Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Wasabato ujumbe wenu huu hapa

Status
Not open for further replies.
Hayo mageuza aliyafanya kabla ya kukamatwa na kuuwawa ambapo aliezea tukio zima na atakae msaliti,ni wapi imeandikwa pasaka ni kusherekea ujio wake na mateso yake?,pili ikiwa wayahudi walisherekea pasaka kwa kuchinja mwanakondoo kwa ishara ya damu Je sadaka ya Yesu ni ipi?,tatu swali langu hukumalizia kujibu yaani ufufuko wa Yesu Je mnaamini ilo?

Sadaka ya Yesu ni kufa msalabani na ndio Pasaka mpya... Kusulubiwa na kufa kwake ili akomboe ni agano jipya baada ya ile ya kuchinja kwa sababu ile ilikuwa pia ni ishara ya ukombozi kutoka Misri na mwanakondoo mpya ni Yesu.
 
Sisi tunaadhimisha hivi pasaka(kama Yesu alivyoagiza) Matthew 26:26-28 And as they were eating, Jesus took bread, and blessed it, and broke it, and gave it to the disciples, and said, Take, eat; this is my body. And he took the cup, and gave thanks, and gave it to them, saying, Drink ye all of it; For this is my blood of the new testament, which is shed for many for the remission of sin. Na pasaka iliadhimishwa kuelezea ujio wa Yesu duniani na mauti yake. Na hivyo sisi tunakumbuka mauti yake kwa kunywa divai(kama damu ya Yesu) na mkate(kama mwili wa Yesu). Ile nyingine ya kipagani wanayoiita easter sisi hatuna sehemu nayo maana kiukweli ni sikukuu ya kumbukumbu ya mungu ishtar. Kumbuka pia, sikukuu nyingi za kidini leo, ni matokeo ya upagani uliovikwa vazi la ukristo ili kuficha maovu yao.

Kwani huo mkate na divai mnakunywa kanisani au? Na Ntuzu kasema mnasherekea mara nne kwa mwaka kwa kuwa hakuna siku maalumu je pasaka ya Easter ina siku maalum? Mbona kika mwaka inabadilika tarehe au mwezi..

Pili wayahudi wa sasa wanasherekeaje pasaka yao?

Je hao Wayahudi wa zamani walikuwa wanasherekea mara nne kwa mwaka kama nyie?

Kwanini nyie msherekee mara nne, je Biblia inaruhusu hivyo?

Je hiyo mara nne kwa mwaka si tayari kwenu mmesha jiwekea muda maalum wakati Bible haijaonyesha muda maalum so hamna tofauti nao.
 
Last edited by a moderator:
Wapendwa,

nimeshangaa sana kusikiliza radio yenu inayoitwa Morning star na kukumbana na kashfa za ajabu juu ya makanisa mengine nashangaa mhuburi anasema eti makanisa mengine wakiomba wanakuwa kama wameingiwa wazimu,haitoshi akaendelea makanisa mengine yanayoitwa ya walokole wakihubiri wanaongea kama wamelewa au wameingiwa wazimu.

Nyie wasabato nyie hamjui biblia wala utendaji kazi wa Roho mtakatifu.

Ngojeni niwaambie nyie wasabato mnaojifariji mnamjua Mungu kuliko makanisa mengine.

Mimi nimeokoka na nimejazwa Roho mtakatifu,nikianza kuomba najikuta nimezama kwenye upako wa Roho mtakatifu,manake ni kwamba Roho mtakatifu sasa anaishi ndani yangu na ananiongoza kwa mambo yote ninayofanya hapa duniani.

Hao mnaofikiri wameingiwa wazimu ni kwamba wamejazwa Roho mtakatifu,kumbuka Yesu alipopaa mbinguni aliwaahidi wanafunzi wake wabaki Jerusalemu mpaka wajazwe Roho mtakatifu.

Mnakumbuka walivyojazwa Roho mtakatifu watu waliwadhihaki wakisema wamelewa kumbe ulikuwa UPAKO WA ROHO MTAKATIFU.

Nawashangaa sana enyi wasabato badala ya kupambana na shetani mnahangaika na makanisa Yenye imani kama yenu,huu ni uwezo mdogo wa kuelewa maandiko matakatifu.

Enyi wasabato vita yetu siyo ya damu na nyama bali ni katika ulimwengu wa ROHO.

Kaeni kama mlivyo na tutawaombea ili Mungu awatoe hayo yaliyo kwenye moyo wenu.

Siungi mkono kukashfu madhehebu mengine, lakini ni kweli kwamba baadhi ya waumini wakisali ni kama wameingiwa na wazimu na wanakuwa kama wanamlazimisha Mungu ajibu maombi yao wakati tunafundishwa kwamba Mungu anajibu maombi yetu kwa muda anaopenda na kwa namna anayopenda na si kwa kuwazimishwa na watu waliookoka au ambao hawajaokoka. Kuna zaburi moja inasema "tunapanga na Mungu anatekeleza [kwa jinsi anavyoona inafaa kwake]."
 
Sadaka ya Yesu ni kufa msalabani na ndio Pasaka mpya... Kusulubiwa na kufa kwake ili akomboe ni agano jipya baada ya ile ya kuchinja kwa sababu ile ilikuwa pia ni ishara ya ukombozi kutoka Misri na mwanakondoo mpya ni Yesu.
Mkuu ilo Swali nimemuuliza Msabato anipe jibu au wewe ni msabato na ndio jibu lenyewe..
 
Hebu someni haya maandiko myachambue ndugu zangu
Matendo 13:9 , Matendo 19:11-12, Matendo 10:3-5
Waefeso 1:12-13 Waefeso 4:11-12. Wakolosai 2:16-17.Wathesalonike wa 1, mlango wa 1:4-5.
Soma kwa kutulia na umakini
 
Ntuzu mbona hamtoi majibu humu au maswali magumu?
 
Mkuu ilo Swali nimemuuliza Msabato anipe jibu au wewe ni msabato na ndio jibu lenyewe..

Teh teh teh tuwasubiri wenye dini yao... Ila me najiulizaga tu hivi wale Mitume walikuwa dini gani na Yesu mwenyewe je? Na wazazi/Walezi wake walikuwa dini gani.. Na hivi Mitume,manabii na Yesu mwenyewe walukuja kuleta dini?
 
Wathesalonike wa 1 ule mlango wa 1:4-5.
Kuna kupokea injili ya Maneno matupu na injili yenye nguvu katika Roho mtakatifu.
Neno la Mungu linapohubiriwa katika Roho mtakatifu na nguvu, lazima ile nguvu isababishe maajabu.
Shida ipo kwa hawa wanaohubiri au wanaoifikisha injili kwa Maneno matupu
 
Teh teh teh tuwasubiri wenye dini yao... Ila me najiulizaga tu hivi wale Mitume walikuwa dini gani na Yesu mwenyewe je? Na wazazi/Walezi wake walikuwa dini gani.. Na hivi Mitume,manabii na Yesu mwenyewe walukuja kuleta dini?

Dini ya makka ya kulipuana kwa mabomu iyoo!
 
Teh teh teh tuwasubiri wenye dini yao... Ila me najiulizaga tu hivi wale Mitume walikuwa dini gani na Yesu mwenyewe je? Na wazazi/Walezi wake walikuwa dini gani.. Na hivi Mitume,manabii na Yesu mwenyewe walukuja kuleta dini?
Yesu ni zaidi ya dini,binadamu ni zaidi ya dini,neno la Mungu ndio uzima bhana ukishika ilo ndio uzima wenyewe,haya mambo mengine yamejaa utashi wa wanadamu,kama hawapendani duniani watapendana Mbinguni?
Love is my religion..
 
Sijui ni lugha ipi ilitumika na huyo mchungaji,lakini kama hoja ni hii uliyoileta,mie sioni kashfa hapo zaidi ya mtu kusimamia kile anachoamini kuwa si sahihi.Sasa kama wewe unapinga,basi mjibu kwa hoja kwa nini wewe unaamini katika kunena kwa lugha.Dini tumezikuta zikiwa nyingi wakati Mungu ni mmoja tu,lazima turuhusu mijadala yenye criticism ndani yake ili kujua nani anasema kweli.Wasabato wanayo hoja na wananukuu maandiko yanayoonyesha kuwa mitume walinena kwa lugha zilizoeleweka,nyinyi walokole mna hoja gani kuhalalisha unenaji wa lugha isiyoeleweka?tena kuna mahali biblia imezungumza sana mambo haya nadhani ni Paulo akizungumzia matatizo ya kunena lugha za malaika zisizoeleweka kwa wanadamu.Kwa hiyo kunena kwa lugha za malaika hakuhalalishi presence ya holy spirit tu,kwani hata shetani ni malaika na anapenda kuigiza mambo ya Mungu ili kudanganya watu vizuri. Cha msingi tufuate kanuni ya Yesu,"mtawajua kwa matunda".Wewe unayenena kwa lugha,tukikutazama mwenendo wako,tutamuona Yesu?Wewe unayejiita msabato,tukikutazama mwenendo wako,tutamuona Yesu kristo aliye bwana wa sabato?mwisho naomba niseme,tusikasirishwe na wale wanaopingana na imani zetu,kama hawajatukana wala kuvunja sheria ila wametoa tu hoja,tuwajibu kwa hoja,hivyo ndivyo bwana Yesu alishindana na mafarisayo hata wakamkimbia!tuachane na "smokescreen christianity",tuwe wakristo kwa imani na matendo.
 
Kwani huo mkate na divai mnakunywa kanisani au? Na Ntuzu kasema mnasherekea mara nne kwa mwaka kwa kuwa hakuna siku maalumu je pasaka ya Easter ina siku maalum? Mbona kika mwaka inabadilika tarehe au mwezi..

Pili wayahudi wa sasa wanasherekeaje pasaka yao?

Je hao Wayahudi wa zamani walikuwa wanasherekea mara nne kwa mwaka kama nyie?

Kwanini nyie msherekee mara nne, je Biblia inaruhusu hivyo?

Je hiyo mara nne kwa mwaka si tayari kwenu mmesha jiwekea muda maalum wakati Bible haijaonyesha muda maalum so hamna tofauti nao.

tofautisha makanisa, yapo makanisa yaliyozaliwa kutokana na tafsiri za kibiblia ila lipo lililozaliwa kabla ya biblia na kuzaa biblia!
 
Last edited by a moderator:
Wapendwa,

nimeshangaa sana kusikiliza radio yenu inayoitwa Morning star na kukumbana na kashfa za ajabu juu ya makanisa mengine nashangaa mhuburi anasema eti makanisa mengine wakiomba wanakuwa kama wameingiwa wazimu,haitoshi akaendelea makanisa mengine yanayoitwa ya walokole wakihubiri wanaongea kama wamelewa au wameingiwa wazimu.

Nyie wasabato nyie hamjui biblia wala utendaji kazi wa Roho mtakatifu.

Ngojeni niwaambie nyie wasabato mnaojifariji mnamjua Mungu kuliko makanisa mengine.

Mimi nimeokoka na nimejazwa Roho mtakatifu,nikianza kuomba najikuta nimezama kwenye upako wa Roho mtakatifu,manake ni kwamba Roho mtakatifu sasa anaishi ndani yangu na ananiongoza kwa mambo yote ninayofanya hapa duniani.

Hao mnaofikiri wameingiwa wazimu ni kwamba wamejazwa Roho mtakatifu,kumbuka Yesu alipopaa mbinguni aliwaahidi wanafunzi wake wabaki Jerusalemu mpaka wajazwe Roho mtakatifu.

Mnakumbuka walivyojazwa Roho mtakatifu watu waliwadhihaki wakisema wamelewa kumbe ulikuwa UPAKO WA ROHO MTAKATIFU.

Nawashangaa sana enyi wasabato badala ya kupambana na shetani mnahangaika na makanisa Yenye imani kama yenu,huu ni uwezo mdogo wa kuelewa maandiko matakatifu.

Enyi wasabato vita yetu siyo ya damu na nyama bali ni katika ulimwengu wa ROHO.

Kaeni kama mlivyo na tutawaombea ili Mungu awatoe hayo yaliyo kwenye moyo wenu.

Kwani wasabato wako huku? nenda kawahubirie kanisani kwao halafu uwapigie rikabandarashika,
 
Teh teh teh tuwasubiri wenye dini yao... Ila me najiulizaga tu hivi wale Mitume walikuwa dini gani na Yesu mwenyewe je? Na wazazi/Walezi wake walikuwa dini gani.. Na hivi Mitume,manabii na Yesu mwenyewe walukuja kuleta dini?

Yesu alikuja kuokoa kilicho potea au alikuja na wokovu ZEKARIA 9:9
 
Yesu ni zaidi ya dini,binadamu ni zaidi ya dini,neno la Mungu ndio uzima bhana ukishika ilo ndio uzima wenyewe,haya mambo mengine yamejaa utashi wa wanadamu,kama hawapendani duniani watapendana Mbinguni?
Love is my religion..

Nashangaa hata maandiko yanasema ukimpenda jirani unaye muona Mungu wa mbinguni utampenda na usipompenda jirani unaye muona Mungu wa mbinguni utampendaje?.
 
Yesu ni zaidi ya dini,binadamu ni zaidi ya dini,neno la Mungu ndio uzima bhana ukishika ilo ndio uzima wenyewe,haya mambo mengine yamejaa utashi wa wanadamu,kama hawapendani duniani watapendana Mbinguni?
Love is my religion..

Good but you need more than that
 
tofautisha makanisa, yapo makanisa yaliyozaliwa kutokana na tafsiri za kibiblia ila lipo lililozaliwa kabla ya biblia na kuzaa biblia!

Mkuu ndo umesamarize hayo maswali yangu au la? Kwa hiyo hilo Kanisa lililo zaa Biblia ndo lina ruhusu kusherekea Pasaka mara 4 na wale Wayahudi walikuwa wanasherekea mara nne maana walikuwa hawajui wa sherekee lini Pasaka yao kweli?
 
Wathesalonike wa 1 ule mlango wa 1:4-5.
Kuna kupokea injili ya Maneno matupu na injili yenye nguvu katika Roho mtakatifu.
Neno la Mungu linapohubiriwa katika Roho mtakatifu na nguvu, lazima ile nguvu isababishe maajabu.
Shida ipo kwa hawa wanaohubiri au wanaoifikisha injili kwa Maneno matupu

utatofautisha vipi maajabu ya nguvu za shetani zitokazo "Nigeria" na maajabu ya nguvu za roho mtakatifu zitokazo mbinguni?ni kweli muda wote Yesu alihubiri kwa maajabu?hakuna muda alizungumza maneno matupu kwa ajili tu ya kufafanua bila maajabu?mitume wote na manabii walihubiri kwa maajabu?Leo hii wewe unajifunza Yesu "wa kusoma vitabuni",akiwa complete,wakati ule watu walijifunza Yesu mpya,ambaye hajawahi kuwako popote duniani,unafikiri kati yako wewe uliyeletewa Yesu complete vitabuni,na wale ambao hawakuwa na biblia iliyojaa mafundisho na miujiza ya Yesu,nani anahitaji msaada mkubwa wa kimafundisho ikiwemo maajabu ili kujenga imani ndogo ya punje ya haradali?fikiria sana swali hili mkuu,utafakari kwa kina.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom