Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

mwawado... nyota njema huonekana asubuhi. Wengine tulipoonesha dalili tukaonwa tuna "chuki". Tatizo la viongozi wa Tanzania siyo elimu, siyo kabila, siyo wapi wamesoma, na kwa hakika siyo dini zao.. tatizo la viongozi wetu ni uwezo.

Bado tunafanya makosa ya kufikiria msomi=kiongozi bora! au mwenye mvuto=kiongozi bora..!!! Swali ni tunapimaje uwezo kabla hawajapewa madaraka? Maana kama Lau alipewa nafasi (promotion as a matter of fact) hili linasema nini kuhusu uwezo wa yule aliyemteua? au mchakato wa uteuzi wake?

I cosign Mwanakijiji!! Ulimbukeni wetu unatugharimu sana. Once again please read "The Confessions of an Economic Hitman" by John Perkins to see how companies like Sagem function and where and how people like Pinda and Masha fit in.....
 
Wakuu,

Nifahamisheni Ngeleja ana matatizo gani? Najua Masha kweli kazi imemshinda lakini Ngeleja mbona kama anajitahidi japo wizara yenyewe imejaa mizengwe.

Inatakiwa waziri apewe madaraka yote ya kuja na vision mpya juu ya energy. Huo umeme wa mafuta na maji pekee hautatutosha huko tunakoenda na itakuwa gharama kubwa.

Kuna haja ya kuwa na miradi midogo midogo ya umeme ya kiwilaya badala ya miradi mikubwa mikubwa ambayo kukiwa na tatizo nchi nzima inatikisika.

Taarifa ya timu ya wanasheria wa TANESCO ilibaini kuwa mkataba huo hauna nguvu za kisheria na kuamuru uvunjwe. Mkataba ukavunjwa rasmi Agosti mosi, mwaka 2008.

Hata hivyo, wakati mkataba huo unavunjwa uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa fedha zilizopaswa kurejeshwa Serikali hazikuwa zimerejeshwa zote.

Imebainika kuwa fedha zilizorejeshwa hadi mkataba unavunjwa ni jumla ya dola 7,674,186 za Marekani (zaidi ya Sh bilioni 7.7), huku dola za Marekani 23,022,412 (zaidi ya Sh. bilioni 23) zikibakia kwa Richmond na mrithi wake Dowans.

Siri ya wizi mkubwa Richmond
 
at this point ninaungana kabisa na maoni yako kwa 100%, kwamba wakati umefika kwa Lau kufikiria tena kama kweli he belongs kwenye siasa hasa za taifa.

Again, ninajaribu kumtafuta kujua na kusikia his side of this story, kabla sijatoa my final hukumu

Unauma na kupuliza!

Mwawado kasema categorically "siasa sio nafasi yake...ni vema ajiuzulu." Wewe unamwambia "naungana na maoni yako 100%" halafu unaweka vi-disclaimer!

Simama uhesabiwe. Au kaa chini "tusubiri sheria ichukue mkondo wake."

Na ukisamama nchale!

Ukikaa ukamtetea wakaja kum-fire nchale!

Ukikimbia mpaka soo liishe atakuona umemsaliti, nchale!
 
Last edited by a moderator:
mwawado... nyota njema huonekana asubuhi. Wengine tulipoonesha dalili tukaonwa tuna "chuki". Tatizo la viongozi wa Tanzania siyo elimu, siyo kabila, siyo wapi wamesoma, na kwa hakika siyo dini zao.. tatizo la viongozi wetu ni uwezo.

Bado tunafanya makosa ya kufikiria msomi=kiongozi bora! au mwenye mvuto=kiongozi bora..!!! Swali ni tunapimaje uwezo kabla hawajapewa madaraka? Maana kama Lau alipewa nafasi (promotion as a matter of fact) hili linasema nini kuhusu uwezo wa yule aliyemteua? au mchakato wa uteuzi wake?

Hilo mimi nilibishanaga sana na Sam kule bcstimes.com kuhusu Nchimbi na wengine kama yeye. Sijui kama watu walinielewa....
 
Hilo mimi nilibishanaga sana na Sam kule bcstimes.com kuhusu Nchimbi na wengine kama yeye. Sijui kama watu walinielewa....

sasa na kuelewa!

quote me: kwa kadiri mawazo yetu juu ya viongozi wetu yako vile vile, na kwa kadiri ya kwamba viongozi hao wanatufikiria sisi (wananchi) tuko pale pale, basi uongozi wa Taifa letu utaendelea kuonesha matatizo yale yale na kutupeleka kule kule. Hadi tukatae.
 
Mkuu Mwawado,

- Hili la vitambulisho limenishitua kuliko yote ya negative yanayomuhusu niliyowahi kuyasikia toka awe waziri, maana kama nilivyowahi kusema huko nyuma siyajui sana yanayomuhusu kwenye level ya uwaziri, lakini hili limenishitua sana kwa sababu on the record personally nilimuonya toka day one anapewa uwaziri wa ndani kuwa stay away form this national ID thing maana kuna wanaokutega wakunase kwenye hilo na nikawaomba ndugu zake wa karibu wamkumbushe maneno yangu kuwa awe muangalifu na hili na ikibidi alikalie mbali sana maana ninawajua wote waliokuwa wakimtafuta kwenye hili la national ID,


Sauti ya umeme - Wazee wa FMES!

Tatizo vijana hatusikii mbele ya "mafanikio". Nakumbuka sana hatua yako ya kumuonya kuhusu huo moto...

Tanzanianjema
 
- Ni kweli mengi sana yamesemwa hapa JF kuhusu Lau, lakini naomba kuwakumbusha wale wote waliokuwa na haraka za kudai kujiuzulu kwa Lau, kuliko Sophia Simba, kwamba wazazi wangu waliponipeleka shule kwa mara ya kwanza, waliniambia kua wanataka nijifunze kufikiri for my own na kujua kusema yes and no at the right time, na sio anything else, to this day they all regret hayo maneno waliyonifundisha maana yamewaumiza wao kuliko anybody else, hasa la mimi kufikiri na kuamua on my own badala ya kusubiri kufikiriwa na kuamuliwa na wengine!

Unauma na kupuliza!

Mwawado kasema categorically "siasa sio nafasi yake...ni vema ajiuzulu."

Wewe unamwambia "naungana na maoni yako 100%" halafu unaweka vi-disclaimer!

Simama uhesabiwe. Au kaa chini "tusubiri sheria ichukue mkondo wake."

Na ukisamama nchale!

Ukikaa ukamtetea wakaja kumfire nchale!

Ukikimbia mpaka soo liishe atakuona umemsaliti, nchale!

- Again ninakubaliana na Mkuu Mwawado kwa 100%, kwamba huenda siasa sio mahali pa Lau, Mkuu Kiranja samahani kwa kukukwaza na msimamo wangu ila kama kawaida Wamarekani walinifundisha umuhimu wa ku-practise Due Process inapotokea ishu zinazowahusu bin-adam ambao hata muumba wao yaani Munyazi Mungu anakubali kuwa amewaumba na mapungufu makubwa na bila ukamilifu,

- Huwezi kusimama kuhesabiwa bila ya kuwa na facts zako mwenyewe on the ishu, eti unataka na mimi nikurupuke nisimame nihesabiwe nikiwa na facts kama za Dr. Masau? Hizi amri za kusimama na kukaa chini vipi ukizielekeza kwa mkeo au watoto wako maana hapa kabla ya kujiunga si huwa tunajaza majibu kwenye sheria inayosema kuhusu umri wetu kwamba sisi ni watuwazima hapa JF, sasa tukianza kuamrishana kuhusu kusimama na kukaa chini itakuwaje mkuu si itakuwa kazi kubwa kwa Mods?

Mbona ulikuwa umetulia mkuu vipi ugonjwa umerudi tena nini? Unafikiri mimi huwa ninakurupuka kurupuka na hukumu bila facts? Au na facts kama za Dr. Masau? Sio zangu hizo na wala huwa sina haraka, majuzi zimerushwa hukumu weee za Pinda bila maelezo yake nilisema haya haya kuwa nataka due process kwanza, nataka kusikia side ya Pinda, jana imetoka ndio nimetoa hukumu.

Lakini samahani sana kama nimekukwaza kwa kuwa na mawazo tofauti na yako ya kumsulubu Lau, bila all the facts.

Wazee wa sauti ya umeme - FMES!
 
Mwawado hakusema "huenda"! Understand that. He was categorical, Masha ajiuzulu. Ukikubaliana nae 100% hakuna cha disclaimer za due process hapo!

- Baada ya kusikia side ya waziri Lau, ndio nitasema hukumu yangu, ila kwa sasa ninakubaliana na Mkulu Mwawado kwa 100%, kwamba huenda siasa sio mahali pake Lau kwa sababu ninaamini na kujua kua Mwawado anajua mengi sana ya Lau kutokana na nafasi yake ndio maana amefikia kusema aliyosema tayari, ila mimi sina facts zote ndio maana categorically ninasema "huenda" mpaka nitakapokuwa na facts zote, ila kwa sababu ya heshima yangu kwa Mwawado ndio maana nikajitokeza na kumuunga mkono kwa 100%..

We'll bypass the other puerile mumbo jumbo. It's just bizarre.

Bizzare? Bwa! ha! ha! off course, hukumu bila all the facts kama kesi ya Masau you are damn right ni bizzareee bwa! ha! ha! ha!

Wataliano wana neno moja wanasema Fugazzii, maana yake ni fakeness!
 
Ni imani yangu kuwa Mh. J.K ameishapata fundisho la kutumia usahiba na undugu kama kigezo cha uteuzi kenye cabinet na ngazi nyingine nyeti za uongozi za serikalini. Matokeo ni kwamba utendaji umekuwa mbovu na anapata kigugumizi kuwakemea. Mara nyingi amesaidiwa na presha za wananchi na vyombo vya habari vilivyowalazimisha wajihudhuru......Braza...biashara ya duka ukimweka ndugu akuuzie tu, utaingizwa hasara na utafilisiwa...ukimweka rumande...wazazi na dugu wengine watakujia juu eti unataka kuharibu undugu???. Njia pekee ni kumwajiri mtu kwa uwezo wake bila kajali kama sio ndugu au rafiki...akikuharibia mambo..unamsweka ndani na hutapata lawama. Mh. J.K ajifunze kutokana utendaji mbaya wa maswahiba wake...Mifano anaiona, mawaziri aliowaweka kutokana na uwezo wao, wanafanya kazi na zinaonekana.
 
Last edited:
FMES,
Mkuu samahani huyu dogo Masha nadhani LIMBUKENI.. unajua tena kuna vijana waliochukua muda mwingi sana masomoni wakashindwa kuutumia umri wao ktk nyanja nyinginezo, kisha wanapokuja kuwa watu wazima wakakabidhiwa madaraka basi ndio Ujana wao huanza hapo..

Jamaa amekuwa ktk viwanja kama vile ndio kwanza kapata Barekhe..yaani kila kona mshikaji Masha hivi Masha vile halafu anaharibu kishenzi hadi nyumbani.. mimi nadhani Masha hakuutumia ujana wake vizuri...hivyo anachanganya kazi na kile wanachosema wazungu - I want to find myself.. any Idea what that means! - Mtu kachanganyikiwa..
 
FMES,
Mkuu samahani huyu dogo Masha nadhani LIMBUKENI.. unajua tena kuna vijana waliochukua muda mwingi sana masomoni wakashindwa kuutumia umri wao ktk nyanja nyinginezo, kisha wanapokuja kuwa watu wazima wakakabidhiwa madaraka basi ndio Ujana wao huanza hapo..

Jamaa amekuwa ktk viwanja kama vile ndio kwanza kapata Barekhe..yaani kila kona mshikaji Masha hivi Masha vile halafu anaharibu kishenzi hadi nyumbani.. mimi nadhani Masha hakuutumia ujana wake vizuri...hivyo anachanganya kazi na kile wanachosema wazungu - I want to find myself.. any Idea what that means! - Mtu kachanganyikiwa..

- Mkuu Bob, yaani hili la national ID limeniacha hoi sana mkuu sina hata la kusema.
 
pole masha....kila mtu,huwa anaface chalenging time..jikaze!

sijaona lolote la serikali ya JK la kuni impress..

km issue ni utendaji mbovu,wote wako guilty,including JK mwenyewe,so wote wawe nje!ala!

uchaguzi 2010 ndio huoo umekaribia,no wonder tunataka kuonyeshwa kuna linalofanyika..

pole masha kwa kufanywa 'scape goat..

hata mkinishushua,mie nampenda masha!
 
Hofstede said:
Mimi nafikiri ntaonekana nipo mlengo tofauti. Hivi nchi yetu imekosa priorities? katika kutekeleza miradi yake?. Huu mradi wa National ID mimi binafsi naona ni ULAJI ulitengenezwa makusudi na watu kama ilivyokuwa wa RADA na NDEGE YA RAIS ili kujipatia chao mapema. Kwa mfano mradi huu ungefanyika taratibu katika kipindi cha miaka kumi tukasema tutahakikisha watanzania wote wanakuwa na vitambulisho Serikali ingekosa nini hapo?. Kuchukua $154mill kuzichoma kwa mkupuo ni ufisadi usihitaji any explanations kuu justify. Barabara hazipitiki, wanafunzi wanagoma hakuna mikopo haitoshi, Wananchi hawana ajira kwa nini wasingetumia fedha hizi kuanzisha mashamba ya kisasa ambayo yangeajiri watanzania masikini. Mradi huu nina ufaninisha na Mradi wa "SPEED GOVERNER" Haukuwa chochote zaidi ya ulaji tu. Nani leo anazungumzia speed governor?, basi tusishangae 10 years to come watanzania wote wakawa wametupa ID zao na hakuna wa kuwauliza ID zao popote pale (Tshs 200 Billion kissed on the air and washed in the ocean).

Vitambulisho hivyo hata vikija na chip inayobeba taarifa zote za mtu bado mimi kwa Mtazamo wangu ni "USELESS", kwani watanzania wengi bado masikini na hawatafaidika na chochote kwa mradi huu, wala usalama wetu wa Taifa hautayumba hizi ni mbinu za kuuziwa mbuzi kwenye Gunia. Tuwawezeshe kwanza watanzania ili nchi iwe na Neema mpaka hapo itakapovutia wahamiaji kuja Tanzania basi MRADI Huu utakuwa na maana kubwa.

Hebu tuwe na vipaumbele vya miradi siyo kuangalia miradi yenye ulaji na itakayowahakikishia watawala kuendelea kutawala. This is Nonsense project for the Current situation in Tanzania .

Muzee hapa tupo pamoja..Tena ZAIDI YA 100%.

Kila siku tunasikia jinsi serikali yetu inavyolalamika kusema haina fedha ku-cover mambo mbalimbali ktk kuwahudumia wananchi wake. Iwe ktk kuinua kilimo, kujenga miundombinu, kuboresha huduma za afya, kuwaweza wananchi kujiajiri, n.k.

Akili ya kawaida kabisa inamtuma mtu kuona kuwa kunapokuwa na UHABA au UPUNGUFU, ni shurti kufanya OPTIMIZATION (sijui kiswahili chake, samahani) na kutazama VIPAUMBELE VYAKO. Ktk mduara wa umasikini unaotuzunguka mtu anakuja na kusema tutengeneze vitambulisho kwa bilioni 200, inabidi uanze kujiuliza iwapo kuna- kuishirikisha AKILI..
 
Muzee hapa tupo pamoja..Tena ZAIDI YA 100%.

Kila siku tunasikia jinsi serikali yetu inavyolalamika kusema haina fedha ku-cover mambo mbalimbali ktk kuwahudumia wananchi wake. Iwe ktk kuinua kilimo, kujenga miundombinu, kuboresha huduma za afya, kuwaweza wananchi kujiajiri, n.k.

Akili ya kawaida kabisa inamtuma mtu kuona kuwa kunapokuwa na UHABA au UPUNGUFU, ni shurti kufanya OPTIMIZATION (sijui kiswahili chake, samahani) na kutazama VIPAUMBELE VYAKO. Ktk mduara wa umasikini unaotuzunguka mtu anakuja na kusema tutengeneze vitambulisho kwa bilioni 200, inabidi uanze kujiuliza iwapo kuna- kuishirikisha AKILI..

Ain't a big deal. Kitambulisho kimoja buku kumi tu. Kwani wewe ulitaka utengeneze kimoja kwa bei gani? Wenzetu wanatengenezewa kimoja kwa bei gani huko majuu?

Gharama ya kitambulisho kimoja ni sawa na gharama ya mchango wa sekondari kata kwa kichwa.

Alternatively, kama mnaona nongwa sana basi serikali isichangishe tena michango ya kata. Hizo bilioni 200 ziende kugharamia ujenzi wa sekondari kata. Ila kila mtu akitaka kitambulisho alipe mwenyewe buku kumi yake.

.........ndiyohiyo
 
Ain't a big deal.

Good..

This shows how far the mind of typical 'educated' Tz-nian can think ..Then I can imagine mtu asiyeelimika kijijini yuko ktk hali gani.

Bil 200 unaona sio big deal sio, mtu akikujia hana nguo, hana chakula, anasumbuliwa na maradhi etc..kitu cha kwanza kumpa ni KITAMBULISHO chenye kuonesha DNA..Sivy😀 ?


CONGRATULATIONS..!!
 
Last edited by a moderator:
- Leo nimeongea na wabunge wetu kama watatu ambao wamenihakikishia kua wiki inayokuja yote yatawekwa wazi yaani ukweli wote kuhusu hii ishu bila vificho, kwa hiyo tutasubiri ukweli wote next week.
 
Uchaguzi Mkuu unakuja, SISIEMU, JK na serikali yake wanatafuta pesa za kampeni kupitia KAGODA v.2
Huu mradi wa ID ni KAGODA nyingine, tutapiga kelele lakini at the end Tembo aliye chumbani atatumia nguvu na kuupitisha ili mradi SISIEMU ina fungu lake pale, you watch...
 
wandugu,

..hizi habari naona kama zina ka-harufu ka ushabiki na ufisadi.

..inaelekea kuna vita ya kifisadi ktk kugombea tender ya kutengeneza vitambulisho vya taifa.

..inavyoelekea Masha amejiunga na kundi moja kati ya makundi ya kifisadi yanayopambana.

..wananchi nao ambao kwa sababu zao binafsi wamemchoka Masha wamejiunga na kundi lingine la kifisadi dhidi yake.

..kwa mtizamo wa haraka-haraka hicho ndicho kinachoendelea.

NB:

..wananchi tuwe makini hapa. remember Frederick Sumaye?

..mnakumbuka alivyokuwa anasakamwa na Padri Slaa na Mchungaji Mtikila, kwa niaba ya wanamtandao, kwa kukodisha shamba la eka 7 pale Kibaigwa, wakati Mkapa na Yona wanajimilikisha mgodi wa Kiwira?

..sina uhakika kama Sumaye hana madudu yake aliyoyafanya. lakini ninachojaribu kusisitiza hapa ni wananchi kuelewa the motive behind haya makundi yanayopingana. tujaribu kuchunguza kama haya makundi yako kusimamia maslahi ya kweli ya wananchi.

..jambo lingine sasa hivi kuna mafisadi ya miaka ya 80 ambao wanawangangania mafisadi wa mwaka 2000. naomba kutoa dokezo tu kwamba Spika Samuel Sitta ni fisadi aliyeifilisi mamlaka ya uendeshaji makao makuu Dodoma -- CDA. sasa leo eti ndiyo amegeuka kuwa mdau wa kupiga vita ufisadi.
 
Uhondo wote ni huu hapa chini kutoka nipashe la leo: -

Waziri Masha aibua matata

KOSA LA KWANZA
Masha anadaiwa kumfahamisha Mwenyekiti huyo wa Bodi ya Zabuni ya Wizara kwamba, amepokea malalamiko kutoka kwa kampuni hiyo na kumhoji pamoja na mambo mengine, uhalali wa kuenguliwa kwa kigezo cha kutoambatanisha nakala ya mapatano (Joint Adventure Agreement)......(nafikiri ni Joint Venture).......Masha alitakiwa kuomba ushauri tu (kama hajui procurement procedures) kuwa awajibuje hiyo barua......

KOSA LA PILI
.................Masha aliitaka bodi hiyo itoe nafasi kwa waombaji wote wa zabuni waliotimiza vigezo vilivyopo kwenye Nyaraka za Awali za Kuingia kwenye Zabuni (PD) wapewe nafasi ya kuendelea na hatua ya pili ya mchakato huo.........hakuna tofauti na alichokifanya Lowassa kwenye mchakato wa RDC


KOSA LA TATU
......... hali ambayo ilimfanya Waziri Masha awasiliane naye tena na kumtaka apate ushauri kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa kile alichodai kuwa ni kuepuka hisia na malalamiko kutoka kwa waombaji.....BIG NO Mr Masha........kuingilia kwako zoezi la mchakato wa zabuni ni ukiukaji wa taratibu za procurement........na hii ndio italeta mtafuruku kutoka kwa makampuni mengine (yaliyofuzu) kuishitaki serikali......hence hasara..........

Wakati hayo yakiendelea, habari za uhakika zinasema kwamba Katibu Mkuu Kiongozi alimuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupeleka taarifa ya utekelezaji kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri baada ya Katibu Mkuu huyo kumpelekea taarifa ya utekelezaji.............

Hata hivyo, inadaiwa kuwa hatua hiyo ya Katibu Mkuu Kiongozi, haikumridhisha Waziri Masha kwa madai kwamba, hakumhusisha kwa vile yeye ndiye atakayeiwasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri na ndiye atakayewajibika kwa maamuzi yoyote yatakayofanyika wizarani kwake bila kujali kwamba maamuzi hayo yalipata baraka za Katibu Mkuu Kiongozi au la...........Hivi kuna Cabinet Paper inayoandikwa wizarani bila ya Waziri husika kuiona?........


* SOURCE: Nipashe

........kutokana na habari ya Nipashe nimejaribu kuainisha makosa ya Mr. Masha.........
 
Back
Top Bottom