Watanzania wameendesha makampuni ya usafirishaji abiria nchini lakini Serikali inaamini hawawezi kuendesha kampuni ya Mwendokasi

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
876
4,101
Sikutegemea Mradi wa kubeba abiria Dar es Salaam akabidhiwe kampuni ya kigeni. Usafirishaji ni sekta ambayo Watanzania wanafanya vizuri sana. Nchi nzima mabasi yanamilikiwa watanzania wenzetu. Wanasafirisha abiria bila kelele wala malalamiko tena kwa mabasi mazuri yenye huduma zote.

Kafulila na wenzake walipoambiwa kubinafsisha wakakimbilia kwenda kutafuta wageni kwa kigezo kwamba Watanzania hawana uwezo wa kufanya hizi kazi. Naomba kuuliza kuna mgeni anamiliki dala dala au zinimilikiwa na Watanzania? Kuna kampuni ya mabasi ya wageni au makampuni haya ni ya watanzania?

Watumishi wa umma kama ninyi biashara imewashinda mnaamini kila Mtanzania biashara imemshinda? Leo hii wapo watanzania wanaweza kukopesheka magari huko China wakalipa taratibu sawa na ambavyo huyu Mwarabu anakwenda kufanya.

Kwanini tufikie kukabidhi kila kitu kwa wageni? Tuambieni kuna ugumu gani wa kusimamia mradi wa Mwendokasi hadi tukamtafute RAIA wa kigeni aje kutuongoza? Tuliomba kura za kubinafsisha kwa wageni kila kitu?
 
Sikutegemea Mradi wa kubeba abiria DAR es salaam akabidhiwe kampuni ya kigeni. Usafirishaji ni sekta ambayo Watanzania wanafanya vizuri sana. Nchi nzima mabasi yanamilikiwa watanzania wenzetu. Wanasafirisha abiria bila kelele wala malalamiko tena kwa mabasi mazuri yenye huduma zote.

Kafulila na wenzake walipoambiwa kubinafsisha wakakimbilia kwenda kutafuta wageni kwa kigezo kwamba Watanzania hawana uwezo wakufanya hizi kazi. Naomba kuuliza kuna mgeni anamiliki dala dala au zinimilikiwa na Watanzania ? Kuna kampuni ya mabasi ya wageni au makampuni haya ni ya watanzania ?


Watumishi wa umma kama ninyi biashara imeqashinda mnaamini kila Mtanzania biashara imemshinda? Leo hii wapo watanzania wanaweza kukopesheka magari huko china wakalipa taratibu sawa na ambavyo huyu Mwarabu anakwenda kufanya.

Kwanini tufikie kukabidhi kila kitu kwa wageni? Tuambieni kuna ugumu gani wa kusimamia mradi wa Mwendokasi hadi tukamtafute RAIA wa kigeni aje kutuongoza? Tuliomba kura zakubinafsisha kwa wageni kila kitu?
Uendeshaji wa Mabasi ya mikoani ni tofauti na mabasi ya mjini.
 
Sikutegemea Mradi wa kubeba abiria DAR es salaam akabidhiwe kampuni ya kigeni. Usafirishaji ni sekta ambayo Watanzania wanafanya vizuri sana. Nchi nzima mabasi yanamilikiwa watanzania wenzetu. Wanasafirisha abiria bila kelele wala malalamiko tena kwa mabasi mazuri yenye huduma zote.

Kafulila na wenzake walipoambiwa kubinafsisha wakakimbilia kwenda kutafuta wageni kwa kigezo kwamba Watanzania hawana uwezo wakufanya hizi kazi. Naomba kuuliza kuna mgeni anamiliki dala dala au zinimilikiwa na Watanzania ? Kuna kampuni ya mabasi ya wageni au makampuni haya ni ya watanzania ?


Watumishi wa umma kama ninyi biashara imeqashinda mnaamini kila Mtanzania biashara imemshinda? Leo hii wapo watanzania wanaweza kukopesheka magari huko china wakalipa taratibu sawa na ambavyo huyu Mwarabu anakwenda kufanya.

Kwanini tufikie kukabidhi kila kitu kwa wageni? Tuambieni kuna ugumu gani wa kusimamia mradi wa Mwendokasi hadi tukamtafute RAIA wa kigeni aje kutuongoza? Tuliomba kura zakubinafsisha kwa wageni kila kitu?
Zabuni ya wazi ilitangazwa kwenye vyombo vya habari. Waulize hao wasafirishaji wa ndani kama waliona au hawakuiona kabla hujaanza kulaumu kama vyama vya upinzani.
 
Sikutegemea Mradi wa kubeba abiria DAR es salaam akabidhiwe kampuni ya kigeni. Usafirishaji ni sekta ambayo Watanzania wanafanya vizuri sana. Nchi nzima mabasi yanamilikiwa watanzania wenzetu. Wanasafirisha abiria bila kelele wala malalamiko tena kwa mabasi mazuri yenye huduma zote.

Kafulila na wenzake walipoambiwa kubinafsisha wakakimbilia kwenda kutafuta wageni kwa kigezo kwamba Watanzania hawana uwezo wakufanya hizi kazi. Naomba kuuliza kuna mgeni anamiliki dala dala au zinimilikiwa na Watanzania ? Kuna kampuni ya mabasi ya wageni au makampuni haya ni ya watanzania ?


Watumishi wa umma kama ninyi biashara imeqashinda mnaamini kila Mtanzania biashara imemshinda? Leo hii wapo watanzania wanaweza kukopesheka magari huko china wakalipa taratibu sawa na ambavyo huyu Mwarabu anakwenda kufanya.

