Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

Na ndio maana midahalo nyakati za uchaguzi ni ya muhimu sana. Pamoja na kuwa mgombea anasimama kupitis chama flani na sera za chama, ni muhimu kuutambua uwezo binafsi wa mgombea. Chama kinaweza kuwa na sera nzuri lakini msimamizi wa sera ambae ni raisi asipokuwa na weledi na umadhubuti wa kusimamia na kutimiza sera basi inaangusha nchi.

Ni muhimu kupima uwezo binafsi wa individuals na kwa kuanzia, midahalo itakuwa ya muhimu sana kupembua chuya na mchele.
 
Takukuru haina uwezo wa kuzuia wala kukemea rushwa .. Ni taasisi ambayo ipo tu

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums

Umemsoma Hosea humu leo kafanya nini na anasema anafanya nini?
 
Kwani hao waliouwa mwangosi,mvungi,mbwambo,ally zona na wengineo leo wapo hapa jf? TUNAHITAJI KUBADILI MFUMO FISADI NA SI KUBADILI MAJINA YA WATU. TUNATAKA CHAMA KITAKACHOTULETEA KATIBA MPYA YA WATZ BAADA YA CCM KUCHAKACHUA MAONI YETU NA KUWEKA YAO YA KIFISADI ILI WAENDELEE KULIIBIA NA KULIHUJUMU TAIFA KWA FAIDA YAO BINAFSI.

Mbona chacha wangwe na Nyerere umewasahau?
 
mmeona UKAWA wananguvu ndo mnaanza kubadili kauli tulizoea ile inayosema angalia chama mafiga matatu leo imekuwaje uwe wazi
 
Ingawa naona upo shallow sana kwa kutonielewa juu ya kukuelewesha kote huko, ngoja nitumie njia nyingine ya kukuelewesha;

Umeshawahi kuwa na wadhifa upi kwenye chama chako?
haa haa nadhani wewe uko shallow katika kueleweka, hueleweki, unajing'atang'ata tu! Narudia tena nani hao unaowaita wenye chama? Acha blah blah!
 
Hujamfahamu huyo dada kwa uislam, huwa hana agenda nyingine, ameona chama chake hakina mgombea muislam mwenye mvuto, sasa anajifanya yeye hajali chama. Akiwekewa Lipumba na UKAWA huyu atamchagua. Yeye akili yake imeegemea dini tu.
kiujumla hilo ni kweli, nimemfuatilia sana, yeye anashabikia ccm kwa kuwa rais ni kikwete, akiondoka naye anatimua
 
Hiyo ni mifano miwili tu niliyokuwekea ili kudhihirisha hoja yangu lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, Tanzania hakichaguliwi chama anachaguliwa kiongozi. Hata huko UKAWA mtachaguwa chama? au kiongozi? UKAWA si chama. Fikiri.

Katika kufikiri ninaona Chama kinabadili mikakati kutuaminisha ati Chama si kitu bali mtu. Sio wewe miongoni mwa waliosapoti misimamo ya chama Siku zote? Imekuwaje Leo?
 
Katika kufikiri ninaona Chama kinabadili mikakati kutuaminisha ati Chama si kitu bali mtu. Sio wewe miongoni mwa waliosapoti misimamo ya chama Siku zote? Imekuwaje Leo?

Mpaka sasa hivi nakisapoti chama. Chama sera zake husimamiwa na nani? Fikiri.
 
kiujumla hilo ni kweli, nimemfuatilia sana, yeye anashabikia ccm kwa kuwa rais ni kikwete, akiondoka naye anatimua

Nimekuwa mwana CCM toka siku kilipoanzishwa. Kabla ya hapo nilikuwa TANU.

Sikubaliani na wazo la kila mwanachama bali naheshimu utaratibu na maana ya chama.

Sikukubaliana kabisa na sera na uongozi wa Nyerere lakini haikunifanya niache chama, nilijuwa kuwa yupo wrong na kuna siku atajuwa hilo, na kweli alijuwa hilo na akakiri, kuwa yeye siyo malaika na kuna makosa aliyafanya tuyaache.
 
haa haa nadhani wewe uko shallow katika kueleweka, hueleweki, unajing'atang'ata tu! Narudia tena nani hao unaowaita wenye chama? Acha blah blah!

Wenye chama ni wanachama waliolewa madaraka.
 
Nimekuwa mwana CCM toka siku kilipoanzishwa. Kabla ya hapo nilikuwa TANU.

Sikubaliani na wazo la kila mwanachama bali naheshimu utaratibu na maana ya chama.

Sikukubaliana kabisa na sera na uongozi wa Nyerere lakini haikunifanya niache chama, nilijuwa kuwa yupo wrong na kuna siku atajuwa hilo, na kweli alijuwa hilo na akakiri, kuwa yeye siyo malaika na kuna makosa aliyafanya tuyaache.

Kama ulikua tangu enzi za tanu....siku zako zinahesabika....anza kutubu vua gamba....uwe msafi na umkubali Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha....ukiri utatu mtakatifu.....as well.....unakaribia kufa trust me
 
Katika kufikiri ninaona Chama kinabadili mikakati kutuaminisha ati Chama si kitu bali mtu. Sio wewe miongoni mwa waliosapoti misimamo ya chama Siku zote? Imekuwaje Leo?

Kufikiri kwako ni makosa. Watu hujinadi kwa kuelezea watafanya kuhakikisha sera za chama wanazitekeleza, isitoshe, hata hizo sera zinatungwa na watu. Ni hao watu ndiyo nnasema mimi, tusiburuzwe tukawaweka wasiofaa.

Chama bora ni cha wenye viongozi bora na si bora viongozi.
 
Kama ulikua tangu enzi za tanu....siku zako zinahesabika....anza kutubu vua gamba....uwe msafi na umkubali Yesu kuwa Bwana na mwokozi wa maisha....ukiri utatu mtakatifu.....as well.....unakaribia kufa trust me

Hakuna ajuwae ataondoka lini, wacha kukufuru. Wanaondoka waliozaliwa leo na yote ni shani yake Allah.
 
Kufikiri kwako ni makosa. Watu hujinadi kwa kuelezea watafanya kuhakikisha sera za chama wanazitekeleza, isitoshe, hata hizo sera zinatungwa na watu. Ni hao watu ndiyo nnasema mimi, tusiburuzwe tukawaweka wasiofaa.

Chama bora ni cha wenye viongozi bora na si bora viongozi.

Apo mwisho ungemalizia.....kama sisiemu
 
Back
Top Bottom