Wasifu wa Elimu wa Dr. Mary Mwanjelwa

You are very right MTM kwani hii inaondoa kabisa motisha kwa watu kusoma kwa kuelimika na kuleta maendeleo badala yake watu wanashindana kwa vyeti na majina ambayo haya reflect uhalisia wa elimu. Inasababisha watu kupenda kupanda haraka haraka kwenye ecademics hata kama hakuna merits. Hii hali ni kila mhali hadi vyuo vikuu inasikitisha sana baadhi ya wanaojiita profesors ukiangalia walivyo ufikia utatamani kulia no wonder hakuna maendeleo bali malumbano tu yasiyoisha.

Kuna uhaba mkubwa wa specialists kwenye idaraza na faculties za vyuo vikuu vyetu na hakuna vetting kabisa watu wengi wamesomea fani zinazofanana ambazo ni rahisi kupata zile ngumu hakuna anayeenda kusomea..Inashangaza hata madaktari wameanza kuchakachua elimu zao utaona wanaenda kusoma vitu ambavyo havi add value kwenye taaluma zao (Japo wao si sana lakini mwanzo wa ngoma ni lele). Tujiangalie sana tunakoenda tutabakia kuwa watumwa tu simply hatuna think tank na baadaye ikijadhihirika basi ndiyo hivyo tutaanza kualika expatriates from abroad.

Lakini pia tukumbuke elimu imerahisishwa sana na ukuaji wa technology so siyo lazima wote wanaosoma kwa muda mfupi na kwa ditance learning ni vihiyo bali hii trend ya politicianas na technochrats kutokuwa honest kwenye academic ikizoeleka baadaye ita develop kuwa culture so ni bora kuwe na adhabu kali kwa watakao onekana kukosa maadili ili kujenga socila capital.

Thanks Mkuu....

Kinachosikitisha zaidi ni kwamba hao national guardians ndio wanaoongoza mbio za uongo na kujibandika kila uwezo hapa duniani... siku hizi profesa vulata, profesa tibaijuka, profesa JK na hata profesa mwanjelwa vinawekwa kwenye pot moja tu.

it has become a nation bora liende
 
Kwani umri wake ukoje? Mbona anaonekana kama kijana lakini Elimu ya msingi mwaka alio anza hauendani na sura yake kabisa angalieni usikute kafoji hata mwaka wa kuanza shule ya msingi.
 
kwa elimu ya kidato cha sita ameshika nafasi hizi

Placer Dome Tanzania (Gold Mine)------->Manager - Liason & Corporate 2001 - 2005
Two Wings Pegasus Ltd - Tanzania-------->Manager 2000 - 2001
(PSRC) --------------------------------------> Assistant Information Officer 1999 - 2000
Agakhan Foundation------------------------->Administration Officer 1998 - 1998


baada ya kupata advanced diploma

PSI Tanzania ----->Director 2006 -2010

Hii nguvu sijui ameitoa wapi! who is behind her???


Kuna Habari ndugu yangu mmoja aliwahi kunijuza baada tu ya huyu mwanadada kuingia bungeni kuwa anaye mtoto ambaye baba yake mheshimiwa hivyo anayo nguvu kubwa halafu usijaribu kumchezea huyu.
 
Kwani umri wake ukoje? Mbona anaonekana kama kijana lakini Elimu ya msingi mwaka alio anza hauendani na sura yake kabisa angalieni usikute kafoji hata mwaka wa kuanza shule ya msingi.
Mkuu, Huyu dada ni mtu mzima kidogo,sema ana baby face....hayo ya elimu mimi hayanihusu. What i want from her ni achape kazi
na aachane na blaah blaah zisizokuwa na msingi kama baadhi ya wabunge wenzake ndani ya ccm
 
Huyu nashauri tumtafute kule dodoma aweke mambo yake sawa. Watanzania tusiwe watu wa kudanganywa danganywa hivi hivi. Hivi waandishi wa habari pale Dom jnne mnawaeza kushindwa kupata jibi?
 
MBONA HATA MAJIMAREFU NI DR!! :thinking:
Tunachotaka na huyu atiambie ukwei kama naye ni Dr. (mtaalam wa miti shamba) au lah, Huoni hapa amezusha tafrani??? Mana ukimcheck uson kafanania na Dr. wa miti shamba/wa kienyeji. Ukija kwenye makablasha unakuta ni Dr. wa kizungu. Hili limekaaje??
 
Afu haka kamtindomtindo haka ka watu kupenda kuveshwa elimu wasiokuwa nazo lazma kuna siku tu moto utawaka. Wakati wenzao wanasoma hawa walikuwa wanatumbua starehe, leo wenzao wametoboa na wao wanataka waonekane wasomi. Si msome MEMKWA kama mnapenda usomi!!????Mbona walimu kibao wanafundisha mitaani???Wabunge wetu wengi tukiwauliza katika shule walizosoma watutajie majina ya classmates zao watano watano tu, naimani kutakuwa na sintofahamu nyingi sana.

Kama vile waajiri wetu/vyuo vyetu vinavyohakiki uhalali wa watumishi wapya/wadahiliwa wapya, nashauri hata wabunge kama waajiriwa na wao pia vyeti vyao vikaguliwe. Muajiri wa watu hawa asijifanye hajui kama zoezi hilo ni muhimu kwa kubaini watu wanaoungaunga mambo. Zoezi hili lingefanyika mara moja au mbili na wanaobainika wakatiwa ndani, katabia haka kangeisha. Unakuta mtu toka utotoni na shuleni anatumia jina flani, from no where leo mbunge unashangaa anatumia jina lingine tofauti, ukiuliza ili kupata ufafanuzi hupati hata sentensi moja iliyonyooka. Huu ujanjaujanja hautatutoa hapa tulipo. Wabunge nao vyetu vyao vikaguliwe kama sisi wengine tunavyofanyiwa tukiitwa kujiunga na chuo au tukipata ajira.
 
Kweli NN yuko right miafrika bana ndivyo tulivyo..sasa hayo majina yanasaidia nini? Ila sishangai, una sura nzuri kidogo na Ma Dr Dr kwenye cv ukienda kwa bosi wa kiswahili unategemea nini.......
 
Mshikachuma save your breath bro,Mary mpiganaji wa nini ndugu yangu?kama ni kupata nafasi kusikokuwa na majibu sawa lakini si kingine,she is just an opportunist huo u director wa PSI kwa nini haja specisfy wa nini kwa sababu PSI kuna directorate nyingi ikiwemo ED ambayo hakuwa nayo na wala asingeweza ipata.Kwa nini hajasema chuo gani kilimpa heshima ya U Dr?
 
kwa elimu ya kidato cha sita ameshika nafasi hizi

Placer Dome Tanzania (Gold Mine)------->Manager - Liason & Corporate 2001 - 2005
Two Wings Pegasus Ltd - Tanzania-------->Manager 2000 - 2001
(PSRC) --------------------------------------> Assistant Information Officer 1999 - 2000
Agakhan Foundation------------------------->Administration Officer 1998 - 1998


baada ya kupata advanced diploma

PSI Tanzania ----->Director 2006 -2010

Hii nguvu sijui ameitoa wapi! who is behind her???

Teh teh teh.
Narubongo, unashangaa mwenye stashahada kuukwaa ukurugenzi? Tanzania is more than what me and you are aware of!
Pale Baraza la Kiswahili la Taifa kuna mtu ana elimu ya kidato cha sita na anang,ang'ania kushikilia kitengo ilhali kuna watu wenye shahada zao wanasota. Nimtaje?
 

Teh teh teh.
Narubongo, unashangaa mwenye stashahada kuukwaa ukurugenzi? Tanzania is more than what me and you are aware of!
Pale Baraza la Kiswahili la Taifa kuna mtu ana elimu ya kidato cha sita na anang,ang'ania kushikilia kitengo ilhali kuna watu wenye shahada zao wanasota. Nimtaje?

Mtaje haraka sana
 
Vitu vya utata kwa CCM siyo issue, mengi ya utata yanapita mikononi mwa serikali hii: Utata wa rushwa kwa Siyoi ulipita, utata wa elimu kwa baadhi ya mawaziri wake nao ulipita, utata wa kuzaliwa kwa yule aliyekuwa Mwenyekiti wa UVCCM nao ulipita, utata wa Richmond/Dowans, utata wa issue ya Mwakyembe, na TATAS nyingi tu!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Sasa wewe umeleta wasifu wa huyu muh.ili tufanyaje? Wananchi hatujali elimu ya mtu wala wasifu wake....tunachojali ni utendaji wake wa kazi tu basi. Maana kama ni elimu viongozi wa serikali ya ccm wamesoma hadi mwisho wa dunia'lakini hakuna chochote wanachoki
fanya zaidi ya kuwaibia wananchi tu (full ufisadi). Alafu kwanini usihoji u DR wa Kikwete?. Kwanza huyu Mary mwanjelwa ni mpambanaji sana kwa kuwatetea na kuwaletea maendeleo wakazi wa mkoa wa Mbeya....sema hili lichama alilokwenda (ccm)
ndilo linalomuharibia.
Kaka/Ndugu wasifu ndio kila kitu upambanaji bila kuwa na wasifu ni kazi bure,mtu muongo hafai kuwa kiongozi,uongo ni uongo kwa hiyo kwa kuwa muongo anaondolewa heshima ya kuwa kiongozi hata angekuwa mpambanaji(sijui anapambana na nini)tuache ushabiki na turejea kwenye habari yenyewe ambayo ni kudanganya wasifu sasa wewe UNAKURUPUKA na upambanaji ulitakiwa ukanushe kwa maelezo kama yaliyoandikwa hapo juu.
 
na hakuna media hata moja inayohoji hizi elimu

as a country we are f%^&*d

media nao wamekuwa complicit kwenye hili la kuendekeza hawa watu
 
dawa ni kuondoa kabisa hii ubunge maalum period

wanaotakiwa kuwepo bungeni ni waliochaguliwa na wanaanchi tosha
 
Kwa taarifa A - Level Siha Secondary School ilianza 1991 na si 1983. Tutadanganywa kwa mengi!!!!!
 
Back
Top Bottom