Kwanini tufikie kukabidhi kila kitu kwa wageni? Tuambieni kuna ugumu gani wa kusimamia mradi wa Mwendokasi hadi tukamtafute RAIA wa kigeni aje kutuongoza? Tuliomba kura zakubinafsisha kwa wageni kila kitu?
True mbona bm wameweza na huduma za maana kila root
 
Sikutegemea Mradi wa kubeba abiria DAR es salaam akabidhiwe kampuni ya kigeni. Usafirishaji ni sekta ambayo Watanzania wanafanya vizuri sana. Nchi nzima mabasi yanamilikiwa watanzania wenzetu. Wanasafirisha abiria bila kelele wala malalamiko tena kwa mabasi mazuri yenye huduma zote.

Kafulila na wenzake walipoambiwa kubinafsisha wakakimbilia kwenda kutafuta wageni kwa kigezo kwamba Watanzania hawana uwezo wakufanya hizi kazi. Naomba kuuliza kuna mgeni anamiliki dala dala au zinimilikiwa na Watanzania ? Kuna kampuni ya mabasi ya wageni au makampuni haya ni ya watanzania ?


Watumishi wa umma kama ninyi biashara imeqashinda mnaamini kila Mtanzania biashara imemshinda? Leo hii wapo watanzania wanaweza kukopesheka magari huko china wakalipa taratibu sawa na ambavyo huyu Mwarabu anakwenda kufanya.

Kwanini tufikie kukabidhi kila kitu kwa wageni? Tuambieni kuna ugumu gani wa kusimamia mradi wa Mwendokasi hadi tukamtafute RAIA wa kigeni aje kutuongoza? Tuliomba kura zakubinafsisha kwa wageni kila kitu?
Wangepewa hata Allys Star ya Shinyanga ingekuwa poa tu 😅😅🙏🙏
 
Hizo daladala zenyewe nyingi ziko hoi, hazina service za uhakika. Usilinganishe kabisa uendeshaji wa mwendokasi na daladala, one man show vs kampuni yenye mambo mengi ni vitu viwili tofauti.
Kabisa !
 
Hizo daladala zenyewe nyingi ziko hoi, hazina service za uhakika. Usilinganishe kabisa uendeshaji wa mwendokasi na daladala, one man show vs kampuni yenye mambo mengi ni vitu viwili tofauti.
Ulipaswa kuwa mtumwa
 
Sikutegemea Mradi wa kubeba abiria DAR es salaam akabidhiwe kampuni ya kigeni. Usafirishaji ni sekta ambayo Watanzania wanafanya vizuri sana. Nchi nzima mabasi yanamilikiwa watanzania wenzetu. Wanasafirisha abiria bila kelele wala malalamiko tena kwa mabasi mazuri yenye huduma zote.

Kafulila na wenzake walipoambiwa kubinafsisha wakakimbilia kwenda kutafuta wageni kwa kigezo kwamba Watanzania hawana uwezo wakufanya hizi kazi. Naomba kuuliza kuna mgeni anamiliki dala dala au zinimilikiwa na Watanzania ? Kuna kampuni ya mabasi ya wageni au makampuni haya ni ya watanzania ?


Watumishi wa umma kama ninyi biashara imeqashinda mnaamini kila Mtanzania biashara imemshinda? Leo hii wapo watanzania wanaweza kukopesheka magari huko china wakalipa taratibu sawa na ambavyo huyu Mwarabu anakwenda kufanya.

Kwanini tufikie kukabidhi kila kitu kwa wageni? Tuambieni kuna ugumu gani wa kusimamia mradi wa Mwendokasi hadi tukamtafute RAIA wa kigeni aje kutuongoza? Tuliomba kura zakubinafsisha kwa wageni kila kitu?
Huduma ya usafiri wa mabasi ungefaa kuwa tenda ya ndani tu
 
Zabuni ya wazi ilitangazwa kwenye vyombo vya habari. Waulize hao wasafirishaji wa ndani kama waliona au hawakuiona kabla hujaanza kulaumu kama vyama vya upinzani.
Unaelewa kulinda rasilimali za nchi? Kwa hiyo wewe unaamini zabuni kutangazwa kwenye magazeti ndio ushindani? Kwamba waarabu unaamini walishinda zabuni au wametumia connection
 
Ulipaswa kuwa mtumwa
Elewa nilichoandika wacha kukurupuka. Umpe owner wa Top Jesus Group aendeshe mwendokasi, naamini hawezi hata kidogo. One man show sio sawa na kampuni, kampuni zina mambo mengi
 
Mboni wapo wanaoendesha biashara ya daladala miaka na miaka na biashara zao hazijafa, sema mambo ya umma huko wiziwizi kuiba nje nje na wakiiba hawafanywi kitu

Kama wapo mbona hamjawatumia miaka yote kuiendesha uda na brt mpaka zimekufa kifo cha mende?

Mlikuwa mmelala?
 
Kama wapo mbona hamjawatumia miaka yote kuiendesha uda na brt mpaka zimekufa kifo cha mende?

Mlikuwa mmelala?
Wewe unaelewa ninachokuambia Mali ya Umma unaelewa namaanisha nini? Shamba la Bibi kila mtu anajichotea tu na hafanywi kitu
 
Kwa nauli za mwendokasi, kampuni ya usafirishaji mikoani ikijiendesha Kwa namna hiyo inakufa hapo hapo. Basi la zaidi ya milioni 500 linajiendesha Kwa nauli ya 1000 unadhani Kuna mmiliki hajui hiyo hasara?
 
Back
Top Bottom