Nyani Ngabu, jamaa anaboa sana, sijui ndio miongoni mwa waliotegemea kufaidika na mgao? Duuh... kweli njaa mwana haramu, unaweza kuuza mwanao Albino hivi hivi.
FM,Ni haki ya Kuhani kuhoji msimamo wetu. Ni vizuri akituhoji ili tuwe na uhakika zaidi ya tunayoyasema. Kwa kuhoji kwake kumesaidia kuweka wazi chain of command serikalini. Kuna wengine tumefaidika na hilo. Kwa kuhoji anatufanya tuangalie upya kile tunacho take for granted. Hajakosea kuhoji. Ikiwa wote tunakubaliana basi hapatakuwa na mjadala. Na hata tukifika mwisho wa mjadala si lazima tukubaliane.
Amandla.....
Kuhani hapa umekosea. Mtendaji mkuu wa wizara ni Katibu Mkuu na si waziri. Ndiyo maana barua zote zinazoandikwa kwenda kwenye wizara zinakuwa addressed kwa Katibu Mkuu na si waziri. Na barua zote rasmi katika wizara zinaandikwa kwa niaba ya katibu Mkuu na si waziri. Mawaziri, waziri Mkuu na Rais si watumishi wa serikali ( civil servants) wao ni political appointees. Kiutendaji basi, bosi wa watumishi wote wa serikali ni Katibu Mkuu Kiongozi. Huyu ndiye bosi wa Katibu Mkuu na si waziri. Katibu Mkuu Kiongozi ni mshauri mkuu wa serikali kiutendaji. Kwa bahati mbaya kwa muda mrefu makatibu wakuu walikubali kufunikwa na mawaziri kiasi cha mawaziri kujisahau. Masha amempelekea malalamiko Pinda kwa sababu yule ndiye bosi wake. Pinda nae atamshauri Rais ambae ndiye bosi wa wote hawa. Mwenye makosa hapa ni waziri Masha na si Luhanjo. Ingawa inauma lakini yeye si Mtendaji Mkuu wa Wizara.
FDR ukweli uliosema hautaeleweka leo, lakini nakuhakikishia kuwa katika muda mfupi ujao utaeleweka.wakuu wana jf, id deal haina tofauti na twin tower project, id za wapiga kura na kadhalika, mkuu wa medani na wengine mimi ninapenda kujiridhisha juu ya utaratibu wa cs kuwasiliana na accounting officer wa wizara eti kwa nia ya kuepusha ushawishi/maslahi yanayohisiwa juu ya lawrence fortu masha!!! Mimi naamini hapa kuna suala la msingi la kumtizama kwa jicho la uchunguzi mnyalu luhanjo, ninaona kuna game ya kuuficha ukweli wa makusudi kuwa cs naye ana agenda binafsi juu ya hii project, yeye ktk deal ya namna hii ni lazima awe invisible lakini si kwa wale anaowachukulia minutes ktk kikao na rais wetu, najaribu kumuangalia luhanjo zaidi hapa kuliko mtu yeyote yule na ninashauri hawa akina fmes na wenzake wamungalie mzee luhanjo kimaadili na tuanzia pale alipokuwa maliasili akiwa na zakhia then foreign na sasa ikulu yetu, kumbukeni kilichompata mrithi wake salehe pamba na tycoon star tv kwa kumgusa tu kijana severe!!! Marsha ameingia ktk mpambano ambao nadhani alitegewa na akaingia aliposituka ameamua kuwa jasiri kupigana kwa kila aina ya silaha aliyo nayo, ninachokiona hapa ni mkono mrefu wa mengi na genge lake ambalo limejizolea umaarufu usiowastahiki ktk jamii, inanifadhaisha sana ninapoona ikulu ikimbeba mengi ktk hadhara kama ndiye mlipa kodi kiongozi tanzania. Kijana mwenzetu haitaji sisi vijana kughiribiwa kuwa hatufai bali ni msaada wa dhati wa kupambana na maadui ambao sasa wanaleta hoja kuwa eti sisi vijana si lolote!! Marsha anapaswa kusimama ktk kweli na siyo kinyume, ktk hili anaweza akawa shujaa au muhanga. Nini nafasi yetu sisi wana jf ktk sakata hili la kumuangamiza kijana huyu mchanga ktk siasa ila anayeonekana tayari purukushani zinamkomaza?? Je sisi ni sehemu ya kushabikia fitina na kuiasi kweli?? Najutia kuiona jf ikihukumu watu eti kwa sababu kila kukicha magazeti ya mtu fulani yamemng'angania marsha? Nimeona mabandiko ya magazeti yetu humu mbona hatupendi wala hakuna ktk yenu ninyi wakulu tunawaowaheshimu humu aliyethubutu kubandika rai ya leo na viambatanisho vyake?!!! Mungu atubariki na sasa tuanze kuwa wakweli rohoni mwetu kabla hatujafanya chukizo kwa wenzetu.
