Sultan MackJoe Khalifa
JF-Expert Member
- Nov 24, 2022
- 5,508
- 11,264
Wateule wa Rais Katibu Mkuu, Katibu Mwenezi, Makamu Mwenyekiti Taifa, Wenyeviti na Makatibu wa CCM Mikoa, UVCCM, UWT na Mawaziri, siwaoni wakimsaidia Mama Samia, Rais na Mwenyekiti wa Chama Taifa kujibu hoja za uwekezaji wa bandari!
Kwenye maamuzi ya Rais Samia siku za nyuma waliitisha press, makongamano na maandamano ya kumuunga mkono.
Mfano mmoja wapo ni suala la pesa za mikopo, Mama Samia alitetetewa na ngazi zote za chama na serikali ndani na nje ya Bunge, kwenye swala la mikataba ya bandari siwaoni, wamepatwa na nini?
Wajitokeze wawe wawazi wanapinga au wanaunga mkono uwekezaji wa bandari, sambamba na kujibu hoja zote za kupotosha na za kweli kuhusu mikataba ya bandari!
Kwenye maamuzi ya Rais Samia siku za nyuma waliitisha press, makongamano na maandamano ya kumuunga mkono.
Mfano mmoja wapo ni suala la pesa za mikopo, Mama Samia alitetetewa na ngazi zote za chama na serikali ndani na nje ya Bunge, kwenye swala la mikataba ya bandari siwaoni, wamepatwa na nini?
Wajitokeze wawe wawazi wanapinga au wanaunga mkono uwekezaji wa bandari, sambamba na kujibu hoja zote za kupotosha na za kweli kuhusu mikataba ya bandari!
Kila waziri anaongea yake kuhusu Bandari, Wananchi wanazungumzia MKATABA!
Rais Samia aliwahi kumtukana waziri wake kwamba alifanya 'nonsense'. Limekuja suala ya kuuza bandari sasa kila waziri na wanasiasa wanainuka kutetea uuzwaji huo wanaongea nonsense! Lukuvi kajitutumua akajikuta nonsense yake inaeleza umuhimu wa kuvutia wawekezaji. Wananchi wanazungumzia MKATABA...
www.jamiiforums.com