Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Status
Not open for further replies.
Ndugu we mbona si mwelewa Neno la Mungu haliwezi kubadilishwa na mtu yeyote na
Bwana Mungu sio kigeugeu eti kwamba leo anakwambia hiki na kesho anabadilisha sio bhana kama unavyofikiria wewe jaribu kuwa mwelewa,
Balikiwa..

Naomba kueleweshwa hivi sabato ni Jumamosi ? Na ni kila anayesali siku hiyo ni msabato?
 
Hivi hakuna Biblia za Kiswahili?

Zipo lakini niliamua kutumia hiyo ya kiingereza maana hiyo inawezekana ku copy na ku paste wakati za kiswahili haiwezekani(kwa zile nilizonazo).
 
Naomba kueleweshwa hivi sabato ni Jumamosi ? Na ni kila anayesali siku hiyo ni msabato?

Sabato kwanza kabisa humaanisha Kumbuka. Na unakumbuka nini, ni kumbukumbu kuwa Mungu aliniumba alikuumba na aliumba kila kitu. Na hii ilifanyika kwa ajili ya mwanadamu ili kukumbusha tukio hilo la mhimu(maana mwanadamu ni msahaulifu). Pasipo kumbukumbu hiyo, ni sawa na kukiri kuwa ulimwengu huu ni matokeo ya uibukaji na nadharia nyingine nyingi. Na Mungu aliamua kutenga siku moja tu kwa ajili ya kumbukumbu hiyo, ambayo ni siku ya saba, tena Yesu mwenyewe alisema ndiye BWANA WA SABATO. Na siku hiyo ya saba ya kila juma, ni siku ya jumamosi kulingana na kiswahili chetu.
Kama una swali zaidi karibu.
 
Naomba kueleweshwa hivi sabato ni Jumamosi ? Na ni kila anayesali siku hiyo ni msabato?

Sabato ni jumamosi.Kumbuka kuna kalenda 3 duniani.Gregorian ambayo tunatumia sisi,Arabic na Kalenda ya Israel.kalenda ya israel ndio kalenda ya tangu zamani haina siku 28,29 au 31.kila mwezi ni siku 30.Si kila anaesali jumamosi ni msabato,hata waisrael wanasali jumamosi ili sio wakristo.kama una swali zaidi karibu!
 
Wakristo gani hawaruhusu kunywa pombe kidogo bila kulewa?
Hawali kitimoto eti ni haramu wakati kila kilichoumbwa na mungu mwanadamu usikiite haramu?
Hawabatizi watoto?
Hawavuti tumbaku hata kama ni dawa?
Hawaabudu siku ya j2?
Hawaneni kwa lugha?
Hawafungishi ndoa za wajawazito?(wanakupima kutumia dr wao kama mwanamke ni mjamzito kabla ya kukufungisha ndoa)
Wana idara nyingi za elimu za kukuza mtoto mpaka awe mkubwa kama vile taasisi ya elimu na sio kanisa?

Hawa hawawezi kuwa wakristo labda ni waislamu.

Duuuuuh!!kweli we ndo umepotea kabisaa,nadhani upo nje ya kuitwa mkristo..
 
Naomba kueleweshwa hivi sabato ni Jumamosi ? Na ni kila anayesali siku hiyo ni msabato?

wanao sali jumamosi ni wayahudi na waadventista wa sabato. siku ya sabato ni jumamosi soma quran, soma kamsi, katikisimu, dictionary, biblia, encyclopedia utapata majibu.
 
Naomba kueleweshwa hivi sabato ni Jumamosi ? Na ni kila anayesali siku hiyo ni msabato?

1. Ni kweli Sabato ni Jumamosi
2. Ni kweli pia kuwa kila anayesali Jumamosi ni msabato kwa maana kwamba neno msabato lina maana ya mtunza sabato.

Hata hivyo, lazima uelewe kwamba kuna madhehebu yapatayo 500 ambayo husali na kutunza Sabato ya Siku ya Saba kama ilivyoagizwa na Mungu (Kutoka 20:8). kwa mfano:

Seventh-day Adventists Church
Seventh-day Pentecostal
The United Church of God
Seventh-day Adventist Reformed Movements
etc.
Makanisa haya yana mafundisho na imani tofauti japo kuna baadhi ya maeneo kama hilo la Sabato wanashabihiana.
 
mada nzuri na mada kama hizi nazipenda sana, maana biblia inasema katika kutoka 20:8-11,ikumbuke siku ya sabato uitakase,na sio kuikumbuka tu,bali tunaishi kwa amri kumi zinazoonesha upendo wa Mungu kwetu so kama huishiki sabato ina maana unaikana kweli na neema ya Bwana wetu yesu kristo,na kiukweli mtoa mada alichokifanya ni kuja na upanga kama petro badala ya kumtanguliza YESU, ukitaka miujiza ya kweli mtafute YESU ambaye ni BWANA WA SABATO,atkuonesha hutokuwa kama ulivyo,utakuwa na kitu cha ziada....... zaidi soma hapa unajua kuna wadanganyao? ni hao wachungaji wanaokusomea kafungu kamoja na kubaki kueleza tu juu ya neema bila wajibu. YEREMIA 23:1-2,EZEKIEL 13:22, ISAYA 30:10, YEREMIA 25:31......WAMEASI SHERIA NA KUZIPINDUA............ISAYA 24:1,3,5-6. JIPANGE TOKA HUKO MIMI NILIKUWA MLOKOLE LAKINI NIMEKUTANA NA YESU SASA, AMENIBADILISHA mimi nayachunguza sasa maandiko mi mberoya, ukimjua bwana wa sabato atakufundisha sana tena utashangaa mtafute utamwona........
 
Hivi jamani hamjui Wasabato walitengwa huko Marekani maana hawakuamini dhana ya Utatu Mtakatifu....??? Mpaka kahaba Hellen G White anaaga dunia alikuwa haamini uwepo wa utatu Mtakatifu...

Walikuja kuamini uwepo wa Utatu Mtakatifu kwa shingo upande miaka ya 1900....Ndipo wakakubalika kama ni dhehebu...

Hili Dhehebh lilikuwa ni kundi la Wanaharakati waliolaaniwa...
SDA ni moja ya strange religion on Earth.............

The four Cult Religion
Seventh Day Adventist
Jehova Witness
Mormon
Christian Scientist


Unazijua sifa na tabia za CULTS? kama huzijui ni hizi hapa

1. Identifying Feature #1: Cults have a single powerful leader who becomes the cult’s messiah.
The leader is a charismatic individual who focuses attention on himself and becomes more of a source for truth than God.

2. Identifying Feature #2:The cult leader’s word, his teachings, become absolute truth.
They overshadow the teachings of the Bible.


3. Identifying Feature #3:Cults manipulate.Cults use pressure tactics and deception to recruit members, and they coerce members into submission, into staying. Satan uses pressure, coercion, and force

4. Identifying Feature #4:Cults appeal to miracles as a sign of their “divine” credentials,especially when their teachings contradict Bible truth

5. Identifying Feature #5:Cults isolate.Cults isolate converts not only from the outside world but even from their families—a very dangerous thing.
 
kuna jamaa wao ile amri ya ikumbuke siku ya sabato wanasema shika kitakatifu siku ya Bwana....
sipati picha ya hao wanao edit maandiko siku ya mwisho
 
Mkuu Ngereja shukrani sana kwa ufafanuzi wako, maana kila mara mkuu tedo anakuja na visimulizi vyake vya sda kama cult. Nadhani kuanzia leo amefahamu na sidhani kama ataendelea na hiyo stori yake maana sda hawana kiongozi wa kudumu badala yake kila miaka mitano anachaguliwa kiongozi mpya.
 
Last edited by a moderator:
Sasa nyinyi mnatofauti gani na Mafarisayo...???? Nyinyi ni typical Mafarisayo..

Binafsi naamini katika Ufarisayo, sijui wewe ni Msadukayo hauamini katika kiyama na maisha baada ya kifo?

Imani ya Ukristo imejengeka katika msingi wa Ufarisayo.
 
Kama Sabato ni Jumamosi sawa, naomba ufafanuzi wa Law 25:3-8. Barikiwa

Iko hivi Binti Sayuni, sabato licha ya kutolewa kama kumbukumhu ya uumbaji, lakini pia Mungu aliagiza iwe siku ya kupumzika. Kwa hiyo, si mara zote utakazoona neno sabato ukajua ni siku ya kukumbuka uumbaji, bali pia hutumika kuwakilisha pumziko. Ndio maana watumishi wana kitu kinaitwa sabatical leave. Kwa hiyo basi, waisraeli walikuwa na mapumziko mengi yaliyoitwa sabato, mfano sabato ya kupumzisha nchi baada ya kuilima kwa miaka sita wa saba inapumzishwa. Na ndio maana hata kuna sura zinaeleza sabato kama wingi(kwa kiingereza wakitumia neno Sabbaths).
 
Last edited by a moderator:
Binti Sayuni, ili kutofautisha sabato na sabato ya siku ya saba kwa fungu hili lifuatalo Leviticus 23:16 Even to the morrow after the seventh sabbath shall ye number fifty days; and ye shall offer a new meat-offering to the LORD.
Hapa anaongelea sabato ya saba baada ya sabato ya kwanza tokea sherehe husika. Hapa haitajwi kama siku ya saba bali kama pumziko lililoidhinishwa. Hebu ona pia hapa Paulo anapoeleza kuhusu kutohukumiwa kwa mambo mbalimbali na sabato hapa ameitumia kama wingi kuwakilisha sabato za mapumziko ya kawaida na sio sabato ya siku ya saba, hebu ona hapa.
Colossians 2:16 Let no man therefore judge you in food, or in drink, or in respect of a holy-day, or or the new-moon, or of the sabbaths:
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom