Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Huyu Masha ni fisadi hafai kashapenyeza kakampuni kake anataka awini tenda sasa kikampuni chake hakina sifa ya hiyo tenda ndio anaanza kuwa mapepe namna hiyo!
HIVI KWA MTU ANAETUMIKIA TAIFA KWA MASLAHI YA TAIFA , HAWEZI KUWA NA MAWAZO KAMA YA MASHA , HAWA NI WATU WALIOINGIA NDANI YA CABINET ILI KUCHONGA DILI ZAO ZIKAE VIZURI SIJUI KWANINI JK HAJAMWAJIBISHA HUYU! ANATUZALILISHA VIJANA!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Sipendi kutumia neno ujinga lakini kama ingekuwa anayesema maneno haya hajui kusoma na kuandika ningeweza kutumia maneno hayo lakini ukweli ni kwamba kuna juhudi za makusudi za kuthubutu kugeuza hoja nzito kuwa "ugomvi binafsi" na hiyo imekuwa ikitumika kama kinga na wahalifu wengi hapa nchini na kwa kweli wamefanikiwa sana kujilinda na kuokoka katika mikono ya dola na hata katika vyombo vingi vya habari.

Manji amefanikiwa kwa mtindo huu kwa kila uovu wake, anepenyeza rupia katika vyombo vya habari na kwa kuwa hawezi kupenyeza Thisday na KULIKONI wataandika na watu watasema, "si unaona, huo ni ugomvi wa Mengi na Manji".

Iko mifano mingi na hat hivi karibuni, Masha alitumia watu fulani kusema, matatizo yaliyotokea ni ugomvi wa wachaga dhidi ya Wasukuma, akatokea mtu akasema hata Masha mwenyewe si msukuma na miongoni mwa wanaoshangilia kuanguka kwake ni Wasukuma.

Wakati wa Mkapa magazeti ya RAI na Mtanzania na kipindi cha Jenerali On Monday kulikuwa na taarifa nyingi za kuikosoa serikali, baadhi zikiwa zinatoka hata bila ya Jenerali Ulimwengu kujua zinatoka wapi, lakini watu akiwamo mkapa na wafuasi wake wakawa wanasema ni "ugomvi wa Jenerali na Mkapa". HUU NI UJINGA AMA UPOTOSHAJI HATARI SANA.

Ni lazima tujadili HOJA kwa HOJA kwa kuangalia FACTS zilizopo. Ni UJINGA usio mfano kwa mfano Juma akigombana na Joni halafu Juma akiona Joni anaiba akawaita polisi, polisi waseme, "aaha Juma ana ugomvi na Joni".... huyo atakuwa polisi asiyejua kazi zake. Katika mafunzo ya upelelezi, moja ya watu muhimu wanaotoa taarifa za kweli za uhalifu ni watu wanaogombana kwa kuwa atatoa taarifa zote akijua mbaya wake atashughulikiwa.

Hizi hoja za kusema yaliyotokea kuhusu Masha yana uhusiano na ugomvi na Mengi, ama kama alivyoanza rafiki yangu Paparazimuwazi kwamba "Mengi amempata Masha" si sahihi kabisa tunapotoka na tutajikuta anaibuka Mramba anasema, "Hosea na Feleshi ni Wasukuma wana chuki na Wachaga na Wapare na sasa wanamuacha msukuma mwenzao Chenge"

Hapa Masha kaingilia zabuni na yeye mwenyewe anakiri kwamba hana mamlaka ya kuingilia lakini analazimika kutetea "maslahi ya umma". MAsha anaitetea kampuni ambayo imeenguliwa. Walioshiriki zabuni hiyo wote wanasema hawajajulishwa kampuni zilizoenguliwa na hivyo kushangaa kampuni anayoitetea Masha ilijuaje kwamba wameenguliwa kama si yeye aliyewaibia siri ya zabuni?

Kama alivyosema Dk. Slaa, taratibu za zabuni kwa sheria ya manunuzi zinaelekeza taratibu za kampuni kufuata isiporidhika na matokeo na Waziri hatajwi katika taratibu hizo, KUNA NINI hata Masha aingilie tena akiwa mwanasheria aliyebobea na ambaye miaka ya nyuma aliitetea kampuni nyingine iliyoishitaki serikali baada ya kuenguliwa katika zabuni ya vitambulisho na leo ni Masha huyo ambaye yuko Wizarani akiwa upande wa serikali.

Mkuu halisi hapa umeua kabsaaa, nafikiri hii itakuwa nyundo muhimu sana kwa FMES coz ameendelea kumtetea jamaa yake ingawa kwenye lile sakata la Masha V/S Mengi aliamua kuna mkono na akaanza kumcrash mshikaji wake masha..... hahahaha ngoja tuone nini kitatokea
 
This project stinks! Kama ilivyokuwa Rada. Kama ilivyokuwa ndege ya mheshimiwa. Kama ilivyokuwa Richmond. Mimi ningedhani kuwa huu wakati mgumu tulionao ungetupa sababu tosha za kuufukia na kuusahau. Au na wenyewe ni moja ya Stimulus package ya bongo?
 
- Mkuu wangu Maane si unaona sasa, nimekuuliza swali umejibu something else, numekuomba record ya Mengi kumaliza viongozi kama ulivyoanza mwenyewe, sasa tizama ulivyonijibu hal;afu sasa hivi utasema ninakutisha kumbe huwezi kuweka ukweli wa hyabari zako tu, sasa naomba tena kukuuliza unao ukweli wa viongozi waliowahi kumalizwa na Mengi kama ulivyodai mwenyewe kama huna kubali tuendelee na kuakta ishus.

Thanxs!

Hahahaha mkuu Fmes naona sikuhizi naona unapenda sana huu msemo maana huko nyuma nilishaona post moja umesema hivi hivi kuwa hapa hatutishani mara hakuna haja ya kuniogopa blaa blaaa nikabakia kucheka tu mi mwenyewe doh,, n'way mkuu kanyaga twende.........
 
Makampuni mbona yanafahamika tu ila kila kampuni ina kigogo nyuma yake.....Sina uhakika kama Masha alishawahi kuhusika na hili dili,sikuwahi kusikia kabisa na hata kama ikiwa ni kwa usiri Mkubwa sana!

To mention but a few
1. Former home affairs Minister..huyu hata passport mpya alipiga dili
2. Waziri wa zamani wa maji
3. ...................

As I said, nobody knows who the 8 companies are. Wewe mwenyewe huyajui hayo makampuni na umeandika madudu haya
 
Tatizo siyo Masha ila ni watu ambao wana Fuatilia hiyo dili.kuna wakati hapa Africa kusini nilishawahi kumuona waziri mmoja naye akifuatilia hiyo dili.

ila so far kuna mawaziri watatu wanafukuzia hiyo dili na sijui nani ataipata...watakaangana wao kwa wao!

Hata juzi kuamishwa kwa Katibu wa Wizara ya mambo ya ndani ni kutokana na hii ishu.Kuna kipindi flani Mhe. Rais ilibidi atengue uteuzi wa Afisa mtendaji wa hii kampuni baada ya kugunduliaka ulikuwa umeandaliwa mpango wa kifisadi.

Muunwgana alionya sana kuhusu hili dili na akamwambia Masha asimamie vyema na Rushwa isijitokeze.SAGEM ni kampuni kubwa na imefanya kazi kubwa sehemu mbali mbali ila Rushwa na haya makampuni makubwa haieoukiki.

Haukutaja kampuni ndiyo maana nikastukia. Nilidhani unazungumzia ya hao wafaransa. Pili, hii National ID Agency imeanza lini? Tatu, Kazi yake nini? Nne, agency ni wakala na chief executive wake anawekwa na waziri na si Rais. Rais angeweza kumuagiza waziri wake atengue uteuzi na si vinginevyo. Ingekuwa vyema kama ungefafanua zaidi habari yenyewe. Rais gani alihusika n.k.
 
Last edited:
Uhondo wote ni huu hapa chini kutoka nipashe la leo: -

Waziri Masha aibua matata

2009-01-29 10:14:05
Na Waandishi Wetu

Mchakato wa kupata mzabuni wa kutekeleza Mradi wa Vitambulisho vya Taifa, umezua mambo, baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, kudaiwa kuingilia mchakato huo, kinyume cha Sheria ya Manunuzi ya Umma.

Habari za uhakika ambazo Nipashe imezipata, zinaeleza kuwa Masha anadaiwa kufanya hivyo akidai kutoridhishwa na hali halisi ya mchakato huo kabla hata matokeo ya kupatikana kwa mzabuni hayajatangazwa.

Vyanzo mbalimbali vya habari serikalini vimepasha kuwa Masha alifikia hatua hiyo, baada ya Bodi ya Zabuni ya Wizara kuiengua Kampuni ya Sagem Securite ya Uhispania katika mchujo wa kumpata mzabuni atakayetekeleza mradi huo ambao ni nyeti na muhimu kwa usalama wa nchi.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, kampuni hiyo ni kati ya makampuni 54 yaliyoomba kupewa zabuni hiyo, lakini ilienguliwa katika mchujo wa tatu, baada ya mchujo wa kwanza kuyaengua makampuni 33 na kubaki 21 na mchujo wa pili, kuyaengua makampuni 13 na kubaki manane tu.

Uchunguzi wa Nipashe umebaini kwamba wajumbe wanaounda Bodi ya Zabuni ya Wizara hiyo, ni pamoja na Kamishna wa Magereza, Mkurugenzi Mkuu wa Uhamiaji, Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji na mchakato wa zabuni hiyo uliwahusisha pia maofisa kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru) na Usalama wa Taifa.

Haijafahamika sababu hasa iliyomsukuma Masha hadi kuamua kuitetea kampuni hiyo kwa nguvu zake zote.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu, Masha anadaiwa kuingilia mchakato huo akidai kupokea malalamiko kutoka kwa kampuni hiyo, kwa madai kwamba wameonewa kwa kuenguliwa kwenye mchakato kwa vigezo ambavyo havikuwapo katika nyaraka za awali za kuingia kwenye zabuni.

Taarifa zinasema kuwa Masha baada ya kupata malalamiko hayo, Novemba 4, 2008, alimwita Katibu Mkuu wa Wizara, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni na Mratibu wa Vitambulisho vya Taifa ofisini kwake, mjini Dodoma.

Katika kikao hicho, vyanzo vyetu vinasema Masha anadaiwa kumfahamisha Mwenyekiti huyo wa Bodi ya Zabuni ya Wizara kwamba, amepokea malalamiko kutoka kwa kampuni hiyo na kumhoji pamoja na mambo mengine, uhalali wa kuenguliwa kwa kigezo cha kutoambatanisha nakala ya mapatano (Joint Adventure Agreement).

Ofisa mmoja mwandamizi serikalini akielezea kukerwa na kujitosa kwa Waziri Masha katika mchakato huo alisema kuwa ilifika mahali akadai waziwazi kuwa kampuni ya Sagem Securite ilikuwa imesukiwa makakati wa kung\'olewa kwenye mchakato wa zabuni kwa sababu ilionekana ni tishio kwa kampuni nyingine.

Kutokana na hali hiyo, chanzo hicho kimesema kuwa Masha aliitaka bodi hiyo itoe nafasi kwa waombaji wote wa zabuni waliotimiza vigezo vilivyopo kwenye Nyaraka za Awali za Kuingia kwenye Zabuni (PD) wapewe nafasi ya kuendelea na hatua ya pili ya mchakato huo.

Kutokana na shinikizo la Masha, vyanzo vyetu vinasema Katibu Mkuu wa Wizara alimwandikia barua Mwenyekiti wa Bodi ya Zabuni na kumpa maelekezo ya kutaka kurejewa upya kwa mchakato ili kuiingiza kampuni hiyo na nyingine zilizokuwa zimeenguliwa awali.

Vyanzo vyetu vinasema kwamba Bodi ya Zabuni baada ya kupitia maelekezo ya Katibu Mkuu, ilitoa ufafanuzi, ambapo pamoja na mambo mengine, ilieleza kuwa imeridhika kwamba, hakukuwa na upungufu wowote katika kazi ya uchambuzi waliyoifanya na waombaji wote walioenguliwa, ikiwamo Sagem Securite walienguliwa kihalali.

Taarifa mbalimbali kutoka serikalini zimearifu Nipashe kuwa Katibu Mkuu aliridhika na majibu ya Bodi ya Zabuni, hali ambayo ilimfanya Waziri Masha awasiliane naye tena na kumtaka apate ushauri kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa kile alichodai kuwa ni kuepuka hisia na malalamiko kutoka kwa waombaji.

Wakati hayo yakiendelea, habari za uhakika zinasema kwamba Katibu Mkuu Kiongozi alimuagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupeleka taarifa ya utekelezaji kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri baada ya Katibu Mkuu huyo kumpelekea taarifa ya utekelezaji.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa hatua hiyo ya Katibu Mkuu Kiongozi, haikumridhisha Waziri Masha kwa madai kwamba, hakumhusisha kwa vile yeye ndiye atakayeiwasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri na ndiye atakayewajibika kwa maamuzi yoyote yatakayofanyika wizarani kwake bila kujali kwamba maamuzi hayo yalipata baraka za Katibu Mkuu Kiongozi au la.

Kutokana na hali hiyo, vyanzo vyetu vinasema kwamba Masha alimwandikia Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, barua akimlalamikia Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo kwa madai ya kumwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuwasilisha taarifa hiyo kwenye kikao cha Baraza la Mawaziri bila kumhusisha yeye kama Waziri.

Waziri Masha alipoulizwa na Nipashe kwa njia ya simu jana kutoka mjini Dodoma kuhusu tuhuma dhidi yake za kuingilia mchakato wa kupata mzabuni wa mradi huo, hakukiri wala kukanusha.

``Aliyekwambia nimeingilia mchakato, muulize huyo. Mimi ninafanya kazi yangu kama waziri,`` alisema Waziri Masha.

Pia, alipoulizwa kama amemwandikia barua Waziri Mkuu `kumshtaki` Luhanjo, Waziri Masha alimweleza mwandishi kuwa: ``Kama barua nimemwandikia Waziri Mkuu, ni confidential (siri), sihitaji kukueleza hilo wewe.``

Wakati hayo yakijiri, PPRA imeeleza utaratibu wa zabuni na jinsi ya kulalamika kama mwombaji hakuridhishwa na matokeo.

Ofisa mwandamizi wa PPRA aliiambia Nipashe kuwa mzabuni anayeona ameonewa kwenye utoaji wa zabuni anapaswa kutoa malalamiko yake kwa Katibu Mkuu wa Wizara husika, wakati Masha anaonekana kufanya kwa niaba ya mzabuni, kampuni ya Sagem Securite.

Akizungumza na Nipashe kwenye ofisi hizo jana, ofisa huyo aliyekataa kutajwa gazetini kwa sababu si msemaji wa mamlaka hiyo, alisema endapo mzabuni huyo hataridhika na maamuzi yatakayotolewa na Katibu Mkuu anatakiwa kuwasilisha malalamiko yake PPRA.

Ofisa huyo alisema kwa mujibu wa Sheria, mlalamikaji huyo anapaswa kuwasilisha malalamiko yake ndani ya siku 28 za kazi mara baada ya majibu ya mchakato wa zabuni kutoka.

Alisema endapo mzabuni huyo hataridhika na maamuzi ya PPRA anatakiwa kwenda Mahakama ya Rufani za Zabuni, Public Procurement Appeals Authority (PPAA), ambayo ndiyo ngazi ya juu kabisa.

Alisema kama zabuni imeshatangazwa na mkataba kusainiwa na pande husika, basi mlalamikaji hana haja ya kupitia kwanza PPRA na badala yake anatakiwa kuwasilisha malalamiko yake moja kwa moja PPAA.

Mradi wa vitambulisho vya taifa ni kati ya miradi mikubwa ya serikali ukikadiriwa kuwa utagharimu Sh bilioni 200.

* SOURCE: Nipashe
 
Mimi nafikiri ntaonekana nipo mlengo tofauti. Hivi nchi yetu imekosa priorities? katika kutekeleza miradi yake?. Huu mradi wa National ID mimi binafsi naona ni ULAJI ulitengenezwa makusudi na watu kama ilivyokuwa wa RADA na NDEGE YA RAIS ili kujipatia chao mapema. Kwa mfano mradi huu ungefanyika taratibu katika kipindi cha miaka kumi tukasema tutahakikisha watanzania wote wanakuwa na vitambulisho Serikali ingekosa nini hapo?. Kuchukua $154mill kuzichoma kwa mkupuo ni ufisadi usihitaji any explanations kuu justify. Barabara hazipitiki, wanafunzi wanagoma hakuna mikopo haitoshi, Wananchi hawana ajira kwa nini wasingetumia fedha hizi kuanzisha mashamba ya kisasa ambayo yangeajiri watanzania masikini. Mradi huu nina ufaninisha na Mradi wa "SPEED GOVERNER" Haukuwa chochote zaidi ya ulaji tu. Nani leo anazungumzia speed governor?, basi tusishangae 10 years to come watanzania wote wakawa wametupa ID zao na hakuna wa kuwauliza ID zao popote pale (Tshs 200 Billion kissed on the air and washed in the ocean).

Vitambulisho hivyo hata vikija na chip inayobeba taarifa zote za mtu bado mimi kwa Mtazamo wangu ni "USELESS", kwani watanzania wengi bado masikini na hawatafaidika na chochote kwa mradi huu, wala usalama wetu wa Taifa hautayumba hizi ni mbinu za kuuziwa mbuzi kwenye Gunia. Tuwawezeshe kwanza watanzania ili nchi iwe na Neema mpaka hapo itakapovutia wahamiaji kuja Tanzania basi MRADI Huu utakuwa na maana kubwa.

Hebu tuwe na vipaumbele vya miradi siyo kuangalia miradi yenye ulaji na itakayowahakikishia watawala kuendelea kutawala. This is Nonsense project for the Current situation in Tanzania .
 
Last edited:
Nakupata vizuri. Ila kama kujifanya na yeye yuko jikoni ungetegemea atoe ka positive spin kuhusu mtu wake. Eti yeye akaenda kummalizaaa.

But then here is another thing, right, say ni msaliti, okay, huyu insider wa upande wa Masha amekuwa wa kwanza kujua kwamba hili bombshell limefika kwa Mengi, sio ingebidi insider wa Mengi ndio ajue kwamba we stumbled on this smoking gun against nemesis wetu and this and that? Unless ni mtu wa Masha ndio ali leak-isha soo akali-direct Mengi's way, kwa hiyo anajua Mengi amelipata! I mean, you follow me, right? Insider wa Masha katoa leak kwamba Mengi kapata nyeti! Amejuaje? Hahahaaaaaa, No, no, you tell me, am I missing inklings here?


Yaani i was about to say the same thing umeniwahi...hii issue inaonekana hao insider wa masha wame leak issue kwa Mengi..ndiyo maana wanasema duniani hakuna siri...siri ni yako mwenyewe ila dont ever include a friend or boyfriend/girlfriend or wife/husband...

Smart thinking!!!
 
Yaani i was about to say the same thing umeniwahi...hii issue inaonekana hao insider wa masha wame leak issue kwa Mengi..ndiyo maana wanasema duniani hakuna siri...siri ni yako mwenyewe ila dont ever include a friend or boyfriend/girlfriend or wife/husband...

Smart thinking!!!

You would keep secrets even to your Cupcake?..mmmhhhh.....okay
 
siri ni yako mwenyewe ila dont ever include a friend or boyfriend/girlfriend or wife/husband...

Smart thinking!!!

Muhimu kuangalia wa kushare nae siri as kuna watu madomo kaya ambao midomo yao haina break-wanahusudisha unews breaker aka umbea. Hawa hawachelei sio tu kuvujisha siri za wenzao, bali hata siri zao wenyewe!
 
Hili jambo inaonekana lilikuwa linafuatiliwa kwa ukaribu sana, nimepata bahati ya kuangalia TBC1 kipindi cha majibu ya papo kwa papo, the way Dr. Slaa alivyokuwa na confidence, I was shocked with Masha's position.
 
Nadhani Masha anahitaji kujitizama upya, marafiki aliyonao sidhani kama wanamshauri vizuri. Kuna mambo mengi ambayo wangeweza kumshauri na asingefikia hapa lakini sijui ni kwa sababu ya kulewa madaraka au bado kuna "utoto" fulani. Kuongoza wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi sio kitu cha mzaha, kwa mtu ambae ni serious, tusingekuwa tunamuona ktk mabaa akivinjari kama waziri huyu anavyofanya
 
Naomba murekebishe kidogo hapo, maana tunaweza kupoteza radha ya jambo hili. NIDA ni kifupi cha National Identification Authority. Hii ni mamlaka na sio Agency. Naomba tuendelee kusogoa kutokea hapo sasa
 
Suala la Vitambulisho ni la Muungano, hivyo kwa mfumo wa Agency huwezi kulitekeleza upande wa pili wa Muungano, ambao ni Zanzaibar. Kutokana na ukweli huu, ikaamuliwa ianzishwe Authority ambayo mfumo wake inaweza kufanya shughuli zake hadi Zanzibar
 
Masha,Masha,Masha,Masha. . . . . hivi ni nani hasa? Ana umuhimu gani kwa taifa? Kama mtu anaboronga na ameshaonesha udhaifu,uzembe na ukosefu wa maadili according to the code of ethics basi awekwe pembeni.Kubembeleza wakosefu ni wizi pia.Na tusipoangalia tabia ya kuwalea wezi inaendelea kushika kasi.
 
"Uzuri wa mzee Mengi huwa hapendi kuendekeza ubishi au malumbano, huwa analimaliza taratibu kwa sauti ndogo kabisa lakini kichwani mipango moto"
Naweza kukubaliana na huo usemi hapo juu na kwa kuongezea ni kwamba Bw.Mengi is very influencial and reserved at the same time.
 
Back
Top Bottom