FDR ukweli uliosema hautaeleweka leo, lakini nakuhakikishia kuwa katika muda mfupi ujao utaeleweka.
Marsha pamoja na matatizo yake, kwenye hii issue ya IDs anatetea ukweli na kama waziri mhusika ni yeye mwenye dhamana hatimaye kuwajibika kwa lolote lile litakalotokea wala siyo Luhanjo. Tena la ajabu nu kuwa katibu mkuu wake ana amua makusudi kumwandikia CS kisirisiri bila ya kumhusisha waziri wake, na issue ambayo anailalamikia ni kwamba waziri hakukubaliani na double standards zilizotumika kuengua wazabuni wengine wakati huo huo kuna wengine waliokuwa na short-commings more serious waliopewa nafasi za kuzirekebisha. Anachotetea Marsha ni double-standards zilizotumiwa!
Waziri Marsha baada ya kutokubaliana na katibu mkuu wake (wa wakati huo) akatoa wao kuwa PPRA iliangalie hilo swala kwa undani na watoe uamuzi kama hiyo evaluation process ilikuwa fair kwa wazabuni wote. PPRA ndicho chombo cha juu kuliko vyote kisheria kwenye mambo ya zabuni. Katibu mkuu wake akalikwepa hilo na kumwandikia Luhanjo waraka ambao ulimfanya Marsha naye amwandikie bosi wake, waziri mkuu.
Kwenye hili swala FDR Jr. umegusa raw-nerve; hebu kumbuka ni nani alianzisha mchakato huu - Mungai! Mungai + Luhanjo = 1; Tena la kuchekesha ni kuwa huyo katibu mkuu aliyemwandikia Luhanjo barua sasa hivi hayupo tena wizarani hapo, ila bado ana watu wake ambao waliinyofoa barua hiyo na kumpa Slaa. Hili dili lilisukwa na Mungai na agents wake ambao bado wapo wizarani na hata wengine wao wapo kwenye idara yenyewe ya vitambulisho ya Mr. Dickson Mwaimu (mlarushwa ile mbaya) pamoja na IT expert wake aliyetimuliwa/demoted Immigration akapelekwa Mbeya baada ya kupokea rushwa kwenye tenda ya passport - baadaye akaenda Uingereza - Oxford - akasomea MSc na aliporudi Mungai akamhamishia kwenye hiyo agency. Kwenye hili wanaoomba Marsha lizwe wako kibao; payroll hiyo ni ndefu ingawa wengine wataambulia bia tu!
Marsha alichofanya cha kuuliza na kutoa option ya kuhusisha PPRA ni sawa. Motive zake za kufanya hilo, who knows ila la uhakika nitakalo lisema milele ni kuwa huu mradi ulisha sukwa mapema mno na walaji walishajiweka tayari na pesa wanazo, Marsha kachafua hali ya hewa. Kuna katibu mkuu mstaafu aliyeteuliwa kuwa consultant kwenye huo mradi hadi leo wamemweka kando kwa vile haeleweki eleweki!
La kuchekesha ni hilo kampuni la Sagem (nime-Google) mbona limepata matenda ya vitambulisho mengi tu Africa (over 15 projects) na hata huko Nigeria walikohonga eventual walipewa kazi. Hata huku majuu FBI, FBI certifies Sagem Sécurité's new MorphoTopTM biometric sensor - find BIOMETRICS , Secret Service, Interpol na idara nyingi nyeti ulimwenguni wanawatumia. Labda inawezekana kuwa wanazaipata kazi zote kwa kuhonga! Or they are just good technically kwa hivyo inawezekana wazabuni wenzao kwenye zabuni la vitambulisho bongo waliwashtukia na kuamua kuwaengua kimafya! Kama ni hivyo basi wamezidiwa kete kijanja na wangojee kwingine.
La mwisho ni kwamba kuna issue ya kutumia model ya Malaysia katika utoaji wa vitambulisho vyetu ambalo linzaungumziwa mara nyingi; hivi hawa wa Malaysia wa utaalamu kweli au ni madalali wa Sagem; Nimekumbana na article hii nikabaki mdomo wazi, inawezekana hao hao Sagem tukawa tunawakubali through the back door! Just a thought. Soma hili; ThirdFactor | Sagem Sécurité selected by Malaysia for new biometric ID system
ZalendoHalisi
ZalendoHalisi na FDR Jr.
Mimi binafsi hii issue ya Masha kwa taarifa ambazo ninazo lakini kwa kuzingatia kuwa hadi sasa mamlaka halali zinapitia shauri hili niliamua kukaa kimya ili niendelee kuona nini kinafanyika.
Sitasema hasa yale ambayo ninayajua juu ya vitambulisho kwa sasa hivi lakini kinachoendelea zaidi ni kujaribu kum-eject Masha katika system. Na hii suala ya vitambulisho imekuja just by the way lakini vita iliyopo kati yake na baadhi ya 'vingunge' ni kubwa sana. Masha kwa wao anaonekana kuwa ni threat na potential katika siasa za sasa na za baadae. Kinachotafutwa ni kuhakikisha anakuwa-marginalized kwa kiwango chochote na kwa gharama yeyote ile. Katika watu ambao wametumwa kummaliza Masha si Mengi pekee the list is long. Nadhani Masha kwa sasa hana kitu cha kupoteza ni vema akapigania kuonesha maovu yaliyojijenga kwani katika hili la ID wengi wanahusika na ni kweli linafanana kabisa la 'Twin Tower'. Nina hakika huko mbele ya safari kuna wazito watakuja kupanda kizimbani kujibu tuhuma dhidi yao.
tunakowenda siko yani tu Mengi akiwa hamtaki mtu basi anamzushia uongomalafu anajiuzuru.....Nasema Masha ataibuka mshindi kwenye hili na wote mtaaibika.- Mkuu Zalendohalisi, mbona ulipotea sana bros kulikoni?
- Tunasema hivi jina la ndugu Lau limechafuka sana ni distraction kwa mkuu wa kaya na taifa kwa ujumla, cha muhimu ni vyema akakaa pembeni tu na wakati muafaka ni sasa.
tunakowenda siko yani tu Mengi akiwa hamtaki mtu basi anamzushia uongomalafu anajiuzuru.....Nasema Masha ataibuka mshindi kwenye hili na wote mtaaibika.
tunakowenda siko yani tu Mengi akiwa hamtaki mtu basi anamzushia uongomalafu anajiuzuru.....Nasema Masha ataibuka mshindi kwenye hili na wote mtaaibika.
FDR, you are not doing justice to JF and to your self in your analysis above.
a) Luhanjo & Mengi: Hii ni myth kubwa kuwa hawa wanashirikiana. Luhanjo inafahamika wala hapokei simu za Mengi, na Mengi akiwa na shida Ikulu anamwingia JK moja kwa moja, haangaishani na Luhanjo.
b) Issue ya tender ya ID ni suala la ulaji, tatizo ni kuwa UWT wako ndani sana katika hili kwa ajili ya usalama. Masha kaingia mkenge kwa kuchukua taarifa za siri (briefings toka kwa PS wake) na kujaribu kuzitumia 'kuwasaidia' wazabuni. Angesubiri hizo taarifa zikatoka rasmi, wala tusingesikia kelele hizi. Tatizo ni kuwa kama angesubiri pia, window of opportunity ya kuwasaidia wazabuni wake ingekuwa haipo. Na pia hakujua (au alijua akapuuzia) kama taarifa alizopewa na PS pia ziliishafika Ikulu kwa mkondo wa UWT.
c) Mengi na magazeti yake hapa ni kama tai kaona mzoga. Hakuna kipya walichokitengeneza, ila madudu yote wanayanasa na watu wengine wengi tu wa magazeti. Ni wachache wenye ubavu wa kuandika jinsi ilivyo. Magazeti hayatengenezi matukio. Masha anatengeneza matukio, na wajanja wanayatumia hayo matukio kuonyesha udhaifu wake.
Huu uwezo finyu (myopic view) wa Masha hauukuanza leo (toka TOL, IMMA, Uchaguzi 2000 Sengerema, Vurugu 2005 Nyamagana, etc) ila wakati huo hakuna aliyekuwa na shida naye sana. Sasa ukiweka hayo yote plus Mengi Siku Saba, Mauaji ya Albino, Keko Mramba/Yona, Mademu Rose Garden, Watoto Vifo Tabora, Barua kwa Pinda, etc hata watetezi wake wanakosa nguvu. Utazuia kipi? Masha anawapa silaha mahasimu wake, kummaliza mwenyewe.
Mmeganda ghafla! Mnasoma?
Alomuradi usitupandikize vijidudu au virusi! 😀Mmeganda ghafla! Mnasoma?