Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Status
Not open for further replies.
Mkuu pleo nakukumbuka ntakujibu hoja zako nikitulia!

Usiwe na hofu ndugu Nakumbuka!
 
Last edited by a moderator:
Ivi mtu akisema Yesu ni Bwana Wa sabato Maana Yale ni nini? Kwamba sabato iliishia kwa Yesu au pale msalabani au vp?

Naomba Msaada wenu wake! Maana Nahisi kuna Watu wanashindwa kuelewa au wanapotezwa na wafasili wabaya Wa maandiko!

Cc: Blueband Basluma Original Eiyer etc all

Mkuu ntuzu pole na hongera kwa kazi hii njema unayoifanya. Tatizo ninaloliona humu, jamaa zetu wenye upako wa roho mtakatifu hawaji na mafungu. Wanataka tufanye ubishi badala ya kuelekezana. Hata hivyo tuko pamoja na ingekuwa vyema wakatueleza maana ya hiki ulichowauliza. Tuko pamoja nimeingia humu ndani.
 
Mkuu pleo nakukumbuka ntakujibu hoja zako nikitulia!

Usiwe na hofu ndugu Nakumbuka!

pamoja mkuu, naukukubali sana msimamo wako kwa unachokiamini.
 
Last edited by a moderator:
Inategemea umeanzia kuhesabia wapi...
Ukianzia Wednesday kwa mfano, siku ya saba itakuwa Tuesday...

Nawashukuru sana wapendwa kupitia humu jf kwa sasa mmenifumbua macho nami mwenyewe ni mkatoliki lakin nilipoichukua biblia na kuisoma kwa makini na kuuliza maswali mbalimbali kuhusiana na dini gani ambayo ni ya kweli neno la Mungu limenifumbua macho ndo nimejua ya kuwa waadventista wasabato ni watu wanaojifunza kweli iliyomo kwenye biblia na kwa sasa nimeacha kuabudu masanamu yaliyochongwa,ibada za wafu,na nimeacha kutubu dhambi zangu kwa mapadri ila kwa sasa nimeamua kufuata kanisa ambalo linatunza sabato ya Bwana Mungu wetu,nawashauri ndugu zangu ambao hawaijui na hawaitunzi sabato waweze kuitunza
Asomaye na afahamu;
Balikiwa ninyi nyote..
 
Ivi mtu akisema Yesu ni Bwana Wa sabato Maana Yale ni nini? Kwamba sabato iliishia kwa Yesu au pale msalabani au vp?

Naomba Msaada wenu wake! Maana Nahisi kuna Watu wanashindwa kuelewa au wanapotezwa na wafasili wabaya Wa maandiko!

Cc: Blueband Basluma Original Eiyer etc all

Bwana Yesu anaposema yeye ni Bwana wa sabato hasemi hivyo kwa mara ya kwanza wakati akiwa hapa duniani. Ukisoma katika kitabu cha Kutoka 20:8... anasema hivi Ikumbuke siku ya sabato uitakase, siku sita fanya kazi yako, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA Mungu wako penye nyekundu panaonyesha kuwa yeye Mungu ndiye mmliki wa sabato na sio mwandamu anayeimiliki. Na ikumbukwe pia kuwa, Yesu kristo ni nafsi katika miongoni mwa nafsi tatu za uungu. Kwa hiyo Yesu kristo hapo anaposema yeye ni Bwana wa sabato anarudia tu kauli ya miaka mingi nyuma aliyoitoa katika mlima wa sinai wakati wa kutangaza amri kumi kwa waisraeli. Na anaonyesha umiliki wa siku hiyo ya sabato.
 
Last edited by a moderator:
Wasabato sio wakristu,ebu watueleze wako dini gani,maana kuna watu wanasema ni wapagani
 
kapamba65, barikiwa sana kwa kuigeukia kweli ya Mungu inayofundishwa na waadventista wasabato tena isiyochanganywa na mambo ya wanadamu.
 
Last edited by a moderator:
kapamba65, barikiwa sana kwa kuigeukia kweli ya Mungu inayofundishwa na waadventista wasabato tena isiyochanganywa na mambo ya wanadamu.

Nami nashukuru kwa kuelewa neno la Mungu linavyotuasa kwa kuikumbuka siku takatifu ambayo bwana aliitenga akaitakasa na kuibariki
Ila nawashauri mzidi kuniombea na maombi yenu ndio yatakayonikomaza katika imani hii..
Barikiwa..
 
Last edited by a moderator:
Wasabato sio wakristu,ebu watueleze wako dini gani,maana kuna watu wanasema ni wapagani

Wakristo ni watu gani hasa?. hebu soma hapa Paulo akimhutubia mfalme Agripa
Acts 26:27-31 King Agrippa, believest thou the prophets? I know that thou believest. Then Agrippa said to Paul, Almost thou persuadest me to be a Christian. And Paul said, I would to God, that not only thou, but also all that hear me this day, were both almost, and altogether such as I am, except these bonds. And when he had thus spoken, the king rose, and the governor, and Bernice, and they that sat with them: And when they had gone aside, they talked between themselves, saying, This man doeth nothing worthy of death, or of bonds.
Kwa hiyo wakristo kwa maana nyepesi na ya haraka ni watu wanaoishi kama alivyoishi kristo. Na Paulo kwa kuwa alikuwa mkiristo aliwaambia watu aliokuwa akiwaandikia mojawapo ya nyaraka maneno haya yafuatayo Niigeni mimi kama mimi ninavyomuiga Kristo. Kumbe mkristo ni yule anayeiga mambo aliyoyaishi kristo mfano.
1. Wanaitunza sabato maana luka 4:16 anasema na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa deaturi yake.
2. Wanaonyesha upendo kwa kila mtu anayewanzunguka
3. na mambo mengine mengi aliyoyatenda Yesu kristo.
Kwa hiyo sisi waadventista wa sabato, ni wafuasi sio tu wa kristo bali ni wafuasi watiifu wa kristo. Maana Yesu alisema maneno haya yafuatayo
Mkinipenda mtazishika amri zangu. Sisi ni watiifu kwa kristo maana amri zake tunazishika kama alivyotuomba kufanya hivyo, tofauti na wengine wanaojiita wafuasi wa kristo huku wakibagua amri za kushika, na hata wengine kufuta kabisa baadhi ya amri as waliona zinawabana katika uongo wao.
 
Nami nashukuru kwa kuelewa neno la Mungu linavyotuasa kwa kuikumbuka siku takatifu ambayo bwana aliitenga akaitakasa na kuibariki
Ila nawashauri mzidi kuniombea na maombi yenu ndio yatakayonikomaza katika imani hii..
Barikiwa..

amina, mimi naahidi kukuombea maana safari ya imani pasipo maombi inakuwa ngumu sana. Maana siraha yetu ya kumshinda shetani ni mojawapo maombi.
 
Kuna hiki kizazi chenu cha nyoka ambacho hamjui madhara ya kuanza kumsengenya mtu kutokana na msimamo wake kiimani na dini yake ambapo kwa kukosa sehemu ya kuonesha udhaifu wenu kwenye kuwaza mnatumia majukwaa ya kijamii! Just go on...

....Je unaweza wazuia wakoseshaji? au hao wasengenyajii kama uwaitavyo? mi nikushauri tu ushike sana ulichonacho..maana vikatisha tamaa vipo ila ole wake yeye aviletae hivyo...pia si kila kisemwacho juu yako wakichukulia kama kilivyo ni busara kuchanganya na akili zako kabla ya kufanya maamuzi...ingawa najua maneno ndio yalileta mapinduzi tunisia, kimbali rwanda na sasa hapo CAR...
 
Bwana Yesu anaposema yeye ni Bwana wa sabato hasemi hivyo kwa mara ya kwanza wakati akiwa hapa duniani. Ukisoma katika kitabu cha Kutoka 20:8... anasema hivi Ikumbuke siku ya sabato uitakase, siku sita fanya kazi yako, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA Mungu wako penye nyekundu panaonyesha kuwa yeye Mungu ndiye mmliki wa sabato na sio mwandamu anayeimiliki. Na ikumbukwe pia kuwa, Yesu kristo ni nafsi katika miongoni mwa nafsi tatu za uungu. Kwa hiyo Yesu kristo hapo anaposema yeye ni Bwana wa sabato anarudia tu kauli ya miaka mingi nyuma aliyoitoa katika mlima wa sinai wakati wa kutangaza amri kumi kwa waisraeli. Na anaonyesha umiliki wa siku hiyo ya sabato.

Vizuri Basluma Original nami pia niongezee kidogo kwa kuangalia katika historia ya uumbaji pale.
Hebu tusome hapa:

Genesis 2:1-3
Thus the heavens and the earth were finished, and all the host of them. [SUP]2 [/SUP]And on the seventh day God ended his work which he had made; and he rested on the seventh day from all his work which he had made.

[SUP]3 [/SUP]And God blessed the seventh day, and sanctified it: because that in it he had rested from all his work which God created and made.


Nimetumia red kuonyesha siku ya Saba (Sabato) kama ilivyotajwa wakati wa uumbaji. Nimetumia blue kuonyesha kile Mungu alichoifanyia(matendo) siku ya Saba.
Mungu anapoibariki siku hii ya Saba, anapoitakasa, anapopumzika anatenda akionyesha kwamba yeye ndiye mmiliki wa hiyo siku. Kwa hiyo anaposema yeye ndiye bwana wa Sabato maana ni kwamba yeye ndiye mmiliki wa hiyo.Hata sisi wanadamu ni mali yake pia. Kama sote tu mali yake, na Sabato ni mali yake kwa nini tusiitunze Sabato kwa vile wote yaani wanadamu na Sabato sote ni mali yake? Ikumbukwe kwamba hata Yesu alipokuwa hapa ulimwenguni aliitunza Sabato.

Luke 4:16
[SUP]16 [/SUP]And he came to Nazareth, where he had been brought up: and, as his custom was, he went into the synagogue on the sabbath day, and stood up for to read.

So Yesu ametuonyesha mfano katika hili la Sabato!
 
.
.
.
Katika hili moja uko kinyume cha Mungu, pia angalia jinsi Yesu alivyobatizwa na Yohana katika mto kwa maji mengi na ubatizo mnaoufanya..! Usifanye kinyume na unayemwabudu!!!! Tuonane kanisani Sabato ijayo!

samahani mkuu najaribu kukuelewa ila imekuwa ngumu, sijui unamaanisha nini kwa hili, kabla ya ubatizo wa Yohana ulikuwepo wa Musa na mingine pia, kwa nini umechagua mmoja tu wa Yohana kama sahihi?
Ningeomba unipe ubatili wa ubatizo wa Musa na wengineo kabla na baada ya Yohana bila kusahau wa sasa kwa makanisa unayoyafahamu.
 
Bwana Yesu anaposema yeye ni Bwana wa sabato hasemi hivyo kwa mara ya kwanza wakati akiwa hapa duniani. Ukisoma katika kitabu cha Kutoka 20:8... anasema hivi Ikumbuke siku ya sabato uitakase, siku sita fanya kazi yako, utende mambo yako yote, lakini siku ya saba ni sabato ya BWANA Mungu wako penye nyekundu panaonyesha kuwa yeye Mungu ndiye mmliki wa sabato na sio mwandamu anayeimiliki. Na ikumbukwe pia kuwa, Yesu kristo ni nafsi katika miongoni mwa nafsi tatu za uungu. Kwa hiyo Yesu kristo hapo anaposema yeye ni Bwana wa sabato anarudia tu kauli ya miaka mingi nyuma aliyoitoa katika mlima wa sinai wakati wa kutangaza amri kumi kwa waisraeli. Na anaonyesha umiliki wa siku hiyo ya sabato.


Nashukuru sn wakuu Basluma Original Na Blueband kwa majibu yenu!


Niseme hivi kwamba Sabato iliumbwa kwa ajili ya mwanadamu na si mwanadamu kwaajili ya sabato! Na kwa Maana Hiyo basi! Sabato iko juu ya mwanadamu !

Wayahudi walikosea sn kumuhukumu Yesu juu ya sabato wakisahau kwamba yeye ni Bwana! Na muumbaji!

Na kwa Maana Hiyo sabato haikuishia kwa Yesu au msalabani
 
Last edited by a moderator:
SDA is an occultic religion. Mkubali mkatae, kama kweli mnajua historia someni history ya mwasisi wenu John Miller. Usimsahau nabii wa uongo Hellen.G.White. Kama sabato ni pumziko basi sisi tumepumzishwa na tunaendelea kupumzishwa na Bwana wa Sabato.
(Mathayo 11:28). Nyinyi endeleeni kushika siku. Okokeni leo.
 
SDA is an occultic religion. Mkubali mkatae, kama kweli mnajua historia someni history ya mwasisi wenu John Miller. Usimsahau nabii wa uongo Hellen.G.White. Kama sabato ni pumziko basi sisi tumepumzishwa na tunaendelea kupumzishwa na Bwana wa Sabato.
(Mathayo 11:28). Nyinyi endeleeni kushika siku. Okokeni leo.

Wewe umeokoka?? Ni kosa kubwa kusema umeokoka wakati bado unaishi katika dunia ya dhambi,Unaposema umeokoka ina maana wewe dhambi huna,kitu ambacho si kweli.Hao hao mnasema mmeoka huku mnakamatwa ugoni.kumbuka kama wewe umeokoka ina maana humwitaji tena YESU,kwa maana YESU alikuja kwa wenye dhambi na sio watakatifu kama nyie.Kama YESU mwenyewe alisema YEYE si mwema bali BABA WA MBINGUNI,Wewe ni nani sasa unaemzidi YESU.Ole wenu nyie wanafiki.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom