Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Waziri Masha na Kashfa ya Vitambulisho

Don't get your hopes up high....inawezekana akarushiwa vi-softballs halafu mkaishia kuikandia clouds na watangazaji wake....
 
Eeh Mzee,

sasa ina maana magazeti ya Mengi yaliandika habari za uzushi?makanjanja bwana...watu hawana ushahidi..

tusubiri kuona watu wakilipa Fidia.Madhara ya siasa za Kuchafuana

Waandishi wetu wa habari wengi wao ni wavivu, nimehisi wengi huingia humu JF wakiziona habari humu hata ziwe za uzushi wao huzipamba na kuzifanya ni zao. Hawajui wengine humu JF hutowa vitu vichwani mwao, vya kusadikika.

Kiranga, komo.

Na kama ni kweli hao waandishi walitawanya habari za uongo bila kuwa na proof za hayo waliyo-yaandika, astahili yao wakipigwa mafaini tena naomba yawe heavy, labda ndio watakoma kupotosha wasomaji wa magazeti.
 
Gazeti limeshafanya kazi yake ya kuupasha umma kama limeandika habari za uongo..., Mhe. Masha anachoweza kukifanya ni kulishitaki kudai fidia na gazeti kuomba msamaha..., akifanya hivyo tutaamini kuwa yuko safi ila akikanusha tu kwa maneno haitamsaidia kwani jina limeshachafuliwa na watu watajua anaogopa kufikisha jambo mahakani kwani kuna uwezekano wa kutokea ushahidi ambao utakuwa vigumu kujitetea na hivyo kummaliza kabisa kisiasa
 
Capo di tutti Capi Kuhani,

Anayetakiwa kusaini mkataba ni Katibu Mkuu na si waziri! Yeye ndiye accounting officer. Kujiingiza mawaziri kwenye hili matokeo yake ndiyo hayo tuliyoyaona Buzwagi!

Mimi sipingi waziri kuonyesha concern. Ninachopinga ni kuingilia utaratibu uliowekwa. Kwa kufanya hivi tunakosa wa kumlaumu mambo yakienda kombo. Waziri anasema yeye alifanya kwa nia njema tu na si mtaalamu. Wataalamu wanasema walishindwa kumpinga waziri kutokana na kumheshimu. Mwisho ya yote ndiyo hayo tunayoyaona kila siku; barabara zinajengwa anakotoka waziri wa infrastructure, vyuo vya elimu vinajengwa alikotoka waziri wa elimu n.k. Mbaya zaidi, kutokana na kuamini nia njema ya hawa wanasiasa, watendaji wanakubali business card kama ishara ya power of attorney! Wote hawa, bila shaka, walifanya hivyo kwa nia njema na uzalendo kwa nchi yao!

Amandla.........

Kama Kuhani anavyohoji sababu ya kum-bypass Waziri katika maamuzi ya Wizara, mimi nauliza kazi ya Waziri ni ipi? Ni kwenda kwenye hafla mbalimbali ambapo mawaziri wanatakiwa wawepo, kuhudhuria mikutano nje ya nchi, kwenda kupresent bajeti na kujibu maswali bungeni? Kama hizi ndizo kazi za waziri, basi hakuna haja ya kuwa nae.

Katibu mkuu kiongozi na makatibu wakuu wa wizara wanatosha kufanya kazi hizo (tupunguze matumizi).

Kwa iliyopo sasa inaonyesha kuna viongozi ambao hawana kazi au hawaelewi kazi zao, na kuna wale wanaofanya kazi kupita mipaka kwa vile hawaelewi kazi zao. Wanafanya kwa uzoefu tu.

Majukumu ya Waziri ni nini?
 
Gerald amuulize alipokuwa huko anakoshukiwa kuwa alikutana na hao wakola alifikia Hoteli gani?? Ataje jina la hiyo hotel, namba ya chumba alichofikia na tarehe alizokuwa huko tuone kama hazioani na hizo zilizoandikwa gazetini!!
 
Lakini
Mtu kama waziri anaweza kuwa na paasport mbili yani moja ya kidipromasia ya serikali ya Tz harafu nyingine yake binafsi ambayo ni yamarekani ama ya UK.

Hivyo basi nini kinafanyika? Anaongea na SEGIM tukutane tarehe 5 lakini hiyo ni tarehe 1 anarudi bongo na pass lake lakidplomasia anatulia tarehe 1 ,2 na 3 bongo.Harafu anachukuwa pass lake binafsi la marekani anakamata NISSAN lake huyo nairobi anachukuwa pipa lake lake pale anapiga mkutano wake wa saa 2 ama 3 anakamata pipa lake anashuka Nairobi harafu hapohapo anaunganisha na nissan lake anaiingia Tarime
kufanya ziara .
 
Hivyo basi nini kinafanyika? Anaongea na SEGIM tukutane tarehe 5 lakini hiyo ni tarehe 1 anarudi bongo na pass lake lakidplomasia anatulia tarehe 1 ,2 na 3 bongo.Harafu anachukuwa pass lake binafsi la marekani anakamata NISSAN lake huyo nairobi anachukuwa pipa lake lake pale anapiga mkutano wake wa saa 2 ama 3 anakamata pipa lake anashuka Nairobi harafu hapohapo anaunganisha na nissan lake anaiingia Tarime
kufanya ziara .
Sasa hizi ndio hadithi za kusadikika!
 
wanandugu nina mawili matatu nitashukuru yakipata nafasi,huku businyalo mida hiyo inaniweza nikawa ofside,mhe waziri masha MB anadai kuwa yeye binafsi hawajui SAGEM
maswali yangu nikama ifwatavyo;

malamiko ya SAGEM aliyopata alipelekewa na nani? kwa mdomo au kwa maandishi,na kama ni maandishi je hayo maandishi yako wapi?


inakuaje aitetee kampuni asiyeijua?tena anawatetea kwa waziri mkuu? je alitaka kuingiza mkenge mhe pinda MB?

kulikuwa na tatizo gani kwa mhe masha MB,pale alipopata malalamiko hayo asipeleke kwa katibu mkuu wa wizara yake?ktk barua yake kwa Mhe pinda MB,Mhe Masha MB alikiri kutokuwa na mamlaka ya kisheria, je ni nani mwenye mamlaka ya kisheria kati Mhe Pinda MB na bodi ya mananunuzi ya wizara?

wakati Mhe Masha akiwa dodoma,ktk kamati ya Mhe Masilingi MB (nje,ulinzi na usalama ya bunge), Mhe Masha MB alitaka kuitumia riporti ya kamati ya tathmini kama riporti ya kumlinda, Je Mhe Masha MB alipata wapi ripoti hiyo? kwa elimu yangu kiduchu ya maswala ya utawala bora,hili huweza kuwa kosa kubwa,kwa kauli yake tu mwenyewe Mhe Masha MB,ingetakiwa apelekwe kwenye vyombo vya sheria

Ktk mkutano wake jana Mhe Masha MB na waandishi wa habari jana,Mhe Masha MB alidai kuwa taarifa za evaluation committee zilivujishwa ''kimaksudi'' kwa neno lakigeni ''delibarately'', je yeye kama waziri alichukua hatua gani kisheria ya hao walio vujisha taarifa?

la mwisho (kumradhi)
je Mhe Masha MB ana huhakika kuwa SAGEM hawana kesi ya rushwa Nigeria? je kama ushahidi ukiletwa kuwa SAGEM wana kesi ya rushwa ya ''mradi wa vitambulisho nigeria,yupo tayari kujiuzulu?

hayo tu

jioni njema
 
je Mhe Masha MB ana huhakika kuwa SAGEM hawana kesi ya rushwa Nigeria? je kama ushahidi ukiletwa kuwa SAGEM wana kesi ya rushwa ya ''mradi wa vitambulisho nigeria,yupo tayari kujiuzulu?


Everyday I fall in Love with JF ama kweli is the mighty home of great thinkers!!
 
Masha ni kijana na Joseph Kusaga ni kijana wanaelewana kaka.

- Mkuu Fairplayer, kumbe una akili sana Joe ndiye mmiliki wa Clouds, kwa mara ya kwanza Joe alipoenda kununua vyombo vya kisasa US, vya muziki wa disco lake, tulifuatana pamoja na tukafikia ka Masha, akiwa Georgetown kule DC in the 90s, sasa unafikiri Masha ni mjinga kwenda Clouds na sio kwingine?

- Angalia msije pata ugonjwa wa moyo wakuu! siamini kwamba keshop kutakuwa anything zaidi tu ya kumsafisha tena big time, naona wengi tummeondoka bongo siku nyingi.
 
Quote:
je Mhe Masha MB ana huhakika kuwa SAGEM hawana kesi ya rushwa Nigeria? je kama ushahidi ukiletwa kuwa SAGEM wana kesi ya rushwa ya ''mradi wa vitambulisho nigeria,yupo tayari kujiuzulu?

- Mkuu wangu masa mbona ninakuaminia sana bro, rushwa ya Nigeria waziri ajiuzulu Tanzania are you serious au ni April Fool leo?
 
- Mkuu Fairplayer, kumbe una akili sana Joe ndiye mmiliki wa Clouds, kwa mara ya kwanza Joe alipoenda kununua vyombo vya kisasa US, vya muziki wa disco lake, tulifuatana pamoja na tukafikia ka Masha, akiwa Georgetown kule DC in the 90s, sasa unafikiri Masha ni mjinga kwenda Clouds na sio kwingine?

- Angalia msije pata ugonjwa wa moyo wakuu! siamini kwamba keshop kutakuwa anything zaidi tu ya kumsafisha tena big time, naona wengi tummeondoka bongo siku nyingi.

Kwa hiyo hapa ni mwendo wa kujuana juana na kulindana lindana, scratch my back I will scratch yours. Waarabu wa Pemba hujuana kwa vilemba.

Watanzania wanaotegemea ukweli na nguvu ya vyombo vya habari walie tu.
 
- Mkuu Fairplayer, kumbe una akili sana Joe ndiye mmiliki wa Clouds, kwa mara ya kwanza Joe alipoenda kununua vyombo vya kisasa US, vya muziki wa disco lake, tulifuatana pamoja na tukafikia ka Masha, akiwa Georgetown kule DC in the 90s, sasa unafikiri Masha ni mjinga kwenda Clouds na sio kwingine?

- Angalia msije pata ugonjwa wa moyo wakuu! siamini kwamba keshop kutakuwa anything zaidi tu ya kumsafisha tena big time, naona wengi tummeondoka bongo siku nyingi.

Heheheheheheee...duh mazee na wewe bana....who don't you know? Lol

Eniwei, inawezekana una point...........tusubiri tuone hiyo kesho....
 
Heheheheheheee...duh mazee na wewe bana....who don't you know? Lol

- Mkulu mwenzangu Nyani heshima mbele bro, ndio maana JF siku zote tunakuwa tofauti na wengine wote katika this game, maana huwa tunawajua karibu wanaotengeneza habari za taifa letu kuanzia kwenye siasa na hata kwenye sekta zingine, sasa nilitaka tu kuweka ukweli kuhusu matumaini ya hiyo kesho,

- Anytime ukisikia kiongozi amekimbilia kwenye station flani na sio zingine basi ujue kuna sababu, kiongozi asiyekwua na sababu huita wote sikuwahi kusikia Mwalimu, akiita station moja tu!
 
Kwa hiyo hapa ni mwendo wa kujuana juana na kulindana lindana, scratch my back I will scratch yours. Waarabu wa Pemba hujuana kwa vilemba

Mkwere pia alisema Lazima uliwe ili ule something like that....
 
- Mkuu wangu masa mbona ninakuaminia sana bro, rushwa ya Nigeria waziri ajiuzulu Tanzania are you serious au ni April Fool leo?

Mzee wa Sauti,

Hapa bwana nilikuwa naonyesha SAGEM wananuka rushwa Nigeria sasa kama Lau anawapigia chepeto Tanzania basi naye ni mla rushwa ni vizuri apumzike afanye kazi alobobea na aliyo na umahiri nayo ya sheria

Masanilo
 
Mzee wa Sauti,

Hapa bwana nilikuwa naonyesha SAGEM wananuka rushwa Nigeria sasa kama Lau anawapigia chepeto Tanzania basi naye ni mla rushwa ni vizuri apumzike afanye kazi alobobea na aliyo na umahiri nayo ya sheria

Masanilo

- Mkuu wangu hivi hujasikia kwamba tayari ana barua toka ubalozi wa Nigeria kwamba hii Sagem ni safi, kinachotakiwa hapa ni video ya mkutano wake na Sagem kama ulifanyika kweli kule Geneva,

- Unakmkumbuka Fujirmori wa Peru, Spy Chief wake aliwahi kupatikana na this kind of soo, lakini wakali wakamtolea video, akajizulu na kufungwa jela pia sasa hapa bila video, itakua ngoma ya mganda maana kumbuka jamaa ni mwanasheria tena aliyebobea.
 
Swala la rushwa ya Nigeria liko valid sana katika kesi ya Tanzania. Ikiwa inaonekana kwamba Waziri Masha anaenda "out of his way" kuwakingia kifua SAGEM, bila kufuata utaratibu, kunaweza kunuswa harufu ya upendeleo/ rushwa.

Ikijulikana kwamba SAGEM wamehusishwa na rushwa huko Nigeria, kujulikana huku kutaipa dhana kwamba Waziri Masha ananufaika kirushwa rushwa kutoka SAGEM nguvu, kwa sababu SAGEM wataonekana kuwa na historia ya rushwa.

Kwa hiyo tusitake kusema kuwa issue ya rushwa ya Nigeria haihusiki Tanzania. kuna kitu kinaitwa "track record" on the part of SAGEM and "reasonable suspicion" on the part of Waziri Masha.

Ukiweka moja na moja unaweza kupata uelewa kwa nini watu wanauliza maswali mengi.

Kuna mambo mengine ya serikali yanataka siyo tu haki itendeke, bali pia ionekane kutendeka.Kuna mambo mengine yanataka sio tu rushwa isifanyike, bali pia ionekane kutofanyika.
 
- Mkulu mwenzangu Nyani heshima mbele bro, ndio maana JF siku zote tunakuwa tofauti na wengine wote katika this game, maana huwa tunawajua karibu wanaotengeneza habari za taifa letu kuanzia kwenye siasa na hata kwenye sekta zingine, sasa nilitaka tu kuweka ukweli kuhusu matumaini ya hiyo kesho,

- Anytime ukisikia kiongozi amekimbilia kwenye station flani na sio zingine basi ujue kuna sababu, kiongozi asiyekwua na sababu huita wote sikuwahi kusikia Mwalimu, akiita station moja tu!

Una pointi hapo mazee. Hata mimi nimewaambia watu humu wasiwe na mategemeo ya juu....la sivyo wanaweza wakajikuta wanashangaa wenyewe....
 
- Sasa akisema kwamba yeye hakujua kwamba hii kampuni imewahi kuhusika mna rushwa huko nyuma, na kwamba angejua mapema asingeikubali then what? Sasa hapa unahamisha soo kwa ubalozi wetu Abija wkamba wao ndio hawakumtaarifu waziri au serikali yetu kwamba ile kampuni ina utata, lakini kama kuna usahidi waziri alifahamishwa mapema lakini hakusikia then kweli, lakini waziri tayari ameshaenda kupata barua toka ubalozi wa Nigeria, kwmaba sagem wako safi sasa mkuu huoni kwamba hapo kuna a weak ishu hata kabla ya kumuuliza?

- Knowing all the facts za hii kesi sasa hivi ni kwamba kumefanyika papara katika kuifuatilia hii ishu, as the results wahusika walishituka mapema na kuanza ku-cover their backs, barua za siri zilizokuwa zina-leak walikuwa ni wao in the control we lost this one, tena big time kwa sababu the bigger ishu tayari ameshaipangua, sasa eti hii ya Sagem kuwa na historia ya rushwa ndio itambana, hapana I am not that naive kuamini hayo ya sagem na rushwa kuwa ni ishu.
 
Back
Top Bottom