Lugha na uwezo wa kuwasiliana kwa ufasaha ni muhimu sana. Ndio njia pekee uwezo na ujuzi alionao mtu unaweza kudhihirika, kusambazwa na kutunzwa kwa ajili ya Watu wengine.
Lazima Utumie lugha kwa usahihi. Na sio kiingereza tu.. shida yetu leo hata kiswahili hatujui. Tunaandika mambo kama tuna mtindio wa ubongo.. funny enough hata Radio presenters (who once were the pinnacle for excellence) Kiswahili chao ni utumbo wa kiwango cha Lami ya Kibaha!
Hatuna tena namna sahihi ya kuucondition Umma maana kinacholetwa kwao kwa sasa ni majanga matupu, iwe Filamu, Makala, Hadithi, Hotuba, Nyimbo, Mashairi, Tenzi, Nk hakuna kinachoandikwa kwa weledi.. na kinachozingatia matumizi sahihi ya lugha kinaitwa "boring".
Matokeo yake kila kitu kwa sasa kinawalenga Watu wenye kiwango kikubwa cha ujinga. 🙂