Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

Watanzania, Msichaguwe Chama Chagueni Kiongozi

kama tukifuata mtu badala ya chama ccm kuna mtu gan mwenye sifa ya kuchaguliwa ? maana wote wameshindwa kutatua matatizo ya watanzania sasa ni zamu ya wapinzani

Hakuna kura ya chama kuna kura za watu. Na wewe unatakiwa uwe huru kumchaguwa unaeona anafaa. Usilazimike kuchaguwa mgombea anaewekwa na wenye vyama hata kama unamuona hafai. Utakuwa hukuitendea haki nafsi yako.
 
  • Thanks
Reactions: jme
Tatizo ao viongozi awajamini kwenye izo kura za maoni kila mgombea ana makundi yke na hela za kununulia kura
 
Ndiyo inabidi wananchi tusiburuzwe na wenye vyama. Tusikubali kuchaguliwa kiongozi na chama, tuliweza kwa Kikwete, tuliweza kwa Shibuda, kwanini tushindwe sasa?
Toa mifano harisi wa vitu au kitu kinachoweza fanywa na wananchi,maana watawala wao wanatenda kabisa rafu za wazi na polisi wanawalinda bila aibu.
 
Huyu ndie anaitwa FaizaFoxy mwanamke anayeipenda ccm pamoja na katiba iliyopendekezwa na wahununi wenye malengo machafu na nchi yetu.

mwana mama huyu baada yakuona mahakama yake ya kiislam(mahakama ya kadhi) ccm hawataki kuyatekeleza, sasa naona amepata akili nakuona ukawa ndio mkombozi wake.

taratibu lile jinamizi la ccm limeanza kumtoka.

hongera sana, leo umekuja na mada zuri sana, lakn kaa ukielewa kwamba mgombea tutakayempendekeza wanainchi ni dr.slaa ukate ukumbali ukweli ndio huo.

Uwanja ni wako na una haki ya kubwabwaja na kuhororoja upendavyo.

Slaa alibwagwa na Kikwete na kwa maadili mabovu aliyonayo huyo atakuwa ni chaguo lako lakini nnauhakaika hatokuwa chaguo la Watanzania wengi wanaopenda maadili mema.

Mimi sitomchaguwa Slaa hata akibaki kuwa ni mgombea pekee.
 
Hilo ndiyo wazo duni, usichaguwe vyama chaguwa kiongozi.
lakini kumbuka mwaka 2010 ccm mliikataa ni sera ya chagua mtu mkasema ccm ndo inaleta amani hivyo chagueni ccm wapinzani wanaleta vita sasa mwaka huu mtaweza kweli?
 
Wakati tunaingia kwenye mwaka wa heka heka za uchaguzi wa Wabunge na wa Rais.

Nawaasa Watanzania wasichaguwe chama bali wachaguwe kiongozi.

Mfano mzuri ni kama tuliouonesha mwaka 2005, wakati tulipomchaguwa Kikwete kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii. Ushindi alioupata Kikwete wa zaidi ya kura 80% ni dhahiri ulikuwa si kwa kuchaguliwa na wana CCM bali hata wa upinzani na wasio na vyama.

Mfano mwingine ni wa John Shibuda, pale alipoihama CCM na kuhamia Chadema, wana CCM wa jimbo lake wengi walimpa kura zao bila kujali yupo chama kipi. Huo ni uzalendo na unaonesha jinsi Tanzania tunavyoweza kufanya maamuzi bila ya kuburuzwa na chama au wenye chama.

Viongozi wazuri tunao, tena tusingoje wale wanaojitokeza tu kuzitaka hizi nyadhifa kwa udi na uvumba. Tutazame katika jamii, tunapomuona anaefaa kuongoza, hata kama si mwanasiasa, bali tukimuona kuwa haa huyu anafaa kuongoza, tumlazimishe, tumsimamishe, tumchaguwe.

Tukianza kuchaguwa viongozi na si chama tutakuwa sisi wenyewe tumeshakuwa viongozi.Tuanze kwa kujiongoza wenyewe kwa kuchaguwa tukitakacho na si kuburuzwa na wakitakacho wenye vyama.

