitia ikabidi nitumie zile PrEP ndani ya mwenzi mmoja , aise zile dawa zilinipelekesha sana.
 
Hapo nimekupata mkuu, Tuzidi kumuomba mungu huu gonjwa siyo kabisa, kuna case fulani nilipitia ikabidi nitumie zile PrEP ndani ya mwenzi mmoja , aise zile dawa zilinipelekesha sana.
prep? upo mazingira ya hospitali au unaishi na mwathirika?
vinginevo itakuwa ulimeza pep mkuu na sio prep.
 
prep? upo mazingira ya hospitali au unaishi na mwathirika?
vinginevo itakuwa ulimeza pep mkuu na sio prep.
Okay mkuu, itakua pep, Maana walinipa zakunywa kwa mwenzi mmoja tu. Nilidandia sehemu isiyo salama,
 
Back
Top Bottom