Watanzania tuna la kujifunza kutokana na matatizo tuliyopata, somo la kwanza ni kulaaniwa na Sheria kwa kuidharau na kujichukulia maamuzi wenyewe

Watanzania tuna la kujifunza kutokana na matatizo tuliyopata, somo la kwanza ni kulaaniwa na Sheria kwa kuidharau na kujichukulia maamuzi wenyewe

Pakome

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2024
Posts
1,541
Reaction score
916
Watanzania tuna la kujifunza kutokana na matatizo tuliyopata, somo la kwanza ni kulaaniwa na Sheria kwa kuidharau na kujichukulia maamuzi

Matatizo tuliyokuwa nayo Serikali pamoja na Wananchi tungeyatatua kwa kufuata Sheria za nchi pamoja na za Kimataifa na kuheshimu uwepo wa Mahakama duniani lakini badala yake tulijichukulia Sheria mkononi na kuunda vurugu zilizokuwa na laana ya Sheria ndani yake

Yaani kwamba Sheria ilitulaani ikidai tumeidharau badala ya kufuata suluhu Mahakamani tukaamua kuumizana

Hatakama Serikali pamoja na Wananchi tulikuwa na makosa tungepelekana Mahakamani na sio kuraruana kama simba kwasababu Simba hajui namna nyingine ya kujitetea zaidi ya kurarua adui
 
Mbona unahaha sana gen z si mchezo aisee🤣🤣🤣🤣🤣
 
Kwa aina ya watawala tulionao awamu ya sita ni ngumu sana kupata haki Kwa kutegemea mahakama.Lugha nzuri ambayo CCM wataielewa ni maandamano ambayo yanaambatana na kuchomwa Mali za viongozi kama vile nyumba,vituo vyao vya mafuta,magari Yao maana tunarudisha Kodi zetu walizotukamua
 
Kwa aina ya watawala tulionao awamu ya sita ni ngumu sana kupata haki Kwa kutegemea mahakama.Lugha nzuri ambayo CCM wataielewa ni maandamano ambayo yanaambatana na kuchomwa Mali za viongozi kama vile nyumba,vituo vyao vya mafuta,magari Yao maana tunarudisha Kodi zetu walizotukamua
Ila kuna Sheria za Kimataifa pia sidhani kama hazina nguvu kama madai yetu ni kuwa Sheria za ndani zinachelewa
 
Mimi ni Mwanasheria sitizami upande mmoja, Serikali na Wanachi sote kwa pamoja tulikosea hatukuwa sahihi
Sawa sawa, yaliyotokea Zanzibar ndio yaliotokea Bara, Tena Zanzibar ni mbaya zaidi maana wakala walikuwa wanafukuzwa vituoni kuliko na kutishiwa usalama, Ila watu hawakufanya Fuji, walitaka ila kongozi wao aliwambia watulie tutakwenda na Sherita zilizozidi hizi sheria za hapa nchini.
Kiongozi ni aliyekuwa mwanasheria wa serikali Ila CCM walimfukuza ndio akawa wa upinzani.
 
Kweli mkuu. Nachukia sana watoto wa kimaskin tunatumika na wapuuzi wachache kwa selfish Interests zao ..
 
Mahakama zenyewe zimelaaniwa. Zinafuata maagizo ya waliolaaniwa badala ya kufuata sheria.
 
Mahakama zenyewe zimelaaniwa. Zinafuata maagizo ya waliolaaniwa badala ya kufuata sheria.
Lakini kumbuka kuna za Kimataifa katika Sheria ya Kimataifa hata kama za ndani zimeshindwa
 
Kweli mkuu. Nachukia sana watoto wa kimaskin tunatumika na wapuuzi wachache kwa selfish Interests zao ..
Hawa vijana wameshindwa kumbana aje ili na yeye aonje joto kama yeye anajificha anaogopa nini mbona wao hawaogopi
 
Lakini kumbuka kuna za Kimataifa katika Sheria ya Kimataifa hata kama za ndani zimeshindwa
Maandamano ni kinyume cha sheria?

Kuua wezi / waharibifu wakati wa maandamano imeruhusiwa kwenye sheria gani?

Kuua watu waliojikalia ndani kwao au nje mtaani kwao imeruhusiwa kwenye sheria gani?
 
Mimi ni Mwanasheria sitizami upande mmoja, Serikali na Wanachi sote kwa pamoja tulikosea hatukuwa sahihi
Kumbe ni mwansheria. Nilidhani wewe ni jaji. Kuwa mwanasheria hakuwezi kuweka haki kwa mambo yanayoendelea sasa.
 
Kumbe ni mwansheria. Nilidhani wewe ni jaji. Kuwa mwanasheria hakuwezi kuweka haki kwa mambo yanayoendelea sasa.
Kwa haya yaliyotokea, Wananchi pamoja na Serikali sote tuna makosa
 
Back
Top Bottom