Tukianza hivyo, hata vyama vyetu vitaweka viongozi tuwatakao na si wawatakao wenye vyama.

Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.

Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, ili tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.

Tayari mshaanza kuweweseka, mwanzoni mlikuwa mnasema chagua ccm, leo mmeona ccm imeoza mbele ya macho ya watanzania mnabadili wimbo eti oo chagua mtu msichague chama.Hapo bado mtayasema mengi kwani mchuma majanga ula na wenzake.
 
sawa tutachagua mtu na sio chama ila huyo mtu hawezi kutoka ccm
 
TAKUKURU wapo na kila mwaka wanazidi kupata uzoefu na sisi wenyewe inabidi tuwe macho. Tunapoona kuna kutoa na kupokea rushwa tusifumbe macho.

TAKUKURU wapo lakini hawana meno.
Wanaishia kukamata manesi kwa rushwa ndogo ndogo za Tshs. 5,000. Chukulia mfano mdogo tu wa wale 'wasimama barabarani' wenye nguo nyeupe ambao rushwa zao ziko nje nje.
 
  • Thanks
Reactions: 999
Kama unanisoma humu JF ungejuwa kuwa kama ningekuwa mhafidhina basi kwanza ningekuwa namsifia Nyerere na hata nisingeyaona makosa yake. Fikiri.

Tundu Lissu kwa kutokuwa mhafidhina na kwa kuweza kuyaona na kuyasema wazi makosa ya Nyerere namkubali, lakini ananikera pale anapoiga sauti za wachungaji wa Jangwani anapowasilisha hoja zake.
Jiandae kukereka kwa kipindi kirefu kijacho. Huyu ndiye rais wako kuanzia Novemba mwaka huu.
 
Toa mifano harisi wa vitu au kitu kinachoweza fanywa na wananchi,maana watawala wao wanatenda kabisa rafu za wazi na polisi wanawalinda bila aibu.

Hiyo kwa Waswahili wa pwani hujulikana pia kama bokoboko.

Kuwa makini unapoandika, unabadilisha maana ya maneno hata sielewi nikujibu nini. Sasa harisi aka bokoboko lina uhusiano upi na hii mada?
 
Haya ndiyo maazimio ya cc - ccm Zanzibar. Baada ya ccm kujua wamechafuka na chama chao hakikubaliki tena, waliazamia kupiga kampeni za kuchagua mtu ili watu wasiangalie maovu ya ccm!. Ff hii inajulikana.
a
Mara zote Kikwete amekuwa msaliti wa umma kwa kufuata maazimio ya chama chake. Mfano sahihi ni BMK. Amebariki mchakato na amepokea draft ya Warioba, ameikubali na akaenda mbele zaidi na ku isaini. Ccm walipoikataa kwamba haina maslahi kwao, wakapanga na namna ya kuivuruga, na bahati nzuri kwake wakamtask kuvuruga, AKAVURUGA KWA UTASHI WA CHAMA.

Amekaa na watetezi wa katiba ya wananchi, wamepatana mchakto wa katiba usitishwe, lakini ccm wakamgomea, wakaendeleza hadi hapo wlaipo sasa. Na yeye kama mwanaccm mwaminifu, ameshindwa kusimamia maazimio yale aas if hayakuwepo, na sasa anatekeleza matwaka ya ccm.

Hatutachagua mtu bila kuangalia chama chake kwa sababu chama ndicho kitakachomwongoza na kumpa dira katika uongozi wake wote!.

Acheni kudanganya watu Faizafoxy. Huyu mtu hataunda serikali nje ya chama chake, hatekelezi sera zake nje ya chama chake, hatengenezi mfumo nje ya misingi ya chama chake, hatekelezi ilani nje ya zile za chama chake. Iweje leo mseme tuchague mtu bila kuangalia chama? Hii ni nini?

Vinginevyo atangaze yeye ni mgombea binafsi hana chama, tutamwangalia kwa namna ile lakini tutahitaji kujua anaunda serikali kwa utaratibu upi iwapo anashinda.

Hii kampeni ninaona ni kutaka kuficha makovu ya ccm kwa sababu haitakiwi, halfu tujikute tumewapa uongozi waendelee kutunyonyoa wakavu wakavu!.

Aidha mtu ana chama tutamwangalia na chama chake, ama awe binafsi bila chama tutamtathimni muundo wake pendekezwa wa serikali yake ukoja.

Kuchanganyachanganya mambo hapa ni hila na hatukubali




Wakati tunaingia kwenye mwaka wa heka heka za uchaguzi wa Wabunge na wa Rais.

Nawaasa Watanzania wasichaguwe chama bali wachaguwe kiongozi.

Mfano mzuri ni kama tuliouonesha mwaka 2005, wakati tulipomchaguwa Kikwete kuwa kiongozi mkuu wa nchi hii. Ushindi alioupata Kikwete wa zaidi ya kura 80% ni dhahiri ulikuwa si kwa kuchaguliwa na wana CCM bali hata wa upinzani na wasio na vyama.

Mfano mwingine ni wa John Shibuda, pale alipoihama CCM na kuhamia Chadema, wana CCM wa jimbo lake wengi walimpa kura zao bila kujali yupo chama kipi. Huo ni uzalendo na unaonesha jinsi Tanzania tunavyoweza kufanya maamuzi bila ya kuburuzwa na chama au wenye chama.

Viongozi wazuri tunao, tena tusingoje wale wanaojitokeza tu kuzitaka hizi nyadhifa kwa udi na uvumba. Tutazame katika jamii, tunapomuona anaefaa kuongoza, hata kama si mwanasiasa, bali tukimuona kuwa haa huyu anafaa kuongoza, tumlazimishe, tumsimamishe, tumchaguwe.

Tukianza kuchaguwa viongozi na si chama tutakuwa sisi wenyewe tumeshakuwa viongozi.Tuanze kwa kujiongoza wenyewe kwa kuchaguwa tukitakacho na si kuburuzwa na wakitakacho wenye vyama.

Tukianza hivyo, hata vyama vyetu vitaweka viongozi tuwatakao na si wawatakao wenye vyama.

Nasema haya kwa kuwa nimeona katika vyama vyetu vya siasa vyote, kuna tabia ya kura za maoni. Wananchi wanaweza kuwa na mgombea wao wakampendekeza agombee lakini ikifika kwenye vyama wanakatwa na kuwekwa wale wawatakao wenye vyama. Hii si demokrasia tuitakayo na huleta uvunjifu wa amani.

Ni wakati muafaka sasa Watanzania tusikubali kuchaguwa wamtakae wenye vyama, tunataka tuwe na viongozi tuwatakao wananchi tulio wengi. Tunataka na wagombea huru, wasio na vyama pia wawepo, ili tuwachaguwe tuwaonao wanatufaa na si wanaowafaa wenye vyama.
 
Kama unanisoma humu JF ungejuwa kuwa kama ningekuwa mhafidhina basi kwanza ningekuwa namsifia Nyerere na hata nisingeyaona makosa yake. Fikiri.

Tundu Lissu kwa kutokuwa mhafidhina na kwa kuweza kuyaona na kuyasema wazi makosa ya Nyerere namkubali, lakini ananikera pale anapoiga sauti za wachungaji wa Jangwani anapowasilisha hoja zake.

..Uhafidhina si kumsifia Nyerere tu,ni kutobadilika katika msimamo wako juu ya jambo fulani..Ushabiki wako kwa ''chama cha magamba'' unaonekana dhahiri shahiri,hususani kwa Kikwete,ni lipi baya afanyalo,bila kupepesa macho ukalikemea?
Je kwa kauli hii hapo chini hujatanabaisha ubaya wa upinzani kwa ujumla wao kana kwamba hakuna mwenye unafuu,ilhali ukamithilisha chama chako na tindikali aina ya "Dihdydrogen Monoxide"

Upinzani ni kama mtu asiyejuwa kuogolea, ni lazima ayaogope maji hata ya swimming pool na lazima awatishe wenzake kuwa hiyo ni "dihydrogen monoxide"(uki''refer'' CCM) lakini akijifunza kuogelea na kuwa mtaalam, utamuona mwenyewe akiitafuta "dihydrogen monoxide" na kuisifia(KWA LIPI HASA?), msome aliyejuwa kuogelea kabla yako:

Ndio maana nikasema nafarijika kuona ukibadili msimamo wako juu ya uchaguzi wa mtu kama kiongozi na si Chama.
 
nafarijika umelegeza msimamo..si mhafidhina tena...

Kaka huyo hana lolote la maana ameamua kuwa hivyo baada ya kuona ccm haiuziki mbele ya macho ya watanzania
 
  • Thanks
Reactions: 999
TAKUKURU wapo lakini hawana meno.
Wanaishia kukamata manesi kwa rushwa ndogo ndogo za Tshs. 5,000. Chukulia mfano mdogo tu wa wale 'wasimama barabarani' wenye nguo nyeupe ambao rushwa zao ziko nje nje.

Tatizo kubwa nilionalo la rushwa ni uhafifu wa adhabu tutowazo. Ni wakati muafaka tuchaguwe viongozi watakaokwenda bungeni na kubadili hizo sheria za hukumu za rushwa.

Napendekeza hukumu ya adhabu ya rushwa iwe ni kifo kwa rushwa kubwa au ndogo kwa anaetoa na anaepokea.

Tuone zikiwekwa adhabu namna hiyo kama rushwa haijawa historia.
 
Kaka huyo hana lolote la maana ameamua kuwa hivyo baada ya kuona ccm haiuziki mbele ya macho ya watanzania

CCM kinabaki kuwa chama bora Tanzania mpaka hii leo, lakini kumbuka, Tanzania huwa hatuchaguwi vyama tunachaguwa viongozi na ukinisoma vizuri kwenye post namba moja nimeweka mifano hai.
 
..Uhafidhina si kumsifia Nyerere tu,ni kutobadilika katika msimamo wako juu ya jambo fulani..Ushabiki wako kwa ''chama cha magamba'' unaonekana dhahiri shahiri,hususani kwa Kikwete,ni lipi baya afanyalo,bila kupepesa macho ukalikemea?
Je kwa kauli hii hapo chini hujatanabaisha ubaya wa upinzani kwa ujumla wao kana kwamba hakuna mwenye unafuu,ilhali ukamithilisha chama chako na tindikali aina ya "Dihdydrogen Monoxide"



Ndio maana nikasema nafarijika kuona ukibadili msimamo wako juu ya uchaguzi wa mtu kama kiongozi na si Chama.

Kikwete ni Rais bora zaidi ya yeyote tuliyewahi kumpata Tanzania hii. Hilo hata wewe ukilipima kwa vigezo vya Marais wa kabla yake utalikubali ukipenda usipende.

Naamini kuwa chama bora Tanzania hii hadi hii leo ni CCM.

Narudia, Tanzania hii hatuchaguwi vyama tunachaguwa kiongozi na tusibweteke tuoneshe mfano mwema kama tulivyouonesha mwaka 2005 tulipomchaguwa Kikwete bila kujali itikadi zetu za vyama.
 
Umenena vema mama

Mimi ni muumini mzuri wa mgombea binafsi, hawa vyama wanatuyumbisha tu!
 
Kaka huyo hana lolote la maana ameamua kuwa hivyo baada ya kuona ccm haiuziki mbele ya macho ya watanzania

..kuna msemo vijana wa uswahili wanapenda kuutumia..''wamebana wameachia''
napata na ''tashwishi'' kilichompelekea hasa kuwa na msimamo huu kwa sasa..Je suala ya kadhi limemvunja moyo juu ya matumaini aliyokuwa nayo kwa chama chake?..Nipo kwenye kizungumkuti...
 
Back
Top Bottom