A
Anonymous
Guest
Nilifika Babati kusubiri basi kwa ajili ya kuelekea mkoa fulani, wakati nipo pale nilihisi njaa, niliamua kutafuta sehemu mojawapo wanaopika pale hususan wanaokaanga chipsi ili nile.
Nilipokelewa vizuri na kuoneshwa sehemu ya kukaa, niliagiza chipsi, nikaletewa lakini zilikuwa za baridi sana. Nikamuambia aliyeniletea kuwa siwezi kula zikiwa zabaridi ilibidi achukue na kuniambia nisubiri ambazo zipo jikoni.
Wakati nasubiri nikiwa kwenye meza Wanawake wawili walikuja kwenye banda lile la chipsi miongoni mwao alikuwa ndiye mmiliki, Wanawake hao walitoka kuuza Chipsi kwa abiria walio kuwa kwenye mabasi hapo stendi.
Kilichonishangaza ni kwamba hawakuwa wanazingatia usafi wakati wa uuzaji wao na hata mazingira yao.
Katika meza niliyo kaa kulikuwa na bakuli la chumvi ambalo limechanganyika na stick, kila mmoja alipokuja kuchukua chipsi kwa ajili ya kupelekea abiria walikuwa wakichukua chumvi na zile stick kwa mikono yao na hakukuwa na kitu maalum cha kuchukulia chumvi.
Nilipokelewa vizuri na kuoneshwa sehemu ya kukaa, niliagiza chipsi, nikaletewa lakini zilikuwa za baridi sana. Nikamuambia aliyeniletea kuwa siwezi kula zikiwa zabaridi ilibidi achukue na kuniambia nisubiri ambazo zipo jikoni.
Wakati nasubiri nikiwa kwenye meza Wanawake wawili walikuja kwenye banda lile la chipsi miongoni mwao alikuwa ndiye mmiliki, Wanawake hao walitoka kuuza Chipsi kwa abiria walio kuwa kwenye mabasi hapo stendi.
Kilichonishangaza ni kwamba hawakuwa wanazingatia usafi wakati wa uuzaji wao na hata mazingira yao.
Katika meza niliyo kaa kulikuwa na bakuli la chumvi ambalo limechanganyika na stick, kila mmoja alipokuja kuchukua chipsi kwa ajili ya kupelekea abiria walikuwa wakichukua chumvi na zile stick kwa mikono yao na hakukuwa na kitu maalum cha kuchukulia chumvi.