Watanzania wanaotumia LinkedIn ni washamba

Watanzania wanaotumia LinkedIn ni washamba

Wewe ndio hujaelewa kabisa mada unaonekana ni kilaza japo unataka kujitutumua uonekane ni intelectual.
Mimi nina connections na watu 4000 nakosa nini kwa mfano.

Hatupo hapa kwenye hii mada eti kwa sababu tupo desperate sana na connections za wabongo la hasha.

Ila tupo hapa kuelimishana na watanzania wenzetu wajue umuhimu wa kufanya connections na watu mbalimbali na kwa mfano mimi nikikuomba connection haimaanishi kwamba mimi nahitaji unisaidie inawezekana nikakuomba connection wewe halafu badae nikakusaidia vile vile"HAPA NDIPO KUNA MISUNDERSTANDING".

Huu ustaarabu ndio watu weusi wameukosa,mimi naweza nikawa Senior kwako na wewe ni Junior lakini still nikakuomba connection hata kama hauna faida kwangu!

Hivi unajua maana ya neno MTANDAO?
Iko hivi wewe unaweza ukawa hauna faida kwangu na mimi nikawa sina faida kwako directly lakini tukaconnect then badae kuna mtu may be uliconnect naye ataniona umuhimu wangu atanitafuta, na mimi pia kuna watu wangu nilioconnect nao watakuona umuhimu wako watakutafuta.

Mwisho kabisa,nimewahi kutafutwa nikapewa kazi za maana mara 2 kupitia Linkedin bila kuomba only my CV impression thus why naijua umuhimu wake nyinyi ambao mnafikiri linkedin ni kama facebook au instagram endeleeni na mashauzi yenu.
Wewe unayehangaishwa na mambo ya kipumbavu pamoja na watu wa aina hiyo hamfai LinkedIn. Yawezekana hao uanowasema wameconnect na ninyi kwa kuwa hawawafahamu, lakini usishangae utakapoweka wazi upumbavu wako ukala block au ukawa ignored. Kama hapa tu mnaonekana kupwaya, itakuwaje LinkedIn?

Kwa watu wa aina yako na mtoa mada, hamtapata conncetions za Watanzania wengi ambazo ninyi mnaziita "kutaka urafiki" kwa sababu wanawafahamu viwango uchwara vyenu. Mtaconect na aho wasiowajua ambao hata hivyo hawatakuwa na airtime na ninyi.

Kwa moyo wa upendo na huruma, ninafeel namna mnafeel kwa kubaguliwa wakati pia mnandoto za kusonga mbele na kuwa na connections mbalimbali kwa aspirations tofauti zikiwemo mahusiano, taaluma, uchumi, elimu, biashara, n.k. n.k

Please try to make transform your level of understanding and attitudes before finger pointing at others for ignoring you. Siyo kila connection is worthy your time and dreams. Usilazimishe mahusiano. Hao wachache wanaokukubali, shirikiana nao kwa upendo katika kuboresha maisha na kutengeneza milango mingine kwa sasa na hata baadaye. Mtu asipokupokea usimtukane kwa kuwa humfahamu na hujui anamalengo gani na zaidi hujui kama ni wa msaada kwako au ni majuto yako.

Mungu anaweza kuwa amekupa mtu mmoja na pengine hata nje ya mitandao au nje ya nchi ambaye ni kiungo muhimu katika ndoto na juhudi zako za kusonga mbele kuliko hao unaolazimisha wakuunge. Kumbuka watu wapo na mipango n amalengo yao na si lazima wawe kwenye mipango yako. Hivyo ustaarabu si kuwalaumu na kuwatukana eti hawajakuunga. Kwa heri.
 
Kwani lazima uwe na connections nyingi kiasi hicho we unazo ngapi?
 
Hivi hajapatikana rijali wa kumtolea huyu mdada nyegezi zake akaacha hiki kiherehere Cha kufatilia yasiyomuhusu
 
Habarini za leo wakuu,

Leo nimeona niwaletee mada hii wakuu.

Katika uchunguzi wangu niliofanya Linkedln nimegundua watanzania wenye akaunti LinkedIn

1. Ni washamba kwa maana kwamba hawajui maana ya mtandao wa LinkedIn

2. Profile zao za kitoto kwa maana kwamba hazivutii kabisa. Hawaja zipambanua vya kutosha, sijui wanakwama wapi.

3. Ukiwaomba urafiki hawakubali ni washamba sana. Wanadhani ule mtandao ni sawa na facebook.

4. Hasa hawa wanaofanya kazi kwenye vikampuni na vitaasisi vizuri ndio wanao jidai zaidi kwa vile wapo makazini basi hawaoni haja ya kutumia LinkedIn zaidi. Ila siku wakitumbuliwa ndio wanaanza kukuru kakara za kutafuta connection LinkedIn

5. Wanajiona sana na ndio sababu hawakubali kuwa na connection na watu wengine. Ndio sababu utakuta jitu lina connection ya watu 10 kwenye LinkedIn yake. Huu ni ushamba wa hali ya juu na ni aibu.
Wewe unadhani mtu akikuomba urafiki anakuomba kazi sio, acheni ushamba dunia imebadirika hii.

Mtu kama Bill gates tajiri wa dunia ana connect hadi na wakulima waliopo afrika wala hajali anaelewa nini maana ya LinkedIn.

6. Sijui shida iko wapi kwa watanzania wenzangu. Nyie mlio makazini mnakwama wapi kujipambanua kwenye account zenu za LinkedIn.

Wakuu nisaidie kuwaponda hawa watu mimi nimeishia hapa.

Watanzania wa LinkedIn wanaboa sana.

Utakuta kijamaa kinafanya kikazi cha mshahara laki saba basi kinavimba kichwwaaaaaaaa. Ukikiomba urafiki hakikujibu kinakaa kimya tu.

Je ungekuwa na mishahara kama ya kwetu ungefika wapi wewe.

Funguka acha ushamba wenzako tunachati na akina Jenifer Lopez Linkedln tunashauriana mambo mbalimbali.

Acheni ushamba na vikazi vyenu vya mishahara ya mboga.

Umeanza vyema tu katika Kuijenga Hoja yako na niliipenda, ila huku mwishoni umemalizia kwa Dharau na Ujivuni. Sasa Wewe pia ndiyo Mshamba!
 
Embu tuanzie hapa mtupe info kwa full details za huo mtandao then tutajua chakuwachamba(jokes) hao WANAZENGO.
 
Hakuna point ya maana yoyote uliyo andika zaidi naona lengo lako lilikua kujisifia una mshahara mkubwa
Haya lipia tangazo
 
Ndio maana tukasema watanzania hawajui matumizi ya Linkedin.
Kwa hayo majibu unayotoa ndio inadhihirisha wazi kwamba maneno ya mtoa mada ni kweli.
Haiwezekani niwaombe connections Directors/CEOs wa nchi mbalimbali wa Kenya,Dubai,Pakistan,Oman,Qatar na wana accept requests bila mashaka halafu wewe kapuku umeajiriwa sijui ni office clerk/administrator ndio uniogope kukubali request yangu na kuanza kunata kwa kipi cha maana ulichonacho au una kitu gani cha kuibiwa/kutapeliwa?
Kwani lazima?

Unaelewa kwamba kila mtu ana uhuru wa kuitumia LinkedIn anavyotaka?

Wengine hawataki network kubwa, wanataka kuwa Linked na watu wachache tu.

Wengine wamekataa kabisa hata kuingia huko LinkedIn?

Unaelwa Social Media zinavyo commoditize user info?

Unaelewa kwamba Social Media za "bure" zote, unalipia kwa kuwapa data zako na za network yako?

Kwani ni lazima kuwa na network ya watu wengi?

What's next? Utalaumu watu ambao hawapendi marafiki wengi, kwa sababu ni washamba, hawajui manufaa ya urafiki?

Unataka kuwapangia watu maisha?

Huoni kwamba kutaka kuwapangia maisha watu wasiokujua wala kukujali ndiyo ushamba wenyewe hapa?
 
Kwani lazima?

Unaelewa kwamba kika mtu ana uburu wa kuitumia LinkedIn anavyotaka?

Wengine hawataki network kubwa, wanataka kuwa Linked na watu wachache tu.

Kwani ni lazima kuwa na network ya watu wengi?

Whats next? Utalaumu watu ambao hawapendi marafiki wengi, kwa sababu hi washamba, hawajui manufaa ya urafiki?

Unataka kuwapangia watu maisha?

Huoni kwamba kutaka kuwapangia maisha watu wasiokujua wala kukujali ndiyo ushamba wenyewe hapa?
Duh kwa namna hii watu wa nchi yangu yangu wanatia aibu kwenye ishu ya utandawazi
 
Kwani lazima?

Unaelewa kwamba kila mtu ana uhuru wa kuitumia LinkedIn anavyotaka?

Wengine hawataki network kubwa, wanataka kuwa Linked na watu wachache tu.

Wengine wamekataa kabisa hata kuingia huko LinkedIn?

Unaelwa Social Media zinavyo commoditize user info?

Unaelewa kwamba Social Media za "bure" zote, unalipia kwa kuwapa data zako na za network yako?

Kwani ni lazima kuwa na network ya watu wengi?

What's next? Utalaumu watu ambao hawapendi marafiki wengi, kwa sababu ni washamba, hawajui manufaa ya urafiki?

Unataka kuwapangia watu maisha?

Huoni kwamba kutaka kuwapangia maisha watu wasiokujua wala kukujali ndiyo ushamba wenyewe hapa?
Mkuu hili jiwe limelenga penyewe nini
 
Mkuu hili jiwe limelenga penyewe nini
Penyewe wapi?

Mimi hata sina LinkedIn.Sijawahi kuwa nayo na sitakaa kuwa nayo. Na siihitaji.

Na Facebook nina marafiki wawili.

Umaarufu ulinifuata nikaukataa.

Na ndivyo nimeamua hivyo.

Sasa utataka kunipangia niishi unavyotaka wewe?

Wewe watu wasiokujua wakikukatalia kuungana LinkedIn kwa nini unaumia sana?
 
Duh kwa namna hii watu wa nchi yangu yangu wanatia aibu kwenye ishu ya utandawazi
Aibu ni pale unapotaka kulazimisha kila mtu afanye kama unavyotaka wewe.

Unaelewa kwamba kila mtu ana historia tofauti, na unapoona wewe umejua leo, watu wengine wameshapita miaka ya tisini huko?

Watu tumeona Geocities Rings, nini LinkedIn?

Unaelewa Geocities Rings ni nini na zilikuwepo kwenye internet mwaka gani mpaka mwaka gani?

Unaelewa security risks za LinkedIn?

Unaelewa identity theft ni nini?

Unaelewa commoditization of social media data ni nini?

Unaekewa kwamba wewe ukiwa unakaa kwenye matako ya dunia unaweza ku afford data zako kuwa all over the place, lakini kuna watu wako duniani kwenye high security risk na identity theft, na LinkedIn ni source ya information nyingi sana kwa identity thieves?

Unaelewa profiling?

Unaelewa kwamba wewe na mimi hatuishi dunia moja?
 
Aibu ni pale unapotaka kulazimisha kila mtu afanye kama unavyotaka wewe.

Unaelewa kwamba kila mtu ana historia tofauti, na unapoona wewe umejua leo, watu wengine wameshapita miaka ya tisini huko?

Watu tumeona Geocities Rings, nini LinkedIn?

Unaelewa Geocities Rings ni nini na zilikuwepo kwenye internet mwaka gani mpaka mwaka gani?

Unaelewa security risks za LinkedIn?

Unaelewa identity theft ni nini?

Unaelewa commoditization of social media data ni nini?

Unaekewa kwamba wewe ukiwa unakaa kwenye matako ya dunia unaweza ku afford data zako kuwa all over the place, lakini kuna watu wako duniani kwenye high security risk na identity theft, na LinkedIn ni source ya information nyingi sana kwa identity thieves?

Unaelewa profiling?

Unaelewa kwamba wewe na mimi hatuishi dunia moja?
Wabongo bwana kwa porojo hawajambo ili mradi tu aupindishe ukweli.
Kwani ukikubali udhaifu utapungukiwa nini kiranga.
 
Wabongo bwana kwa porojo hawajambo ili mradi tu aupindishe ukweli.
Kwani ukikubali udhaifu utapungukiwa nini kiranga.
Hujajibu hoja. Unaleta viroja.

Udhaifu unao wewe unayetaka kulazimisha watu wakukubali urafiki kwa nguvu.

Yani mtu hakutaki uwe rafiki yake, wewe unataka uwe rafiki yake kwa lazima.

Huoni kwamba huo ni udhaifu?
 
Hakuna mtu nimemlazimisha kuniunga urafiki ila tulikuwa tunapeana mawaidha na kuwafundisha umuhimu wa kuwa na connections nyingi Linkedin.
Wewe ukikataa kuaccept request yangu hujanikomoa maisha yangu yatabaki yaleyale.
Hujajibu hoja. Unaleta viroja.

Udhaifu unao wewe unayetaka kulazimisha watu wakukubali urafiki kwa nguvu.

Yani mtu hakutaki uwe rafiki yake, wewe unataka uwe rafiki yake kwa lazima.

Hioni kwamba huo ni udhaifu?
 
Hakuna mtu nimemlazimisha kuniunga urafiki ila tulikuwa tunapeana mawaidha na kuwafundisha umuhimu wa kuwa na connections nyingi Linkedin.
Wewe ukikataa kuaccept request yangu hujanikomoa maisha yangu yatabaki yaleyale.
Mimi nitakataa vipi request yako wakati LinkedIn sina, sitakuwa nayo na wala siihitaji?

Na unaanzaje kumfundisha mtu kwa attitude ya kwamba ni mshamba, ilhali humjui na hujui sababu zake za kukataa kuwa na network kubwa?

Kwa nini unafikiri kuwa na network kubwa ni muhimu kwa kila mtu?

Unaelewa kuna watu wanajali quality kuliko quantity?
 
Kumbe hizi hoja zote zimekuja baada ya kuambiwa ni washamba?usipaniki hilo ni neno la kawaida tu na mtu yeyote aweza kuwa mshamba mahali fulani.

Kwa mfano mimi ni mtoto wa mjini nimezaliwa dar town ila nikienda kijijini na wao wanaweza kuniona mimi mshamba kwa sababu kuna vitu vyao vya shamba mimi sivijui.
Mimi nitakataa vipi request yako wakati LinkedIn sina, sitakuwa nayo na wala siihitaji?

Na unaanzaje kumfundisha mtu kwa attitude ya kwamba ni mshamba, ilhali humjui na hujui sababu zake za kukataa kuwa na network kubwa?

Kwa nini unafikiri kuwa na network kubwa ni muhimu kwa kila mtu?

Unaelewa kuna watu wanajali quality kuliko quantity?
 
Back
Top Bottom