Watu wa NIDA wana majibu ya hovyo jamani..

Watu wa NIDA wana majibu ya hovyo jamani..

Hizo hongohongo ndo zinafanya baadhi ya wafanyakazi wapenda hela ndogondogo kuwa na majibu ya hovyo ili wewe ambaye haujatoa hizo hela,ukate tamaa na ikiwezekana uwalainishe kwa vihelahela hivyo.Wajinga sana baadhi ya wafanyakazi wa serikali.
Yaani,.
 
Taasisi zote za serikali zimeoza hakuna penye nafuu, hospitali, mashule, tra, nssf kote hakuna penye nafuu.

Nachelea kusema matatizo yameanzia juu huko. We all know uwezo wake, usitegemee huku chini kuwe na ufanisi.
 
Mboso aliimba " na kwanza ndo tunajidaiiii... Kama afisa wa nida .....Sijui Nini na Nini tambaaa"


Anajua Majamaa walivyo watu wa hovyo

Nikanakwamba wao ndo wanatupa uraia wa kuwa watanzania 😂😂😂😂aisee
Itakua walimfanya kitu na yeye😃😅😂😂
 
  • Kicheko
Reactions: a45
Ndio uoga tunao sema ulishindwa kuwapa live pale pale? yaani wamekujibu hovyo umekaa kimya umekuja humu na fake ID kullalamika? ndio sehemu ya kulalamikia? ulishindwa nini kulalamikia pale na kuwapa Black and white? Tuache huu upoyoyo
Mie sipendagi kuongea ongea mkuu mtu anitukane na mimi kimjibu siwezi
 
Ni kukosa akili tu, mtu mwenye akili huwezi kumjibu hovyo mtu aliyekuja kupata huduma unayoitoa.
Tena mtu hajui utaratibu badala ya kumwelekeza unamtukana seriously??
 
Pole sana ila huo ndio uhalisia wa waajiriwa wengi hasa serikalini na taasisi kubwa kubwa.

Kuna siku nipo CRDB nikaomba yule teller anibanie risiti za malipo na invoice yake azigonge na mhuri wa malipo, akanijibu sio kazi yake namchosha. Nikamuuliza si ni wewe umenihudumia nielekeze wapi nikapate hiyo huduma akajibu usinichoshe pisha wengine wapate huduma. Nikamwambia sitoki hii n kazi yako mpaka uikamilishe hata kwa kutokupenda, akajinunisha akafanya huyo nikasepa zangu.

Hawa watu ni wa ajabu sana.

NB: KWA MLIOAJIRIWA TEKELEZENI WAJIBU WENU WA KUWAHUDUMIA VIZURI WANAOHITAJI HUDUMA KWENU. KAZI MLIOMBA WENYEWE ILA MKISHAZIPATA MNAENENDA KINYUME NA UTARATIBU.
Eti usimchoshe mwee!
 
Ungekuwepo mfumo wakuwa report, yani nivyema watumishi wote nchini wavae t-shirt au sale amazo ziko na maelezo ya Jina lake, na namba ya upekaa ya utumishi, pawe na mfumo wa kumriport wenye orodha ya matukio mtu unawaza chagua kwanini umemriport,
Mfumo unaweza toa alert sehemu husika ikiwa namba of reports kwa mtumishi huyo zinaongezeka
Sidhani kama hata wana huo mda wa kuskiliza kero za wananchi
 
Back
Top Bottom